Tipstipstor
JF-Expert Member
- Nov 29, 2021
- 1,528
- 3,352
Ahlan Ahlan bik
Habari zenu wana Jf, wadau wa soka na wapenzi wa wana lunyasi, giants of Africa, Simba Sc.
Jana nilipata safari kidogo kutoka Bergamo kwenda katika jiji la bandari, Piraeus nchini ugiriki .Jiioni nikiwa naitazama bahari ya meditterenian katika kitongoji cha Freattyda nikawa nawaza kuhusu maendeleo na mabadiliko ya soka ya klabu yangu pendwa barani Afrika nayo si nyingine zaidi ya Simba Sc.
Simba Sc inabidi tufanye mabadiliko ya sera zetu hususani katika suala la kiufundi.Sina shaka hata kidogo juu ya weledi wa watu wanaofanya kazi katika utawala.Nazungumzia mkurugenzi mtendaji ,CEO mheshimiwa Barbara Gonzalez na wanabodi wote wa simba. Suala kubwa la kwanza linalohitaji mabadiliko ni katika Scouting team yetu ,jinsi gani tunasaka wachezaji wa kuweza kuivusha simba kimataifa.
Inanipa wasiwasi sana kuona klabu changa kama Singida big stars inaweza kuleta wachezaji mahiri sana kutoka taifa la brazil kuja kuichezea timu isiyojulikana barani Africa huku sisi tukistruggle kupata wachezaji wa maana. Hili liangaliwe mno.Uwekezaji unaofanyika simba ni mkubwa hivyo lazima kazi ya scouting team ifanywe kwa jicho la mwewe katika kuleta wachezaji watakaoipa thamani simba.
Pili, ni kuhusu usajili wa makocha na wachezaji, tujenge utaratibu wa kuhakikisha pindi tunamtimua kocha na kuleta kocha mpya basi tumpe nafasi ya kuteua benchi lake zima la ufundi.Wengi tunapiga kelele kuwa tunataka chemistry ya wachezaji uwanjani ila tunasahau kuwa makocha pia wanahitaji chemistry!! Muunganiko ambao utawawezesha kufanya kazi kwa ufanisi wa hali ya juu.
Makocha wakubwa wote wanapopewa kazi katika timu huku barani ulaya huwa na kawaida ya kuchagua timu ya makocha watakaofanya nao kazi na ni jukumu la klabu kuwapa mikataba ili wamsaidie kocha mkuu ila kwa huko Tanzania hali ni kinyume kabisa unakuta kocha anasajiliwa na timu halafu anapangiwa watu wa kufanya kazi nae.Ni sawa umchukue pisi kali ya kigiriki hapa Athens halafu uilete huko tanzania uilishe ugali au makande..it won't work out!! Vyakula vya hapa ugiriki ni tofauti na vya huko bongo ,atalazimika tu kula ikiwa hakuna chakula kingine ili asife njaa ni sawa na hawa makocha tunaowaleta.
Tuhakikishe kuwa tunawapa nafasi ya kuchagua watu wa kufanya nao kazi na pia tuwape muda atleast misimu miwili tuone nini wanaweza kuifanyia klabu yetu pendwa na ikitokea hatujaridhishwa nao basi tunatimua benchi lote la ufundi.
Sio kocha unamtoa serbia halafu msaidizi unampangia ni lazima awe Matola (mtanzania), hawafahamiani hata falsafa zao za ufundishaji n.k halafu unataka kikosi kiwe na chemistry ndani ya wiki mbili ili hali hao makocha wenyewe wanaweza kukaa miezi miwili hawaelewani falsafa zao.
Tatu, ni lazima kocha apewe nafasi ya kurecommend ni wachezaji gani anawahitaji katika kikosi chake, haiyumikiniki unamleta kocha halafu wachezaji unasajili tu bila ya matakwa ya kocha.Unakuta kocha anahitaji mshambuliaji mrefu ili aendane na falsafa yake ..kwa maana anaweza kumsaidia hata kwenye kudefend set pieces ila timu inasajili striker mfupi kama kichuya ambaye hata hawezi kuruka juu ku-win aerial duels. Management ya klabu iache kusajili kwa mihemko ,inabidi impe nafasi kocha ajiridhishe kwanza iwapo huyo mchezaji anayetaka kusajiliwa ataisaidia klabu ama laa.
Mwisho kabisa napenda kutanguliza shukrani zangu kwa uongozi wa simba ,benchi la ufundi na wachezaji kwa ujumla kwa ushindi wa kwanza katika ligi kuu ya NBC. Tumpe ushirikiano kocha Zoran Maki na wachezaji wajitume waache makundi.
Sio kwasababu Kocha Zoran kakataa baadhi ya wachezaji ndio hao waliobaki wacheze chini ya kiwango ili tu wamtengenezee kocha mazingira ya kufukuzwa.
Habari zenu wana Jf, wadau wa soka na wapenzi wa wana lunyasi, giants of Africa, Simba Sc.
Jana nilipata safari kidogo kutoka Bergamo kwenda katika jiji la bandari, Piraeus nchini ugiriki .Jiioni nikiwa naitazama bahari ya meditterenian katika kitongoji cha Freattyda nikawa nawaza kuhusu maendeleo na mabadiliko ya soka ya klabu yangu pendwa barani Afrika nayo si nyingine zaidi ya Simba Sc.
Simba Sc inabidi tufanye mabadiliko ya sera zetu hususani katika suala la kiufundi.Sina shaka hata kidogo juu ya weledi wa watu wanaofanya kazi katika utawala.Nazungumzia mkurugenzi mtendaji ,CEO mheshimiwa Barbara Gonzalez na wanabodi wote wa simba. Suala kubwa la kwanza linalohitaji mabadiliko ni katika Scouting team yetu ,jinsi gani tunasaka wachezaji wa kuweza kuivusha simba kimataifa.
Inanipa wasiwasi sana kuona klabu changa kama Singida big stars inaweza kuleta wachezaji mahiri sana kutoka taifa la brazil kuja kuichezea timu isiyojulikana barani Africa huku sisi tukistruggle kupata wachezaji wa maana. Hili liangaliwe mno.Uwekezaji unaofanyika simba ni mkubwa hivyo lazima kazi ya scouting team ifanywe kwa jicho la mwewe katika kuleta wachezaji watakaoipa thamani simba.
Pili, ni kuhusu usajili wa makocha na wachezaji, tujenge utaratibu wa kuhakikisha pindi tunamtimua kocha na kuleta kocha mpya basi tumpe nafasi ya kuteua benchi lake zima la ufundi.Wengi tunapiga kelele kuwa tunataka chemistry ya wachezaji uwanjani ila tunasahau kuwa makocha pia wanahitaji chemistry!! Muunganiko ambao utawawezesha kufanya kazi kwa ufanisi wa hali ya juu.
Makocha wakubwa wote wanapopewa kazi katika timu huku barani ulaya huwa na kawaida ya kuchagua timu ya makocha watakaofanya nao kazi na ni jukumu la klabu kuwapa mikataba ili wamsaidie kocha mkuu ila kwa huko Tanzania hali ni kinyume kabisa unakuta kocha anasajiliwa na timu halafu anapangiwa watu wa kufanya kazi nae.Ni sawa umchukue pisi kali ya kigiriki hapa Athens halafu uilete huko tanzania uilishe ugali au makande..it won't work out!! Vyakula vya hapa ugiriki ni tofauti na vya huko bongo ,atalazimika tu kula ikiwa hakuna chakula kingine ili asife njaa ni sawa na hawa makocha tunaowaleta.
Tuhakikishe kuwa tunawapa nafasi ya kuchagua watu wa kufanya nao kazi na pia tuwape muda atleast misimu miwili tuone nini wanaweza kuifanyia klabu yetu pendwa na ikitokea hatujaridhishwa nao basi tunatimua benchi lote la ufundi.
Sio kocha unamtoa serbia halafu msaidizi unampangia ni lazima awe Matola (mtanzania), hawafahamiani hata falsafa zao za ufundishaji n.k halafu unataka kikosi kiwe na chemistry ndani ya wiki mbili ili hali hao makocha wenyewe wanaweza kukaa miezi miwili hawaelewani falsafa zao.
Tatu, ni lazima kocha apewe nafasi ya kurecommend ni wachezaji gani anawahitaji katika kikosi chake, haiyumikiniki unamleta kocha halafu wachezaji unasajili tu bila ya matakwa ya kocha.Unakuta kocha anahitaji mshambuliaji mrefu ili aendane na falsafa yake ..kwa maana anaweza kumsaidia hata kwenye kudefend set pieces ila timu inasajili striker mfupi kama kichuya ambaye hata hawezi kuruka juu ku-win aerial duels. Management ya klabu iache kusajili kwa mihemko ,inabidi impe nafasi kocha ajiridhishe kwanza iwapo huyo mchezaji anayetaka kusajiliwa ataisaidia klabu ama laa.
Mwisho kabisa napenda kutanguliza shukrani zangu kwa uongozi wa simba ,benchi la ufundi na wachezaji kwa ujumla kwa ushindi wa kwanza katika ligi kuu ya NBC. Tumpe ushirikiano kocha Zoran Maki na wachezaji wajitume waache makundi.
Sio kwasababu Kocha Zoran kakataa baadhi ya wachezaji ndio hao waliobaki wacheze chini ya kiwango ili tu wamtengenezee kocha mazingira ya kufukuzwa.