1. Kama ni polisi basi yaundwa tume ya kipolisi (Maofisa waandamizi) kuchunguza ndani ya polisi kikundi cha wauaji.
2. Kama ni Jeshini basi ile idara ya ujasusi yaami Military Intelligence ichunguzwe kama ina maharamia mule.
3. Kama ni kikosi maalum kinounda vya hapo juu ni lazima kichunguzwe uzuri chaongozwa na nani, chalipwa na nani na kina nguvu ipi kiusalama wa nchi.
4. Kama ni TISS basi ijulikane ni idara ipi imepewa jukumu la kuteka, kutesa na kuua watu na kwa idhini ya nani, iwe public.
5. Kama ni raia wa nje wajulikane ama ni raia wazamiaji wa kutoka Ethiopia, Elitrea, Congo DRC au nchi nyinigne za Afrika zenye watu wasokuwa na kazi maalum.
Si twadai kwamba nchi yaongozwa na utawala wa sheria? basio hili liwe ni jambo la mwanzo kabisa kuhakikisha utawala wa sheria washika kazi yake.
Vyombo vya habari jana wamekumbuhswa na mzee Butiku kwamba wao ni mhimili wa nne katika utawala wa nchi kwamba wana jukumu la kuelimisha jamii, kuihabarisha na wana wajibu wa kuhakikisha habari hii ipo wazi masaa 24 ili kieleweke ni nani hawa watu wabaya wanoitia doa nchi.
Hili suala si dogo ni suala kubwa linohusu usalama wa raia na mali zao ambalo ni jukumu la waziri kulisimamia. Pia hili suala laweza kuzalisha hali tata ya usalama wa nchi kwamba kwa mfano kama kikundi ni kutoka nje ya nchi basi tuna shida kubwa.