Ushauri kwa Wakili Mwambukusi na wote Wapinga Mkataba wa Bandari. "Maliza moja kabla ya kuanza jingine"

Ushauri kwa Wakili Mwambukusi na wote Wapinga Mkataba wa Bandari. "Maliza moja kabla ya kuanza jingine"

busar

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2011
Posts
1,071
Reaction score
1,067
Asalam,

Nilifuatilia sana suala la kesi iliyofunguliwa na hawa mawakili. Nikafuatilia hukumu na baada ya hukumu nikajipa muda kufuatilia mitazamo, uelewa, na mipango ya wafungua kesi. Huu ndio ushauri wangu.

1. Zamani sio kama sasa, hasa kwa taifa lililopevuka kama Tanzania, TUHESHIMU TAASISI NA MFIFUMO YAKE.
... mara baada ya ile hukumu mawakili waliosimamia kesi walitoa matamko mawili, la kwanza kama mawakili na la pili ( kwa maelezo ya Wakili Mwambukusi) kama watanganyika. La kwanza lilikuwa sawa, la pili linahitaji washauriwe namna ya kwenda nalo, kinyume chake watakufa kabla ya kutimiza malengo yao.

Wachina wana hekima hii "maliza jambo moja kwanza kabla ya kuanza jingine" na mimi walau ningepata nafasi ningewashauri Wakili Mwambukusi na wengine wamalize kwanza suala la Rufaa ya Kesi waliyofungua kabla ya kutangaza mikakati mingine ya mbeleni au jambo jipya. Hii kanuni sio tu kwa masuala mapana kama haya lkn hata katika maisha binafsi.

Mara baada ya kumsikiliza wakili Mwambukusi nilipata mashaka sana juu ya uelewa wake wa siasa za Tz na akili yangu ikapata hofu kutaka kuamini maneno ya wapinzani wake kuwa muda mwingi huwa kapiga vyombo na jani.

Tanzania inaongozwa na Taasisi. Taasisi ni nzuri zikiwa na watu wema. Ni mbaya zikiwa na watu wabaya. Hii ni bila kujali wanafuata sheria au lah. Kuna suala la kufuata sheria lkn kuna suala la tunu ( virtue). Kwa Tanzania siasa vimepewa vyama na sio mtu binafsi. Walioweka hilo wanajua. Mwambukusi lazima aingie kwenye Chama flan. Hapa napo mtaona tatizo.

2. Heshma kwa viongozi. Pamoja na mengine sana yenye Changamoto, yako yanayopaswa kulindwa. Kuna tofauti ya kukosoa kazi za Bunge na kumkosoa utu wake mbunge mmoja mmoja au Spika. Hapa waliyumba na haipaswi. Inatakiwa kujenga hoja juu ya hoja na sio hoja juu ya mtu labda kama jambo binafsi la mtu linaingilia kimaslahi na jambo husika. Huwezi kuamka asbh ukasema mkuu wangu wa eneo la kazi hana akili, huku ni kutojipa kazi za kutosha. Chambua mwenye akili au asie na akili alifikaje hapo.

3. Wasitafute umaarufu binafsi. Umaarufu binafsi katafute kwa kufanya biashara. Taasisi zina nguvu kuliko mtu mmoja mmoja kwenye Siasa. Chama cha siasa kina watu, kinaweza kuamua kuandamana au lah.

4. Wapime uelewa wa wanaowatetea. Hakuna maana kufa kwajili ya mtu mjinga ambae hajui unamfia kwa lipi. Wakili mwambukusi na wengine wake wapime wanampigania nani, na huyo nani anaelewa ni kwa kiasi gani wana pambana. Inawezekana wanapigania jambo ambalo hata halina maana.

5. Wao na hawa wengine CHADEMA watambue kuwa CCM HAITOTOKA MADARAKANI SASA. Haliwezi kutokea hilo kwa Tanzania. Chadema wanajua, act wanajua, na kila mmoja anajua. La kufanya ni kujaribu kutafuta namna ya Amani ya kuishauri CCM KUFANYA MAMBO VEMA.

6. Tuendelee khiombea amani, utulivu na Umoja nchi yetu
 
Asalam,

Nilifuatilia sana suala la kesi iliyofunguliwa na hawa mawakili. Nikafuatilia hukumu na baada ya hukumu nikajipa muda kufuatilia mitazamo, uelewa, na mipango ya wafungua kesi. Huu ndio ushauri wangu.



6. Tuendelee khiombea amani, utulivu na Umoja nchi yetu
Wewe unalileta shauri lako hapo wakati mmewachongea wamekamatwa na kubambikiwa kosa la UHAINI? Are you a serious guy or you are somehow mentally retarded?
Stop mingling issues in your favor, it won't add up to your expectations.
 
Asalam,

Nilifuatilia sana suala la kesi iliyofunguliwa na hawa mawakili. Nikafuatilia hukumu na baada ya hukumu nikajipa muda kufuatilia mitazamo, uelewa, na mipango ya wafungua kesi. Huu ndio ushauri wangu.

1. Zamani sio kama sasa, hasa kwa taifa lililopevuka kama Tanzania, TUHESHIMU TAASISI NA MFIFUMO YAKE.
...
Mtoa mada tambua kabisa wewe ni mjinga tu
 
Kila mchumajanga hula na wa kwao. Wale wakwepa kodi wa bandari waliowalipa kina Mwambukusi, sasa hivi wapo karibu na radio au tv mkononi wana chai ya maziwa na mikate ya siagi, wakifuatilia tu kinachojiri huko polisi.

Ni familia za kina Mwambukusi tu ndo zitahangaika na ndugu zao.
 
Ulikuwepo nao wakipanga namna na jinsi ya kuandamana?

Wewe ndie mjinga, unaeiombea amani pamoja na wapuuzi wanaoivuruga makusudi.

Shut up.
Mimi ninajaribu tu kuangalia namna bora kufanya hizi mambo.
 
Asalam,

Nilifuatilia sana suala la kesi iliyofunguliwa na hawa mawakili. Nikafuatilia hukumu na baada ya hukumu nikajipa muda kufuatilia mitazamo, uelewa, na mipango ya wafungua kesi. Huu ndio ushauri wangu.

1. Zamani sio kama sasa, hasa kwa taifa lililopevuka kama Tanzania, TUHESHIMU TAASISI NA MFIFUMO YAKE.
... mara baada ya ile hukumu mawakili waliosimamia kesi walitoa matamko mawili, la kwanza kama mawakili na la pili ( kwa maelezo ya Wakili Mwambukusi) kama watanganyika. La kwanza lilikuwa sawa, la pili linahitaji washauriwe namna ya kwenda nalo, kinyume chake watakufa kabla ya kutimiza malengo yao.

Wachina wana hekima hii "maliza jambo moja kwanza kabla ya kuanza jingine" na mimi walau ningepata nafasi ningewashauri Wakili Mwambukusi na wengine wamalize kwanza suala la Rufaa ya Kesi waliyofungua kabla ya kutangaza mikakati mingine ya mbeleni au jambo jipya. Hii kanuni sio tu kwa masuala mapana kama haya lkn hata katika maisha binafsi.

Mara baada ya kumsikiliza wakili Mwambukusi nilipata mashaka sana juu ya uelewa wake wa siasa za Tz na akili yangu ikapata hofu kutaka kuamini maneno ya wapinzani wake kuwa muda mwingi huwa kapiga vyombo na jani.

Tanzania inaongozwa na Taasisi. Taasisi ni nzuri zikiwa na watu wema. Ni mbaya zikiwa na watu wabaya. Hii ni bila kujali wanafuata sheria au lah. Kuna suala la kufuata sheria lkn kuna suala la tunu ( virtue). Kwa Tanzania siasa vimepewa vyama na sio mtu binafsi. Walioweka hilo wanajua. Mwambukusi lazima aingie kwenye Chama flan. Hapa napo mtaona tatizo.

2. Heshma kwa viongozi. Pamoja na mengine sana yenye Changamoto, yako yanayopaswa kulindwa. Kuna tofauti ya kukosoa kazi za Bunge na kumkosoa utu wake mbunge mmoja mmoja au Spika. Hapa waliyumba na haipaswi. Inatakiwa kujenga hoja juu ya hoja na sio hoja juu ya mtu labda kama jambo binafsi la mtu linaingilia kimaslahi na jambo husika. Huwezi kuamka asbh ukasema mkuu wangu wa eneo la kazi hana akili, huku ni kutojipa kazi za kutosha. Chambua mwenye akili au asie na akili alifikaje hapo.

3. Wasitafute umaarufu binafsi. Umaarufu binafsi katafute kwa kufanya biashara. Taasisi zina nguvu kuliko mtu mmoja mmoja kwenye Siasa. Chama cha siasa kina watu, kinaweza kuamua kuandamana au lah.

4. Wapime uelewa wa wanaowatetea. Hakuna maana kufa kwajili ya mtu mjinga ambae hajui unamfia kwa lipi. Wakili mwambukusi na wengine wake wapime wanampigania nani, na huyo nani anaelewa ni kwa kiasi gani wana pambana. Inawezekana wanapigania jambo ambalo hata halina maana.

5. Wao na hawa wengine CHADEMA watambue kuwa CCM HAITOTOKA MADARAKANI SASA. Haliwezi kutokea hilo kwa Tanzania. Chadema wanajua, act wanajua, na kila mmoja anajua. La kufanya ni kujaribu kutafuta namna ya Amani ya kuishauri CCM KUFANYA MAMBO VEMA.

6. Tuendelee khiombea amani, utulivu na Umoja nchi yetu
Kijana unapenda ukuu wa wilaya wap
 
5. Wao na hawa wengine CHADEMA watambue kuwa CCM HAITOTOKA MADARAKANI SASA. Haliwezi kutokea hilo kwa Tanzania. Chadema wanajua, act wanajua, na kila mmoja anajua. La kufanya ni kujaribu kutafuta namna ya Amani ya kuishauri CCM KUFANYA MAMBO VEMA.
Ulianza vizuri kama mtu muungwana na makini mwenye ushauri wenye nia njema kwa mwanaharakati & Mwanasheria Boniface Mwabukusi na wenzake..

Lakini ulipofika hapa kwenye kipengere hiki cha tano tu, ukajionesha wazi kuwa wewe ni nani na lengo la ushauri wako huu ni nini..

Mimi nakuambia hivi, hizi ndizo dakika za mwisho mwisho za serikali ya CCM kutawala. Na usidhani kuwa watu kama kina Mwabukusi wameibuka kwa bahati mbaya na kama vichaa fulani tu. Unajidanganya sana..!!

Watu kama hawa ni mpango halisi wa Mungu kuikoa Tanganyika toka ktk madhabahu ya ushetani na uovu iliyojengwa na kuhudumiwa na CCM kwa zaidi ya miaka 60 sasa na kabla ya hapo TANU & ASP. They are here on purpose. Ukiona wamekufa, ujue kusudi lao limetimia..!

Kama Yesu Kristo alivyokuja duniani kutimiza kusudi la kumkomboa mwanadamu na ku - make headlines nyakati hizo, vivyo hivyo na mwanadamu Mwabukusi na wenzake wa nyakati hizi...

Yesu Kristo aliishi miaka 33½ tu na akatumikia kusudi, alipomaliza kazi, ndiposa kifo kiliporuhusiwa kuuchukua uhai wake na baada ya siku tatu akautwaa tena na kuharibu kabisa nguvu ya mauti..

Boniface Mwabukusi hawatakufa kabla ya kutimiza kusudi walilotumwa kulitumikia, kuongoza ukombozi wa Tanganyika...

Kwa hiyo, lugha na staili anayotumia Mwabukusi, ndiyo lugha inayoeleweka kwa waovu. Ni lugha kali (isiyo na matusi yoyote) lakini Iiyobeba ujumbe mkali unaopenya hadi kwenye mtima nyongo zao kiasi cha kuwapanikisha na wakati mwingine kujikuta wanachukua maamuzi ya kijinga na kipumbavu kama ilivyofanyika juzi kwenye eti uhaini wa kina Mwabukusi huku wakiwaacha wahaini halisi Rais Samia Suluhu Hassan na wenzake huko serikalini..

Harakati hizi ni kwa kutumia lugha zote (kisheria huko mahakamani) na lugha ya siasa kwenye majukwaa ya kiasisa kama waitumiayo sasa kina Mwabukusi, Tundu Lissu na wenzake. Yote yanakwenda pamoja.

Hii kanuni ya chukua moja ulimalize kwanza kabla ya kulianza jingine si kanuni ya kutumika kwenye kila mazingira na Kila nyakati kama vile unamenya embe kwa kisu. Yapo mazingira ya kufanya yote kwa wakati mmoja..

Ndiyo maana kina Tundu Lissu, Freeman Mbowe na CHADEMA wanaendesha mapambano ya kuikomboa nchi kwenye majukwaa ya kisiasa, lakini kina Mwabukusi na wenzake wako ktk viunga vya mahakama wakicheza na lugha ya sheria na wakati huohuo wapo watu kama kina Mch Mbarikiwa Mwakipesile na wengine wengi wakiendesha mapambano ya ukombozi wa nchi hii kwa njia ya maombi kuipiga CCM na serikali yake...

Wewe hujiulizi ni kwanini miaka mingine yote, maombi hufanyika kuiombea serikali na watawala lakini safari maombi yanafanyika kuomba utawala wa CCM na serikali yake uanguke? Hujaona haya??

Kama unafikiri kuwa, safari hii ni sawa na nyakati zile utakuwa umekosea sana. This time CCM must go down to hell...
6. Tuendelee khiombea amani, utulivu na Umoja nchi yetu
Maombi pekee bila haki hayawezi kuleta amani wala utulivu. Hii ni misemo yenye upungufu mkubwa, isiyobeba ukweli halisi na iliyopitwa wakati. Imeandikwa mahali kuwa HAKI (sio maombi) HUINUA TAIFA, lakini DHAMBI (rushwa, mauaji, uonevu wa polisi, kubambika kesi, kuvunja sheria na katiba nk nk) ni fedheha kwa kila mtu na taifa hilo..

Kwa heri..
 
Ulianza vizuri kama mtu muungwana na makini mwenye ushauri wenye nia njema kwa mwanaharakati & Mwanasheria Boniface Mwabukusi na wenzake..

Lakini ulipofika hapa kwenye kipengere hiki cha tano tu, ukajionesha wazi kuwa wewe ni nani na lengo la ushauri wako huu ni nini..
ilo..

Kwa heri..
Dah
Sawa. Lakin CCM haitaachia madaraka kwa walau miaka 50 ijayo. Kuna ukweli wa kulazimika kuishi nao. Huu ni mmojawapo
 
Back
Top Bottom