Ushauri: Umri unaenda sina ninachomiliki

Ushauri: Umri unaenda sina ninachomiliki

Washatuharibia nchi yetu hapo sio pa kukaa tena tatizo mmesoma alafu akili bado zimelala dunia ni kubwa sana na kutembea pia kwenyewe ni shule tatizo ni wewe mwenyewe umeshamaliza kufikiri akili imefika mwisho
 
Kati ya watu usiotakiwa tegemea ni
Ndugu (Tumbo Moja au W Mbali)
Familia
Marafiki

Ukiwategemea Hawa utakufa masikini, hata wawe nacho hawawezi kukusaidia zaidi watapenda uwe hivyo ili uwaheshimu
Uko sahihi ndugu usiwategemee kabisa,,, ukweli wa maisha ni huu hata ndugu zako, marafiki wengi hawapendi utoke kimaisha uwafikie au kuwazidi....wanataka heshima kupitia shida....nina ndugu yangu aliibiwa way back dukani kwake aliyetengeneza mchongo ni ndugu ktk ukoo.
Ukianza kuona mafanikio stay tuned....vita itaibuka kali sana kwahiyo usishangae ukiwa na shida ndugu hawajali BTW wako happy ukifanikiwa they feel uncomfortable hasa kama una roho nzuri ya kuwainua wengine.
 
Uko sahihi ndugu usiwategemee kabisa,,, ukweli wa maisha ni huu hata ndugu zako, marafiki wengi hawapendi utoke kimaisha uwafikie au kuwazidi....wanataka heshima kupitia shida....nina ndugu yangu aliibiwa way back dukani kwake aliyetengeneza mchongo ni ndugu ktk ukoo.
Ukianza kuona mafanikio stay tuned....vita itaibuka kali sana kwahiyo usishangae ukiwa na shida ndugu hawajali BTW wako happy ukifanikiwa they feel uncomfortable hasa kama una roho nzuri ya kuwainua wengine.
Ni afadhali umtafute hata uliye soma nae shule ya msingi(rafiki) kuliko kumtegemea ndugu.Ndugu abaki kwa kupeana taarifa za nyumbani kwa wazazi tu,simama kivyako kuepuka lawama.
 
Salaam wanajamvi,

Jamani naomba mnipe ushauri kutoka kwenu hasa kwa wale waliofanikiwa kimaisha.

Kwanza naweza sema hapa Tanzania kusoma sana ndo kuukaribisha umasikini tu.

Kijana mimi wa kitanzania mwenye elimu ya Bachelor degree na Postgraduate Diploma hadi sasa nagonga 30 years sina cha maana ninachomiliki katika maisha yangu.

Sijui kwa sababu nimetumia muda mwingi kusoma, au hii familia niliyozaliwa ya umasikini ndo chanzo hata sijui.

Nilisoma kwa mkopo wa serikali na postgraduate nikafadhiliwa kwa kujua kwamba nikimaliza nitaingia kwenye system kupitia ualimu wa masomo ya arts imekua ndivyo sivyo.

Umri unaenda sina mtaji sina ndugu wa kuniwezesha kwa chochote kazi zimekua ngumu so nategemea kudra za Mwenyezi Mungu labda nitafanikiwa.

Najishughulisha na shughuli mbalimbali za kujiingizia kipato lakini hakikidhi mahitaji napata hela ya kula, kulipa kodi miezi 2 2 au 1.

Nina mtoto anaishi kwa mama yake, najisikia vibaya kumwona mwanangu anakua lakini hadi sasa baba yake similiki chochote kitakachomsaidia, mama yake ndo anauwezo kwa sasa wa kumjengea mazingira bora coz kipato chake kinatosha kabisa.

Sina ninachomiliki jamani, naombeni ushauri njia bora ya kuishi, namna ya kufanya ili nami niweze kutoka katika dimbwi hili la umaskini, nakiri kwamba nimesoma na kwa sasa sina ndoto tena ya kutaka kuajiriwa nina ndoto ya kujiajiri lakini sijui wapi napata mtaji, labda itokee nipate ajira ya uhakika ya kupata salary bila usumbufu hapo nitajipanga kudunduliza hela nipate japo mtaji.

Umasikini mbaya sana. Na elimu ya Tanzania inachochea umasikini.

Nipeni ushauri jamani ili mwaka 2018 niwe mtu mpya nijue nini nifanye nami nimiliki japo biashara hata ya kuuza juice, banana power hata shujaa vodka.

Ushauri tafadhali, sihitaji maneno ya kejeli nina frustration zangu.

NAWASILISHA
HAUKO PEKE YAKO,WATU WENGI WANA TATIZO/HALI KAMA YAKO!!!
 
ni kama umenigusa na mm yaani ndugu wanataka uwatetemekee wao hawakusaidii kitu
Hapo ndo wanafurahi wamepata ufalme wanaoutaka...dawa ni kuwa responsible kwa maisha yako...jenga hiyo mind set halafu komaa.......
 
Salaam wanajamvi,

Jamani naomba mnipe ushauri kutoka kwenu hasa kwa wale waliofanikiwa kimaisha.

Kwanza naweza sema hapa Tanzania kusoma sana ndo kuukaribisha umasikini tu.

Kijana mimi wa kitanzania mwenye elimu ya Bachelor degree na Postgraduate Diploma hadi sasa nagonga 30 years sina cha maana ninachomiliki katika maisha yangu.

Sijui kwa sababu nimetumia muda mwingi kusoma, au hii familia niliyozaliwa ya umasikini ndo chanzo hata sijui.

Nilisoma kwa mkopo wa serikali na postgraduate nikafadhiliwa kwa kujua kwamba nikimaliza nitaingia kwenye system kupitia ualimu wa masomo ya arts imekua ndivyo sivyo.

Umri unaenda sina mtaji sina ndugu wa kuniwezesha kwa chochote kazi zimekua ngumu so nategemea kudra za Mwenyezi Mungu labda nitafanikiwa.

Najishughulisha na shughuli mbalimbali za kujiingizia kipato lakini hakikidhi mahitaji napata hela ya kula, kulipa kodi miezi 2 2 au 1.

Nina mtoto anaishi kwa mama yake, najisikia vibaya kumwona mwanangu anakua lakini hadi sasa baba yake similiki chochote kitakachomsaidia, mama yake ndo anauwezo kwa sasa wa kumjengea mazingira bora coz kipato chake kinatosha kabisa.

Sina ninachomiliki jamani, naombeni ushauri njia bora ya kuishi, namna ya kufanya ili nami niweze kutoka katika dimbwi hili la umaskini, nakiri kwamba nimesoma na kwa sasa sina ndoto tena ya kutaka kuajiriwa nina ndoto ya kujiajiri lakini sijui wapi napata mtaji, labda itokee nipate ajira ya uhakika ya kupata salary bila usumbufu hapo nitajipanga kudunduliza hela nipate japo mtaji.

Umasikini mbaya sana. Na elimu ya Tanzania inachochea umasikini.

Nipeni ushauri jamani ili mwaka 2018 niwe mtu mpya nijue nini nifanye nami nimiliki japo biashara hata ya kuuza juice, banana power hata shujaa vodka.

Ushauri tafadhali, sihitaji maneno ya kejeli nina frustration zangu.

NAWASILISHA
Vumilia mkuu cdm wakitawala nchi utamiliki kiwanda. Kwani kwa sasa mwanachama wa cdm kujenga kiwanda ni kuwapa ujiko ccm
 
kipindi ulichokua na mkopo wa asilimia 100 ulikua huijui future sio??
Boom lako ulilifanyia anasa,kununua usafiri na kuhonga wanawake sio??
Nadhani mkuu hii mada sio level yako,endelea kuomba ushauri kwny ile thread uliyoanzisha humu jf ya kuulizia mafuta mazuri ya kupaka yatakayokuondolea chunusi na uwe na unang'aa vzr
 
Bro usikate tamaa. Kabla ya 2018 kaa tena chini fikiria nini unataka then anza taratibu kufanyia kazi ndoto yako. Ila uwe mvumilivu. Inaweza kukuchukua miaka mingine kama mitatu hivi ili kuanza kuwa stable kiuchumi. Ukitaka mabadiliko ya ghafla utafeli.
 
Hapo ndio hufikia point nalaumu sana mfumo wetu wa elimu ya kibongo kutufanya kuajiriwa tu no matter umesoma kufikia kiwango gani.Miaka ya hivi karibuni wameintoduce course ya entrepreneurship kwa baadhi ya fani kwa level ya chuo kikuu lakini huwezi kujiajiri kama hauna mtaji na taasisi za kifedha hupewi mkono kama hauna assets.
Changamoto ni nyingi mpaka kuja kufanikiwa kibongo bongo ndio maana hujipa tumaini kwa kusema "life begins at 40" you still have 10 years ya kupambana
 
Napata kitu hapa ntakifanyia kazi nataka 2018 uwe mwaka wa mageuzi makubwa ya kiuchumi kwangu
 
Pole brother,unapotaka Kumove jaribu kuangalia unanini mkononi, mfano wewe hapo tayari ni msomi umeelimika upo tofauti na wengine wengi anza na ulicho nacho mkononi /jirani kione ni fursa jitume fursa namba 1 inakuelekeza zingine nyingi.
 
Back
Top Bottom