Ushauri kwa wizara ya elimu ifute adhabu ya viboko kuwanusuru walimu na wanafunzi

Ushauri kwa wizara ya elimu ifute adhabu ya viboko kuwanusuru walimu na wanafunzi

Kiranja wa jamii

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2023
Posts
441
Reaction score
1,065
Nimekuwa nikiitafakari sana hii adhabu ya viboko mashuleni kila ninapoona taarifa ya mwanafunzi kuumizwa na mwalimu kichukuliwa hatua kwa kumuumiza mwanafunzi

Ni wazi kwamba kuna wagonjwa wengi wanakufa hospitali kwa uzembe wa madaktari, kuna abiri wengi wanakufa kwa ajiri kwa uzembe wa madereva, kuna vibaka wengi wanafanya uharifu mtaani kwa uzembe wa polisi na kuna watu wengi wamefungwa gerezani bila makosa kwa uzembe wa wapelelezi na wanasheria.

Hata hivyo kelele za malalamiko ya jamii juu ya hizo kada nyingine si sawa na kelele za jamii pale mwalimu anapomuumiza mwanafunzi kwa adhabu ya viboko. Jamii itaongea, itatukana, itatoa dhihaka na viongozi watachukua hatua

Ifahamike kwamba siandiki haya kwa kujaribu kutetea wala kuunga au kuwatetea walimu wanaotoa adhabu ya viboko kupitiliza na kinyume na utaratibu. Binafsi naamini adhabu ya viboko haifai na imepitwa na wakati mashuleni.

Ukisoma sheria ya utoaji adhabu ya viboko shuleni na muongozo wake utaungana na mimi kuwa hii adhabu imepitwa na wakati na haifai kuendelea kutolewa mashuleni kwasababu ni ya mtego kwa walimu na endapo wazazi na wanafunzi wangekuwa makini na sheria hii walimu wengi wangekuwa gerezani

Kwa mfano; mwongozo unataka kwa kosa kubwa mwanafunzi aadhibiwe fimbo nne tu tena anayetakiwa kuadhibu ni Mkuu wa shule.

Hapa kwenye fimbo nne kwa kosa kubwa! Ikumbukwe wanafunzi wengi wanaadhibiwa kwa makosa ya uchelewaji, utoro, kupiga kelele, kutoandika nukuu. Haya yote sio makosa makubwa yanayostahili adhabu ya fimbo. Hapa mwanafunzi anatakiwa kuonywa na kushauriwa tu.

Kuna baadhi ya wanafunzi ni jeuri, wana lugha za matusi, wanavuta bangi, na ukorofi mwingine wa ujana kiasi wanawapandisha hasira walimu kwa makusudi. Unategemea mwanafunzi anayempandishia mwalimu, anayeweza kumtukana au kumvimbia mwalimu asichapwe fimbo zaidi ya nne na achapwe na mkuu wa shule tu au ili mwalimu mwingine amchape fimbo apewe kibali cha maandishi kufanya hivyo.

Hapa unajiuliza, ni walimu wangapi wanauvumilivu huo? Watavumilia kwa muda gani?

Kwa hiyo hapa utagundua kuwa ni kama hii adhabu ilishafutwa ila haijatolewa tamko tu.

Ushauri wangu ni kuwa wizara ifute kabisa adhabu ya viboko ili walimu wawe salama na wanafunzi watakaovunja sheria za shule watafutiwe utaratibu mwingine

Binafsi naamini tukijenga utamaduni wa kutochapa fimbo shuleni wanafunzi watazoea, walimu watazoea na wazazi watazoea na kizuri zaidi wanafunzi wakorofi adhabu yao ikiwa ya kufukuzwa shule na kutafutiwa utaratibu mwingine itawajenga kujiepusha na makosa ya mara kwa mara kuliko hizi fimbo wanazochapwa mara kwa mara
 
Nimekuwa nikiitafakari sana hii adhabu ya viboko mashuleni kila ninapoona taarifa ya mwanafunzi kuumizwa na mwalimu kichukuliwa hatua kwa kumuumiza mwanafunzi

Ni wazi kwamba kuna wagonjwa wengi wanakufa hospitali kwa uzembe wa madaktari, kuna abiri wengi wanakufa kwa ajiri kwa uzembe wa madereva, kuna vibaka wengi wanafanya uharifu mtaani kwa uzembe wa polisi na kuna watu wengi wamefungwa gerezani bila makosa kwa uzembe wa wapelelezi na wanasheria.

Hata hivyo kelele za malalamiko ya jamii juu ya hizo kada nyingine si sawa na kelele za jamii pale mwalimu anapomuumiza mwanafunzi kwa adhabu ya viboko. Jamii itaongea, itatukana, itatoa dhihaka na viongozi watachukua hatua

Ifahamike kwamba siandiki haya kwa kujaribu kutetea wala kuunga au kuwatetea walimu wanaotoa adhabu ya viboko kupitiliza na kinyume na utaratibu. Binafsi naamini adhabu ya viboko haifai na imepitwa na wakati mashuleni.

Ukisoma sheria ya utoaji adhabu ya viboko shuleni na muongozo wake utaungana na mimi kuwa hii adhabu imepitwa na wakati na haifai kuendelea kutolewa mashuleni kwasababu ni ya mtego kwa walimu na endapo wazazi na wanafunzi wangekuwa makini na sheria hii walimu wengi wangekuwa gerezani

Kwa mfano; mwongozo unataka kwa kosa kubwa mwanafunzi aadhibiwe fimbo nne tu tena anayetakiwa kuadhibu ni Mkuu wa shule.

Hapa kwenye fimbo nne kwa kosa kubwa! Ikumbukwe wanafunzi wengi wanaadhibiwa kwa makosa ya uchelewaji, utoro, kupiga kelele, kutoandika nukuu. Haya yote sio makosa makubwa yanayostahili adhabu ya fimbo. Hapa mwanafunzi anatakiwa kuonywa na kushauriwa tu.

Kuna baadhi ya wanafunzi ni jeuri, wana lugha za matusi, wanavuta bangi, na ukorofi mwingine wa ujana kiasi wanawapandisha hasira walimu kwa makusudi. Unategemea mwanafunzi anayempandishia mwalimu, anayeweza kumtukana au kumvimbia mwalimu asichapwe fimbo zaidi ya nne na achapwe na mkuu wa shule tu au ili mwalimu mwingine amchape fimbo apewe kibali cha maandishi kufanya hivyo.

Hapa unajiuliza, ni walimu wangapi wanauvumilivu huo? Watavumilia kwa muda gani?

Kwa hiyo hapa utagundua kuwa ni kama hii adhabu ilishafutwa ila haijatolewa tamko tu.

Ushauri wangu ni kuwa wizara ifute kabisa adhabu ya viboko ili walimu wawe salama na wanafunzi watakaovunja sheria za shule watafutiwe utaratibu mwingine

Binafsi naamini tukijenga utamaduni wa kutochapa fimbo shuleni wanafunzi watazoea, walimu watazoea na wazazi watazoea na kizuri zaidi wanafunzi wakorofi adhabu yao ikiwa ya kufukuzwa shule na kutafutiwa utaratibu mwingine itawajenga kujiepusha na makosa ya mara kwa mara kuliko hizi fimbo wanazochapwa mara kwa mara

Mbadala wake ?
Je, watoto wa shule badala ya kupewa adhabu ya kuchapwa viboko waanze kupewa adhabu ya Kutozwa Faini?
 
Ukiwa na akili timamu mtoto wa miaka 5 na miaka 18 huwezi kuwapa adhabu sawa.

Hao walimu sometimes hasira zao wanahamishia kwa watoto.

Kuna ticha wetu hayo mambo ya kupiga mtu hovyo mara makofi sijui fimbo za mgongo, zilifanya achezee kichapo toka mwanafunzi mbabe huku wanafunzi wengine wakishangilia.
 
Ukiwa na akili timamu mtoto wa miaka 5 na miaka 18 huwezi kuwapa adhabu sawa.

Hao walimu sometimes hasira zao wanahamishia kwa watoto.

Kuna ticha wetu hayo mambo ya kupiga mtu hovyo mara makofi sijui fimbo za mgongo, zilifanya achezee kichapo toka mwanafunzi mbabe huku wanafunzi wengine wakishangilia.
"...hasira zao wanahamishia kwa wanafunzi..." kauli kama hizi ndio msingi wa ushauri nilioutoa. Mwanafunzi akishaumizwa na mwalimu hata ingetokea kwa bahati mbaya jamii mara nyingi huwa haimuelewi mwalimu. Sasa kwanini isifutwe tu?
 
Mbadala wake ?
Je, watoto wa shule badala ya kupewa adhabu ya kuchapwa viboko waanze kupewa adhabu ya Kutozwa Faini?
Watakao ifuta waje na mbadala wake. Watu wa haki elimu, haki za binadamu na makundi kama hayo yanawashambulia sana walimu kwa kutoa adhabu ya viboko hawawezi kukosa mbadala wake
 
"...hasira zao wanahamishia kwa wanafunzi..." kauli kama hizi ndio msingi wa ushauri nilioutoa. Mwanafunzi akishaumizwa na mwalimu hata ingetokea kwa bahati mbaya jamii mara nyingi huwa haimuelewi mwalimu. Sasa kwanini isifutwe tu?
Bahati mbaya ni ipi teacher? Hivi ukitoa adhabu kama muongozo unavyokutaka unapungukiwa nini? Usiniambie fimbo 3 unaweza ua mwanafunzi!

Kimsingi nakubaliana na wewe kwenye kufuta hiyo adhabu sioni tija yake, mimi mwenyewe kama mfano nilikuwa nafaulu masomo ya walimu wanaotumia saikolojia kudili na wanafunzi kuliko anayetanguliza kiboko mbele
 
Nimekuwa nikiitafakari sana hii adhabu ya viboko mashuleni kila ninapoona taarifa ya mwanafunzi kuumizwa na mwalimu kichukuliwa hatua kwa kumuumiza mwanafunzi

Ni wazi kwamba kuna wagonjwa wengi wanakufa hospitali kwa uzembe wa madaktari, kuna abiri wengi wanakufa kwa ajiri kwa uzembe wa madereva, kuna vibaka wengi wanafanya uharifu mtaani kwa uzembe wa polisi na kuna watu wengi wamefungwa gerezani bila makosa kwa uzembe wa wapelelezi na wanasheria.

Hata hivyo kelele za malalamiko ya jamii juu ya hizo kada nyingine si sawa na kelele za jamii pale mwalimu anapomuumiza mwanafunzi kwa adhabu ya viboko. Jamii itaongea, itatukana, itatoa dhihaka na viongozi watachukua hatua

Ifahamike kwamba siandiki haya kwa kujaribu kutetea wala kuunga au kuwatetea walimu wanaotoa adhabu ya viboko kupitiliza na kinyume na utaratibu. Binafsi naamini adhabu ya viboko haifai na imepitwa na wakati mashuleni.

Ukisoma sheria ya utoaji adhabu ya viboko shuleni na muongozo wake utaungana na mimi kuwa hii adhabu imepitwa na wakati na haifai kuendelea kutolewa mashuleni kwasababu ni ya mtego kwa walimu na endapo wazazi na wanafunzi wangekuwa makini na sheria hii walimu wengi wangekuwa gerezani

Kwa mfano; mwongozo unataka kwa kosa kubwa mwanafunzi aadhibiwe fimbo nne tu tena anayetakiwa kuadhibu ni Mkuu wa shule.

Hapa kwenye fimbo nne kwa kosa kubwa! Ikumbukwe wanafunzi wengi wanaadhibiwa kwa makosa ya uchelewaji, utoro, kupiga kelele, kutoandika nukuu. Haya yote sio makosa makubwa yanayostahili adhabu ya fimbo. Hapa mwanafunzi anatakiwa kuonywa na kushauriwa tu.

Kuna baadhi ya wanafunzi ni jeuri, wana lugha za matusi, wanavuta bangi, na ukorofi mwingine wa ujana kiasi wanawapandisha hasira walimu kwa makusudi. Unategemea mwanafunzi anayempandishia mwalimu, anayeweza kumtukana au kumvimbia mwalimu asichapwe fimbo zaidi ya nne na achapwe na mkuu wa shule tu au ili mwalimu mwingine amchape fimbo apewe kibali cha maandishi kufanya hivyo.

Hapa unajiuliza, ni walimu wangapi wanauvumilivu huo? Watavumilia kwa muda gani?

Kwa hiyo hapa utagundua kuwa ni kama hii adhabu ilishafutwa ila haijatolewa tamko tu.

Ushauri wangu ni kuwa wizara ifute kabisa adhabu ya viboko ili walimu wawe salama na wanafunzi watakaovunja sheria za shule watafutiwe utaratibu mwingine

Binafsi naamini tukijenga utamaduni wa kutochapa fimbo shuleni wanafunzi watazoea, walimu watazoea na wazazi watazoea na kizuri zaidi wanafunzi wakorofi adhabu yao ikiwa ya kufukuzwa shule na kutafutiwa utaratibu mwingine itawajenga kujiepusha na makosa ya mara kwa mara kuliko hizi fimbo wanazochapwa mara kwa mara
Hii adhabu kwa wenye akili timamu ni kwamba imefutwa kiaina na walimu wengi kwakuwa ni failures hawaelewi mwisho wa siku wanajikuta magerezani.

Ukiisoma vizuri hii adhabu utagundua mwalimu yupo kwenye hatari kubwa ya kupoteza kibarua pamoja na ndoto zake kuyeyuka anapomuadhibu mtoto halafu akasababisha madhara.
 
Ili tuzalishe kizazi legelege mashoga yaongezeke siyo?
Mtumwa huyu hapa anayeamini fimbo ni suluhisho.

Fimbo haijawahi kuwa suluhisho la utukutu wa mtoto bali humfanya azidi kuwa mtukutu.

Wapo waliosoma shule ambazo hazitoi adhabu ya viboko wapo vizuri mno kimaadili hadi kimasomo.

Binafsi nimeitwa shuleni kwa kosa alilofanya mwanafunzi namna wanavyodili naye kumpa nasaha mbele ya mzazi unakuta mtoto anabadilika anakuwa mwema na hapo hajaguswa hata kiboko kimoja.

Ushoga ni tabia ya mtu haina uhusiano na mtoto kuchapwa ama lah.

Wewe unaonekana dhahiri ni mwalimu hivyo usipobadilika mwenyewe basi utabadilishwa na mkono wa sheria endapo mtoto ataumia hata kwa jeraha dogo tu tutakupeleka mahakamani kwa kosa la kujeruhi.

Natoa ushauri kwa walimu waachane na adhabu hizi za kikoloni maana mwisho wake ni mbaya jamii na serikali watakushambulia hadi unaingia jela.
 
Mbadala wake ?
Je, watoto wa shule badala ya kupewa adhabu ya kuchapwa viboko waanze kupewa adhabu ya Kutozwa Faini?
Kazi ni nyingi shuleni unaweza kumpa adhabu ya kufanya usafi eneo fulani kwa siku ama zaidi ya siku moja kulingana na ukubwa wa kosa.

Kumwagilia maua maji na kutunza bustani ni miongoni mwa adhabu ambazo mwanafunzi ataona ni kubwa zaidi na atajiepusha na kutenda makosa akihofia kufanya kazi hizo.

Adhabu za viboko ni urithi wa kipumbavu tulioachiwa na wakoloni na sisi tukaendelea kufanyiana Waafrika wakati hao walioiasisi wala hawaitumii kwao.

Afrika ni laana wakati mwingine maana hatuna muda wa kujiuliza na kutafakari badala yake ni kuiga tu vitu tulivyokuta tunafanyiwa na wakoloni. Too pathetic.
 
Kwani Ushoga unatokana na kutokuwepo adhabu za viboko?

Wee kweli nati za ubongo wako zimelegea. Lol
Mkuu kuna majitu humu yamekulia kwenye mateso tangu utoto wao hadi ukubwani yanadhani kuteseka ndiyo suluhisho la matatizo yao.

Sasa mtu kama huyu eti anasema adhabu ya viboko ikiondolewa tutazalisha mashoga.

Sasa sijui nani alimwambia ushoga unazuiliwa kwa viboko.

Watu kama hawa wameathirika kisaikolojia kwahiyo bado wanaishi katika ulimwengu wa zama za mawe.

Walimu wanaojitambua wameachana na habari za kuchapa watoto wamegundua ni mtego kwao.

Nimekuwa nikidili sana na masuala haya ya kutoa elimu mashuleni kuhusu adhabu na huwa nawashauri walimu kuachana na kutoa adhabu za viboko kwani nimeshuhudia walimu wengi wamehukumiwa kunyongwa hadi kufa na wengine wamefungwa vifungo virefu kwa kusababisha majeraha kwa mwanafunzi.
 
Mikwaju ndio mpango mzima. Charaza Nondo mpaka wajione wapo vitani
Unaonekana umelelewa na mama wa kambo umekulia bakora ndiyo maana umeathirika kisaikolojia.

Acha kuwadanganya walimu wenzako watajiingiza kwenye mtego wapoteze ajira na waishie gerezani kizembe sana.

Mimi ni mmoja wa wadau wa kutetea haki za binadamu nimekuwa nikizunguka maeneo tofauti tunapopata taarifa za mwalimu kumshambulia mtoto na kwakweli binafsi nimeshiriki kuhakikisha walimu kadhaa wamefungwa kwa kutofuata sheria na muongozo wa utoaji adhabu mashuleni.

Huwa najitolea bure kabisa ili mradi kuhakikisha haki za binadamu zinalindwa kikamilifu.

Walimu wasipoacha kwa hiyari yao kuchapa watoto bila utaratibu basi their final destination ni jela.
 
Hao walimu baadhi wanavypenda kuchapa ikitolewa wataumwa
Sikio la kufa haliskii dawa.

Walimu wanaojifanya kutozingatia utoaji wa adhabu mashuleni huwa tunawashughulikia kisheria kuhakikisha wanaishia jela ambayo ndiyo sehemu yao waliyoichagua.

Wapo walimu wenye kujielewa ninaofahamiana nao wao walishaapa hawatoshughulika na kuchapa mtoto wa mtu maana usipokuwa makini utapoteza vyote ajira na maisha ya kuwa huru mtaani.

Mara nyingi walimu wanaopenda kutoa adhabu ya viboko ni empty vichwani mwao hivyo ukali wao wanatumia kama defense kuficha ukilaza wao.
 
"...hasira zao wanahamishia kwa wanafunzi..." kauli kama hizi ndio msingi wa ushauri nilioutoa. Mwanafunzi akishaumizwa na mwalimu hata ingetokea kwa bahati mbaya jamii mara nyingi huwa haimuelewi mwalimu. Sasa kwanini isifutwe tu?
Kwanini umuumize?? Ujue mpaka jambo linakua kubwa ni kwamba ticha anakua kapiga kwelikweli.
Mtoto anachapwa mpaka anachanika mkono.

Adhabu isifutwe
 
Kwanini umuumize?? Ujue mpaka jambo linakua kubwa ni kwamba ticha anakua kapiga kwelikweli.
Mtoto anachapwa mpaka anachanika mkono.

Adhabu isifutwe
Kifaa kinachotumika ni fimbo ambayo bila kutarajia inaweza kusababisha jeraha hasa ikipasuka na kipande cha fimbo kuchana sehemu ya mkono au bila kutarajia fimbo ikagusa sehemu ya kidole kikavimba hasa kwa wenye ngozi laini

Ikumbukwe kuwa, mtoto akishakuwa na jeraha au uvimbe ni vigumu jamii kuelewa kwasababu wao "focus" yao itakuwa kwenye jeraha au uvimbe hata kama alichapwa fimbo moja tu!

Kitu kingine kinachonishawishi kushauri tamko la kufuta hii adhabu ni pale linapotokea tatizo kwa mwanafunzi kuumizwa, hakuna anayekumbuka kuangalia dhamira ya Mwalimu iliyomsukuma kutoa adhabu aliyotoa

Kuna watu nimeona wameshauri kuwa adhabu mbadala kama kumwagilia maua, kufyeka, kulima, kufanya usafi, nk zitolewe kwa wanafunzi wanaofanya makosa. Hawa wamesahau kuwa hizi shughuli hazipaswi kupandikizwa vichwani kwa watoto kama adhabu badala yake wanatakiwa kujengewa mazingira ya kupenda shughuli za mikono kwani mbeleni zinaweza kuwa msaada kwao

Adhabu ni tendo analofanyiwa mtu kumuonywa kufanya jambo baya. Kwa maana nyingine tendo hilo lazima liwe la kuumiza au kumnyima mtu uhuru au haki fulani kwasababu amevunja sheria. Tukiwazoesha watoto kuwa kumwagilia maua ni kazi za wenye makosa tutakuwa tunatengeneza jamii ya aina gani?

Kuna shule moja mtoto alipoteza maisha kwa kuangukiwa na jiwe wakati wanachimba kifusi, wahusika wa shule ile waliyopitia wanayajua. Kuna shule watoto walikutwa wanazimbu chemba za choo zilizoziba (kwa matumizi yao mabaya), bado ilionekana walimu wamekosea

Mbaya zaidi anayependekeza watoto wapewe adhabu za kumwagilia maua au kufanya usafi anajiita "mtetezi wa haki za binadamu". Yaani kwake kufanya usafi anataka iwe adhabu isiwe kazi ya kawaida na ya kuwajenga watoto wapende kufanya usafi

Mimi nadhani adhabu ndogo ndogo zinawezakuwa kama kupigishwa magoti bila kujali kwa muda gani kulingana na kosa, kukalishwa chini, kunyimwa fursa zinazopatikana shuleni kama kufungiwa kushiriki michezo (kama ni mwanamichezo), kuzuiliwa kushiriki masomo kwa kipindi fulani (suspension), na wenye makosa makubwa kufukuzwa shule kama ilivyo kwa sasa

Nashauri adhabu ya fimbo ifutwe lakini mbadala wake haiwezi kuwa shughuli za mikono kwasababu "adhabu" ni tendo la kumuonya mtu hivyo tendo hilo lazima liwe lisilo la kawaida
 
Sikio la kufa haliskii dawa.

Walimu wanaojifanya kutozingatia utoaji wa adhabu mashuleni huwa tunawashughulikia kisheria kuhakikisha wanaishia jela ambayo ndiyo sehemu yao waliyoichagua.

Wapo walimu wenye kujielewa ninaofahamiana nao wao walishaapa hawatoshughulika na kuchapa mtoto wa mtu maana usipokuwa makini utapoteza vyote ajira na maisha ya kuwa huru mtaani.

Mara nyingi walimu wanaopenda kutoa adhabu ya viboko ni empty vichwani mwao hivyo ukali wao wanatumia kama defense kuficha ukilaza wao.
Si kweli kwamba walimu wanaotoa adhabu ya viboko ni "empty". Huo ni mtazamo wako na kukosa uzoefu wa kushughulika na tabia za watoto / vijana wanaokua. Kuna wazazi pia wanachapa watoto wao nyumbani nao ni "empty"! Serikali hadi leo imeshikwa na kigugumiza kufuta kabisa adhabu ya viboko shuleni nao tuseme wako "empty" lakini unataka wewe unayejiita "mtetezi wa haki za binadamu" ambao mnatetea hadi zile haki za "kishetani" ndo tuone mna akili. Hapo umepuyanga.

Itoshe kusema adhabu ya viboko inatakiwa kufanyiwa tathimini upya lakini si kweli kwamba wanaoitekeleza hawana akili.
 
Back
Top Bottom