Ushauri: Rais Samia na wapinzani, kubalini kuelewana kwenye hili la Katiba Mpya

😀😀😀😀😀😀😀

Huu ni uongo takatifu hahahahaahahah.

🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Katiba mpya haiwezi kuja pasipo kuwa na maelewano baina ya pande mbili, hivyo basi chama tawala na vyama pinzani vikae vielewane kila kitu kitakuwa sawa. Nawasalimu kwa jamuhuri ya muungano.
 
Lazima akimbie
You Chadema guys are very low kwa kweli.

Hivi hizi hekaya mnakuwa mnasimuliana ili mchekeshane tu au kufurahisha genge??? Hahaahahahahahahahahaha

Kwamba Mheshimiwa rais lazima akimbie???

😀😀😀😀😀😀
 
Haizuiliki, ni ajenda ya wananchi. Mheshimiwa rais awe makini na akubali maelewano, vyama vya upinzani wamempa mkono wa heri kwa kuomba kukutana naye lakini amejikausha mpaka sasa.
Kumbe na wewe hueleweki unaongea kishabiki.

Kwenye bandiko kuu unasema ngwe hii ya kwanza katiba kupatikana ni ngumu halafu kwenye post hii unasema haizuiliki.

Unafuata tu mkumbo kama NYUMBU sio??
 
Katiba mpya haiwezi kuja pasipo kuwa na maelewano baina ya pande mbili, hivyo basi chama tawala na vyama pinzani vikae vielewane kila kitu kitakuwa sawa. Nawasalimu kwa jamuhuri ya muungano.
Kazi iendelee......

Mkuu unajua kwamba hapa nchini CDM ndio wanajiona wao ndio "Vyama pinzani "???

Yaani kwao wao NCCR na ACT na CHAUMA wote ni CCM??
 
Wanakwambia ni haki ya wananchi kudai katiba 😅 na ipo kisheria ila wao wanakosa lugha ya staha tu wanataka kutukana na kushurutisha mamlaka
 
Kumbe na wewe hueleweki unaongea kishabiki.

Kwenye bandiko kuu unasema ngwe hii ya kwanza katiba kupatikana ni ngumu halafu kwenye post hii unasema haizuiliki.

Unafuata tu mkumbo kama NYUMBU sio??
Nachokisema ni muhimu kwa rais kukutana na wapinzani, sisemi kuwa ni lazima katiba upatikane ndani ya awamu hii.

Hii ya kuwapuuza ndiyo inawafanya waanze kuwa na mashaka na matokeo yake inaleta vita majukwaani.

Wanaweza kukutana na kuelezana kwa uwazi na ukweli kuwa mchakato utaanza baada ya uchaguzi 2025, na pia walau Mh. Rais akakubali kuifanyia maboresho sheria ya uchaguzi.
 
Kazi iendelee......

Mkuu unajua kwamba hapa nchini CDM ndio wanajiona wao ndio "Vyama pinzani "???

Yaani kwao wao NCCR na ACT na CHAUMA wote ni CCM??
Lakini bila kupepesa macho huo ndio ukweli, ACT ilianzishwa kama CCM B, na NCCR mageuzi ilianzishwa na TISS. CUF iliyokuwa moto nayo tayari ilishaingiliwa na CCM na kufa rasmi.
 
Kwani rais si amesema atakutana nao!!! Au mnachotaka ni lazima iwe ndani ya wakati mliopanga nyinyi??

Halafu, rais akikutana na NCCR ACT na CHAUMA na CDM wote kwa pamoja si itatosha?? Maana kukutana na mmoja mmoja inaweza kuwa ngumu kwa sababu ya ratiba za rais, protokali na mambo ya COVID-19.

Halafu ni kipi kinachokwambia kwamba amewapuuza??? Si unajua kwamba mama hajafikisha hata miezi minne madarakani??

Halafu pia inaonekana hata akikutana na Chadema hakuna kitakachokuwa na wala asipoteze her valuable time maana Chadema wanam-regard mama kama Magufuli wa kike. Wewe unaonaje mkuu???
 
Hapo kwenye lugha za maudhi wengi wamewashauri waache lakini naona ndio utamaduni wa CDM.
Hata mimi sipendezwi na baadhi ya kauli za CDM.
 
Wanasema ni agenda ya wananchi, hahahaahahah wananchi wapi?? Hawa si wamekataliwa nchi nzima juzi tu kwenye sanduku la kura? Hata mbunge mmoja hawajapata hahahahahaah
Wananchi kwa sasa wanahitaji stable income,huduma za afya,maji,umeme,barabara na elimu za uhakika ndio hayo mengine yatafuata wakishashiba.
 
Wanasahau Tzn sio Marekani wala Kenya kila nchi inautamaduni wake wa kutafsiri uhuru kwa mujibu wa sheria,utamaduni na mazingira.

Rais alisema wakosoe kwa staha na wawe constructive sio kutukana na kumdharirisha hayo ni matumizi mabaya ya Uhuru.

Hakuna haki bila wajibu wala uhuru usio na mipaka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…