Ushauri: Umri unaenda sina ninachomiliki

Ushauri: Umri unaenda sina ninachomiliki

Umeandika kwa uchungu sana, ni kweli wakati mwingine unaweza kuhisi hauna bahati kwenye maisha kwa kukosa hiki na kile, mara nyingi katika nyakati hizo huwa napenda kwenda muhimbili au ocean road hospital kama nipo Tanzania, pale nitaona watu wenye shida za ukweli, kwa kufanya hivyo, nitatazama mbingu na kumshukuru Mungu baba kwa kuniinulia uso wake na kunifadhili, afya njema na uhai ni zawadi kubwa kwangu kutoka kwa Mungu, hayo mengine ni ziada. Usikate tamaa endelea kupambana maisha hayana formula, wala hautaweza kuipata formula hapa JF.
Mkuu umenena kweli
 
Umeomba msaada lakini hujatufungukia vizuri hivo itakuwa ngumu mtu kukushauri nini ufanye ili upate kuwa mpya 2018

Inatakiwa ueleze how much you have so itakuwa vyepesi mtu kuku shauri nini ufanye kutokana na kiasi ulichonacho vinginevyo utapewa pole tu.
 
Naomba niongezeee kidogo,hakuna ndugu anayetaka Ndugu yake afanikiwe kimaisha bora mtu baki anaweza kukusadia ukatoka kimasha sio Ndugu.
Hili Mi nakataa inategemea na malezi yenu tokea udogoni km mlilelewa kwa upendo Wa kupendana nyinyi kwa nyinyi mtasaidiana tu! Ni mifano kbao ya ndugu walioshikana mikono mpk wakatusua
 
30miaka bado hujachelewa anza hata na mtaji wa laki moja,usichague kazi mwaka mmoja tu ukitulia mabadiliko utayaona ila uvumilivu ndio siraha namba moja
 
Umesema unafanya shughuli ndogo ndogo zinazokusaidia kulipa kodi, ni shughuli zipi hizo na mtaji wake ni kiasi gani? Tunaweza kushauriana namna ya kupanua hizo hizo shughuli zako ndogo na zikawa kubwa
Naomba unisaidie Mimi mawazo mkuu
 
Pole sana ndugu yangu, ila kanuni ya waliowengi iliyopelekea wakafanikiwa ni mbili tu
1. Spend less, save more
2. Invest wat u ar willing to lose
Nilijarib and it works
 
Acha kuifikiria degree yako, kufanya hivyo inakuZuwia kujitoa kwa hicho kidogo unacho kifanya kwa kuwa unafanya kwa kungojea matunda ya degree. Wapo wasio na degree lakini kuna sehem nao walikosea na kupotea muda na pesa. Umri wako sio mkubwa na unabahati ya kuwa na degree ambayo inakupa kiburi cha kujilipua kwa ku take risk kibiashara kwakua unajia unapo pa kuegemea. weka vyeti kabatini wala hakuna anye kujua kama wewe ni msomi, jichanganye na hao std IV fanya nao kaZi huku ukitumia upe wa Degree. Sikupi pole bali nakutia Moyo, bado mapema usivute shuka, bado mapema fungua macho .
 
Kati ya watu usiotakiwa tegemea ni
Ndugu (Tumbo Moja au W Mbali)
Familia
Marafiki

Ukiwategemea Hawa utakufa masikini, hata wawe nacho hawawezi kukusaidia zaidi watapenda uwe hivyo ili uwaheshimu
ni kama umenigusa na mm yaani ndugu wanataka uwatetemekee wao hawakusaidii kitu
 
Salaam wanajamvi,

Jamani naomba mnipe ushauri kutoka kwenu hasa kwa wale waliofanikiwa kimaisha.

Kwanza naweza sema hapa Tanzania kusoma sana ndo kuukaribisha umasikini tu.

Kijana mimi wa kitanzania mwenye elimu ya Bachelor degree na Postgraduate Diploma hadi sasa nagonga 30 years sina cha maana ninachomiliki katika maisha yangu.

Sijui kwa sababu nimetumia muda mwingi kusoma, au hii familia niliyozaliwa ya umasikini ndo chanzo hata sijui.

Nilisoma kwa mkopo wa serikali na postgraduate nikafadhiliwa kwa kujua kwamba nikimaliza nitaingia kwenye system kupitia ualimu wa masomo ya arts imekua ndivyo sivyo.

Umri unaenda sina mtaji sina ndugu wa kuniwezesha kwa chochote kazi zimekua ngumu so nategemea kudra za Mwenyezi Mungu labda nitafanikiwa.

Najishughulisha na shughuli mbalimbali za kujiingizia kipato lakini hakikidhi mahitaji napata hela ya kula, kulipa kodi miezi 2 2 au 1.

Nina mtoto anaishi kwa mama yake, najisikia vibaya kumwona mwanangu anakua lakini hadi sasa baba yake similiki chochote kitakachomsaidia, mama yake ndo anauwezo kwa sasa wa kumjengea mazingira bora coz kipato chake kinatosha kabisa.

Sina ninachomiliki jamani, naombeni ushauri njia bora ya kuishi, namna ya kufanya ili nami niweze kutoka katika dimbwi hili la umaskini, nakiri kwamba nimesoma na kwa sasa sina ndoto tena ya kutaka kuajiriwa nina ndoto ya kujiajiri lakini sijui wapi napata mtaji, labda itokee nipate ajira ya uhakika ya kupata salary bila usumbufu hapo nitajipanga kudunduliza hela nipate japo mtaji.

Umasikini mbaya sana. Na elimu ya Tanzania inachochea umasikini.

Nipeni ushauri jamani ili mwaka 2018 niwe mtu mpya nijue nini nifanye nami nimiliki japo biashara hata ya kuuza juice, banana power hata shujaa vodka.

Ushauri tafadhali, sihitaji maneno ya kejeli nina frustration zangu.

NAWASILISHA
Maneno yako yamenigusa sana kiongozi.

Pole sana.
 
Umenena vyema.

Anachokipitia jamaa, watu wengi wanapitia ikiwemo mimi.


Alichokisema, nimekipitia.


Nilidharauliwa kwa umasikini wangu japo ni digrii, ila sasa ninaheshimika eti kwa pesa zangu, na sasa wananipiga mizinga, japo sina pesa kihivyo.


Ndugu, marafiki, wengi ni wanafiki tu.
Aika mleu oko
 
Mwanangu amka acha kulialia kunja roho kunjua sura tafuta network mjini wanaojua kusoma ramani, kuna maboya town wanamiliki hela nyingi tunawachukuliaga tu kwani nn? Umasikini unatesa sana usikubari kuishi kinyonge ni bora kuishi muda mfupi wenye raha kuliko miaka mingi ya shida na dharau, kila mtu mjini ni hustler hata yule pastor wako anakuthamini kutokana na kiwango chako cha sadaka.
 
Me nakushaur ujikite ktk bsness ...me n former teacher nmefundsha English medium kadhaa hapa dar Nina miaka 24 nmeacha kaz mapema mwaka huu na nmejiajir Nina vibal toka maliasili ninauza kuni znalipa sana ......ila ka hauna mtaj kabisa nakushaue ebu hangaika upate jpo lak nne ...uanze kwenda kwa wakulima wa Mihogo ununue kwa kuanzia robo eka then unaenda kuuza sokon ...aidha mwenyew au kuptia madalali .......au unawzann cha kufanya ....jipange jiamin kuwa jasir ur the best mambo yanawezekana
kuni unauzia wapi mkuu?? nna shamba langu maeneo ya vigwaza nlitaka kukata miti nichome mkaa ila mlolongo nlopewa huko maliasili ilibid niweke pause kwanza,,vibali ulipataje??
 
Nafundisha chuo masomo ya hotel na tourism ila kulipana ni kwa shida sana tena kidogo kidogo so unajikuta huna cha maana unachokifanya kupitia malipo hayo zaidi ya kula na kulipa kodi tena kwa mbinde kwelikweli,endapo kama ningekua nalipwa kwa wakati tena hela yote nna uhakika ningepata mtaji tu ila ndo hivyo magumashi tupu mkuu
Nakushauri, ufanye kazi hapo kwa malengo. Hao hawatakuja kukulipa vizuri kama unavyotaka, na kwamba wanafanya hivo ili uendelee kupiga kazi kwao huku ukipiga kiaina.

Kuna usemi unasema kwamba "ili uweze kupiga hatua/kufanikiwa haijarishi unapata Shilingi ngapi bali unaweka akiba Shilingi ngapi".

Nakushauri, uanzishe vijimradi vidogo vidogo vidogo vidogo kama vile kutengeneza na kuuza "ice cream" na ubuyu, Mpesa, kuuza vocha za jumla, nakadhalika. Vijimradi hivi vitakujengea uwezo wa kutokuwa mtumwa/tegemezi kwa hao hajamaa 100%. Naukisha simama unasepa ili kujipa muda wa kutosha kusimamia mijimradi vyako.

Nikutowe wasiwasi, kwanza hujachelewa kutusua, pili siyo kweli kwamba ili uanzishe biashara lazima uwe na mtaji mkubwa kama unavyodhani. Wengi waliotusua walianza na mitaji kiduchu muno ila walikuwa na malengo ya kufika mbali na walisimamia vema biashara zao.

Nakushauri uanze na hicho kidogo unachopata kwa kuanza na kijimradi kulingana kipato/uwezo wako. Cha msingi hakikisha unasimamia mwenyewe kwani ndiyo siri ya mafanikio ktk biashara yoyote iwe kubwa/ndogo.

Ni hayo tu....
 
Pole sana bro unanikumbusha mbaaaaali na huwa nasema cku zote km mm nimefanikiwa kupata jpo pakupunguzia ukali wa jua bc naamini hata ninyi mnaosota ss hv ipo cku yenu hakuna kukata tamaa ktk watu walikuwa na nyota ngumu ni mm 5 years nazurula tu!
 
Back
Top Bottom