Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Nashangaa why Europe apt Ni cheap dhan TZ?mkuu kule apt ni cheap kutegemea na unapoishi.

Finland ni more cheap mkuu.Tatizo ni wapi utaupata unga wa kupikia ugali???na sisi wabongo hasa sisi akina "Mura" bila ugali is nothing.
Alafu ukiwa unasuka rasta basi utaopoa mademu wa kizungu mpaka basi.
nasikia Europe tailoring ina pesa sana.... naomba mlio majuu mtujuze katika hilo... vipi fabrics pia zinaenda kama botswana na zimbabwe...?
 
Dah,inabidi nifanye mchakato wa kurudi tena huko mkuu.
Na this time ntakuwa kijana mwema sana.
Nirudi europe nikale ugali na uyoga,maana naogopa kula nyama za wazungu because halal shop zilikua sii nyingi,hope now days halal shop zipo sasa.
Mkuu una nikumbusha kigoma wale watu wanapiga sana uyoga... kipindi cha mvua wanakubali kunyeshewa ili wavune hiyo kitu kuna muda una waona kabisa jinsi wanavyoula mbichi ule mteke mteke alafu wa njano ya binzari
 
Weka nia utafika tu siku moja!
Inshaallah... na ndio najaribu kujichanga mzee naangalia jinsi ya kwenda na kuanza hata na kabiashara kachap chap una pata hata USD 50 hata 100 sio unaenda alafu ujaongeza kitu katika akiba uliyoenda nayo mzee... haya mambo ni kujiongeza ukiambiwa kitu una fikiria zaidi ya pale weka loss na profit na loss ikitokea unakuwa tayari kukabiliana nayo, faida ikitokea pia ndio mwanzo wa kufanikiwa ila unaongza mbinu zaidi
 
Ila kama unaenda south njia salama ni ya ndege tu... Kata return ticket... Ingia booking.com book room then print booking conformation ibebe ukifika huko unawaonesha tuuu unapita!!

Njia ya boda si nzuri sana

Isanga family
 
hii kitu ni kweli hata rafiki zangu wananipa ukweli halisi....

"Botswana is just fine, we r very friendly. U will b safe here. If u want to enjoy Botswana don't go against the law.
I want to buy some fabrics there (Tanzania)"

Botswana pako fresh Sana mkuu, kama utakua na vibali vyakuishi. Huwezi ukaishi Botswana kama kwa Madiba. Huku sheria IPO. [emoji41] [emoji41]

Sent from my TECNO H5 using JamiiForums mobile app
 
well shukrani sana ngoja nisevu hii booking site
Ila kama unaenda south njia salama ni ya ndege tu... Kata return ticket... Ingia booking.com book room then print booking conformation ibebe ukifika huko unawaonesha tuuu unapita!!

Njia ya boda si nzuri sana

Isanga family
 
nasikia Europe tailoring ina pesa sana.... naomba mlio majuu mtujuze katika hilo... vipi fabrics pia zinaenda kama botswana na zimbabwe...?
Mkuu unajua nilitokea 44KJ pale mbeya nikiwa na utaalam wa kilimo na mifugo ingawa sikua na cheti,so nilivyoenda europe nikabezi kwenye mambo hayo tu thats why nikaenda Australia na New Zealand,but nilibahatika kufika mpaka Helsinki nikawa napiga kazi kwenye warehouse moja hivi long stand job,but tatizo nilikua na girlfriend Tz na nilinuacha mja mzito so akawa kajifungua ikabidi nirudi home,Then wakati nikijiandaa kutimka tena nikaanza kuuguliwa na "mshua"so nikamuuguza for two yrs but mungu akampenda zaidi,baada ya hapo sikuona aja ya kuondoka kumuacha bi mkubwa na wadogo zangu wakiwa wanasoma,ikabidi nitumie amount niliyokua nayo kuwasomeshea wadogo zangu na pia nikaewekeza some where...but madogo wote wapo chuo kikuu mmoja yupo mlimani na mwingine Jordan Moro,mwingine ni wakike alisoma education Chuo kimoja Tabora now days yupo Texas alipata shavu huko mji mmoja unaitwa Houston.
So mkuu europe ni kujilipua tu na ukifika kule usichague kazi.
 
Asante kwa kutupa experience hii!! Hahahaaa jamaa ukawa unamuwaza Tz sweat heart sepenga!!! Duuu
 
Mkuu JF ni familia moja takatifu sana...so mwenye idea nzr anaitoa kwa roho moja.
 
Naona kuna watu bado wanawaza kuchonga barua za mwaliko.

Hayo mambo inawezekana yalikuwepo huko nyuma ila sasa hivi yanatiliwa maanani sana.

Ila kwa ushauri wa maana sana ni kwamba sasa hivi huwezi kwenda nje ya nchi khasa Ulaya au Marekani na Canada kama huna kazi ya uhakika au mfadhili wa uhakika kama wewe ni mwanafunzi.

Hata yule mwalikaji nae anabanwa na mambo mengi na khasa uhakika wa wewe kurudi na wanaweka dhamana kabisa.

Kuhusu Malta wao siku hizi wameweka viza ya makazi ya kudumu kwa wale waotoka nje ya bara la Ulaya lakini lazima uwe na kiasi kisichopungua Euro 200,000.

Hivyo tayari wanaangalia watu wenye uwezo kifedha.

Mkiona watu wanakuwa wazito ufahamu kuwa mambo ni mazito.
 
Mkuu Izzo ninaswali!! Nivigezo gani umepanga kwayule atakaekua tayari kuwapokea hao wegine mwezi huo wasita kama Mungu atatujalia kupafika. Lazima vigezo viwepo coz, kuna wengine tunaishi tandale kwamtogole, mbayazaidi nyumba ya urisi. Hapa mjomba pale mama mdogo, chumba chatatu binam na familia yake. Bado usiku nymba ya2,keroza Bar makelele hadi kunakucha vilevile wengi wetu lugha haipandi. Sasa sijui utaongea nini nahuyo Mtoto waki Malta wakati hamuelewani? Namengine mengi. Naomba vigezo na masharti, tuzingatie. Asante.

Sent from my TECNO H5 using JamiiForums mobile app
 
Hahahahahahaha, baba peponi ushafika hadi useme chai inafanana na yapeponi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…