Ushauri: Rais Samia, kwenye teuzi za DED's na DAS's ifae sana watoke kwa Maafisa Elimu Kata (AEK's) wenye sifa wapo wengi

Ushauri: Rais Samia, kwenye teuzi za DED's na DAS's ifae sana watoke kwa Maafisa Elimu Kata (AEK's) wenye sifa wapo wengi

balimar

JF-Expert Member
Joined
Sep 18, 2015
Posts
7,743
Reaction score
13,657
Salaam!

HALMASHAURI ndio Ofisi pekee zinazotekeleza Sera na Utendaji wa siku kwa siku wa serikali hasa zile za Mitaa. Kiukweli Maafisa Elimu Kata ndio wanayo mawanda mapana sana kwenye kusimamia shughuli za serikali anzia taaluma kwenye kata zao, miradi ya ujenzi wa majengo ya serikali na kuhamasisha Maendeleo huko Katani na uzoefu wa kushawishi wananchi kwenye Maendeleo kitu ambacho ni Adimu sana kwa sasa.

Uzoefu huo adimu sana wanajua namna ya kusimamia hasa miradi, waajiriwa wa serikali (walimu) shule za Msingi na Sekondari na mwisho ni ule uzoefu walionao kukaa hata maeneo ya vijijini kabisa ambapo Maafisa wengine hawawezi. Hawa ni field officers kweli kweli.

Tatizo la kuwa Maafisa Elimu Kata ni kukosekana kwa Magodfather (tabia inayoota mizizi nchi hii) na watu wa kuwasemeasemea. Lakini kama Madam SSH atapitia uzi huu, hakika hutojuta kuwachagua maafisa hawa kwani wana uwezo mkubwa na wana nidhamu sana za kiutumishi. Kwahiyo kazi ni yake kuwaibua ili wamsaidie kazi na hatimae HALMASHAURI zipae kimaendeleo.

Hivyo, Ofisi za teuzi zikiwa makini Maafisa Elimu Kata ni 'recruiting post' kwa nafasi yoyote ya DED au DAS kwenye ngazi ya halmashauri.

Kila la kheri Madam SSH!
 
Salaam!

HALMASHAURI ndio Ofisi pekee zinazotekeleza Sera na Utendaji wa siku kwa siku wa serikali hasa zile za Mitaa. Kiukweli Maafisa Elimu Kata ndio wanayo mawanda mapana sana kwenye kusimamia shughuli za serikali anzia taaluma kwenye kata zao, miradi ya ujenzi wa majengo ya serikali na kuhamasisha Maendeleo huko Katani na uzoefu wa kushawishi wananchi kwenye Maendeleo kitu ambacho ni Adimu sana kwa sasa.
Huku kwetu maafisaelimu Kata Wana elimu ya diploma utawapeleka wapi? Mama anatakiwa awakumbuke na kuwateua wale wote wamama waliotia Nia kugombea ubunge na kukosa tena ni watumishi wa umma.
 
Huku kwetu maafisaelimu Kata Wana elimu ya diploma utawapeleka wapi? Mama anatakiwa awakumbuke na kuwateua wale wote wamama waliotia Nia kugombea ubunge na kukosa tena kwenye title
Kwenye thread yangu nimelizingatia sana hilo

Elimu na swala la Msingi

Maana ya Afisa Elimu Kata maana yake lazima aanzie DEGREE na kuendelea

Wapo Maafisa Elimu kata wana Masters mpaka PhD

Tatizo ni kutotambuliwa kwa hawa jamaa ila uwezo wanao na ndio 'hub' huko katani kwenye maendeleo

Mtu anaeweza kuendesha kata kimaendeleo hawezi kushindwa kuendesha HALMASHAURI

Wanao weredi mkubwa sana ila uzoefu na elimu zao ndivyo vizingatiwe naamini watamsaidia sana Rais

Kimsingi wana 'Peculiar Character (PC)'
 
Dah nchi ngumu hii. MAMA TEUA HARAKA HUKU MITAANI NAZI NA MAYAI YA KIENYEJI YAMEADIMIKA.

Watu wanaroga balaaa!
 
Nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya (DED) ni kubwa sana.haendi kusimamia elimu tu, mirandi ya maendeleo ya elimu Bali uchumi na fedha za halmashauri, Afya, Maji, Mazingira, kilimo etc. Hivyo inahitaji mtu mwenye uelewa mpana na kumbuka anasimamia watu zaidi ya 2000 waajiriwa wa Wilaya.

Sasa ukikosa ueledi, busara, hekima ubunifu na uelewa wa Mambo kwa upana wake. Wale walioko Chini yako watafanya lolote kukuharibia na maendeleo kwenye Wilaya yako yatakuwa zero na kila Mara utapata hati chafu.

Hivyo afisa elimu kata hawana uzoefu huo sorry to say this. Ni wachache Sana 1 Kati ya 10,000 wanaweza kuhimili nafasi ya ukurugenzi Wilaya.

Hivyo waendelee kuandaliwa wapandishwe vyeo Hadi ukuu wa idara wapewe nafasi za kukaimu nafasi za ukurugenzi ili kupata uzoefu mwisho wapatiwe nafasi.

Nakataa Katukatu wao wasio na uzoefu Kama maafisa kata kupewa nafasi za ukurugenzi.

Kuna wakuu wa idara na other senior officers kwenye kila Wilaya watizamwe hao wenye sifa Bora, naamini wanaweza kuwa DAS au Wakurugenzi na siasa ziwekwe pembeni maana hizi ni nafasi za utendaji sio siasa.
 
PhD zenyewe unazungunzia kutoka chuo gani?
Ninachofahamu mtu akiwa Awarded PhD ni Dr. huyo kama Madelu, Kakulwa et. al

Sasa title ya Chuo sio inshu kwasababu kichwani kwake ana maarifa ya PhD

Mi nimejikita sana kwenye uzoefu wao wa kufanya kazi kwenye serikali za mitaa na uwezo wao kuhimiri mikiki ya vijijini na kutembea site ukilinganisha na field nyingine

Kama tunataka watu wenye uwezo wa ufuatiliaji basi Maafisa Elimu Kata ni wenyewe

Mfano mdogo tu ni miradi ya EquipT na sasa Sequip. Majengo yale wao ndio 'focal person'

Hawa watu ni hazina kwa taifa hili ila wa kuwasemea semea ndio hawapo na Elimu sio kigezo pekee cha Utendaji kazi isipokuwa Uzoefu ndio kigezo cha Msingi
 
Ninachofahamu mtu akiwa Awarded PhD ni Dr. huyo kama Madelu, Kakulwa et. al

Sasa title ya Chuo sio inshu kwasababu kichwani kwake ana maarifa ya PhD..
Kama kuna afisaelimu Kata mwenye PhD ya chuo kikuu Cha DSM anyooshe kidole na aseme Yuko Kata gani Tanzania. Tutampigia debe ateuliwe. Pia elimu yake asiwe ameunga unga.
 
Salaam!

HALMASHAURI ndio Ofisi pekee zinazotekeleza Sera na Utendaji wa siku kwa siku wa serikali hasa zile za Mitaa. Kiukweli Maafisa Elimu Kata ndio wanayo mawanda mapana sana kwenye kusimamia shughuli za serikali anzia taaluma kwenye kata zao, miradi ya ujenzi wa majengo ya serikali na kuhamasisha Maendeleo huko Katani na uzoefu wa kushawishi wananchi kwenye Maendeleo kitu ambacho ni Adimu sana kwa sasa.
Mbona Afisa Elimu Kata (AEK) ni chini sana..? Umewaruka DEO's
 
Nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya (DED) ni kubwa sana.haendi kusimamia elimu tu, mirandi ya maendeleo ya elimu Bali uchumi na fedha za halmashauri, Afya, Maji, Mazingira, kilimo etc. Hivyo inahitaji mtu mwenye uelewa mpana na kumbuka anasimamia watu zaidi ya 2000 waajiriwa wa Wilaya.

Sasa ukikosa ueledi, busara, hekima ubunifu na uelewa wa Mambo kwa upana wake. Wale walioko Chini yako watafanya lolote kukuharibia na maendeleo kwenye Wilaya yako yatakuwa zero na kila Mara utapata hati chafu.

Hivyo afisa elimu kata hawana uzoefu huo sorry to say this. Ni wachache Sana 1 Kati ya 10,000 wanaweza kuhimili nafasi ya ukurugenzi Wilaya.

Hivyo waendelee kuandaliwa wapandishwe vyeo Hadi ukuu wa idara wapewe nafasi za kukaimu nafasi za ukurugenzi ili kupata uzoefu mwisho wapatiwe nafasi.

Nakataa Katukatu wao wasio na uzoefu Kama maafisa kata kupewa nafasi za ukurugenzi.

Kuna wakuu wa idara na other senior officers kwenye kila Wilaya watizamwe hao wenye sifa Bora, naamini wanaweza kuwa DAS au Wakurugenzi na siasa ziwekwe pembeni maana hizi ni nafasi za utendaji sio siasa.
Nakubaliana na wewe kwenye baadhi ya mambo ila kuna mengine sikubaliani kabisa na wewe

Mosi, hawa jamaa ni watendaji wakuu kwenye HALMASHAURI mfano miradi mingi mtambuka kama miradi ya Tasaf, ujenzi wa madarasa, usimamizi wa rasilimali watu, kuhamasisha maendeleo, kushiriki mazoezi ya kitaifa kama vile SENSA, uchaguzi, mwenge n.k ni uzoefu adimu sana kupata kwa masenior wanaokaa Ofisini hawajui mambo mengi

Mbili, Maafisa Elimu Kata wananyumbuka sana kutokana na nafasi zao. Ni kweli Mkurugenzi na Katibu utawala wa Wilaya ni nafasi zinazotakiwa unyumbukaji sana maana anadeal na zaidi ya Idara moja. Maafisa hawa kwa uzoefu wanaoupata wanaweza kuicheza ngoma hii kwa ufasaha kwani karibuni mazoezi mengi yanayofanywa na serikali kwenye ngazi ya jamii wanashiriki moja kwa moja.

Ukiachana na mambo mengine, hawa jamaa ni seniors kwenye idara zao. Maana yake walishatumika sana kwenye nafasi ya ualimu, ukuu wa shule na hatimae wamekuwa Maafisa Elimu kata. Kiukweli inahitajika upembuzi wa kina lakini hawa jamaa wanaweza na wenye sifa wapo isipokuwa wa kuwapigia debe ndio hawapo
 
Usinikumbushe Deo ( afisaelimu secondary) wa Halmashauri ya meru Huku Arusha , hata kuandika barua ya kuomba kazi kwa kiingireza hawezi. Sijajua alisoma wapi na ana elimu gani.
HaahhHahahhhaa.... Kwani unadhani Prof. Assad alikosea kusema vile??
 
Kama kuna afisaelimu Kata mwenye PhD ya chuo kikuu Cha DSM anyooshe kidole na aseme Yuko Kata gani Tanzania. Tutampigia debe ateuliwe. Pia elimu yake asiwe ameunga unga.
Mkuu wangu hii sentensi ni general sana

Elimu yake isiwe ya kuunga unga una maanisha nini?
Civil servant lazima awe anaunga unafanya kazi unaenda kusoma unafanya tena kazi unaenda kusoma hawa wana uzoefu kulikoni hao wa 'one way'

Pili, sitegemei kuwa PhD inatolewa Udsm peke yake nchi hii. Wapo baadhi ninaowajua ni PhD candidates na Masters sio Udsm tu na vyuo vingine

Mwisho lakini si kwa ulazima, nadhani wapimwe mchango wao kwenye utumishi wa umma na kuonekana wanafaa wateuliwe na sio vimemo weee kila uchao

Serikali hasa Ummy Mwalimu anajua honourable contribution kwenye maendeleo kutoka kwa hawa watu

Nadhani time is due and the available vaccant is theirs
 
Kwenye thread yangu nimelizingatia sana hilo

Elimu na swala la Msingi

Maana ya Afisa Elimu Kata maana yake lazima aanzie DEGREE na kuendelea

Wapo Maafisa Elimu kata wana Masters mpaka PhD

Tatizo ni kutotambuliwa kwa hawa jamaa ila uwezo wanao na ndio 'hub' huko katani kwenye maendeleo

Mtu anaeweza kuendesha kata kimaendeleo hawezi kushindwa kuendesha HALMASHAURI

Wanao weredi mkubwa sana ila uzoefu na elimu zao ndivyo vizingatiwe naamini watamsaidia sana Rais

Kimsingi wana 'Peculiar Character (PC)'
Ni sawa
 
Mbona Afisa Elimu Kata (AEK) ni chini sana..? Umewaruka DEO's
Nimeainisha majukumu wanaofanya kila siku na nafasi iliyopo

DEO ni specific kwenye Elimu unlike Afisa Elimu Kata (AEK)
 
Back
Top Bottom