Ushauri: Nataka nikope 10millions niache kazi serikalini, ili nijiajiri

Karibu sana kwenye haya maisha ya kujiajiri,ni raha mustarehe,fursa zipo kibao,,hakuna cha bosi wala mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Naona kama anachelewa kuja...tena anaingia na mtaji wa mil 10...watu tuliingia bila mia moja na maisha yakaenda....sipendi wanaomtia ujinga eti aendelee kuajiriwa wakati anafanya kazi zake.

kwa mujibu wa vipimo vya mkemia mkuu
 
Tatizo moja ndugu zetu,mukipata pesa nyingi munawaza kufunga Bar.Sasa fikiria vizuri usijemaliza pesa na kazi huna.
Huku nje kusikie tu hivyo hivyo.Na kibaya utakua unasikia kauli kali tu kila siku wakati kibarua huna."Asie fanya kazi na asile"
 
Umenena lililojema ila kama itamchukua 10 yrs kuipata hiyo 10m kwa kazi hiyo anayofanya ni bora atoke fasta achukuwe huo mkopo na a hit the ground like a real man.

kwa mujibu wa vipimo vya mkemia mkuu
 
 
Nakupa akili ndogo sn na ya kijinga sana ambayo nina ushuhuda kbs jinsi mtu wangu wa karibu alivyotoboa kijinga jinga...alikopa m.10,mwezi wa 6 mwaka jana...tupo nae mbeya...akanunua mahindi debe 7500 alinunua debe za 9,500,000 akanunua dawa zA kupuliza kuyahifadhi na gharama ya kuyasafirisha hadi kwake sowetto kutoka mbeya vijijini alitumia 100,000/- akaweka store hadi mwezi wa kumi na moja kati kati akauza kwa debe moja 16,000/- bei ya jumla kipindi ambacho sokoni debe la mahindi nin18,000/- akapata zaidi milion 18 +...kwa uoga wake akalipa deni bank akanunua kiwanja halafu mwaka huu ameshindwa ht kuweka debe mbili store...kama unaogopa hela huwezi kuipata naukiipata haikai...na siku zote elimu yako ndo umasikini wako linapokuja swala la biashara...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu niambie ni biashara gani hiyo nianzishe na mimi kama hutojali?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maamuzi yoyote unayofanya kutokana na pesa inayopita mikononi mwako yanaweza kukufanya kuwa tajiri ama masikini.

Pesa yoyote inayopita mikononi mwako iwe ya ku save ama kukopa inaweza kukufanya kuwa masikini ama tajiri.

Maamuzi yoyote unayofanya iwe kuajiliwa ama kujiajili yanaweza kukufanya kuwa tajiri ama masiki.

Pesa sio msingi wa mafanikio ni kifaa kinachokusaidia kufikia mafanikio ama malengo yako.

Hatuachi kazi kwakua tuna mtaji wa kufanya ama tunapenda kuajili wenyewe. Tunaacha kazi wakati tunapoona muda tunaoutumia kumzalishia boss ni mwingi kuliko muda tunaoutumia kuzalisha vyakwetu binafsi. Unapoona mshahara kwa mwezi ni sawa na faida unayoipata kwa ulichokianzisha wakati unatumika kotekote.

Ushari wangu.
Usikope 10mil, kopa 6mil tu baada ya miezi mitatu pima faida unayoipata kutokana na uwekezaji wa 6mil. Tathimin Kama inalingana na mshahara au lah! Ukiwa smart itakuwa zaidi ya mshahara wako.

Asante

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakushauri usiache kazi,mara upatapo huo mkopo tafuta mtu mwamininifu umuajiri aweze kuendesha biashara yako,au tafuta business partner,wewe uwekeze kwenye mtaji na yeye awekeze kwenye nguvu kazi,mara baada ya kuona matokeo chanya ndio uache kazi.
Pole sana kusikia unachoka sana na ukirudi nyumbani wewe ni kulala tu? Vipi humpi huduma yake shemeji? Au majirani wanakusaidia kuhudumia.
Jiajiri mkuu uwe huru bhana!

kus
 
Acha Kazi haraka,mafanikio ni imani.Utapigika sana tu ila usikate tamaa,jambo moja tu fanya saving ya mishahara yako ukipata pesa kiasi fulani cha kutosha kuanza biashara yako anza,mkopo achana nao kwanza,wingi wa pesa sio mafanikio.wazo lako na jinsi utakavyo litekeleza ndio litakalokufanikisha start small with Mtaji kidogo utafanikiwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Safi sana ndugu ushauri wako ni mzuri sana,huwezi kuanzisha biashara ukamuweka mtu aifanye tena ikiwa changa itakufa tu........namshauri mleta mada aache kazi mara moja akiwa na hiyo mil.10 aanze biashara na hela kidogo asiiweke yote aweke kidogo ikifeli atakuwa amejifunza ataweka tena ..........kufanya biashara ukiwa umeajiriwa ni kujidanganya tu na kupoteza nguvu pesa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mawazo finyu sana haya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Safi sana ushauri mzuri sana huu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha kumuogopesha mwenzako wewe kila mtu ana njia yake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We jamaa bhaaana... unaishi mfumo wa elon musk...
Embu jiongeze kidogo.... uwe unaangalia nyanja zoote... mada.. mazingira ya kazi... kipato.... n.k

Haya uyo elon musk na masaa yake 17 anaringana na mlinz wa duka la wahindi masaaa 24...

We tulia acha uoga... risk taking ndio njia nyepesi ya mafanikio....


Sent from "La -Vista"
 
Hii mikazi ya serikalini hatuwezi kutoka baadhi ya wakubwa kwenye hizi ofisi Wana roho mbaya ukipata chance itumie ila kabla hujaacha hakikisha una biashara ya kueleweka, sio lazma kazi ndio ufanikiwe ni uoga wetu tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…