Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Denmark ni nchi ya scandinavia... Ni nchi yenye maisha ya raha na amani sana japo ni nchi ndogo... Njia rahisi kwenda huko unaweza kwenda as tourist then ukifika huko unapambana upate wa kumwoa hata kwa makaratasi tu ili upate kibali cha ukaazi.
Alafu nikitaka kwenda sauzi.kwa gari.nikifika mipakani nitaulizwa tiketi ya kurudia yaani kama kwenye ndege?
 
Dah asante mkuu kwa kuleta uzi huu mimi nimeplan kuhamia marekani mwaka huu mwishoni panapo majaaliwa kuna kakaangu atanialika hebu naomba kujua Visa ya kwanza ni muda gani wanakupa na ameniambia atanitafutia kazi kwa mwezi kiasi kadhaa mana kuajiriwa bongo mshahara wote unaishia kwenye matumizi hebu naomba msaada kujilipua usa inakuaje au ndo trumph atanirudisha kwetu mkuu asante
 
Mkuu visa inategemea na kaka'ko anakualika huko kwa muda gani.
 
Huko unakokwenda pia kuna matumizi, tena kama ni hizi kazi za unskilled labour utajikuta wewe ni mtu wa hand to mouth. Kinachoumiza sana ni kodi ya nyumba, watu wengi inabidi wafanye kazi mbili ili kupata pesa ya ziada.
 
Mkuu, jiandae kuzungukwa na defender leo jioni. Bwana yule hataki kukosolewa
 
Huko unakokwenda pia kuna matumizi, tena kama ni hizi kazi za unskilled labour utajikuta wewe ni mtu wa hand to mouth. Kinachoumiza sana ni kodi ya nyumba, watu wengi inabidi wafanye kazi mbili ili kupata pesa ya ziada.
Kwa kuanzia kukaa kupo mkuu kwa huo mwaka pia kufanya kazi mbili sio mbaya mkuu je baada ya Visa kuisha unaweza ukajilipua mkuu
 
Mkuu, usitusahau nyumbani ukifika kwa Trump.
Twakuombea Heri lengo lako litimie
 
Nmepata mchongo wa kwenda japan na mwenyeji wangu kaniambia fursa za kazi kibao na nkifika natafutiwa mwanamke tunafunga ndoa napata kikaratas maisha mengine yataendela. Kwa mwenye uzoefu na inchi hiyo ningependa kujua mengi
 
Mkuu utawakumbukaa ndugu walaa jamaa ujee ukawasalimiee ..au ndio ilee utawaambiaa mtaona majaliwaa mungu akipendaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…