USHAURI: Tubadili mfumo wa viti maalum, vifutwe!

hawana maana ...sasa kama Vick kamata eti mbunge sasa anaoingea nini bungeni kama sio kwenye kujipaka mapoda tu na kujibinua binua

Afadhali huyu anae jipaka poda na kujibinua binua kama unavyosema, maana yuko active, je wanaosinzia, kujamba na kukoroma?
 
Wafutwe ama kupunguzwa, ni wengi mno hawana mchango wowote, angalia bunge la sasa viti maalum ni upupu mtupu.
Wengi ni mashangingi tu hawana la maana kule mjengoni zaidi ya kuliletea taifa mzigo wa gharama zisizo za lazima.
 
System yetu inatudanganya kwamba wanawawakilisha akina mama zetu ni wizi mtupu. Hiyo cost ya representation is just high kuwalipa 100 plus kama wawakilishi wasiochanguliwa na wawakilishwa. Affirmative yes wenzetu wanataka kuwezeshwa lakini iwe kwa kuwapa opportunity ya kugombea na sio kwa kupewa kama ilivyo kwa sasa...sina mfano mzuri lakini najua ipo mifano mingi tu ya kuigwa na sisi :frusty:
 
Tatizo hilo zigo linatokana na masharti ya wafadhili; sasa sijui cost benefit analysis inasemaje? Je, hiyo cost inakuwa covered na wafadhili tu au na sehemu ya kodi ninayolipa? Au ni kodi yangu tu? Je, tuna - benefit nini kama Taifa?
 
Siku zote huwa najiuliza sana hawa wabunge wa viti maalumu ni wa nini??? Hawatakiwi kbisa kuwepo. nadhani ni jambo muhimu liingizwe kwenye katiba mpya kuondoa kabisa.

Hili liendane na wabunge wa kuteuliwa na Rais, hawa pia hawatakiwi sana sana rais anatumia nafasi hii kutoa rushwa kwa watu...mfano Rais Mpaka kumteua Dr. Lamwai, marehemu chief fundikira, Rashid H. Rashid, makongoro Nyerere; rais Kikwete kumteua Thomasi mwang'onda, Zakia Megji. Kamna ni uwaziri basi katiba mpya tuingize kipengele wabunge wasitokane na wabunge ili raisi awe na wigo mpana wa kuchangua kama ni muhimu kwake
 
Ni kweli huyu mkubwa amenena, wanawake tunapaswa tupiganie nafasi zetu za heshimu, ukimshinda mwanamume na uwakilishi pia unaheshimiwa. siyo huu ambao kila mmoja anaona tumependelewa na wakubwa ndiyo wanataka kila wakiwaona vitimaalum wanaota ngono tu. Tutapigania kina mama mbona wanaume wengi sasa wanaelewa uwezo wetu!!!!
 
Tushalisema sana hili jambo hapa. Huyu Katibu baada ya kuona hilo ametumiaje mamlaka yake ku influence mabadiliko zaidi ya kusema tu (which is appreciated, coming from the corridors of power and with the risk of alienating a whole lotta bigwigs)
 
mbaya ni hasara tunayopata kwa ili suhala lisilo na tija kwa wataifa wala kina mama
wanawake wanazidi kutaabika tu, hii imewekwa kujiosha kwenye mashirika ya kimataifa ili kupata misaada
na anayeumia zaidi ni sisi wananchi wa kawaida kwa kutozwa kodi kulipa mishahara ya hawa viti maalumu


Tushalisema sana hili jambo hapa. Huyu Katibu baada ya kuona hilo ametumiaje mamlaka yake ku influence mabadiliko zaidi ya kusema tu (which is appreciated, coming from the corridors of power and with the risk of alienating a whole lotta bigwigs)
 
Ni mzigo kwa taifa na kuongeza idadi ya kura za ndiyooooo!!!! kwa chama chenye wabunge wengi, mwishowe ni kupitisha maamuzi na sheria mbumbumbu, tunazojutia hapo mbeleni, kwani wengi tu ni rubber stamp ya ruling elite. (Umaalum unamwakilisha nani maalum, anyway?)
 
hawana maana ...sasa kama Vick kamata eti mbunge sasa anaoingea nini bungeni kama sio kwenye kujipaka mapoda tu na kujibinua binua
Kigogo Kigogo hapo kwenye red kaka du umenivunja mbavu kwi kwi kwiiiiiiiiiiiii,kujibinua binua ili amurushe roho mzee
 
Wabunge wa viti maalum hawatakiwi kabisa, ni kulitwisha mzigo Taifa. Inashangaza mtu kama Ana Abdala amekuwa ni Mbunge kwa zaidi ya miaka 30 bungeni lakini mpaka leo ndiyo kusema hana uwezo wa kusimama jimboni na kuomba kura?
 
Hata kesho vifutwee na sio kwamba tunawaonea wivu hapana hawana tija na hawafanyi kitu chochote!! Kuhusu uroda tuwaulize wao wathibitishe. Lakini kuna ushaidi wa kimazingira!!!!!
 
Huu ni ufisadi mwingine ambao wananchi wa Tanzania wamebebeshwa!Mpaka lini mali zetu zitafujwa namna hii kwa maslahi ya watu wachache?
 
mkuu umeona, sasa hiyo ni kuwezesha au kubaka nafasi, bora hata wangekuwa wanapewa miaka mitano tu hakuna kurudia KITI MAALUMU na sio 102 ni vingi mno, vifutwe hayo ndio maoni yangu
ni mzigo mkubwa kwa bibi yangu kijijini
na shangazi yangu pia kwa kulipia kodi watu walemaisha bora
huu ni wakati wananchi kushika hatamu

Wabunge wa viti maalum hawatakiwi kabisa, ni kulitwisha mzigo Taifa. Inashangaza mtu kama Ana Abdala amekuwa ni Mbunge kwa zaidi ya miaka 30 bungeni lakini mpaka leo ndiyo kusema hana uwezo wa kusimama jimboni na kuomba kura?
 
Nimelipigia kelele hili muda mrefu tu humu. Tunaigharamia sana SIASA huku huduma muhimu kwa WATANZANIA ikidorora vibaya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…