Ushauri: Lwandamila afukuzwe haraka sana Yanga

Ushauri: Lwandamila afukuzwe haraka sana Yanga

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Huyu ni kati ya makocha wabovu kabisa waliowahi kuifundisha yanga katika kipindi cha miaka 20 iliyopita , ni mara mia kazi hiyo angepewa Kataraia Minziro .

Wana Yanga mtakubaliana na mimi kwamba tangu ameichukua timu hii , kile kiwango cha kimataifa ilichokuwa inacheza timu yenu , kile kiwango kilichoifanya Tanzania ijivunie yanga kimepeperuka mithili ya Njiwa wa uganga .

Fukuzeni huyu jamaa haraka sana kuinusuru timu yenu na aibu inayokuja .
 
Embuu subria,letee habari jwa upolee na kwa hoja.
 
Mkuu kila siku unapenda makocha wafukuzwe wewe unanufaika na nini wakifukuzwa
Huyu ni kocha mbovu kabisa , kama Manji anamtaka si ampe kazi quality group ?

Kumbuka ukiua hizi simba na yanga ndio umeua soka la nchi hii masikini isiyo na hela .
 
Lwandamila achague pakuikuta mizigo yake,kama bandarini au airport achague mwenyewe au akitaka ipakiwe kwenye Taqwa Bus achague ila ajue Jangwani hakanyagi tena.
 
Kuweka kumbukumbu sawa mimi sio Yanga ni Simba damu ila nawajua watani zangu hawana vifua vya kupokea mabaya!huyu kocha kesho pakikucha atakijua kilichomnyonyoa kanga manyoya.
 
Umeshasema wewe ni Simba sasa ubovu wake ni up? Ajabu kufugwa au kuna timu au kocha hafungwi Duniani?
 
Kuweka kumbukumbu sawa mimi sio Yanga ni Simba damu ila nawajua watani zangu hawana vifua vya kupokea mabaya!huyu kocha kesho pakikucha atakijua kilichomnyonyoa kanga manyoya.
Dua la kuku subiri ufukuze kocha wako
 
Back
Top Bottom