Ushauri na Mbinu Mbalimbali Kuhusu Uendeshaji wa Biashara ya Kuosha Magari (Car Wash)

Lughe

Senior Member
Joined
Oct 26, 2010
Posts
116
Reaction score
19


Hi to everyone, and hope you're doin fine.

Nimefikiria kuwa na mradi wa uoshaji magari sambamba na huduma ndogondogo nyingine kama pressure n.k badala ya kutojishughulisha kabisa.

Ni mradi mdogo ila nimeupenda kwani is a free risk and have low operating cost as generally nahjtaji kuwa na:

1. Compressor machine
2. Stand by generator in case of Tanesco power off
3. Water tank 250ltr kwa kuanzia
4. Site/rental

Kwa estimate naweza kusanya zaidi ya 30 thousands per day kwa capital kama ya 2.4millions.

Haya ni mawazo yangu katiki pasua kichwa yangu.

Kwahiyo basi, nawaombeni ushari wenu kuhusu hii idea ya huu mradi kama inamanufaa, vilevile nitafurahi sana kujua maeneo ambayo ni mazuri/location kwa hii shughuli Ubungo, Kimara, Dar es Salaam.

Natanguliza shukrani.

WADAU WENGINE WENYE NIA YA KUENDESHA BIASHARA HII

USHAURI NA MWONGOZO TOKA KWA WADAU

KUANZISHA BIASHARA YA KUOSHA MAGARI
Biashara ya kuosha magari ni mradi wa faida. Iwe una pesa za kutosha kuanzisha biashara kubwa au unataka tu kuanza biashara ndogo na kuweka pesa mfukoni, biashara ya kuosha gari kamwe haikatishi tamaa. Katika chapisho hili, lengo ni kukuonyesha jinsi ya kuanzisha biashara yako ya kuosha gari iwe kama biashara ya wakati wote.

Kuna watu ambao hutumia wakati kuokoa pesa, na kuna watu ambao hutumia pesa kuokoa wakati. Unapoanza biashara ya kuosha magari, kimsingi unalenga watu ambao wanahitaji kutumia pesa kuokoa muda.

Kadiri maisha yanavyozidi kuwa ngumu na jamii zetu zina kasi, sio kila mtu ana wakati wa kuamka asubuhi na mapema na kuosha gari lake kabla ya kuanza majukumu ya kila siku. Hata ikiwa watafanya hivyo, ni kazi kubwa kusafisha eneo la ndani na kuosha matairi yawe safi, sivyo?

Jifunze utaalamu wa kuosha gari
Anza kwa kujifunza kutoka kwa wataalamu. Tembelea huduma yoyote ya kitaalam ya kuosha magari unayojua na ujifunze chochote unachoweza kutoka kwao. Unaweza kujitolea kufanya kazi bure wakati unajifunza.

Pata eneo zuri la kibiashara
Eneo ni muhimu sana kwa biashara ya kuosha gari. Eneo zuri ni nini?

Kwa mwanzo, eneo lako linapaswa kuwa lenye shughuli nyingi na wanaopata mapato ya kutosha ambao wanaweza kumudu kulipia huduma yako. Unakumbuka wakati nilisema unawalenga watu wanaotumia pesa kuokoa muda?

Unatakiwa kuzingatia sana eneo la biashara yako. Watu wanaotembelea maduka ya magari (palipo na mafundi) kawaida wanataka kuosha uchafu kwenye magari yao kabla ya kuendelea na biashara yao. Kwa hivyo, ukipata nafasi karibu na duka la magari ama fundi makenika, unaweza kuwa katika eneo zuri sana kibiashara. Vivyo hivyo kwa maeneo yenye vumbi sana, machafu.

Hakikisha kuna maji ya kutosha
Kuosha gari inahitaji maji, maji mengi. Utahitaji chanzo cha kutosha cha maji, kwa hivyo zingatia kuzingatia kwako eneo. Nimeona watu wanaofungua biashara ya kuosha magari karibu na kijito. Wengine hununua tanki kubwa la kuhifadhi maji na kujaza kila siku.

Ikiwa eneo lako lina kisima cha maji karibu, hiyo inafanya kazi pia. Jinsi ya kupata maji ni juu yako. Jambo moja ninaweza kukuambia ni kwamba hupaswi kuwarudisha wateja wako kwa sababu ya kutokuwa na maji, watakuona kama mtu usiye wa kutegemeka.

Nunua vifaa na vifaa
Jambo moja ninalopenda kuhusu biashara ya kuosha gari ni kwamba unaweza kuianzisha kwa kiwango chochote. Unaweza kuwekeza kiasi kikubwa cha pesa, ikiwa unaweza kuimudu kuanza uoshaji wa kisasa wa magari. Unaweza pia kupata ndoo mbili, kitambaa kimoja na sabuni na kuosha magari ya watu. Njia yoyote unayochagua, utapata pesa ikiwa utatoa huduma nzuri.

Kwa kadiri iwezekanavyo, pata kila vifaa unavyoweza kumudu katika biashara yako. Itaonesha wateja wako unajua unachofanya kweli. Pia utaweza kulipisha ada nzuri kwa kazi yako.

Baadhi ya vifaa hivi ni:
  • Pressure car washer
  • Towels
  • Brushes
  • Chemicals
  • Compressors
  • Conveyor
  • Mobile wash systems, etc

Ikiwa unaweza kununua vifaa hivi tangu unapoanza, sawa. Lakini ikiwa unaanza kidogo, ninashauri uwekeze pesa unayopata kupata vifaa bora kwa biashara yako ya kuosha gari.

Ongeza huduma
Unaweza kuongeza huduma kwa biashara yako ya kuosha gari ili kuongeza mapato. Unaweza kuongeza baa ndogo ili watu wapate kiburudisho wakati wanangojea gari lao. Unaweza pia kuongeza kituo cha kutazama michezo, duka la kubashiri (betting shop), n.k.

Je, ni kazi ya muda tu ama ni ya muda wote?
Kweli, hii inategemea wewe. Ikiwa huna kazi yoyote au biashara kwa sasa, unaweza kuanza biashara ya kuosha gari wakati wote. Usijali, ikiwa unafanya kazi nzuri, hakika itaweka pesa kubwa kwenye mifuko yako.

Ukienda kufanya kazi kwa wakati wote, unaweza kumudu biashara yako jinsi inavyokufaa, unaweza kuanza na mtaji kidogo au usiwe na kama nilivyokwisha sema, na unaweza kufanya kazi peke yako au kuwasimamia wafanyikazi wako moja kwa moja kulingana na kiwango cha biashara.

Ikiwa unapoanza biashara kama kishindo cha upande, utakuwa unaongeza mkondo mkubwa wa mapato. Walakini, utategemea watu wengine kuendesha biashara hiyo, kwa hivyo unahitaji kubuni mfumo / mchakato ambao hufanya iwe ngumu kwao kukudanganya. Kudanganywa ni rahisi sana wakati hausimamii moja kwa moja wafanyikazi wako.

Mwisho
Fanya kazi nzuri. Chukua tahadhari zaidi kulinda magari ya watu na kile kilichomo. Wizi mmoja, kashfa au utovu wa nidhamu utapelekea wateja wako kukukimbia.
 
Good idea mkuu, nina wasiwasi na mtaji kama utatosha.
 
Sawa. Unaweza kuwa mtaji mdogo ila naomba unipe makadirio yako na ukinipa na mfano nitafurahi sana.
 
Mkuu nilipata wazo hilo mapema last month. Nikaenda maeneo ya posta kufuatilia bei ya hizo compressor. Bei ya chini kabisa ni 3,500,000/=. Kwa hiyo jaribu kurekebisha hiyo bajeti.
 
Kama biashara unataka kuifanyia mjini lazima uongeze mtaji ili kuweka huduma ya kisasa zaidi na yenye ushindani.
 
Kwa kuanzia kabla hujafikiria kitu. Piga hesabu ya kuchimba kisima maji..weka kama Million 5 na Generator la umeme Million nyingine 5 na Lease ya eneo at minimum. Kama laki 3 kila mwezi. Baada ya hapo jazia bajeti za lazima na angalia utachukua muda gani ku-break even.

Kutokana na matatizo ya Maji na Umeme. Utavutia wateja kama kama watapata uhakika kwa kusafishiwa magari muda wote. Sio wanachoma mafuta kuja kwako halafu wanakuta vijana wako wanasoma magazeti hakuna maji wala umeme.
 

Mkuu asante kwa mawazo mazuri ya kuwa na sustainable and independent source ya maji lakini kama mradi huu utafanyika DSM maji ya kuchimba kisima yana chumi hivyo hufanya body za magari kuoza (corrosion) yaani kupata kutu (iron+salt=rust)

Hiyo basi lazima utegemee maji ya ruvu toka DAWASCO kwa kujenga underground reservoir tanks au kuweka suspended poly tanks.

Hili ni la kuzingatia sana, pia biashara hii inaweza kuenda samabamba na refreshments au beverages.
 
Ndugu nimefanya utafiti target yako ni kiwango kidgo amapo weye tutakulipa 2500 mpaka 3000 kwa gari na kwa namana mandalizi yako yalivyo , kwako tutaleta gari upukute vumbi wakati tukisubiria siku ya kuosha tukaoshe kikweli kwa wenye viosheo. Unauweka wapi huu mradi wako pale Wami darajani ama? Maana hela yako hii yote itaishia kweneye kunua ma tanki ya maji madogo labda ma2!

Unamiliki gari? Basi nakushauri tembelea car washers hapa Dar uone how serious they are and how this is a serious business amabko kuna shemu ukiambiwa ulipe 50,000/= wala hubishi. Unapeleka gari wanafungua mpaka viti wanavitoa nje wamnalisafisha gari sehemu zote kwa mashine za kisasa ambazo hii 2.4 yako hapa labda itanunua mpira wake wa kurushia maji.

Ina one word nasema JIPANGE. Usilete utani kwenye kazi!
 
Nataka kuinvest Dar, naomba wadau msaada wa mahali naweza fungua car wash Dar ambapo naweza kupata wateja vifaa vyote ninavyo hii biashara ipo ndani ya moyo kuliko fani ambayo nimesomea mpaka chuo.

Kupenda kuosha magari imekuwa ndani ya damu kwani tangu utotoni nilikuwa napenda sana kuosha magari ya baba. Wakati baba alifikiri ananipa adhabu kumbe mm nilikuwa napenda.

Hivyo nimeona nifanye kitu ambacho napenda na nakifahamu. Wadau naombeni msaada wenu. Hii itakuwa ya pili yakwanza stationery nimefungua songea pia ni msaada wenu wanaJF.

THANKS IN ADVANCE
 
Tafuta eneo kuanzia salenda brdge (Ali hassan Mwinyi Road) hadi Mbezi Beach, maeneo ya tangi bovu kuelekea mbele kidogo.

Au maeneo ya msasani na Oysterbay.

Maeneo hayo ndio maeneo yenye watu wanaohitaji zaidi kuoshewa magari na hawajali bei wanajali huduma bora.
 
Mkuu, KIGAMBONI. Hamna Carwash ya maana na kuna watu wengi wanahamia wenye magari ya kifahari na wanauwezo. Fanya survey between Monday-Friday. Jioni wakati wanarudi home kutoka Town. Ukienda weekend utakutana na magari ya watu wanaoenda shamba/Site na beach places haitakupa picha nzuri, ila katikati ya week utapacha picha halisia. Mungu bariki mimi nahamia huko mwakani so I will be u customer too 🙂
 
Duh!

Nasemaga huu u capital sijui nani aliluleta duniani. Niko naosha gari sehemu nimekaa kama masaa mawili.

Nakula supu pemben hapa Sinza nimeona mama mmoja wa kichaga hapa pembeni ya hongera ameshaosha gari zaidi ya 20 hii ni masaa machache niliopo na akila gari ni buku kumi yaani 10,000.

Nimewiwa kukujulisha mwenzangu kama una sehemu nzuri ya biashara na una kile kitu ka kepital ndugu yangu haka kabiashara kanalipa na sidhan kama kanaitaji TRA, yaani tumepaki pembeni tumezagaa kama tunazika msibani kinondoni kumbe unasubiri mwenzio atoke.

Wajasiriamali wa JF pambaneni jamani wakati weni huu baycort iko kwa ajili yenu.

Naihisi bado wanakopesha awa jamaa
 
Unamjua RIZ moja? Anzisha kaaa woshi jijini, kama humjui ndo utamjua.
 
Kumbe Riz zero amemonopilize biashara ya car wash jijini?
 
Hivi waziri wa biashara ni nani, au wa Mazingira, au Tawala za mikoa. Naomba namba ya simu ya mmoja wao nimshauri apige marufuku biashara za kuosha magari kwenye curbs. Ukiingia restaurant kidogo tu ukirudi unakuta huwezi kukanyaga ardhi kufika kwenye gari, mimaji imetanda kila mahali. Wanafanya biashara bila leseni, bila kodi wala usajili, wanaharibu mazingira, wanavuruga mipango miji ya jiji, wanaiba vitu, esp ukikataa kuoshewa. Serikali iko wapi?
 

Kodi yako imekusaidia nini wewe?
 
kodi yako imekusaidia nini wewe?
Ahsante.

Mimi kulipishwa kodi halafu mwingine halipishwi inaniumiza kwa sababu mzigo wa kodi unakuwa mkubwa zaidi.

Tax base ya Tanzania (yani asilimia ya wananchi wanaolipa kodi) ni ndogo mno kwa hiyo kodi na tariffs mbali mbali zinakuwa kubwa. Tunaolipishwa kodi ni wale tulio kwenye uchumi rasmi tu, tunabeba mzigo wa wengine.

Waosha magari ovyo ovyo ambao hawasajili, hawalipi kodi, hawana leseni, wanatuumiza tunaowalipia. Wanachafua mazingira, mimaji kila mahali, wanaharibu mipango miji. Wapigwe marufuku.
 

Inapunguza vibaka!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…