Ego is the Enemy
JF-Expert Member
- Mar 21, 2014
- 8,201
- 16,246
UmenichekeshajeTukiamua kukojoa huku tumesimama inawezekana.
Wazee wa zamani walikuwa nasimama zao..... LoL
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
UmenichekeshajeTukiamua kukojoa huku tumesimama inawezekana.
Wazee wa zamani walikuwa nasimama zao..... LoL
Ulichokiongea ni kweli,nipo hapa Makambako,yote hayo nayashuhudia,watu hawafanani na pesa wanazomilimi,hawana kabisa mpango wa kupendeza.Watu wa hovyo hovyo wanaodeposit hela zao kabisa kabisa wako Makete
Wakinga balaa bwana, kuna kazee ukikakuta dukani kwake kanakula viazi vya kuchoma, hata supu kanaona anasa
Kakipeleka pesa benki kanabeba kwenye rambo lakini kwa mtazamo wa nje huwezi kukadhania
Wakinga/wabena wengi hawafanani na pesa yao
Mkuu salamu ndiyo ilimfanya muoji asitishe kuowa, kisa tuu miongoni mwa watu aliongozana nao alikuwepo kaka yake sijui baba yake mdogo, basi kufika kule kwa yule binti wakakutana na kaka wa yule binti akawasalimia mambo vp wazee basi ndugu yake jamaa alimind na akamshauri usiowe huyu mwanamke basi mwenzangu na mimi ilibidi atii amri, ila ukiangalia salamu ya mambo vp ndiyo chanzo. Na alikua kampa mimba mtoto wa watuBinafsi huwa sipendi MTU anayependekeza salamu. Ujue salamu ni aina ya malipo ama kumnunua MTU moyo wake ili akusaidie kitu Fulani. Ina mana bila ya salamu husaidiwi.
MIE hata ukinipita bila ya salamu afu unarudi umepotea njia nakuelekeza kiroho safi na hata ukinisalimia kama kuninunua ili ndipo nikuelekeze MIE naipotezea salamu yako na kama Nina muda nakupeleka mpaka unakoenda.
Warusi ukiwauliza kitu afu wakakusaidia na ukiwashukuru wanaikataa shukrani yako kwa kuuliza ya nini iyo shukrani. Ina mana wako willing kukusaidia bila hata kuwalipa.
Sasa bongo ndipo utashangaa MTU anakomalia salamu utadhani itamuwekea chakula mezani.
Binafsi sipendi kusalimiwa naonaga kama ni utumwa Fulani yaani ni lazima usalimie kila asubuhi. MIE wangu aishanielewa hakuna salamu hata kama nikitoka kwa wiki nzima. Nikirudi unapita muda kidogo tunaanza story za huku home na huko nilikokuwa.
Wazazi wangu hawakuwa watu wa kudemand salamu kila siku asubuhi. Ilikuwa ni kuamshwa kuwahi shambani basis.
Mpaka umri huu huwa nikienda home salamu ni zile siku za ugeni wiki ikishapita hakuna salamu.
Pia siamini kuwa salamu ndio heshima.
Nina imani masikini anapenda sana salamu mana kwa njia hiyo anajisikia faraja sana anadhani naye anajariwa. Masikini ndiye anayetembelea ndugu zake waliofanikiwa na kuwaongelea na kuringishia watu. Kuwa usinidharau yule karibu mkuu ni mdogo wangu nimemsomesha MIE. Ni kama Mwita weitara akasomeshwa na kaka yake aliyekuwa nauza mayai hapo kipunguni saivi sijui wanakaa kivule.
Ni mfano tu nimetolea hapa kwa karibu mkuu.
Salamu ni muhimu ila isiwe lazima jamani .yaani kuna watu wanaifanya kuwa basic needs kwao.
Binafsi nikiwaga home kwetu huwa siishi kwa furaha mana kila unayepishana naye yabidi u pay attention kwake na umpatie salamu tena usimame mpige story kidogo.sasa ole wako uje upite usalimie ukipunga mkono nakuambia ,Fulani anaringa kisa akasoma ,ama ana Hela.
Ila nikiwa town salamu sio lazima naishi kwa Uhuru hakuna MTU anayejiliza kuwa umetupita bila ya salamu rafiki.
Binafsi kunyenyekea ama kunyenyekewa sipendi.
Haya shikamooni wana jf wote waliozaliwa 65 kurudi nyuma. Wa 66 mpaka 1990 mambo vipi. Waliozaliwa 90 mpaka 2020 mnipe heshima Yangu
Unadhani kwa salamu Umepata nini katika maisha yako hata nisingekusamia si ungebaki na shida zako zilezile ama kuna kitu kimeongezeka.
Binafsi I hate salamu ingawa ni opener ya maongezi. Kuna watu naowakubali sana binafsi unamuuliza MTU kitu anakujibu mwishoni unashukuru na kumpatia salamu yake unasepa. Watu wa ivyo huwa naowanga ni matajiri rohoni kwao ni matajiri rohoni mwao!!!!!
Hao huwa wanatumwa ku deposit hela za maduka makubwa au ya jumla wala sio matajiri. Kama unaenda sana benki utawaona wengi tu hata waswahili usitishike mkuu wametumwa hao.
🤣🤣ABSA TZ
M Consult PA wangu atakuelekeza Boss.
Atakuwa mshirikina sio bure.Kuna dogo mmoja mchafu tu hivi kimuonekano anauza karanga mbichi zile zilizokobolewa na kitenga anatembeza kkoo kuanzia asubuhi na jioni ana kijiwe cha kahawa,
Siku nimekutana nae kule mbagala saku ana nyumba kubwa afu kali kinyama, na nje pana fremu 4 kuna duka kubwa tu anauza mke wake, aliniambia kwake lkn kiukweli sikuamini adi nilienda kuuliza maana nilikokua nimeenda ni karibu.
Kesho yake kaja kuniuzia karanga ilibidi nimuulize kujua labda alikua na maisha mazuri kabla, ndio akaniambia yale yote niliyoyaona yamechangiwa kwa 90% na kuuza karanga, yaani ananunua gunia zima mbichi zilizokobolewa akaomaa akitembeza na zingine anakaangia kashata adi analimaliza kwa mwezi mmoja na akikosa sana faida ni laki 7.
Aisee usidharau usiemjua
Jamani muache uchafu.Tutakuja kulaumiana bure.Hii hali wahanga wakubwa ni WANAWAKE NA ZILE NJEMBA ZINAZOISHI KIBISHOO MJINI.
Kwangu imewahi kunitokea mara 2 lkn hapa nitaeleza hii moja ambayo imepelekea kumpata huyu mama wa watoto wangu.
Mwaka fulani nikiwa zangu DASALAMA nilikuwa nina tabia ya kwenda kisuper market fulani kupata bidhaa za hapa na pale, sasa kulikuwa na mhudumu mmoha nilimwelewa saaaaaaana, nikajaribu kumsemesha lkn wapi, na hata uvaaji wangu kwa kweli haurudhishi nywele mtihani kuchana, ndevu kama brash ya chachandu, lkn pia kila nikienda huwa nilikuwa naenda na pikpk yangu Boxer, nilimfukuzia yule manzi kama miezi miwili na nusu na sikupata hata namba yake. Mwisho ikawa nikienda pale namsalimia nanunua vitu niwezavyo kwa 30k yangu ndukiiii. Ukapita mwezi bila mm kutokea pale, nyuma huko ile PISI ikaacha kazi yake nami nilikuwa sijui, ikatokea siku moja yule pisi amekuja kwa ajili ya ishu za biashara yake ofisini kwetu. Lahaulaaaaaaa anayemuona anazunguka kwenye kiti ni mimi na nina mamlaka kidogo ya kumtuma mtu na akatii, ile pisi kwanza ilishtuka mm kuniona pale, mi nkaona isiwe kesi nikateremka chini ili niende zangu pata lunch, ila nimefika mapokezi nikajisahau napiga soga na dadaetu wa pale mapokezi ile ikawa inateremka ngazi ikanikuta pale down, akanisalimia nikaitikia akaniambia samahani kuna kitu nimesahau atarudi ili tuongee, mi nkasema fresh huku nikiondoka nje kabisa ya ofisi na kuwasha gari yangu kaliii, yule dada akaniwahi kuomba lift mi nkampatia na sikutaka kabisa mazoea sijui ya kuulizana ilikuwaje wala nn, sikutaka kumpa hata nafasi hiyo nikambwaga alipotaka mi nkaenda pata BIRIANI fureeeesh. Sasa nilivyorudi yule demu akakoma lazima nimuhudumie mm, akalazimisha mi nkamhudumia akaomba no yangu tangia hapo nimemzalisha watoto 2.
Swala la kutokidhi vigezo ni sawa...ila kama uliumia nakukataliwa pia.Mwaka 2014 nilipanda kivuko kuelekea kigamboni, pembeni yangu alikaa mtoto mzuri kama mwarabu fulani hivi ana kishepu cha maana kweli kweli, nika msalimia akakausha nikarudia tena mara ya pili akaitikia kinyonge kwasababu ya mwonekano mijdevu, nywele hazijachanwa suruali jeans na tisheti form six chini kiatu tlavota
Nikamuomba namba akaniuliza wewe unaona mimi ni saizi yako! nikamjibu nisamehe.
Baadae mwaka 2014 mwishoni nilikuwa nahitaji mtu wa manunuzi kwa mkataba wa miezi 6 katika project yangu kati ya watu 45 walio apply kuomba hiyo kazi mmojawapo nilimfananisha nayeye.
Niliwaita watu wa tatu na huyu niliye mdhania akiwepo kwaajili ya interview hakuamini alichokiona maana aliponiona alinikumbuka maana ilikuwa ni miezi kama mitatu imepita.
Walifanya interview lakini yeye hakukidhi vigezo hivyo hakupata kazi,
Na alinifuata personally kuniomba radhi na kunishawishi nimpe kazi kwani ana miaka miwili bila ajira sikuweza kupata nafasi.
Mpaka sasa sikuweza kuwasiliana naye tena ingawa mwaka 2017 alikuwa akinitumia sms za salaam kiukweli sikuweza kumjibu mtu akitweza utu wangu huwa nampuuza jumla
WADADA ACHENI MAJIVUNO
Ni mawazo ambayo wengi tunayawaza laikini mwishowe yanatufanya tushindwe kua na bidii kwa kuhisi flani kafanikiwa kwa ushirikina sio kwa bidii zakeAtakuwa mshirikina sio bure.
Lazima ajute mkuu, hata mimi ningejuta pia,So anajuta kua kapoteza nafasi ya umarioo?
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Jamani muache uchafu.Tutakuja kulaumiana bure.
Kwa sababu hua mnapenda kujiona wa matawi sana kumbe wa kawaida tu[emoji1787][emoji1787][emoji1787]wanaume mnatuchora sana wadada
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]sasa mkeo unamuita demu na wewe[emoji2] mi nikajua umemuacha single mother
ni kweli ndoa bahati sio kila mtu anayo , japo mwenzangu alijitoa kimasomaso ,maana mimi nikiambiwa tafuta mwanaume wa maana uolewe hii kauli siielewi[emoji2] sasa mi nitafute mwanaume namtafutia wapi
Sio kweli ni hulka tu au tabia ya mtu....Mara nyingi wanaoongoza kupendeza sanaa hawanaga kitu kabisa
Wenye pesa hawajali sana mambo ya kuvaa vaa
Kwa vile yeye ni katibu mkuu ndio asisalimie? Alishindwa nini kusalimia, kujitambulisha na kuomba huduma? Tujenge utamaduni wa kuheshimu kazi za watu wakiwa maofisini kwao hata kama umewazidi cheo.Juzi tu NMB Dodoma:
Jamaa flan kavaavaa tu afu na midevudevu hivi
Kaenda NMB ATM kakuta na wadada wa benki wameweka meza ya kutoa huduma kwa wateja pemben hapo. Akafika tu kauliza (bila hata kusalimia).....kwanini kadi yangu inakataa kuniunganisha NMB mkononi
Dada kamjia juu...."kwanza salimia;...vipi habari za huko,...haya tukusaidie nini??"
Jamaa hakupokea. Mie nawaangalia tu.
Dada karudia tena ...."vipi mzima mwenzetu?? Za ulikotoka??!.....mbona umekuja kasi sana??!"....
Jamaa anaeaangalia tu. Mara akauliza...."ivi ni lazima kusalimia/ au kupokea salam ya mhudumu ili nipewe huduma NMB???...
Wakaanza kumshangaa ..."unatokea wapi wewe, yani unakuja kuvamia tu bila kusalimia..." ....wamamzodoa flan.
Jamaa akaingia Benki ndani. Straight kwa Meneja. Nafkiri hakueleza shida aliyopata nje. Alimueleza tu kama kutaka kusaidiwa shida yake. Sijui ndani waliongea nini??
Wametoka na meneja...hadi pale ATM kwenye meza ya wale wadada....meneja akiwa kashika mkononi kadi ya yule mshua....akawambia wale wadada mmoja wao (sikumbuki jina)...
Meneja: .....hebu msaidie Katibu Mkuu hapa kumuunganisha na NMB Mkononi...(Meneja akaongeza:....mkuu hapa utahudumiwa)...mara meneja katuomba wote wa kwenye foleni ya ATM..."naomba ndugu tumpishe kiongozi anajambo kidogo kwenye ATM ...samahani"...wakaingia ATM meneja, mshua na yule dada.
Wakafanya mambo humo ...kidogo wakatoka. Tukaendelea.
Meneja akamsindikiza yule mshua hadi kwenye gari akaondoka meneja anapunga mkono.
Niliwaangalia wale akina dada mavi yalivyowagonga chupi. Walitoa macho sana wakawa na wasiwasi mkubwa....
Walimchukulia poa
Eti eehKwa sababu hua mnapenda kujiona wa matawi sana kumbe wa kawaida tu