Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane. Mwenye Nguvu Mpishe!

Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane. Mwenye Nguvu Mpishe!

Unajua kwa tanzania elimu ya siasa na uraia kuna mapungufu sana........
Kiukweli wapinzani pamoja na serikali wote wanamaeneo wanakosea pia wanapatia.........
Nikianza na wapinzani........hawa mlengo wa hoja zao zimekaa kukosoa serikali sio kwa lengo la kuijenga bali kuiharibia ili nao wapate ridhaa ya wananchi katika kuliongoza taifa.....hili si jambo zuri hata kidogo.......huu ni usanii kabisa....

Nitawapa mfano wa inshu ya sukari.........wabunge wengi wa upinzani walichachamaa sana kwa kuwaambia wananchi kuwa serikali haiwatakii mema kwa kuzia uagizaji wa sukari usio fuata taratibu za kisheria za biashara katika manunuzi........nakumbuka walituhadaa wananchi kuwa sukari haitokuja kushuka maana serikali inakosea......leo hapa mimi nipo kilimanjaro nimetoka kununua sukari kilo 1800. Tokea ilipokuwa 3000. Sasa najiuliza huwa wapinzani wakiongea wanatumia taarifa za wapi.......maana ni kama wanapotosha uma.........mimi naona ni kama wanaweka jitihada nyingi kubeza jitihada zinazofanywa na kupotosha uma wa watanzania.......na asilimia kubwa ya watanzania si wafuatiliahi huwa wanajiridhisha na story za kusadikika ama za mtaani au post za facebook ambazo huwa wanaozipost hawajulikani ni akina nani plus wanamalengo gani.......

Swala la elimu......wanabeza sana maamuzi ya kuweka vigezo ambavyo vitarejesha thamani ya elimu sio kama sasa kila mtu anadegree uchwara halafu uwezo zero kazi kupiga domo tu.....wapinzani wanakazana kuropoka tu ili wapate hii popularity kama ya akina wema na diamond kwa kuropoka.......

Me nasema mh.raisi yupo sahihi kukataza hizi kelele zisizo na tija yeyote ........hawa wapinzani si muda wote.wapo sahihi......wanayohaki ya kuikanya......kuirekebisha na kuikosoa serikali.......ila sio kwa staili hii wanavyofanya ya kuibeza na kuikejeli badala ya kuishauri.............wapinzani hawaongei jipya kazi yao ni kubeza .Unapomkosoa mtu......toa suggestion ......au wazo mbadala ila sio unangojea mwenzako akosee ndipo povu likutoke........tena unatoa kauli za kuhatarisha amani na usalama wa raia........

serikali ni kweli inakosea kuwazuia wapinzani kuongea na uma lakini ni kwasababu wamegundua mnaitumia fursa hiyo kuongea vijembe.....na kukejeli serikali ndio maana wanawabana kwa kila namna .......hata ningekuwa mimi nisingeruhusu mtu ambaye hauna ridhaa ya kuendesha nchi uongee maneno ya uchochezi badala ya kutoa ushauri.......hii kitu alishaifanyaga mbatia mara moja tu......aliishauri serikali kuhusu kuhamisha maofisi yao maeneo ya posta na kuyasambaza maeneo mengine ili kupunguza msongamano wa foleni za magari asubuhi watu wanapokwenda makazini maana msongamano huu unaitia serikali hasara kila siku ya mabilioni......na ndio maana kikwete akamkubali sana akampa nafasi ubunge viti maalumu.........mrema huyo hapo amepewa nafasi anashirikiana na serikali......huo ndio upinzani wa ukweli unatakiwa kuwa sio hawa wakina zitto wanakwenda kusoma vitabu na notes za shule wanakuja kutuletea theory za utabiri hapa.....wanaboa sana......
Mkuu umeandika GAZETI hata sijui ulikuwa unataka nini.....!
 
Wanabodi,

Kama kawaida yangu kutoa ushauri wa bure, huu ni ushauri wa bure kwa Chadema, japo kuandamana na mikutano ya kisiasa ni haki iliyotolewa kihalali ndani ya katiba, nawashauri kwa dhati kabisa, tafadhalini sana msiandamane, na kusitisha hiyo Operesheni UKUTA, ili kuutumia ule msemo wa Kiswahili "Mwenye nguvu mpishe", hata kama una haki, usitake kujipima nguvu kwa kutunishiana misuli na mtu mwenye nguvu zaidi yako, na sio tuu ana nguvu zaidi yako, na tayari, umeishajua ni dikiteta, bali ndio mwenye nguvu ya dola mikononi mwake!.

Misingi ya Katiba na The Rule of Law
Tanzania ni nchi inayofuata misingi ya katiba na sheria, (the rule of law) ambapo inapaswa kuendeshwa kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni, na sio kwa matamko ya viongozi yanayokwenda kinyume cha katiba!.

The Separation of Powers & Check and Balance .
Nchi yetu ina mihimili mikuu mitatu, Serikali, (the executive), Bunge (The Legislature) na Mahakama (The Judiciary). Mihimili hii mitatu, ilipaswa kufanya kazi kwa kujitegemea bila mhimili mmoja kuingilia mhimili mwingine (independence), huki kila mhimili uki act as a watchdog wa muhimili mwingine usivuke mipaka ya madaraka au mamlaka yake yaani (The sepaation of powers check and balance).

Serikali yenye Nguvu, Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo!.
Mihimili hii, inaongozwa na viongozi ambao wana mamlaka kuu kuhusu mihimili yao. President ndio mkuu wa the executive, Spika ndio mkuu wa The Legistlatue, na Jaji Mkuu, ndie mkuu wa The Judiciary, lakini pamoja na nia njema kuwa mihimili yote inamamlaka na hakuna mhimili wowote uliokuwa unapaswa kuwa na mamlaka kuliko mhimili mwingine, lakini kiukweli, mhimili wa the executive ndio mhimili mkuu unaomiliki vyombo vya dola na kuitawala mihimili mingine yote!, hivyo mkuu wa the executive, yaani rais, ndio kila kitu!, akisema!, amesema!.

Rais Magufuli na Uvunjaji wa Katiba.
Tuambiane ukweli, tangu rais Magufuli ameingia madarakani, sio mara moja au mbili amekuwa akitoa kauli tata, zinazokwenda kinyume cha katiba, mhimili wa Bunge na Mahakama ilipaswa kuingilia kati kwa kumcheck mkuu wa the executive, lakini vyombo hivyo vimekaa kimya hivyo kumfanya rais ajisikie kuwa he is always right! kwa kanuni ya "the boss is always right!".

Udikiteta wa Magufuli.
Hoja kama Magufuli ni dikiteta au la, haina mjadala, Magufuli ni dikiteta wa ukweli ambaye hana msalie mtume, na alipoingia tuu madarakani, alianza kuonyesha udikiteta wake right away kwa kuliingilia bunge na mahakama kuziweka chini ya amri zake!. Lile katazo lake la watumishi wa umma hawaruhusiwi kusafiri safari za nje bila kibali chake kupitia kwa Katibu Mkuu Kiongozi, liliwahusu watumishi wote wa serikali, likiwemo bunge na mahakama!, just imagine Jaji Mkuu na Spika wa bunge wakapige magoti kwa rais kuomba kutimiza wajibu wao!.

Baada ya katazo lile, checks and balance zingepaswa kuanzia hapo kwa Jaji Mkuu kumweleza rais huko ni kuingilia uhuru wa mahakama (the independence of the judiciary) hivyo muhimili wa mahakama haukupaswa kujisubmit chini ya the executuve, bali mamlaka hayo ya kuzuia safari za nje, Spika alipaswa kuwa nayo kudhibiti safari za mhimili wa bunge, na Jaji Mkuu alipaswa kuwana nayo kudhibiti safari za mhimili wa mahakama, lakini mihimili hii ilikaa kimya kwa kujisubmit chini ya the executive, hivyo kumfanya rais ndio kila kitu!.

Hivyo sasa rais Magufuli ndio kila kitu, hakuna cha bunge, mahakama, wala katiba, amri ya rais ndio kila kitu na ndio sheria kuu!, hivyo nawashauri Chadema kwa dhati kabisa, wasitishe maandamano yao, wasifanye kabisa mchezo wa kumjaribu Ngosha, wataumia bure!.

Hili la udikiteta wa rais Magufuli, tumeisha lizungumza sana humu
Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...
Rais Magufuli, Waliomchagua Wanajuta!, Wasiomchagua Wanamshangilia ...
Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria ...
Utumbuaji Majipu wa Rais Magufuli: Is It A Right Thing, At The ...
Je, Hizi Terorizing za Ziara za Kushtukiza, Hakutajenga Nidhamu ya ...
Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote | Page ...
Nimetishwa, Kushitushwa na Kuogopeshwa na Kauli Hii ya Rais ...
Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na ...
Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa ...

Ila kitu kimoja kuzuri kuhusu udikiteta wa rais wetu, ni Rais Magufuli ni dikiteta mzalendo!, mwenye uchungu na umasikini wa nchi hii, mwenye nia njema ya kusafisha uozo wote wa uzembe, rushwa na ufisadi, na kulikomboa taifa letu toka kwenye lindi la umasikini uliotopea na kuwa nchi ya maziwa na asali kupitia uchumi wa gesi na viwanda.

Mungu mbariki Magufuli!.

Mungu ibariki Tanzania.

Wasalaam.

Pasco
Rejea za shauri za bure
Ushauri wa Bure Kwa Lowassa: Kwa Vile ni Magufuli, Kubali Matokeo ...
Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Hata kama ni kweli uliibiwa kura; Kaa ...
Ushauri wa Bure kwa CCM: Hope for the best but get prepared for ...
Ushauri wa Bure kwa Mhe. Lowassa: Ili kuilinda Heshima yako ...
Ushauri wa Bure kwa ZZK!-Congratulations..But,,,!, Be Calm!, Keep ...
Ushauri wa Bure Kwa Hon Dr. Harison Mwakyembe (Mb)-Kwa Hili la ...
Ushauri wa Bure Kwa Mhe. Zitto on Escrow Report: Please Keep Quite ...
Ushauri wa Bure kwa CHADEMA: Heri Nusu Shari Kuliko Shari Kamili ...
Ushauri wa Bure kwa Rais Magufuli, Futilia Mbali Utawala wa Sheria ...
Ushauri wa Bure kwa Rais Kikwete, muombe msamaha Lowassa kabla ya ...
Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Usikanyage Arumeru!, Atamponza Sioi!.
Ushauri wa Bure kwa Dr. Shein: Mfute Kazi Haraka, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar ...
Ushauri wa Bure kwa Magufuli, DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es ...


Pascongojaa historia iandikwe. AUE KWA MAMILIONI
 
Kwahiyo unatushauri tuwe kama Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo ili ajiskie always Right.

Huyo Mungu uliemuomba ambariki huyo mvunja katiba ungeanza kwa herufi ndogo jina lake isomeke 'mungu' na sio "Mungu"


Tena tuliosema atakua one term president tulikosea hata term moja hatamaliza kama tutashikilia msimamo wetu Septemba mosi na tunaweza kuigeuza ajenda ikawa ya kumng'oa ikulu.

He should be careful of what he wish for!
Ben ccm ina vibaraka wake kwenye vyama vya upinzani kama Mrema, cheyo, Dovutwa and likes.

Hivi hakuna mabingwa wa mikakati huko kwenye UKAWA mkawa na chama chenu cha kimkakati kwa mfano labda UMD kiandae matembezi ya mshikamano kuunga mkono kauli ya Rais?

Kuna wakati inabidi kumtwisti tu mtu mpenda sifa then mwisho anajiona yeye ndio hana busara.

Kwa upeo wangu taasisi ikiomba kibali Polisi cha matembezi ya mshikamano kumuunga mkono Rais hakuna Polisi wa kuzuiya.

Nadhani ifike wakati akili za watu fulani uende nazo kama zilivyo then mwisho wa siku mjinga anajurikana.

Mfano mimi Matola na wenzangu leo tukitaka kuanzisha chama cha siasa msajili atatukatalia? Na kama atakubali tutaweza vipi kukijenga chama chetu kipya bila kuwafata wananchi na kuwaeleza sera zetu?

Nadhani sasa ni muda muhafaka wa kupractice Umkotho we Sizwe.
 
Kwahiyo unatushauri tuwe kama Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo ili ajiskie always Right.

Huyo Mungu uliemuomba ambariki huyo mvunja katiba ungeanza kwa herufi ndogo jina lake isomeke 'mungu' na sio "Mungu"


Tena tuliosema atakua one term president tulikosea hata term moja hatamaliza kama tutashikilia msimamo wetu Septemba mosi na tunaweza kuigeuza ajenda ikawa ya kumng'oa ikulu.

He should be careful of what he wish for!

Dogo we andamana tu hiyo September 1 uone
 
Bado hawajawai kuonja moto wa jiwe

Watu wanao kuita dikteta ikiwa wewe siyo dikteta
Nibora uwape moto wa udikteta
Ili liwe findisho .

HAWA JK KAWALEA SANA

WALI MTUKANA SANA
WALI MZONGA SANA
WACHA WAKIONE.



"Nataka hao wanaotetea maandamano watangulie wao halafu wataona cha mtemakuni’"
 
Naisikitikia serikali kwa kujiingiza katika confrontation zisizo za lazima, kwa sababu katiba na sheria za nchi zinaruhusu mikutano ya kisiasa ya chama chochote chenye usajili nchini kufanya mikutano ktk mikoa yote ya nchi!. Hili liko wazi na wala siyo hisani ya mtu yoyote kuguarantee haki hii

Sheria haijasema walioshinda peke yake ndo wafanye mikutano katika majimbo yao.

Kwa jinsi ninavyoona, iwapo Watu wataandamana na ikatokea nguvu kutumika hadi kupoteza maisha ya wananchi, basi kuna hatari watu kupelekwa katika vyombo vya kimataifa kama the Hague kujibu mashtaka, kwa maana wananchi hao wanadai kilicho haki kwa mujibu wa sheria za vyama vya siasa kuhusu haki ya kufanya mikutano!

Mbona mlisema mnaenda ICC kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais wa Magufuli imefikia wapi?
 
Pasco bwana!
Sasa Chadema wakisikiliza Ushauri wako si kitakoma kuwa chama cha siasa, maana ground za kufanyia siasa zote zinapigwa libiti!
Ushauri wangu ni kwa Chadema kuachana na siasa za uanaharakati, the politics of confrontation, na badala yake wafanye real politics of development, Magufuli ni dikiteta mzalendo mwenye no sense ya busara zozote when it comes kwenye kumjaribu, Huyu ni mwenye nguvu akisema jambo fulani ni hapana na iwe hapana kweli hataki mchezo.

The right thing to do kwa Chadema ni kwenda mahakamani kuiomba mahakama kutoa tafsiri sahihi ya haki ya mikutano, freedom of lawful assembly, freedom of expression, na political activities hivyo kuonyesha tamko la rais ni batili na kinyume cha katiba na sheria lakini sio kumpinga rais kwa mikutano ya hadhara na matamko ya kutishana na kutunishiana misuli! .

Pasco
 
Dogo we andamana tu hiyo September 1 uone
Chadema wametangulia akili sana, ungejiuliza ni kwa nini mikutano imewekwa mwezi mmoja mbele?
Kuna mabingwa wa mikakati wanazijuwa akili zenu mtalipuka mapovu yote kabla hata tarehe waliotangaza Chadema haijafika Dunia nzima itakuwa inajuwa kwamba kuna tatizo Magogoni.

Mimi ningelikuwa Rais ningewaambia wapinzani anaetaka kuandamana hata kila siku ruksa tu na aandamane.
Hii ndio best medicine aliitumia Nyerere kwa Mrema, aliwaambia Polisi wamwache Mrema tena tu si kwa wanaosukuma gari lake bali wambembe kabisa.

Bado sielewi kama ccm mpaka leo kama wanakumbuka sawasawa misingi ya mwalimu ilikuwa ni ipi!
Ili kuweka kumbukumbu sawa, nchi hii mtu wa kwanza kushtakiwa kwa kosa la uchochezi ni Baba wa Taifa.
 
Haki ya kwenda chooni ni haki ya msingi, darasani mwanafunzi akimtaarifu mwalimu mwenye dhamana kuwa anahitaji kwenda chooni akamkatalia kwa ubabe kisha akajisaidia kwenye nguo naye akamuadhibu na kumuumiza lazima atachukuliwa hatua..
Mikutano ipo kisheria, kuizuia kwa mdomo kibabe haikubaliki. Yeye atume tuu hao askari wake waue watu halafu tuone kama atapona.
Nimegundua hao wanao msapoti hawampendi, wanataka aishie pabaya kama viongozi wengine Afrika walio ishia Uholanzi.
Anashindwa nini kubadili kwanza sheria wakati anao wabunge wengi wa kusema ndiyo na sheria ikabadilika?
Tanzania ni sehemu ya dunia na inaangalia tuu nini kitatokea watie timu hapa. Asituharibie nchi bwana

Asante kwa ufafanuzi wa kumsaidia huyo ndugu kuelewa
Yeye anafikiri Tanzania anayoingoza ni exceptional na iko ktk ulimwengu mwingine wa kwake!
He's wrong na wanaomshangalia kama majuha hawampendi asilani!!
Aaambiwe huyu asije akatuingiza ktk matatizo bureee
 
Kwahiyo unatushauri tuwe kama Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo ili ajiskie always Right.

Huyo Mungu uliemuomba ambariki huyo mvunja katiba ungeanza kwa herufi ndogo jina lake isomeke 'mungu' na sio "Mungu"


Tena tuliosema atakua one term president tulikosea hata term moja hatamaliza kama tutashikilia msimamo wetu Septemba mosi na tunaweza kuigeuza ajenda ikawa ya kumng'oa ikulu.

He should be careful of what he wish for!
Sawa Ben,
You should also be careful what you wish for.
Kuna wengi ambao walikwisha andamana na kukesha na mabango hadi rais akasepa.
Faida iliyopatikana baada ya hapo ni kidogo sana.
Na matatizo yalizalishwa baada ya hapo ni makubwa na mabaya mara 1000 zaidi ya yule rais walieyemuandamania.
 
Nilitegemea uwashauri pia wachukue hatua gani ili dikteta aache udikteta kama andiko langu yenye ushauri. Dikteta hatazamwi tu na kusema shauri yake bali anazuiwa na wasiopenda huo udikteta. Udikteta ukikomaa madhara yake ni makubwa mno anaweza akamwita hata kampeni manaja wake akamchinja. Wenye ujasiri lazima wapambane ili kumdhibiti akaleta madhara makubwa na yeye kuendelea kujifunza kufuata katiba aliyotumia Kuapa kuwa atalinda. Kwa wale tuliowahi kuangalia vita ya Vietnam wanasema FOR OTHERS TO SURVIVE OTHERS MUST DIE. Pasco tumia taaluma yako kutoa maandiko mengi ya viongozi wetu kufuata katiba na kutii sheria kama wazee wetu walivyoasisi. CCM walipa kura zaidi ya million nane, Wapinzani wana kura zaidi ya million sita. Kuna kura zaidi million tisa hazijapiga kura hivyo bado kazi ni kubwa kushindana na wapinzani.
 
Kwahiyo unatushauri tuwe kama Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo ili ajiskie always Right.

Huyo Mungu uliemuomba ambariki huyo mvunja katiba ungeanza kwa herufi ndogo jina lake isomeke 'mungu' na sio "Mungu"

Tena tuliosema atakua one term president tulikosea hata term moja hatamaliza kama tutashikilia msimamo wetu Septemba mosi na tunaweza kuigeuza ajenda ikawa ya kumng'oa ikulu.

He should be careful of what he wish for!
Mkuu Ben kiukweli mimi huwa nina wa admire watu mashujaa kama wewe wenye nia thabiti mioyoni mwao, kauli thabiti midomoni, mwao kama hizi kauli zako humu za one term lakini reality ni nyingine kabisa! .

Hili la one term hamalizi nililisikia kwa yule yule mhubiri ili tuu kuendelea kumdanganya 'jamaa yetu' kuwa ni yeye ndiye aliyeandikiwa, kiukweli hakuna kitu kama hicho na kwa kasi ya udikiteta ninavyoiona hata hiyo 2020 sijui kama tutahitaji uchaguzi wa rais na sisi wananchi tunaolitakia mema taifa hili tutaandamana nchi nzima ili kile kipengele cha ukomo wa two terms kiondolewe Magufuli aendelee tuu kama Nyerere mpaka achoke mwenyewe! .

Nimemuombea kwa Mungu na sio kwa mungu kwa sababu ni Mungu ndie aliyesema tumpe Kaisari yaliyo ya Kaisari na tumpe Mungu yaliyo ya Mungu.

Tembelea ule uzi wangu wa rais wa Tanzania ni yule tuu aliyepangwa na Mungu, maadam ni Magufuli, then ndiye aliyepangwa na Mungu, tuendelee kumuombea

Pasco
 
Ushauri wangu ni kwa Chadema kuachana na siasa za uanaharakati, the politics of confrontation, na badala yake wafanye real politics of development, Magufuli ni dikiteta mzalendo mwenye no sense ya busara zozote when it comes kwenye kumjaribu, Huyu ni mwenye nguvu akisema jambo fulani ni hapana na iwe hapana kweli hataki mchezo.

The right thing to do kwa Chadema ni kwenda mahakamani kuiomba mahakama kutoa tafsiri sahihi ya haki ya mikutano, freedom of lawful assembly, freedom of expression, na political activities hivyo kuonyesha tamko la rais ni batili na kinyume cha katiba na sheria lakini sio kumpinga rais kwa mikutano ya hadhara na matamko ya kutishana na kutunishiana misuli! .

Pasco


Mr Pasco, please hebu naomba nijuze kidogo, inawezekana mimi sielewi.

Hivi hizi "politics of development" ni zipi hizo na zinafanywaje mkubwa?

Na ukimaliza kueleza hebu dadavua na "politics of confrontation" ni zipi hizo na zinafanywaje eti?

Nimeona na kimsikia mkulu wetu mara nyingi naye akisema "watanzania wanataka siasa za maendeleo"... it is a little bit confuses me ninaposikia na kusoma vitu kama hivi!

It is either you and Mr president don't understand the meaning of politics in relationship with development or you purposely try to manipulate people with your own defenition of politics!

That's what I can comment about these fallaciuos statements from you guys!!

Namkumbuka sana Dr Wilbroad Peter Slaa katibu mkuu wa CHADEMA aliyepita aliyeongoza harakati kabambe wakati wa Kikwete hata kuiweka CHADEMA ktk chati ya juu na pengine kuifanya serikali iamke na kufanya kazi ya ziada ktk kutekeleza ahadi zake za kuwahudumia wananchi kwa kutekeleza miradi mingi ya maendeleo japo kasoro za hapa na pale haziwezi kukosekana.

Tell me. CHADEMA ya wakati wa Dr Slaa ilikuwa inafanya siasa za namna gani kati ya hizo ulizozitaja.....development or confrontation politics.........or both?
 
Kwahiyo unatushauri tuwe kama Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo ili ajiskie always Right.

Huyo Mungu uliemuomba ambariki huyo mvunja katiba ungeanza kwa herufi ndogo jina lake isomeke 'mungu' na sio "Mungu"


Tena tuliosema atakua one term president tulikosea hata term moja hatamaliza kama tutashikilia msimamo wetu Septemba mosi na tunaweza kuigeuza ajenda ikawa ya kumng'oa ikulu.

He should be careful of what he wish for!
Mkuu mahakama kibogoyo ndio hizi zilizo wapa ushindi wabunge wa chadema kwenye case zao za uchaguzi. Hakika umenichekesha....
 
ushauri hewa kwa cdm huu. chadema wakumbuke haki haiombwi bali hudaiwa....
Naunga mkono kwa asilimia 100 % chini ya 100% haki haiombwI au kuletewa kwenye kisahani cha chai bali haki hudaiwa, kupiganiwa na ikibidi hata kufia lakini sio kwa mikutano ya hadhara matamko na maandamano, mwenye nchi tuliyempa dhamana hataki hivyo msilazimishe, tumieni sheria, taratibu na kanuni rasmi za kudai haki ikiwemo kumshitaki rais lakini mshishindane na
mwenye nguvu mtaumia bure na hiyo haki inayopiganiwa isipatikane! .

Nawashauri waandishi wa Arusha wakazitembelee zile familia za wahanga wa yale maandamano ya Arusha kuona jinsi mashujaa wale wanavyoenziwa ndipo wajitokeze hiyo September 1. Mtu ukiishakijua kitakachokupata ukifanya jambo fulani na wewe ukafanya na hicho cha kukupata kikakupata, sisi tunasema umejitakia kwa vile ulijua.

Pasco
 
Hizo sababu ulizozisema ndio chadema isimame badala ya wananchi wakatae kabisa na wananchi tuwaunge mkono marufuku mtu mmoja kutumia vyombo vya dola kuvuruga amani ya nchi lazima asimamishwe sasa na sio wakakti mwingine wowote
 
Back
Top Bottom