USHAURI: Ni vema tukajenga utamaduni wa kujisomea vitabu na kuwajengea watoto utaratibu huo

Pamoja na kwamba nakubaliana na wewe katika mambo mengi kuhusu hoja yako, naomba pia kukumbusha kuwa siyo masikini tu wanaopenda udaku na umbeya. Ndiyo maana hata hao unaowasifia wamebobea katika udaku na umbeya.
ni dhahiri kuwa nchi nyingi za africa na baadi nje ya africa,asilimia kubwa ya watu hutumia mda mwingi kuangalia television,kusoma magazeti ya udaku,na mambo yasiyo yamsingi.pia mimi nilishakuwa na tabia hiyo wakati nikiwa kidato cha pili,lakini baada ya kuona hayana msingi sana ,basi nkaanza kuwa na utaratibu wa kujisomea vitabu vya ziada na kupata kujua mengi kwa kadiri nilivyoweza kupata maarifa kwenye vitabu hivyo,sasa ni mda wa kuyafanyia kazi yale niliyo jifunza,nabado naendelea kujifunza kila siku.
 
You're very right. I like reading, though sometimes i find it like am doing too much. I remember in those old days when I wasn't able to have a book of my own, then i'd pick up any piece of paper I may become across with even when walking along the dirty street! I'd pick it up and find out what's written...and you know what? true, know what to read because it's this kind of picking anything and read that made me to be a great fan of Arsenal though at least, am among of the few who can answer why they became Man U fans, or Arsenal Fans and so on! But even more important, I like reading contradicting ideologies; and in fact, sometimes the one that's different from what I believe!
 


Ha ha haaa understood.......
 

wazo zuri sana!!! ila tunaomba uweke walau majina ya hivyo vitabu...sio kwaajili ya watoto tu bali hata wakubwa!!!
 
Kidato cha pili ni balaa kwa asilimia kubwa ya wanafunzi maana ndio baleh zone.

Usomaji wa vitabu ni muhimu maana unajifunza mengi sana katika kusoma, tabu iliyopo how can we stay to read books wakati ratiba ya chakula haieleweki?

Wengi wetu tunafuatilia kwanza suala la msosi kwanza baada ya hapo mambo mengine yanafuatia. Ukiweza kusoma soma maana humo utagundua mambo mengi sana.
 
ukitaka kumfichia mtu mweusi hela weka kwenye kitabu...

Huwa inaniumiza sana "Mtu Mweusi" anapokashifiwa kwa umoja wake (collectively) hasa anapokashifiwa na "Mtu Mweusi" mwenzie. Kama "Mtu Mweusi" anamkashifu hivi "Mtu Mweusi" mwenzake, Wahindi na Makaburu wafanyeje?

Sio kweli kuwa "Watu Weusi" hatusomi Vitabu, tupo tunaosoma na tuna Maktaba za Vitabu Majumbani, tuna Uanachama kwenye Maktaba za Taifa ambako tunakwenda kujisomea!
Unataka kukashfu? Kashfu Wahindi, Makaburu na Waarabu, tafadhali!
 
Must read books for health of your mind.
1.how to stop worying and start living.by dale carnegie
2.the magic of thinking big..by DR david schwartz
3.rich dad,poor dad by robert kiyosaki..
 
Wandugu wakati tuliopo sasa unaitwa information age.

Bila kujisomea hii age itatusumbua sana.

Ilikushindana nayo lazima tuwe watu wa kujisomea na tabia ya kuujisomea huanzia nyumbani.

Mimi ni msomaji sana wa vitabu na credit zote nampa mama yangu. Maza ni la saba na anakazi ya kima cha chini lakini ni mtu anapenda sana kujisomea.

Nyumbani kulikuwa na vitabu kama mwanamalundi, kikosi cha kisasi, tutarudi na roho zetu, dunia uwanja wa fujo, abunuasi, adili na nduguze na vingine vingi na magazeti mengi tu.

Kwa hiyo kitu cha kwanza hakikisha vitabu vipo nyumbani. Watoto ni wadadisi watasoma tu, sasa wewe umejaza bongo movie na series za kikorea halafu unaona ufahari, kabati zima na hamna hata kitabu kimoja.

Dingi hujawahi hata kurudi na gazeti we unarudi na merlin, legend of the seeker na mambo kama hayo unafikiri watoto watapenda kujisomea?

Kama wewe uko hivi nakushauri uchonge shelf la vitabu na uanze kununua vitabu, mbona bei ni sawa na series za jaki bawa.

Jambo la pili ni wewe pia kuweka mfano kwa kujisomea, hata kama haupendi just do it for the sake of your children. Usitegemee wanaokupenda kujisomea wakati wewe mwenyewe ni mtu wa Isidingo na la Mujer.
 
ujumbe mzuri ila umekosea pale ulipojiona bora sana ukaita wengine "pumbavu" ukasahau kuwa wewe unapenda kusoma kwa sababu mama yako alikupa hiyo fursa kwa kuleta vitabu nyumbani. Pengine hawa "wapumbavu" mama zao walikuwa wakijaza kanda za kwaya kama mama yangu. Matokeo yake na mimi nimejikuta napenda kuimba na mtoto wangu nampeleka kwaya ya watoto!
 
sio lazima kusoma vitabu, hata movies pia zinaweza kukontein vitu vilivyoandikwa kwenye vitabu ukizingatia vyote ni kazi ya sanaa
so interest ndo inamfanya mtu achague kati ya movies na vitabu, usilazimishe......
 
Imethibitika vitabu ni bora zaidi, maana inaruhusu akili kujenga taswira yake yenyewe, movie zinalazimisha taswira, na pia hujenga memory na uvumilivu, achana kabisa kuwazoesha watoto movie na TV, atakuwa kopo na kuzoea ku flip flip , no concentration at all

sio lazima kusoma vitabu, hata movies pia zinaweza kukontein vitu vilivyoandikwa kwenye vitabu ukizingatia vyote ni kazi ya sanaa
so interest ndo inamfanya mtu achague kati ya movies na vitabu, usilazimishe......
 
kwanza sio lengo langu kutukana, pili upumbavu ni upumbavu hata kama umesababishwa na kutoenda shule sababu wazazi walikuwa hawana uwezo. yaani hakuna sababu nzuri ya kufanya upumbavu usiwe upumbavu.
 
na vitu vya kuona, kusikia na kusoma hutafsiriwa katika sehemu tofauti ubongoni. ni kazi ngumu kimoja kuwa mbadala wa kingine. huwezi sema badala kusikiliza wimbo ngoja niusome!.
 

inategemea na mtoto wako na movies anazoangalia, kuna nyingine zina mpa courage, kujiamini na zinamfanya mtoto awe na ndoto, hata movies ni bora pia
 

Word....!! Strong argument.
 
inategemea na mtoto wako na movies anazoangalia, kuna nyingine zina mpa courage, kujiamini na zinamfanya mtoto awe na ndoto, hata movies ni bora pia
hatujasema movie ni mbaya cha muhimu ni kuwa balanced. huwezi kujaza DVD kwenye kabati na nyumbani huna hata vitabu vitatu!. watoto watakuwa mbumbumbu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…