Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Plan kwanza kuingia nchi za Kusini mwa Afrika chaka lingine naloona ukitaka kuanzia maisha ni Namibia. Kuna nchi hapa Africa unaweza zitumia kama daraja tu ili kufika mamtoni
Na vip kazi zilizopo nyingi ni manual or professionals work?
 
msaaada mwenye links za scholarships za ughaibuni za 2019-2020, na anayejua koz gan marketable kwa ngazi ya masters kwa mtu ambae amesoma degree ya civil anaweza akasoma na kupata kazi ughaibuni
 
Funguka hapa fursa za Malta mbali na jeshi
 
Haha kinachoendelea kwenye hii game wabongo wengi hawakijui. Cha ajabu hao wanaoona ubahili kulipa hao agents ndo hao hao wanaochezea Pesa bar/mtaani kutafuta heshima.
True,wasichofahamu ni kuwa Visa consulancy/agency ni biashara iko dunia nzima,kusaidia wale wasioweza procedure na technics za kuapply na wale wasiokuwa na supporting documents za kutosha au muda.hawa Agents baadhi wanakuwa na connections balozini hivyo success rate inakuwa kubwa tafauti na ukienda mwenyewe kichwakichwa,ingawa kuna matapeli wengi kwenye hyo tasnia na watu washaliwa sana hela.Nafikiria kuanza kuitumia hii fursa na mimi nianzishe Agency hapa bongo ambayo itakuwa ni Travel agency lakini pia na kushuhulikia Visa,maana naona nawafanyia washkaji bure lakini fadhila hawana wakishapata Viza wakasepa ndo ntolee,hata vizawadi zawadi hata vipafyumu hawatumi,kazi kutamba insta tu.
 

Kabisa mkuu mi mwenyewe nilisaidia sana watu mwishowe nikanyoosha mikono juu!
 
Me ninampango wakujilipua SA,vp wakuu naombeni mwongozo Wa hautua gani za kufuata kuanza safari yangu kwa njia ya basi na pindi nitakapofika kule.

Je kuna boda ngapi mpaka nafika kule?je nini chakuzingatia nifikapo boda au nikiwa safarini?Je nichange pesa hapa au mbele kwa mbele?
 

CC: segito wa kalenga
 

Namna ya kuanza safari yako kwenda South Africa.

Mahitaji ya safari.
1. uwe na hati ya kusafiria

2. Uwe na kadi ya manjano. hii ni muhimu saana maana kupita pale nakonde/tunduma lazima uionyeshe la sivyo watakupiga pesa.Hii wa south africa huwa hawaiulizii saana. wazambia na wazimbabwe ndiyo wasumbufu.

3. Nauli.
-Nauli ya kutoka Dar hadi Harare ni 120000 moja kwa moja. hapo utalala kwenye basi maana safari inaanza usiku wa siku ya pili.
-Nauli ya kutokaHarare hadi South africa haipo flexible maana hata private unapata muda wowote kuelekea Jozi ila tenga 120000.

-Pesa ya matumizi njiani 150000

Jumla ukiwa na laki 400000 kamili unafika J'berg vizuri tu na change inabaki...Kikubwa uwe na mtu anayekupokea. Kama hauna inamaana gharama zitaongezeka.

4.Lingine boda hasa kwa wazambia na wazimbabwe watakusumbua tuambie unaenda kufanya nini unakoelekea...sharti uwe na barua ya mwaliko au anuani ya mtu aliyepo SA. Kama hauna unaomba transist ila Wazambia wanapenda rushwa saana.

Boda inategemea na Njia unayopitia.

Ukipitia Nakonde-lusaka-harare-SA kuna Nne.hii ni Rahisi zaidi.

Ya kuzingatia

-Kwenye Boda kuna wizi kwenye kubadilisha pesa nitakushauri badilisha kwenye western za Bongo.

-Uwe na target South africa sio pazuri kwa maana unaweza kulizwa wahuni wa Afrika wote wapo Jozi.


-Unaweza kuniuliza maswali mengine zaidi.
 
Aupair ni njia rahisi mno kusecure visa ya schengen nje ya mambo ya ndoa.
Aupair nimetafta (kwa njia ya kawaida) sana sijapata, kama unaweza kunisaidia kupata Scandinavia nitashukuru anko lusungo.
 
Jamaa uliyemjibu hapo juu yupo Capetown kwa sasa, ana kama siku nne tokea afike
 
Jamaa uliyemjibu hapo juu yupo Capetown kwa sasa, ana kama siku nne tokea afike
Hivi South Africa zaidi ya kuuza unga unaweza vipi kumake pesa?

Mimi nadhani South Africa tuiangalie zaidi kwa fursa za kibiashara lakini siyo kwa deiwaka otherwise Bongo uwe umepigika hasa sasa unamuuwa kutokomea mazima hapo South Africa utaenjoy sana kuliko waliopo ulaya.
 
Ni kweli South ni pakavu saana ukilinganisha na Ulaya. Panakalika zaidi kwa ishu za kibiashara.

Ila still kuna kazi zinafanyika nimeona watu wanazifanya na zinalipa kuliko bongo. (garage + designers).
 
Wazee hebu tupeane information yaani hili life na hali ya biashara hapa Tz imenifanya niwaze kuhamisha mtaji wangu huko south ila sasa kila nikiwaza nakwenda kufanya biashara gani kichwa kinauma. Mwenye info na connections asaidie hata kwa uchache
 
Wa south nasikia wana husudu hawakawii kukupoteza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…