USHAURI: Tubadili mfumo wa viti maalum, vifutwe!

USHAURI: Tubadili mfumo wa viti maalum, vifutwe!

HIVI NDIVYO VITU AMBAVYO VINATAKIWA VIINGIZWE KWENYE KATIBA ,ni matumizi mabaya ya pesa za walipa kodi
 
Hakuna asiyefahamu kuwa hakuna value addition whatsover kwa kuwa na wabunge wa viti maalumu...zaidi ya hasara kwa taifa ya kuwamaintaini wabunge 102.

Swala la kupiga makofi, mipasho, kuzomea au kuwa na idadi ya wapiga kura ndani ya bunge nk si mambo yenye tija na wala watz hatuyahitaji ktk bunge letu.
 
Jamani wakati wa mchakato wa kuunda katiba mpya tutapendekeza vifutwe kwani havina tija
 
Dk. Kashilila aliwaponda wabunge wa viti maalumu akisema kundi hilo ni mzigo kwa taifa kwa kuwa hawana kazi wanayoifanya zaidi ya kukidhi maslahi ya kisiasa.

Dk. Kashilila alisema ni Tanzania pekee ndiyo yenye wabunge wa aina hiyo ikilinganishwa na nchi nyingine zinazofuata mfumo wa mabunge ya jumuiya ya madola (Commonwealth).


Mtendaji huyo wa Bunge alihoji sababu za kuwepo kwa kundi hilo la wabunge, wakati wabunge wa majimbo wapo. Wabunge 102 kati ya wabunge 350 waliopo bungeni hivi sasa ni wabunge wa viti maalumu.


“Wabunge wa majimbo wapo 239, ndiyo kusema kwamba katika eneo lote la Tanzania hakuna eneo lisilokuwa na uwakilishi bungeni. Ukisema kila mbunge wa jimbo aende jimboni kwake, utakuta nchi yote ipo covered (ina wabunge).

“Sasa unajiuliza kama hivyo ndivyo hawa wabunge wa viti maalumu wa kazi gani
? Wanafanya kazi ipi special (maalumu) ambayo haifanywi na mbunge wa jimbo?” alihoji.

Alipoulizwa iwapo hoja yake hiyo inalenga kushauri wabunge wa viti maalumu wafutwe
, Dk Kashilila alisema: “ Mimi siwezi kushauri moja kwa moja kwamba wabunge hawa wafutwe, ila tunaweza kufanya marekebisho tukaiga affirmative policy ya Uingereza.

“Tukatenga maeneo, kwamba katika kila majimbo kumi ya uchaguzi majimbo manne yawe kwa ajili ya wanawake kama hoja ni kuwa na wanawake bungeni. Hapo vyama visisimamishe wagombea wanaume katika majimbo hayo.

“Kwa kufanya hivyo tutajikuta tumewaondoa hawa wabunge wa viti maalumu ambao kimsingi mimi sioni kazi wanayofanya na badala yake tutakuwa na wanawake bungeni, lakini wanaotokana na majimbo,” alisema.


Wakizungumza na Mtanzania kwa nyakati tofauti, baadhi ya wabunge walitoa maoni tofauti kuhusiana na kauli hiyo, huku baadhi yao wakiipinga wazi wazi kauli hiyo.

Naye Mbunge wa Viti Maalumu, Esther Bulaya (CCM) alimshangaa Dk. Kashilila kwa kutoa mashambulizi makali dhidi ya wabunge wa viti maalumu, huku akisema wabunge hao ni watu wenye mchango mkubwa kwa jamii.


“Hayo ni maoni yake, lakini kusema wabunge wa viti maalumu ni mzigo kwa taifa mimi nadhani siyo sahihi. Wabunge wa viti maalumu wana mchango mkubwa kwa jamii na hata hao walioweka mfumo huu walijua wabunge wa viti maalumu wana mchango.

“Tunafanya shughuli nyingi za kijamii, tumekuwa tukisaidiana na wabunge wa majimbo katika mambo mbalimbali. Pale ambapo wabunge wa majimbo hawatimizi sisi tumekuwa tukiziba mapengo. Kwa hiyo si kweli kusema wabunge wa viti maalumu hawana kazi ya kufanya,” alisema



Maoni yangu:
tunapoteza zaidi ya bilioni 50 kwa miaka mitano kughalimia hawa wabunge wasio na tija kwa taifa wala kwa hao wanawake wanao wawakilisha nadhani tukifuata mfumo wa kiingereza kwa sababu tunafuta huo itakuwa makini zaidi, au kama vipi tuwe na utaratibu ambao wabunge wanatoka kajimboni tu na uwakilishi na ushawishi wao utaoneka wazi wazi, hizo pesa tunaweza kuzitumia kuleta maendeleo makubwa sana, na hawa wakuu wa mikoa na wilaya watolewe pia hakuna kitu cha maana wanachofanya.

SOURCE: MTANZANIA (
Wabunge kikaongoni)
Now you are talking
 
Sehemu kubwa ya wabunge viti maalumu ni vibaraka wa wagodfather waliohakikisha wana teuliwa. kwa sehemu kubwa wabunge hawa uwajibikaji ni mdogo kwa sasbubu hawako acountable majimboni... wanaongeza uwingi bungeni bila tija kwa taifa, wanalipwa pesa nyingi bila kutika jasho.

Wabunge hawa haswa wale kumi ambao raisi anamalaka wa kuwateua kikatiba,, hawana mtu wanaemwakilisha bungeni wapo wapo tu kazi yao ni kuongeza idadi ya kura bungeni kupitisha miswada inayoliangamiza taifa..... wabunge hawa tuwakatae.... ikishindikana ni heri tukabaki na hawa viti maalumu kwa makundi maalum, sio hawa wanaoteuliwa na rais bila kuzingatia wanamwakilisha nani bungeni.....

Kwa mfano, nini tija ya mchungaji mama Rwakatale au mzee Makamba,, Kingunge? Hili janga kwa taifa
 
huu ni ufisadi kwa hawa wabunge wa viti maalum bungeni ni kaaina ya ufisadi
 
wamejazana bungeni lakini no output badala yake ni posho na rushwa kwishney
 
jamani mi naomba kuuliza wabunge wa viti maalum wanamuwakilisha nani bungeni?
 
Mdahalo wa katiba uliofanyika ubungo plaza leo umekuwa tofauti na midahalo ya hapo kabla ile iliyotawaliwa na hisia za vyama vya siasa, enzi hizo hakuna kilichofanikiwa zaidi ya watu kuzomeana na kusodoana tu.
Leo hali ilikuwa tofauti sana kwani washiriki walikuwa watulivu na walipeana nafasi za kila aliyebahatika kupata nasafi ya kuchangia alitoa mawazo yake kwa uhuru tofauti na awali ilivyokuwa.

MAWAZO YALIYONIGUSA NA MAPYA KWANGU NA NINAYOYAUNGA MKONO NI HAYA YAFUATAYO:-

1. Dada anaeitwa Agnes alitoa mawazo yake kuhusu VITI maalum, alisema viti maalum vinarahisisha wanawake kutawaliwa na hata wanapofika bungeni hawana jeuri ya kutoa mawazo huru, kwani ni lazima waendelee kujipendekeza na kuwaabudu waliowawezesha (waliowazawadia)kupata nafasi hizo
MY TAKE.
Hii ni dhahili sana kwani hata mifano ipo wazi, sio wazo zuri kuwapata wabunge hawa kwa mfumo unaotumiwa na viongozi wa vyama vya siasa kuwaweka watu wao, hata pengine ikatamkwa kuwa ni mademu zao, wake zao, dada zao na ndio sababu hata leo utamsikia VITI maalum akijitambulisha kuwa ni mbunge kivuli wa jimbo fulani analoliota, na sio mbunge wa viti maalum wanaona aibu na hawana uhuru kwa kuhofia kuwakera waliowawezesha (waliowazawadia) nafasi hizo n.k.
Ushauri wangu kwenye katiba mpya hizi nafasi za makundi maalum, zisipatikane kupitia vyama vya siasa, ili makundi haya ya wanawake na walemavu, yawakilishwe bila itikadi za kisiasa, hebu jiulize wabunge wa ccm wakiwa wengi na wapo kwa ajili ya wanawake, je watakua sauti ya nani kama sio sauti ya wanawake wa ccm, na hata kwa wle wa cdm na cuf na nccr nao wataishi kiitikadi vilevile hapa makundi maalum hayawakilishwi bali ni unafiki tu wa kisiasa na huu mfumo wao wa kuwapata viti maalum.

2. BABU ALIYETOA MFANO WA KINYONGA.
Babu mzee sana alitoa unabii kama uliwahi kutolewa na Nabii samweli kuwa hatakufa mpaka atakapomuona Yesu, na mzee huyu leo ametoa unabii huo kwa kusema kuwa hatakufa kabla ccm haijafa, akatoa mifano mingi ya kuwataka viongozi wawe waadilifu na akashangiliwa sana.
Mfano alioutoa Babu wa kinyonga kufa akiwa tayari amefikia term(yaani miezi ya kujifungua)ni mfano dhahili akilenga ccm ni lazima ife ili mfumo wa vyama vingi uwe huru na wa haki, hapa sio tu kwa ccm bali hata vyama vya siasa vina jukumu la kufa kiitikadi kiimani na kimienendo na hata kisera/kiorganisation, ili viweze kuwa na mitazamo imara na ya haki ya dhati, na ili viweze kudumu mioyoni mwa wananchi na viweke misingi ya kudumu ya kujiendesha kimgawanyiko wa kiutendaji, ndio tafasiri ya kufa na kufufuka upya, kufa pia kuna maana ya kuwaweka watendaji wenye sifa katika ngazi husika na sio kama ilivyo kwa vyama vyetu hapa tz, vyenye viongozi wanaotumia nafasi zao kuwateua watu kwa vigezo wajuavyo wenyewe na sio uwezo wala sifa dhahili, hapa bila kukubali kuliwa na kufa ili vifufuke upya, hatutaona kipya i swear!!
NIWATAKIE MAATAZMIIO MEMA YA KATIBA MPYA...
 
jinsi mambo yanavyoelekea kubadilika kuna dalili kwamba viti maalum mwisho wake ni 2014. Je itakuwa jambo la mbolea iwapo tanzania itabakia na wabunge wa kuchaguliwa tu!!!!!
 
jinsi mambo yanavyoelekea kubadilika kuna dalili kwamba viti maalum mwisho wake ni 2014. Je itakuwa jambo la mbolea iwapo tanzania itabakia na wabunge wa kuchaguliwa tu!!!!!

Wabunge wa viti maalumu nao pia ni ufisadi....huko bungeni wanawakilisha interest za mabosi wao and not citizen

narudia tena to me viti maalumu ni mzigo kwa taifa.
 
Viti maalumu ni kwa ajili ya wachumba,ma girlfriends,wake wa wanene wa vyama vya siasa,ukiangalia kwa undani utakuta wengi wa wabunge wa viti maalumu wana jamaa zao humo humo mjengoni.hakika sijui wanachokifanya humo mjengoni zaidi ya kujibinua binua na kuombana dili za vimiradi au vitenda
 
Mkuu hiyo writting colour yako haipo sawa, change! Viti maalum visitishwe kwani ni gharama kwa taifa!
 
Ngoja waje wenyewe hapa muone povu lao!
 
Hivi nao huwa wanalamba ile Millioni Tano ya Mbunge kwa maendeleo ya Jimbo?
 
Viti maalumu ni kwa ajili ya wachumba,ma girlfriends,wake wa wanene wa vyama vya siasa,ukiangalia kwa undani utakuta wengi wa wabunge wa viti maalumu wana jamaa zao humo humo mjengoni.hakika sijui wanachokifanya humo mjengoni zaidi ya kujibinua binua na kuombana dili za vimiradi au vitenda


Not true at all, hiyo ni negativity ya wabongo. Ni udhalilishaji mkubwa kuwa eti wanajibinuabinua, hivi kweli hamuoni kazi wanayofanya? na je hao wawakilishi wa majimbo are they working properly kwa maslahi ya wananchi? au ndo mfumo dume mlionao?
 
Back
Top Bottom