Uchaguzi 2020 Ushauri muhimu sana kwa Tundu Lissu tukielekea Oktoba 2020

Uchaguzi 2020 Ushauri muhimu sana kwa Tundu Lissu tukielekea Oktoba 2020

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2020
Posts
4,437
Reaction score
13,836
Ni wazi kuwa Lissu amekuwa mwanaharakati wa kutetea haki za wananchi kwa miaka mingi, pia ni wazi kuwa kwa sasa yeye ndiye mwanasiasa pekee wa upinzani mwenye uwezo wa kumtikisa Magufuli.

Lakini kuna mambo machache ningependa kumshauri ayazingatie atakavyoendelea na kampeni zake kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

1. Aache kumshambulia Magufuli binafsi
Naamini kuna watu wengi tu wamemshauri juu ya hili, ni muhimu sana kulizingatia hili. Ni vema kuielekezea mashambulizi serikali kwa ujumla na chama cha CCM badala ya kumshambulia Magufuli.

Hata Magufuli akitaka kurusha vijembe upande wa pili mara nyingi hua hataji majina ya watu. Anaepusha mgongano wa hoja kugeuka kuwa ugomvi binafsi.

2. Ajikite kwenye matatizo yanayowagusa wananchi wengi
Japo kiubinadamu ni ngumu sana kufanya hili ukizingatia yeye binafsi alivyoteswa na kulengwa moja kwa moja na utawala huu lakini ajitahidi kuachana na 'personal vendetta' dhidi ya serikali akiwa jukwaani.

Watu hawakuchagui ili ukatimize hasira zako bali ili ukatatue changamoto zao. Kuna mengi ya kuongelea kila sehemu, watumishi, wakulima, wafanya biashara, wahitimu wa vyuo n.k

Lakini pia kuna ukatili wa polisi na kuminywa kwa demokrasia na uhuru, bila kusahau sheria na kanuni za kishenzi za awamu ya 5.

3. Ajizuei kutumia lugha kali
Najua Lissu ni bingwa wa kutibua nyongo za wapinzani wake, namshauri sasa kwakua anawania ofisi ya juu kabisa hapa nchini basi ajitahidi kuongea kama rais mtarajiwa. Lugha za kejeli na kukashifu hazifai kutolewa na kiongozi mkuu wa nchi.

Ni hayo tu machache, natumaini ujumbe umefika.
 
Hii miradi binafsi ndiyo imekula pesa ambazo zingeendeleza maisha ya watu na kutatua shida. Tundu Lissu ana hoja. alishasema madaraka ya Rais katika nchi hii hayana ukomo.

Anachofanya ni kuelezea tu Rais huyu alivyotumia madaraka yake katika miaka mitano tu ya utawala wake.
 
#2 kuteswa na kulengwa moja kwa moja na utawala huu hili siliamini mpaka kesho,huyu alilengwa na maadui zake tu wala asitudanganye.

Serikali yoyote duniani ilivyo na mkono mrefu iende ikafanye vitu kitoto namna hiyo wapi na wapi,huyu atakua na maadui zake tu huko ndani ya chama,au aliwahi kumpindishia mtu sheria, au aligongwa na mabeberu moja kwa moja kuchafua taswira ya nchi na wakageuka kumsaidia na kumlazimisha amtukane Rais ambaye sisi wananchi tunaona wazi kua tuna Rais anayetupigania usiku na mchana

NB: inawezekana kabisa mabeberu yamemuwekea hata vinasa sauti na yeye anajua au anahisi, hivyo basi ni lazima kwake kuropoka ropoka ili wamsikie huku yeye pia akilenga mamilioni ya pesa wanayompa yasije yakakata

Tundu ni muhuni tu na siamini kama kuna siku moja MUNGU anaweza kumteua huyu maana hakuna mamlaka inakuja kwa kupiga tu kura isipokua kwa maamuzi ya MUNGU mwenyewe
 
Mbona huu ni mwanzo tu, sera za chama zitamwagwa lakini ni vizuri wanyonge wafahami aliyoyafanya kipenzi chao kwa miaka mitano.
Ni kweli kabisa, kwa muundo wa serikali yetu kile kinachofanywa na serikali kina akisi moja kwa moja msimamo wa rais. Lakini ni vema kuikosoa serikali ya CCM na kuinadi serikali mbadala ya CDM.
 
#2 kuteswa na kulengwa moja kwa moja na utawala huu hili siliamini mpaka kesho,huyu alilengwa na maadui zake tu wala asitudanganye.

Serikali yoyote duniani ilivyo na mkono mrefu iende ikafanye vitu kitoto namna hiyo wapi na wapi,huyu atakua na maadui zake tu huko ndani ya chama,au aliwahi kumpindishia mtu sheria, au aligongwa na mabeberu moja kwa moja kuchafua taswira ya nchi na wakageuka kumsaidia na kumlazimisha amrukane Rais ambaye sisi wananchi tunaona wazi kua tuna Rais anayetupigania usiku na mchana

NB: inawezekana kabisa mabeberu yamemuwekea hata vinasa sauti na yeye anajua au anahisi, hivyo basi ni lazima kwake kuropoka ropoka ili wamsikie huku yeye pia akilenga mamilioni ya pesa wanayompa yasije yakakata

Tundu ni muhuni tu na siamini kama kuna siku moja MUNGU anaweza kumteua huyu maana hakuna mamlaka inakuja kwa kupiga tu kura isipokua kwa maamuzi ya MUNGU mwenyewe
Mkono mrefu mpaka sasa sijasikia waliomshambulia Tundu Lissu,huo mkono mrefu ndo upi?

Mwisho wa Magufuli ndo huu
 
#2 kuteswa na kulengwa moja kwa moja na utawala huu hili siliamini mpaka kesho,huyu alilengwa na maadui zake tu wala asitudanganye.

Serikali yoyote duniani ilivyo na mkono mrefu iende ikafanye vitu kitoto namna hiyo wapi na wapi,huyu atakua na maadui zake tu huko ndani ya chama,au aliwahi kumpindishia mtu sheria, au aligongwa na mabeberu moja kwa moja kuchafua taswira ya nchi na wakageuka kumsaidia na kumlazimisha amtukane Rais ambaye sisi wananchi tunaona wazi kua tuna Rais anayetupigania usiku na mchana

NB: inawezekana kabisa mabeberu yamemuwekea hata vinasa sauti na yeye anajua au anahisi, hivyo basi ni lazima kwake kuropoka ropoka ili wamsikie huku yeye pia akilenga mamilioni ya pesa wanayompa yasije yakakata

Tundu ni muhuni tu na siamini kama kuna siku moja MUNGU anaweza kumteua huyu maana hakuna mamlaka inakuja kwa kupiga tu kura isipokua kwa maamuzi ya MUNGU mwenyewe
Mhuni ni yule anayejibu hoja kwa risasi. CCM imeshakoma kuwa chama cha siasa na kubaki kuwa genge la kigaidi linalotumia mabavu ya dola kuendelea kutawala

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom