Mimi nina uwezo wa kusaidia watu humu kupata US Viza lakini naogopa mwisho wa siku humu watakutangaza ni tapeli.
Mtu anayejuwa kingereza vizuri ukimwambia fomu inabidi ajaziwe hapohapo anakuhisi wewe ni tapeli hata Mimi zamani nilidhani hivyo, kumbe zile fomu zina technics zake za ujazaji.
Kwa mfano Sheghen viza kwangu ndio viza rahisi kwangu ukiwa na cash tu maana wao wanahitaji documents tu, hata Canadian viza haina shida ukiwa na cash unatengezewa karatasi zilizosimama unang'oa viza kama umesimama.
Canada inahitaji sana raslimali watu ila huwa sielewi ni kwa nini Watanzania hii fursa tumeshindwa kuitumia kikamilifu, tena zamani wajanja wote waliotaka kuingia Marekani walipitia Canada kwanza then wakaingilia na border viza kabla Osama hajaharibu utaratibu wa maisha na sept 11 yake.
Kuna Wahindi Fulani niliwachongea mchongo wa Canada waliingiza passport za familia nzima golini kwa invitation moja na wote wamepata viza. Tatizo naliona pale Toronto wabongo wengi hawajielewi.
MTU yeyote anayekutana na magumu Leo kutusua kwenda mbele mnapaswa kumlaani Osama bin Laden kwa nguvu zote, tuliowahi kwenda mamtoni kabla sept 11 haikuwa kama sasa, hata London tulikuwa tunapita na BA free kutoka Heathrow kwenda Gatwick airport bila transit viza. Maisha yalikuwa ni mazuri sana.
Sent using
Jamii Forums mobile app