Ushauri kwa Walevi : Pombe mbaya jamaa jana nimetukanwa sana na Mlevi

Ushauri kwa Walevi : Pombe mbaya jamaa jana nimetukanwa sana na Mlevi

Walevi hawa hawa ambao hawapoteagi njia ya kufika nyumbani kwao au?
Siku moja niliwahi potea asee.
Na huu ni ushauri kwa walevi wote wanaoishi Duniani.

Walevi naongea na walevi wote dunia nzima wale wastaarabu nawaweka pembe ila walevi ambao sio wastaarabu huu uzi unawahusu, mkishalewa tafadharini sana ndugu zangu walevi nendeni mkalale acheni matusi na kuongea lugha chafu na kumtukana mtu wakati huo pombe ishakolea kichwani, kuna watu tuna roho ndogo sana tunaweza tukapita na pumzi yako.

Wewe huwezi ukalewa huko kisha baada ya kulewa unakuja kuniongelea mbovu. Sawa umekunywa pesa zako sasa angalia pesa zako zisije zikakuua kwa ujinga wako. Maana zikikolewa unasema nmekunywa kwa pesa zangu utaniambia nini wewe nini. Ndugu mlevi chunga maneno yako.

Ukishajiona wewe mlevi mbwa huna ustaarabu umelewa basi piga tungi kadhaa ambazo hazikufikishi kile kiwango cha kuongea mbovu jikusanye taratibu nenda ukalale, mlevi ukilewa nenda kalale acha matusi walevi muache kuwatukana watu.

Mbaya zaidi ukiamka asubuhi unajifanya yaan km sio wewe ambae jana ulikunywa mipombe ukaanza kuongea mbovu ukaaanza kutukana mitusi kabisa yaan unajikausha km hukumbuki ulichofanya jana wakati jana umetukana matusi machafu machafu sababu ya mitungi iliyokuzidia, walevi mkishalewa nendeni mkalale.

Nasisitiza, naongea na walevi popote mlipo mkishalewa nawaomba ndugu zangu nendeni mkalale matusi matusi yenu kutukana watu mkishalewa mtajikuta sehemu mbaya mkiwa mmeshauacha mwili, kuna watu hua hawachekelei kusemwa maneno machafu hata km umelewa.

Huu ni ushauri wangu kwako wewe mlevi ambae ukishapiga mitungi pombe inakutuma kutafuta ugomvi na watu na kuanza kuwatukana watu na kuwasema vibaya, nakuhimiza ukishalewa mlevi nenda kalale kwa usalama wako usitafute ugomvi na kuanza kutukana watu matusi.

Kuna watu ukiwaambia maneno maneno yako machafu ukiwa umelewa wana mioyo midogo sana watakutanguliza mbele za haki ukapewe haki yako huko unayostahiri km utakuta kuna mitungi na huko sawa ila umeshafika ulipokua unapataka.

Wafikishieni na walevi wengine wasio na ustaarabu wanao ongea ovyo kutukana watu na kuwasemea maneno machafu baada ya kulewa.

Natanguliza samahani zangu za dhati kwa walevi wote wenye busara ambao wakishalewa wanaenda zao kulala hawana kero wala makelele na watu.

Pongezi nyingi kwenu walevi wote wenye hio tabia ya kulewa na kwenda kulala bila kusumbuana au kusemezana vibaya na watu wengine. Ukiwa wewe ni mlevi ukishalewa unaenda kulala hupigizani kelele na watu wengine chukua pongezi.

Walevi mnaolewa kisha mnaanza kushusha mvua ya matusi kwa watu wengine mjitafakari kifo kipo mlangoni mwenu mtauawa.

Ndio maana polisi wakasema ukijiona umelewa piga simu polisi waje wakuchukue kwa usalama wako sio kwa ubaya, ingawa watu walitafsiri vibaya.
SASA MKUU SEHEMU YA WALEVI UNAENDA KUFANYAJE? muda mwingine kutafuta watu ubaya tu
 
mkuu nina ujuzi mkubwa wa kunoa mapanga,...nipe tenda,..🤒🤒🙄🤔
 
Hiyo ndio tofauti ya mnywaji na mlevi
hakuna cha tofauti inategemea na kichwa cha mtu kuna mtu pombe haimpendi analazimisha hao ndo wanaozingua kuna mtu pombe inampenda hao hawazingui hata akeshe anakunywa hana madhara kwa jamii.
 
Mlevi akikutukana we mpanguse makofi hatorudia tena
leo nimekuta mahali mlevi anakula kelebu za kutosha...

kisa kalewa kisha namfuata mjumbe na kuanza kutukana eti mjumbe achane na familia yake(anahisi anamegewa) ikumbukwe jamaa ni wa chadema jamaa alinyanyuka na kumpiga kelebu za kutosha kumbe bana jama akishalewa ana ropoka kwa mtu yoyote eti anatembea na mke wake
 
leo nimekuta mahali mlevi anakula kelebu za kutosha...

kisa kalewa kisha namfuata mjumbe na kuanza kutukana eti mjumbe achane na familia yake(anahisi anamegewa) ikumbukwe jamaa ni wa chadema jamaa alinyanyuka na kumpiga kelebu za kutosha kumbe bana jama akishalewa ana ropoka kwa mtu yoyote eti anatembea na mke wake
Mjumbe anatembea na mke wake mlevi akishalewa hachagui wa kumtukana
 
Back
Top Bottom