Ushauri: Watoto wanataka kuishi na Baba ambaye aliachana na Mama yao baada ya kuanzisha mahusiano na Mwanaume mwenziye

Ushauri: Watoto wanataka kuishi na Baba ambaye aliachana na Mama yao baada ya kuanzisha mahusiano na Mwanaume mwenziye

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Kuna rafiki yangu mmoja amekutana na changamoto za kifamilia. Yeye ni singo maza, ila huwa tunapeana kampani na ushauri mbalimbali pale panapohitajika.

Waliachana na mumewe, miaka saba iliyopita na walifanikiwa kupata watoto wawili wa kiume; ambao kwa sasa mmoja ana miaka 13 na mwingine 9. Sababu kubwa ya kuachana, ilikuwa fumanizi; na mbaya zaidi baada ya kuachana, yule mwanaume alitafuta mwanaume mwenzie na kumfanya mke, wakawa wanaishi pamoja.

Siku za hivi karibuni, huyu mwanamume aliyezaa na huyu singo maza akawa anawataka watoto wake; anataka akaishi nao. Kutokana na tabia ya huyo mwanaume, mama wa watoto hayuko tayari waende kwa baba yao, kwa sababu anahofia anaweza kuwaharibu watoto kutokana na hiyo kashfa aliyokuwa nayo.

Chakusikitisha usiku huu, huyu singo maza amenipigia simu kuniomba ushauri; kuwa watoto joni ya leo wanalia na wanataka waende kuishi na baba yao. Mama kwa uchungu anafikiria, gharama alizotumia kuwalea na leo watoto wanataka waende kwa baba yao asiyekuwa na msimamo au akili za kiume. Hofu kubwa, baba yao anaweza kuwaharibu.

Nilichomshauri, hili swala walimalize kifamilia; wazazi wa pande zote mbili wakae waangalie namna ya kutatua huo mgongano.

Wakuu, leteni ushauri...
 
Una uhakika anaishi pamoja na mwanaume mwenzake au unaingizwa king usipende kuwaamini wanawake kuna mda wanavutia upande wao.
Ndio maana kwa upande wangu, nimeona lisuluhishwe kifamilia
 
Asiruhusu huyo baba ukute alishaanza kuwachezea hao watoto sasa wameanza kunogewa ,Mungu aepushe hiloo!cha kufanya au anawatia sumu mbaya aende kumshtaki kwa viongozi wa dini au mpk mahakamani.
Japo havikatazwi live vitendo vya kishiga ila bongo hatujafikia kua kama ulaya asehh!!shoga akulele mwana

Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
 
Asiruhusu huyo baba ukute alishaanza kuwachezea hao watoto sasa wameanza kunogewa ,Mungu aepushe hiloo!cha kufanya au anawatia sumu mbaya aende kumshtaki kwa viongozi wa dini au mpk mahakamani.
Japo havikatazwi live vitendo vya kishiga ila bongo hatujafikia kua kama ulaya asehh!!shoga akulele mwana

Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
Hii si kweli kuna penyenye nyingi sana
Huyoo single mother anamtaftia timing mleta uzi
 
Back
Top Bottom