chankele kigoma
Senior Member
- Jan 12, 2017
- 199
- 121
Mkuu umenena kweliUmeandika kwa uchungu sana, ni kweli wakati mwingine unaweza kuhisi hauna bahati kwenye maisha kwa kukosa hiki na kile, mara nyingi katika nyakati hizo huwa napenda kwenda muhimbili au ocean road hospital kama nipo Tanzania, pale nitaona watu wenye shida za ukweli, kwa kufanya hivyo, nitatazama mbingu na kumshukuru Mungu baba kwa kuniinulia uso wake na kunifadhili, afya njema na uhai ni zawadi kubwa kwangu kutoka kwa Mungu, hayo mengine ni ziada. Usikate tamaa endelea kupambana maisha hayana formula, wala hautaweza kuipata formula hapa JF.
Hili Mi nakataa inategemea na malezi yenu tokea udogoni km mlilelewa kwa upendo Wa kupendana nyinyi kwa nyinyi mtasaidiana tu! Ni mifano kbao ya ndugu walioshikana mikono mpk wakatusuaNaomba niongezeee kidogo,hakuna ndugu anayetaka Ndugu yake afanikiwe kimaisha bora mtu baki anaweza kukusadia ukatoka kimasha sio Ndugu.
Naomba unisaidie Mimi mawazo mkuuUmesema unafanya shughuli ndogo ndogo zinazokusaidia kulipa kodi, ni shughuli zipi hizo na mtaji wake ni kiasi gani? Tunaweza kushauriana namna ya kupanua hizo hizo shughuli zako ndogo na zikawa kubwa
ni kama umenigusa na mm yaani ndugu wanataka uwatetemekee wao hawakusaidii kituKati ya watu usiotakiwa tegemea ni
Ndugu (Tumbo Moja au W Mbali)
Familia
Marafiki
Ukiwategemea Hawa utakufa masikini, hata wawe nacho hawawezi kukusaidia zaidi watapenda uwe hivyo ili uwaheshimu
Maneno yako yamenigusa sana kiongozi.Salaam wanajamvi,
Jamani naomba mnipe ushauri kutoka kwenu hasa kwa wale waliofanikiwa kimaisha.
Kwanza naweza sema hapa Tanzania kusoma sana ndo kuukaribisha umasikini tu.
Kijana mimi wa kitanzania mwenye elimu ya Bachelor degree na Postgraduate Diploma hadi sasa nagonga 30 years sina cha maana ninachomiliki katika maisha yangu.
Sijui kwa sababu nimetumia muda mwingi kusoma, au hii familia niliyozaliwa ya umasikini ndo chanzo hata sijui.
Nilisoma kwa mkopo wa serikali na postgraduate nikafadhiliwa kwa kujua kwamba nikimaliza nitaingia kwenye system kupitia ualimu wa masomo ya arts imekua ndivyo sivyo.
Umri unaenda sina mtaji sina ndugu wa kuniwezesha kwa chochote kazi zimekua ngumu so nategemea kudra za Mwenyezi Mungu labda nitafanikiwa.
Najishughulisha na shughuli mbalimbali za kujiingizia kipato lakini hakikidhi mahitaji napata hela ya kula, kulipa kodi miezi 2 2 au 1.
Nina mtoto anaishi kwa mama yake, najisikia vibaya kumwona mwanangu anakua lakini hadi sasa baba yake similiki chochote kitakachomsaidia, mama yake ndo anauwezo kwa sasa wa kumjengea mazingira bora coz kipato chake kinatosha kabisa.
Sina ninachomiliki jamani, naombeni ushauri njia bora ya kuishi, namna ya kufanya ili nami niweze kutoka katika dimbwi hili la umaskini, nakiri kwamba nimesoma na kwa sasa sina ndoto tena ya kutaka kuajiriwa nina ndoto ya kujiajiri lakini sijui wapi napata mtaji, labda itokee nipate ajira ya uhakika ya kupata salary bila usumbufu hapo nitajipanga kudunduliza hela nipate japo mtaji.
Umasikini mbaya sana. Na elimu ya Tanzania inachochea umasikini.
Nipeni ushauri jamani ili mwaka 2018 niwe mtu mpya nijue nini nifanye nami nimiliki japo biashara hata ya kuuza juice, banana power hata shujaa vodka.
Ushauri tafadhali, sihitaji maneno ya kejeli nina frustration zangu.
NAWASILISHA
Aika mleu okoUmenena vyema.
Anachokipitia jamaa, watu wengi wanapitia ikiwemo mimi.
Alichokisema, nimekipitia.
Nilidharauliwa kwa umasikini wangu japo ni digrii, ila sasa ninaheshimika eti kwa pesa zangu, na sasa wananipiga mizinga, japo sina pesa kihivyo.
Ndugu, marafiki, wengi ni wanafiki tu.
kuni unauzia wapi mkuu?? nna shamba langu maeneo ya vigwaza nlitaka kukata miti nichome mkaa ila mlolongo nlopewa huko maliasili ilibid niweke pause kwanza,,vibali ulipataje??Me nakushaur ujikite ktk bsness ...me n former teacher nmefundsha English medium kadhaa hapa dar Nina miaka 24 nmeacha kaz mapema mwaka huu na nmejiajir Nina vibal toka maliasili ninauza kuni znalipa sana ......ila ka hauna mtaj kabisa nakushaue ebu hangaika upate jpo lak nne ...uanze kwenda kwa wakulima wa Mihogo ununue kwa kuanzia robo eka then unaenda kuuza sokon ...aidha mwenyew au kuptia madalali .......au unawzann cha kufanya ....jipange jiamin kuwa jasir ur the best mambo yanawezekana
Hujamsoma alikuwa anamaanisha aside moyo kwa kutizama namba za umri Bali aendelee kupambana mafanikio japo Hata kwenye umri mkubwaKwaio akae hadi miaka 50...?! Usubiri kupandishwa vyeo?!
Nakushauri, ufanye kazi hapo kwa malengo. Hao hawatakuja kukulipa vizuri kama unavyotaka, na kwamba wanafanya hivo ili uendelee kupiga kazi kwao huku ukipiga kiaina.Nafundisha chuo masomo ya hotel na tourism ila kulipana ni kwa shida sana tena kidogo kidogo so unajikuta huna cha maana unachokifanya kupitia malipo hayo zaidi ya kula na kulipa kodi tena kwa mbinde kwelikweli,endapo kama ningekua nalipwa kwa wakati tena hela yote nna uhakika ningepata mtaji tu ila ndo hivyo magumashi tupu mkuu