Ushauri kwa Rais: Shusha mishahara ya wanasiasa na ondoa posho zao peleka kwenye mafuta uikwepe laana ya Magufuli

Ushauri kwa Rais: Shusha mishahara ya wanasiasa na ondoa posho zao peleka kwenye mafuta uikwepe laana ya Magufuli

Punguza mishahara ya wanasiasa wapate angalau robo ya wanachopata Sasa hivi,ondoa posho zote !mikopo yote ya wanasiasa na walipe kodi rasmi ya huo mshahara maana siasa ndio kichaka cha fedha nyingi NCHI HII!!

Pia serikali iache kununua magari ya kifahari, samani za ofisini za kifahari, ziara za kwenda Dodoma makao makuu zisitishwe watumie zoom, email na mitandao, nyumba za serikali za wakubwa viuzwe, watendaji wa serikali kuu na za tawala za mikoa wajipangie nyumba wenyewe kwa kulipa kodi au kukopa mikopo ya muda mrefu NHC mortgages n.k

Listi ni ndefu sana ya jinsi ambavyo serikali inaweza kupunguza matumizi na hii siyo kubana bali kuondokana na matumizi haya ya anasa. Ukienda ofisi ya serikali Denmark, Ufaransa, Ubelgiji utaona ofisi zina samani / fenicha zisizo ghali wala za kifahari na hawa ndiyo wanaotupa misaada au kuitwa wawe wadau wa maendeleo Tanzania lakini hawa wadau wana nidhamu kubwa ya matumizi ya kodi kwa kutojinunulia fanicha za ofisi, magari n.k ya kifahari.
 
Ungemshauri vizuri ila umeharibu kwa kuweka laana ya Magufuli

Kipindi cha Magufuli hiyo mishahara ya wanasiasa ilikuwa hivyo hivyo tu, tena yeye alienda mbali zaidi na kuwajengea mahekalu wastaafu
 
Aisee.....umemsaidia sana kwa huu ushauri.

Hapa hana wa kumlaumu, asipoufuata huu ushauri basi, atakuwa ameamua mwenyewe...

Mungu ni Mwema sana...amepata bahati yakuelezwa kweli na mtoa Post...

Kazi ni kwake ama kazi iendelee, achague kweli aepuke laana..

Machozi ya Wafanyakazi ni dalili mbaya...

Nchi itaangamia kwa Viongozi kukosa MAARIFA na Maono....sijui kwa nini hakuchagua Waziri Mkuu..
Ushauri wa hovyo huu.
Kwa nini hamkumshauri Magufuli kuchunguza kupigwa risasi Tundu Lisu?

Tuacheni na Amani yetu Warundi nyie.
Eti Polepole arudishwe kwenye nafasi yake!!!
Mnataka aje aendeleze biashara ya kununua watu?
 
Ushauri wa hovyo huu.
Kwa nini hamkumshauri Magufuli kuchunguza kupigwa risasi Tundu Lisu?

Tuacheni na Amani yetu Warundi nyie.
Eti Polepole arudishwe kwenye nafasi yake!!!
Mnataka aje aendeleze biashara ya kununua watu?
Kwa akili hizi TZ itaendelea kuwa chakula cha mabeberu hata zaidi ya millennium.

Unadhani hizo risasi ni Tundu Lisu pekee ndiye kawahi kupigwa nazo TZ yote na hakuna wengine waliotandikwa kama yeye au zaidi yake?

Au huwa mnajizima data kwa sababu ya uchawa tu huo hadi mshindwe kuficha upumbavu wenu mbele zetu sisi wa-TZ wazalendo?
 
Kwa akili hizi TZ itaendelea kuwa chakula cha mabeberu hata zaidi ya millennium.

Unadhani hizo risasi ni Tundu Lisu pekee ndiye kawahi kupigwa nazo TZ yote na hakuna wengine waliotandikwa kama yeye au zaidi yake?

Au huwa mnajizima data kwa sababu ya uchawa tu huo hadi mshindwe kuficha upumbavu wenu mbele zetu sisi wa-TZ wazalendo?
Hebu mtaje na mwingine aliyewahi kupigwa risari zaidi ya 30 Mchana kweupe ktk eneo lenye ulinzi wa Serikali
 
Oya

Mi naweza na hawatonifanya kitu!!!

Mbona KWA JPM waliufyata wote wakaimba mapambio!!?

Na Mimi wataniimbia tena watasema naupiga Mwingi kama pele na huku nimeshusha mishahara yao!!
Ukishakaa pale juu hakuna awezaye kukutisha labda nawe uwe ni muoga wa kurogwa tu !!
 
Pia serikali iache kununua magari ya kifahari, samani za ofisini za kifahari, ziara za kwenda Dodoma makao makuu zisitishwe watumie zoom, email na mitandao, nyumba za serikali za wakubwa viuzwe, watendaji wa serikali kuu na za tawala za mikoa wajipangie nyumba wenyewe kwa kulipa kodi au kukopa mikopo ya muda mrefu NHC mortgages n.k

Listi ni ndefu sana ya jinsi ambavyo serikali inaweza kupunguza matumizi na hii siyo kubana bali kuondokana na matumizi haya ya anasa. Ukienda ofisi ya serikali Denmark, Ufaransa, Ubelgiji utaona ofisi zina samani / fenicha zisizo ghali wala za kifahari na hawa ndiyo wanaotupa misaada au kuitwa wawe wadau wa maendeleo Tanzania lakini hawa wadau wana nidhamu kubwa ya matumizi ya kodi kwa kutojinunulia fanicha za ofisi, magari n.k ya kifahari.
UMENENA !!! Hata mimi huwa najiuliza Hao wakubwa wanapokwenda huko duniani kwa waliotuzidi kila kitu je huwa wanajifunza nini kutoka kwao ??! Wenzetu hawana mchezo kwenye nidhamu ya matumizi ya pesa za Nchi !! Sisi huwa tunajifunza nini kutoka kwao ??!! Suti na Tai ??!! Au !!
 
wanaweza kupiga Kura ya kutokuwa na Imani na raisi na akang'oka kesho asubuhi......
Kwa KATIBA yetu, kabla hujapiga hiyo kura, ni raisi shauri lenyewe lifike kwa raisi! Yeye sasa ataamua, ama muendelee na mchakato au yeye avunje bunge!

Unadhani ataamua nini?
 
Pesa yooote inaishi kwa wanasiasa walio wachache kuliko wasio kwenye nafasi hizo. Hapo ubungeni kwa mwezi wanalamba pesa ambayo ingetengeneza mazingira mazuri kwenye hospitali na shulen.
Rais atakayeimbwa kama Hayati J.K.N na kulitoa taifa makuchani kwa wanasiasa, ni yule atakayeweka mifumo ya kinchi kuisimamia nchi na sio kukikutumikia kijani,.
 
Back
Top Bottom