Ushauri tafadhali, Vodacom wameniumiza

Ushauri tafadhali, Vodacom wameniumiza

Uelewa wako ni duni sana ,unajidai kuuliza maswali ili yaonekane ni logic questions kumbe ni upupu,wewe ndo ulimpa access huyo msimamizi wa Laini Yako na ukampa password,Sasa unadhani voda wana vifaa vya kujua kuwa huyu anayekopa ni mmiliki wa Laini au siye!?

Jichanganye kuwashitaki waje wakufirisi Hadi uhame mtaa,,mfano Mimi Laini yangu ya voda inakopesheka Hadi sh 2M Sasa siku nikikuta mtu kaikopa hiyo Hela ni washitaki vodacom au mtu niliyempa access ya Laini yangu?


Kuna haja ya kuanzisha vyuo vya kukuza uelewa Kwa watanzania
Mkuu usijifanye mjuaji kwenye jambo ambalo hulijui na huna uzoefu nalo.

Hii huduma kwanza sikujua km ipo.
Pili sijawahi kuiomba.
Tatu kwenye biashara mara nyingi tunashirikiana na watu wa mshahara.
Huwezi kumpa mtu kazi ya simu pesa na usimpe pin za line husika, hataweza kufanya huduma.

Line zote Tigo, Airtel, Hallotel hawana huduma hii kwenye line ya biashara.
Hata voda walipoanzisha huduma hii ilipaswa watujulishe sisi mawakala tunaomiliki hizo line.
Nadhani nimeeleweka.
 
Tatizo ulishindwa kuishi nae kwa upendo, hivi mtu anakufanyiaje ubaya kama unaishi nae kibinadamu? Ukute mshahara ulikuwa hulipi kwa wakati unajifanya mwamba na kelele nyingi sasa dogo kapiga kwenye mshono. Pambana na hali yako tu 🤣
Kuna watu ni hawaridhiki hata uwafanyie nini unaweza kuta alikua anakaa nae vyema anamlipa vizuri ila ndio kaingiwa na tamaa. Hujawahi ona watu wana mishahara mizuri, maisha mazuri ila ni wezi??
 
Mkuu usijifanye mjuaji kwenye jambo ambalo hulijui na huna uzoefu nalo.

Hii huduma kwanza sikujua km ipo.
Pili sijawahi kuiomba.
Tatu kwenye biashara mara nyingi tunashirikiana na watu wa mshahara.
Huwezi kumpa mtu kazi ya simu pesa na usimpe pin za line husika, hataweza kufanya huduma.

Line zote Tigo, Airtel, Hallotel hawana huduma hii kwenye line ya biashara.
Hata voda walipoanzisha huduma hii ilipaswa watujulishe sisi mawakala tunaomiliki hizo line.
Nadhani nimeeleweka.
Kwenye Laini Kuna huduma nyingi sana,ili kuonesha kwamba umeipenda huduma utabonyeza kitufe,kama hujaipenda acha kubonyeza kitufe husika.


Ni vipi utawaaminisha voda kuwa sio wewe uliyekopa Bali ni msaidizi wako!? Punguza ujuaji
 
Hayo mambo yako ya kukariri darasani weka pembeni. Jamaa ana hoja, hiyo line ni ya biashara, mkataba alioingia nao ni wa huduma ya kutoa na kuweka pesa, huduma hiyo tu. Hoja yake,. Inakuaje, muajiriwa wake ameweza kufanikisha hilo la kukopa bila hao "voda" kumjulisha mmiliki?
Wamjulishe kwa njia gani? Nadhani hata huduma mpya wanapaongeza wanamjulisha kwa njia ya message (ambayo bado itafika kwenye simu hiyo ambayo anayo msaidizi wake) Hoja ya msaidizi amewezaje kukopa milioni 2 inakosa mashiko kisheria maana hata hapo kazini umempa pesa zaidi ya hizo na anasimamia miamala mikubwa zaidi ya hiyo kwa niaba yako na kwa kutumia saini yako(PIN).
 
Ni wajibu wako kulinda taarifa zako ikiwemo neno la siri, kama ulimpa mtu unaemwamini akakosa uaminifu basi wewe ndio unawajibika kwa huo uvunyifu wa uaminifu...

Voda awakukuchagulia mfanyakazi, wala awawezi kujua kama si wewe unakopa ni mfanyakazi wako kwakuwa line wamekuachia wewe uimiliki na kuitunza...

Nguvu kubwa zielekeze kumtafta uyo kijana ili uweze kupata hela za watu.

Maombi yangu ni umpate uyo kijana ili uweze kupata hela ya watu
 
Sio mwanasheria ila hiyo kesi yako hutoboi.
Yani vodacom waanze kusaka kwenye vibanda vya mpesa nani kaajiri nani?

Kila siku wanahimiza umuhimu wa usalama wa nywila zako kua ni zako peke yako, kama nywila zako ilishirikiana na mfanyakazi wako hilo sio kosa lao sasa
 
Ukishapewa Hio Sim Card na Vodacom ni mali yako kwahio ni Majukumu yako kuhakikisha hao wanaokufanyia kazi ni waaminifu au una wamanage..., lolote linaloweza kutokea ni jukumu lako

Ila hio RIBA sidhani kama ni sahihi unless ni Songesha Wakala ambapo alitakiwa kulipa the next day yaani unamrushia arafu unaenda kujaza ili kurudisha.... Inasaidia sana Mawakala ambao practically ni wadau / partners wa Voda

Labda kwa Ushauri wa Voda na Mawakala nadhani huwa kuna mbinu unaweza ukawa na line Mbili Master na nyingine ya ziada (ingawa sina uhakika) ili wafanyakazi wapewe line ambazo hazina options nyingi ambazo zinaweza kumletea Shida mwenye mali (Ukizingatia Watanzania wameshakuwa Vibaka na hakuna Uaminifu)
 
Utaambiwa wewe ndiye umekopa Kwa sababu zifuatazo;

1. Laini imesajiliwa Kwa Jina Lako.
2. Sheria za Tanzania hazitambui kuwa laini yako inaweza Kutumiwa na Mtu Mwingine ndîo maana Hilo NI Kosa Kisheria.
Kîla Mtu anatakiwa atumie laini Yake.

3. Namba ya Siri ya laini na akaunti za Pesa niza MTU binafsi yàani wewe. Hauruhusiwi Kutoa Namba yako ya Siri Kwa Mtu yeyote hata kama ni Mkeo au mtoto au Mzazi.

Hivyo Hapo wewe ndîo utawajibika.

Huyo kijana aliyekopa anaweza pia kukuruka
 
Kitendo cha wewe kutoa password ya lini zako maana ake huyo mtu unamuamini sasa hapo imekula kwako, sawali ni ilikuwaje ukampa mtu mwingine access ya line zako. Lipa deni ndugu
 
Hayo mambo yako ya kukariri darasani weka pembeni. Jamaa ana hoja, hiyo line ni ya biashara, mkataba alioingia nao ni wa huduma ya kutoa na kuweka pesa, huduma hiyo tu. Hoja yake,. Inakuaje, muajiriwa wake ameweza kufanikisha hilo la kukopa bila hao "voda" kumjulisha mmiliki?

Voda hawahusiki Hapo.
Mkataba wa mwenye biashara na mfanyakazi wake hauna uhûsiano na Vodacom.

Voda inajua anayefanya biashara ni mtoa Mada kama ameajiri au hajaajiri hiyo haihusiani
 
Hapa ndipo kwenye hoja yangu.
Hakuna hoja kwa sababu wachangiaji hamwelewi kuwa huo mkopo ni wa voda kwa mawakala pale wanapokuwa wameishiwa float. Ni huduma waliyoianzisha na walikuwa wakipita kwa mawakala kuwataarifu juu yake. Sio mkopo kama mkopo wa kawaida wa nipige tafu au songesha huu ni kwa mawakala na kiasi wanachokupatia kinaendana na kiasi cha miala unachofanya.
 
Hii huduma ya kukopesha kipindi naanza hii biashara haikuwepo na mimi sikujua km ipo hadi yalipotokea yaliyotokea .
Ipoanzishwa walikuwa wanapita wanawahimiza watu wa hop in so kijana wako uliyeamuamini, mpaka ukampa password na line atakuwa alijiunga.
 
Hii huduma haukuwepo kabla hata mimi sikujua km voda wameanzisha huduma ya kukopesha.
Hapa ndipo wachangiaji wengi hawajaelewa. Huduma ya kutoa na kuweka pesa n huduma moja inayojitegemea, kadharika huduma ya kukopa "float" ni huduma nyingine inayojitegemea. Kwa usahihi, inafaa mitandao ya simu waongeze control kuzuia asiyehisika na usajili wa laini kuwa na uwezo wa kukopa / kuingia mkataba katika huduma hiyo pasipo ruhusa ya muhusika.

Voda hawahusiki Hapo.
Mkataba wa mwenye biashara na mfanyakazi wake hauna uhûsiano na Vodacom.

Voda inajua anayefanya biashara ni mtoa Mada kama ameajiri au hajaajiri hiyo haihusiani
Msingi wa lalamiko la mleta uzi ni kukosekana kwa "control" ama kuwepo kwa "control" hafifu zinazonufaisha "third party" bila muhusika mkuu kuwa na taarifa. "Control" inayozuia mtu wa tatu kuweza kijiunga ama kuingia makubaliano kwa huduma mpya kama hizo za mkopo.
Utaambiwa wewe ndiye umekopa Kwa sababu zifuatazo;

1. Laini imesajiliwa Kwa Jina Lako.
2. Sheria za Tanzania hazitambui kuwa laini yako inaweza Kutumiwa na Mtu Mwingine ndîo maana Hilo NI Kosa Kisheria.
Kîla Mtu anatakiwa atumie laini Yake.

3. Namba ya Siri ya laini na akaunti za Pesa niza MTU binafsi yàani wewe. Hauruhusiwi Kutoa Namba yako ya Siri Kwa Mtu yeyote hata kama ni Mkeo au mtoto au Mzazi.

Hivyo Hapo wewe ndîo utawajibika.

Huyo kijana aliyekopa anaweza pia kukuruka.
Taikoni jaribu kufikiria katika mlengo wa biashara na uwekezaji. Hayo uliyoandika hapa yana tija na yana nguvu katika laini binafis, na hata mitandao ya simu wameweka mahitaji tofauti baina ya usajili wa laini binafsi kwa ajili ya huduma za mawasiliano binafsi.

Laini za uwakala ni laini za biashara na hata mahitaji yake katika kusajili ni tofauti, utahitaji taarifa za kitambulisho kwa utambulisho, leseni ya biashara na tin. Kama wametambua haya katika usajili, ni lazima waje na "control" zenye nguvu kulingana na asili ya matumizi za laini hizo.
 
Hapa ndipo wachangiaji wengi hawajaelewa. Huduma ya kutoa na kuweka pesa n huduma moja inayojitegemea, kadharika huduma ya kukopa "float" ni huduma nyingine inayojitegemea. Kwa usahihi, inafaa mitandao ya simu waongeze control kuzuia asiyehisika na usajili wa laini kuwa na uwezo wa kukopa / kuingia mkataba katika huduma hiyo pasipo ruhusa ya muhusika.


Msingi wa lalamiko la mleta uzi ni kukosekana kwa "control" ama kuwepo kwa "control" hafifu zinazonufaisha "third party" bila muhusika mkuu kuwa na taarifa. "Control" inayozuia mtu wa tatu kuweza kijiunga ama kuingia makubaliano kwa huduma mpya kama hizo za mkopo.

Taikoni jaribu kufikiria katika mlengo wa biashara na uwekezaji. Hayo uliyoandika hapa yana tija na yana nguvu katika laini binafis, na hata mitandao ya simu wameweka mahitaji tofauti baina ya usajili wa laini binafsi kwa ajili ya huduma za mawasiliano binafsi.

Laini za uwakala ni laini za biashara na hata mahitaji yake katika kusajili ni tofauti, utahitaji taarifa za kitambulisho kwa utambulisho, leseni ya biashara na tin. Kama wametambua haya katika usajili, ni lazima waje na "control" zenye nguvu kulingana na asili ya matumizi za laini hizo.

Ulichoandika NI Sahihi lakini hata biashara ni binafsi.

Hapo ni suala la uaminifu tuu.

Lakini pia Vodacom wanaweza ichukua hiyo kama changamoto waongeze akaunti Mbili ndàni ya laini Moja àmbayo ina password tofauti
 
Labda kwa Ushauri wa Voda na Mawakala nadhani huwa kuna mbinu unaweza ukawa na line Mbili Master na nyingine ya ziada (ingawa sina uhakika) ili wafanyakazi wapewe line ambazo hazina options nyingi ambazo zinaweza kumletea Shida mwenye mali (Ukizingatia Watanzania wameshakuwa Vibaka na hakuna Uaminifu)
Hapa nimekupata. Laini za uwakala ni laizi za biashara, ni wazi na hata wao wanatambua kuwa kuna "waajiriwa" wanatumia laini hizo kwa niaba ya wamiliki. Ni jukumu lao voda kuweka mipaka katika kuzuia "third party" kujiunga na huduma mpya pasipo muhusika kutoa idhini.
 
Inamana umeajiri mtu ambae hujui details zake vizur, kama unajua kwanin usimtafute mpambane one against one
Mambo unayachukulia kirahisi sana wewe!

Mtu kaiba pesa nyingi, hata kama unazijua details zake itakusaidiaje kumpata, kwani yeye ni mpumbaf kiasi gani apore kwako halafu arudi sehemu ulikompatia?
 
Ulichoandika NI Sahihi lakini hata biashara ni binafsi.

Hapo ni suala la uaminifu tuu.

Lakini pia Vodacom wanaweza ichukua hiyo kama changamoto waongeze akaunti Mbili ndàni ya laini Moja àmbayo ina password tofauti
Swala la uaminifu lina nguvu katika kipengele za kutembea "kuiba" cash.

Kujiunga na kuweza kunufaika na huduma ya mikopo kwa laini ya biashara ni madhaifu ya mfumo wa voda katika kulinda wamiliki wa laini hizo za biashara.
 
Back
Top Bottom