Ushauri namna ya kufanya Service BMW X3

Ushauri namna ya kufanya Service BMW X3

Kama ni hivyo sasa itabidi tununue na ma tool box.....ninachojua mimi nikubadilisha Tyre tu
Sure.. Jinsi unavyokaa nayo na unazidi kuizoea jifunze kufanya baadhi ya vitu mwenyewe.. Itakusaidia sana kupunguza gharama janjajanja..!

Kama kwenye ndoa.. Ukishakaa muda mrefu baadhi ya kesi hakuna kwenda kwa wakwe kushitaki.. Mwenyewe unakuwa Mh. Jaji..!
 
Nilishangaa kabla ya kuwasha break ilikuwa loose! Nikapump ikajaa, nilipowasha ndiyo hiyo haikuzima. Kujaribu kukata kushoto ikawa ngumu. Kama kawaida sikulazimisha nikarejesha kwenye nyumba yake. Nini kifanyike?
Ni,gari gani,kwanza?

Badili oil ya dif kwanza/transfer case kama imechoka. Kama haijachoka basi tia tu mashine ya Diagnosis.
 
Nilishangaa kabla ya kuwasha break ilikuwa loose! Nikapump ikajaa, nilipowasha ndiyo hiyo haikuzima. Kujaribu kukata kushoto ikawa ngumu. Kama kawaida sikulazimisha nikarejesha kwenye nyumba yake. Nini kifanyike?

Mkuu zima switch ya central lock ya 4WD
 
Sijui chochote kuhusu Oils za Atlantic ila BMW najua inataka Castrol na kwenye mfuniko wa engine Oil wamendika.
Mkuu Castrol waliingia mkataba wa marketing na BMW kuwapa promo. Mkataba umeisha, sasa hivi huwezi kuta BMW mpya imeandikwa castrol, cha msingi cheki specs tuu, mfano N52B25 inakubali BMW LL-01: 0W-30, 5W30, 0W-40, 5W-40, depending na mazingira. Kwa bongo 5W-40 itapunguza leakage nyingi sana. Brands depends choice yako, kama Liqui molly, Mobil, BMW Oil, Shell, Total, Atlantic, Castrol, Puma, etc. Binafsi natumia Atlantic Oil, haijawahi niletea changamoto kwenye gari zote.
 
OBD II Scanner ni kale kamashine ka kukuambia matatizo mbalimbali ya gari ata kabla taa ya njano haijawaka kwenye dashboard yako.

Unaweza ukanunua au ukawa unaenda kupima.

Kwa kuanza nakushauri anza kwenda kupima kwa mtu mfano JituMirabaMinne anakupa full report. Maana inakupa summary sana.

Kuhusu namba 4, nakutumia namba za admins inbox.

View attachment 2453685
Mkuu naomba nitumie na mimi namba ya admin inbox. Asante.
 
Tuongee uhalisia kidogo, wewe unafanya haya Kila siku?

Kwa upande wangu mimi sifanyi hayo kila siku kutokana na mazingira yenyewe hasa hiyo ya kulala chini sijui kuangalia chini, na kuhusu vitu vingine Gari inanionesha Kila Kitu kwenye Dashboard Sasa Kuna haja gani ya kufungua Bonnet
Ukitegemea dashboard iko siku utakaanga injini. Hata ndege inachekiwa nje.
 
Ukitegemea dashboard iko siku utakaanga injini. Hata ndege inachekiwa nje.

Usifananishe ndege na gari, taratibu zake za kiusalama ni tofauti sana na kila mtu anajua kwa nini.
Kiuhalisia asilikia 98 ya watu hawafanyi hizo checks kwenye gari kila siku, practically its almost impossible. Wanaoweza hiyo labda ni watu ambao kazi ya ni udereva, gari ndio ofisi yake, hata akipaki tu kidogo unaona hadi anaifuta futa.

Atakaangaje engine akitegemea warning lights, tena gari za Europe??? Temp, oil levels, tyre pressure, sensor malfunctions vyote unaona.
In fact hata gari za mjapan siku hizi zina taa kibao tu.

Nasisitiza tu, kukagua gari physically ni muhimu kila unapopata nafasi
 
Bila shaka ni yule wa karibu na HK Hospital! Yaani hawa jamaa ukienda na vitu vyako, wananuna!

Nishasema humu, kama una Euro make, inabidi ujiongeze haswa kwa suala la kuijua gari yako, nini inataka na wapi utapata vifaa na lubricants. La sivyo utageuzwa gari la mshahara!
Kuna baadhi ya vitu inabidi mmiliki ujiongeze. Mimi gari yangu mambo ya oil nafanya mwenyewe tu napoza elfu 10 kwa ajili ya spana na kupandisha gari juu..
 
Mkuu Castrol waliingia mkataba wa marketing na BMW kuwapa promo. Mkataba umeisha, sasa hivi huwezi kuta BMW mpya imeandikwa castrol, cha msingi cheki specs tuu, mfano N52B25 inakubali BMW LL-01: 0W-30, 5W30, 0W-40, 5W-40, depending na mazingira. Kwa bongo 5W-40 itapunguza leakage nyingi sana. Brands depends choice yako, kama Liqui molly, Mobil, BMW Oil, Shell, Total, Atlantic, Castrol, Puma, etc. Binafsi natumia Atlantic Oil, haijawahi niletea changamoto kwenye gari zote.

Superb!
Ila Castrol ndio imekua Puma baada ya uwekezaji au maana naona kuna containers za Castrol zimebadilika branding yake?

Atlantic nawaelewa sana maana tangu nianza kumiliki viusafiri BMW anakula Atlantic, Mjapani anakula Castrol (zamani ikiitwa BP).

Tofauti na brand hizo siweki[emoji3]
 
Wakuu nimerudi tena, Nadhani mtakuwa mnaniona hapa mara kwa mara Kila nitakapopata changamoto

Juzi kati nilipata safari ya Dodoma nikaenda na Beamer (BMW X3) na ndio ilikuwa kwa mara ya kwanza naenda safari ndefu na hii gari

Wakati naenda muda wa kulifanyia service ulikuwa Bado haujafika zilibaki kama kilometers 1,200 plus nikaenda Dom nikarudi zikabaki kama kilometers 200+ ili zitimie kilometers 3,000 muda wa kufanya service ufike

Sasa Wakati narudi nilivyofika mbezi Taa ya Engine oil ikaniwakia (yellow) nikafika nyumbani, jana nikalipeleka Mikocheni kwa lengo la kuongezwa oil

Mikocheni Coca-cola Garage ya Atlantic lakini nilivyofika jamaa wakanambia kabla ya kuongeza oil itabidi walicheki kwanza kama kuna leakage wakacheki hawajakuta leakage yoyote ila wakanambia itabidi walifanyie Service kabisa maana oil wameikuta ni nzito tofauti na inavyotakiwa (nikakubali)

Waka change Oil na Oil filter Gari ikakaa sawa, nikapewa invoice total ikaja Tsh 483,800,

Ile Quotation Iko hivi

Oil 8 liters 350,000
Filter 60,000

Subtotal = 410,000/=

Vat 18% 73,800

Total = 483,000/=

Swali langu ni kwamba ukilifanyia Gari service na haina leakage yoyote Oil inatoboa hadi next Service au hapa katikati inabidi uiongezee?

Na je kwa situation yangu ya jana ni kweli ilibidi gari lifanyiwe Service au walivutia upande wao wa kibiashara, Wajuzi naombeni mshee experience zenu
View attachment 2453442
Kuna tatizo saana kwenye kuchagua oil sahihi kwa magari used. Mara nyingi kwa gari kama lako, oil recommended inakuwa yenye "viscosity" ndogo. Ila shida iliyopo ni kujua kama mtumiaji wa mwanzo alikuwa anatumia oil ya hivyo ama la.

Kuna kitu kinaitwe "service/maintenance history". Kwa baadhi ya gari tunazoa Japan huwa inakuwepo. Sema imeandikwa Kijapan. Hii ni muhimu saana. Maana kama mtumiaji wa mwanzo alitumia oil ya viscosity kubwa, wewe ukitumia ya viscosity ndogo lazima ipungue mapema.
 
Back
Top Bottom