Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Dah. hao nahisi nitawakosa ila watakaofata itabidi niwepo katika list. Nitakuwa Tz mwez wa 6 . Nakuja kupumzika kidogo then nabadilisha upepo maana SA kwa sasa hakuna issue tena
 
nchi inayokumbwa na upungufu wa chakula kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa... nchi huduma za kijamii si zakulizisha... nchi ambayo mambo mengi hayaendi kama wananchi wanavyotalajia ndo maana hata wewe una sapoti watu waende kusoma watu waende kama wana utaalam hivyo ni hila na hasira zako kwa watu kuona wanaondoka kutimiza ndoto zao kwa kuajialiwa au kujiajiri huko waendapo ambapo wataweza kusave kiasi na kukileta kwao kitaweza kumpa uwezo wa kumiliki greenhous ambayo sasa ni ngumu kwa kijana kumiliki kutokana na gharama kuwa kubwa... wanakaa nyumbani wakiwa wamekata tamaa ya kukosa ajira kukosa mikopo ya kuendeleza au kufikia sehemu ya ndoto zao... njoo na vitu vya kueleweka nyinyi ndio mnataka watu wajiajiri bila ya mitaji alafu hapo hapo kodi ni kubwa rushwa pia mahitaji ya nyumbani (kwa wategemezi)... ni bora mtu kufanya anachoweza kufanya kiliko kushikiliwa akili mental slave ni kitu kibaya watu au mtu ili kuweza kufanikiwa ni lazima afanye kile anachoweza kukifanya kuliko kumpush kufanya hasichoweza hivyo hacha watanganyika wafanye wanachowezafanya bila kuvunja sheria za nchi mkuuu...! mwisho kabisa nibora ukaja na page yako ya kuhamasisha na kuwaonyesha watanganyika njia wanazoweza kupitia ili wafanikiwe hapa hapa maana hii page haiendani na mawazo yako mkuu... ni sawa na yule aliyekuja na post ya bit coin... katika page ambayo si sahihi na wazo lake...
 
upo kigoma mkuu...
 
Dah we ungekua ndugu yng ningefurahi SNA mana nina kaka marekani na uingereza wako wanaweka ngumu kwenda taifa lolote ulaya nimesoma diploma ya engineering ishu ya IT miaka 3 unataka degree nikasome nnje mana ajira kwetu ngumu na kurudi degree bongo alafu ukose kaz ntakua chizi mana umri unaenda bora nnje ntarudi na mtaji na kujiajili ma bro zangu wanataka nibaki bongo nisome mlimani 4 years duh nataman niombe ukaka kwako
 
Kabisa mkuu... Kitu kingine wivu... Wabongo siku zote tunatamani wengine waanguke tukiamini ndo tutainuka!!

Wengi hatupendi mafanikio ya ndugu hata tuliozaliwa nao...


That's correct. Wabongo tunazibiana sisi kwa sisi... waliotusua hawataki kuwavuta waliopo down.

Unakuta mtu amenyaka dili fulani, hawezi kuwastua wengine hata kama yeye hana capacity nayo. Hii ngozi nyeusi hii ni shida sana. Roho mbaya, ushirikina, kuangushana ile ya 'tukose wote', majungu, n.k.

Ndugu nao ni helpless tu. Waweza pata majanga afu ndugu akaibuka week ya pili. Unapata great support kutoka kwa mtu baki ambaye hata hukutegemea.

Ndugu wa damu kabisa yupo vizuri sana kiuchumi, unamuomba akukopeshe laki tatu tu ili ujiajiri kwenye Ujasiriamali, anakuambia hana. Ila kila ukienda kumlilia shida hela ya kula, anakupa na nauli juu. Miafrika tuna ubagamoyo wa ajabu sana mkuu. Ni wachache sana wenye mioyo safi.

The black continent. Penye giza... nuru haiji kwa koroboi.

-Kaveli-
 
Ndugu zako ni mapoyoyo, kama hesabu inapanda vizuri, na kimalkia unakijua jilipue na GRE na English exams then zama kwenye web mwenyewe. Mi nilipita njia hiyo, nikamaliza nikaendelea kupiga mzigo kwa Obama. Bongo kwa likizo tu.
 



Nyuzi kama hizi ni sawa na kuwafundisha Waafrika kuwa Watumwa bila minyororo.
Mnatukumbusha kauli za Kamuzu Banda na Mabutu Seseseko, leo hii Malawi ndio imetoa wafanyakazi wa nyumbani wa kiume (foreign male domestic workers) kuliko nchi nyingine Afrika.
DRC ni katika nchi tajiri Afrika hii lakini waangalie Wakongo wengi walipo, zaidi ya wanaume kukata viuno jukwaani, kuimba na kujichubua. Leo Wakongo sio watu wakula mbwa na nyani.

Hii Tanzania yetu, unaweza kutimiza ndoto yako, hata kuanzia mchimba mkaa mpaka kuwa Mkuu wa Mkoa. Why not? Right here in Tanzania

Tunawapeleka watu wetu kwenda kuosha vyombo, choo na vinyeshi huko barani Ulaya wakati ardhi zetu zina rutuba ya kukutosha na tunaweza kuishi na kuendesha maisha yetu kupitia kilimo?

Tunayajua hayo yote lakini tunahitaji kizazi ambacho kitakachojilipua hapa hapa barani Afrika, kijitoe muhanga na sadaka kwa ajili ya kizazi kipya yaani tutumie muda wetu wote kufanya mapinduzi ya kiuchumi hapa hapa Afrika kama vile wazee wetu walitumia muda wao wote kutukomboa kwenye minyororo ya Wakoloni.

Wakoloni, waliishi vipi na kufanikisha maisha yao hapa Afrika?
Mapinduzi ya Kiuchumi yanahitajika. Hatuondoki Afrika.
 
Wewe unaishi Africa ipi....
unazungumzia Nchi ambayo Raisi anajigeuza kuwa mungu anachosema yeye ndio mwisho Tanganyika hii tuna zaidi ya miaka 50 tangu Uhuru hivi unayohabari Mwaka wa Jana wakulima wa Nyanya walivuna nakulisha Ng'ombe...au Mwenzetu ni miongoni mwa wanufaika wa Nchi hii kiasi kwamba hamjui Taabu wanazokutana nazo wadanganyika.....
 
Hii nchi ya uzulumishi sana.unatafuta kwa nguvu nyingi unanyang'anywa kirahis.mfano mzuri ishu ya viroba.ni bora nijilipue mambele hamna namna.nikuache bro uendelee kupiga porojo mana inaezekana hata wewe haupo bongo land
 
Kama nimekuelewa sana mkuu.
 


Makomanda wenzangu wa mitandaoni, hili sio suala na mtu binafsi, vilio vya Afrika tunavisikia kuanzia Sudan ya Kusini, Misri, Angola, Ethiopia, Somalia nk.
Kuna wenye hali mbaya kuliko hapa kwetu Tanzania.
Na sio kama hatujui wala hatujaupitia au kuutumia mfumo huu wa njia za panya za kujikomboa kiuchumi.
Lazima tuwe na mawazo tofauti. Kama Gaza sehemu inayojulikana kama jela iliyokuwa wazi, wananchi wanabaguliwa na wanaishi kama wakimbizi kwenye ardhi yao, na bado vijana wameweza kujikomboa kiuchumi hapo hapo, sembuse Tanzania?
Tanzania tokea tupate Uhuru wetu, hatuna rekodi Taifa letu limejikomboa kwenye Umasikini, mapambano bado yanaendelea.
Awamu ya 5 inafanya zoezi la ku cleaning the virus and rebooting the system. Tuwe wavumilivu.
 
Mkuu umepita mulemule kwenye mstari hakika waso,i wetu walio wengi ni wasomi wa makaratasi na sio wasomi wa vitendo na ndio maana tukija kwenye practical tunafeli.
Leo hii mtu anaitwa kwenye interview anavyojieleza utasikitika kama mtoto wa sekondari maelezo hayanyoki elimu yetu na sisi wenyewe kutojishughulisha ndio matokeo haya yanakuja kuiaibisha nchi yetu.
Nakumbuka kunaprofesa flani alilia ajira ya magu maneno aliyosema yalidhihilisha alikuwa fake profesa yaani uprofesa wa kuhongwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…