Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

Mimi kila nikienda kutembea sehemu moja hivi walikuwa wanajua mimi ni dw
Dereva tu , kutokana na uvaaji wangu simple na kujichanganya.

Kuna mitaa naenda ,natembelea hawajawahi kujua km mimi ni mtu wa aina gani ,naonekan mlugaluga tu ,maana kuna mda wa kazi nakuwa smart na weekend kuzugazuga tu....


Huwa naruhusu wanchukulie poa tu .....i dont need attention or mtu kuniheshimu kwaajili ya kitu au kwa sabanu ni fulani ....


Heshimu kila mtu , mtu yoyote anaeza kuwa msaaada kwako wakati wowote
 
Kwanza naomba 'nidiclee' kwamba mm ni mmoja wa ME ambae si mtu wa fashion, yani mimi sijui kuvaa kabisa na sina hiyo passion ya pamba pamba. Nishawahi kusemwa sana na ma-ex wangu kuhusu uvaaji wangu lakini haikusaidia kitu.

Sasa weekend iliyopita nilienda sehemu moja flani hivi amazing, chimbo la uhakika haswaa, limejitenga na limetulia kweli. Nilipigilia kipensi changu na ka t-shirt flan hivi local nikachagua sehem nikakaa, kutizama vizuri nikaona kuna meza amekaa mdada mmoja hivi and of coz she is gud looking nikaamua kujitosa angalau kumpa hata hi 'coz tulikuwa wateja 2 tu, nikamfata nikamsalimu.

Yule dada kwanza alinishusha kuanzia juu mpaka chini then akaitikia salamu yangu ki-design kama namsumbua flani hivi. Nikaomba kujumuika nae kama asipojali. Jibu lake ndo lilinitoa confidence kabsa, alinambia: "Kwahiyo kaka unadhani kila msichana akikaa peke yake anahitaji kampani? Hapana sihitaji" Dah, mwanamme nikajizoazoa pale nikarudi nilipokaa. Nilikaa kama masaa ma3 hivi nikaamsha zangu. Sasa kilichotokea jana ndo kimenifanya niandike huu uzi.

Nilipokea maagizo kuanzia J3 ya wiki hii kuwa leo watakuja watu wa Taasisi flani ya kifedha kutoa semina kwa sisi wafanyakazi kwa ajili ya kutushawishi kujiunga na huduma za Taasisi yao, hivyo mimi nikapewa jukumu la kuwakaribisha na kuwapeleka sehemu ambapo semina itafanyika.

Asubuhi mida kama ya saa 3 hv ugeni ukafika, walikuwa watu kama 7 hivi, kati yao alikuwepo yule dada nilieonana naye weekend.

Wakaingia ofisini nikawakaribisha, wakati mkubwa wao anatoa introduction macho nikayakaza kwa yule dada, bahati nzuri tukagonganisha macho, akashtuka flani, nikajua kashanikumbuka.

Baada ya semina kuisha ikafika kipindi cha watu kujiunga sasa kwa walioshawishika. Nikamfata yule dada nikamuomba aje anielekeze namna ya ujazaji fomu. Alivyofika tu, nikamuuliza "Unanikumbuka?" Akachekaaa, akaniambia "Yani wewe, sikutarajia kama unaweza kuwa unafanya kazi huku", nikamuuliza ulitarajia niwe nafanya kazi wapi? Akaishia kucheka tu. Mawasiliano yake kanipa; fresh bila shida kabisa.

Sasa naomba kuuliza wadau, mshawahi kukutana na situation ya namna hii?
Q were sss
 
Miaka mingi zamani kama 10 imepita nilikua nafanya kazi mahali kama mtu wa sales, sasa jioni dakika chache kabla ya kufunga akaja jamaa mmoja kavaa kawaida tu yule jama alikua mstaarabu sana, sasa mimi nikawa namjibu shortcut sana plus muda umeisha nataka kusepa halafu nikaona kama hawezi nunua mzigo wenyewe ulikua kama wa 32 hivi mwaka 2010. Nikamtupa jamaa nikamwambia kesho uje ulete document flani, akaniuliza nije saa ngapi? Nikamwambia saa nne asubuhi jamaa akaga na mimi nikamsahau.

Lahaula saa nne kamili bwana jamaa kaja kapiga magwanda hatari aisee, kumbe ni kanali wa jeshi kachafuka plus ana bodyguard au dreva (sikujua diference), aisee jamaa kumbe alikua head of logistic wa JWTZ Tanzania nzima(alinipa card) yule jamaa alipata huduma ambayo hajawahi pata mahali, akawa mshkaji wangu mno aisee.

Ila sisi wabongo tuna tabia ya kujudge mtu kwa muonekano au mavazi yake mno aisee na nahisi jamaa alijua ile siku ikabidi kesho yake anikomeshe, tokea ile siku mpaka leo naheshimu kila mtu na imenisaidia sana deals nyingi mno.
Kwaiyo ulimuogopa canal...
 
Wanawake walosoma na watumishi wana changamoto sana,wengi wao huachika baada ya kuolewa ndani ya miaka 10 ya ndoa....

Nakubali. Nimeoa mtu wa namna hiyo ndoa yangu imeshikwa na Kamba nyembamba mno ya mahusiano.
Tuna mwaka wa 8 kwenye Ndoa lakini sina uhakika kama huu mwaka wa 8 nitaumaliza na yeye. Kwa kiasi kikubwa kamba ya Ndoa imeshikwa na kaka yangu, akiiachia ndoa imeisha.
 
Kuna siku niliazima gari nikaenda pale best bite kuchukua zaga.

Sasa nilivyoingia ndani nikakutana na pisi tatu za kwenda zinatoka ndani, nikazipa hi zikachuna full kunipandisha na kunishusha, nikaona POA tu nikafuata kilichonipeleka.

Sasa ile natoka nje nikazikuta ziko bize zinajisnap kwenye gari niliyokua nayo, hiii bagoshaaa, mbona walikoma kunijua.

Nilianzisha zogo la maana makusudi kabisa, nikaita mpaka uongozi wa pale nikawaambia wawaambie wateja wao wafute picha zote walizopiga gari yangu otherwise niite Askari pale Obey waniambie wana lengo gani na picha za mkwaju wangu?

😀😀
 
Hapo full kujichekelesha tu
It was a suprise kwangu.

Jirani yangu aliekuwa anajifanya ni boss wa Ikulu mtaani muda wote kanuna na miwani yake mieusi alikuja kunihudumia Chai Ofisini kwa Mama Salma Kikwete wakati wa WAMA, kumbe Alikuwa Office attendant pale tena wale wa oya oya na mie na wenzangu tulienda kupeleka project paper ya ki NGO chetu ambacho ni Hayati kwa sasa kuanzia 2015.
 
Nakubali. Nimeoa mtu wa namna hiyo ndoa yangu imeshikwa na Kamba nyembamba mno ya mahusiano.
Tuna mwaka wa 8 kwenye Ndoa lakini sina uhakika kama huu mwaka wa 8 nitaumaliza na yeye. Kwa kiasi kikubwa kamba ya Ndoa imeshikwa na kaka yangu, akiiachia ndoa imeisha.
Chief pole sana
 
Kuna mheshimiwa mmoja alikua akifika ofisini kwetu kila mtu anatetemeka, siku hiyo kaja kanikuta nikamkazia naongea nae kama mshkaji tu huku namuuliza maswali hadi mwenyewe akaingia ubaridi akaniuliza wewe kabila gani nikamwambia mimi mswahili tu, muda huo tunaongea ofisi nzima wamekimbia namuona boss kajificha anasikiliza tunachoongea, kuanzia siku hiyo yule mzee akija ofisini anaulizia yule mswahili yuko wapi, nikifika namzingua hadi tumekua washkaji kaomba namba yangu akiwa na shida ananicheki, siku hizi hata staff wengine hawamuogopi kivile kama mwanzo
 
Kuna jamaa mmoja alishawahi kunikejeli na kunidhihaki..
Akitaka kunipiga,,hata watu wakimsihi asinipige,,
Anatamba tupewe dk 10 aning,oe meno..yote ya mbele.
Basi alijaza watu sana pale mtaani.

Si unajuwa tena unapohamia mitaa mipya? Watu hawakujui vzr.
niliokolewa na Mzee mmoja Mwenye busara,,ili jamaa asinipige.

Lakini jamaa alikuwa serious kutaka kupigana na mm,
Kiisa cha kijinga kabisa..

Ikawa jamaa kila akiniona,,
ananikoromea,,Mimi nampuuza tu.

Siku moja huyo jamaa alikuja kwenye gym yetu ya mazoezi bila kujuwa.
akataka aanze kujiunga,,ili afundishwe ngumi..

Alipokuja akapewa utaratibu ,
halafu akaambiwa na vijana subiri mwandende afike..
Yeye ndy mpango mzima humu.
Jamaa alishtuka sana aliponiona kumbe mwandende mwenyewe ngumi cherehani ni Mimi..
Jamaa uso wake ulikuwa mdogo kama kijiko cha chai..

Nilichokifanya niliomba jamaa aanze na mimi ulingoni,,
Ili kupima uwezo wake,,

Kilichofata ni mayowe na vilio kutoka kwa jamaa..

Usimdharau usiyemjuwa.,
 
mods kuweni makini na UPDATE ya huu uzi,nashauri baada ya siku mbili muunganishe kwa ule wa RIKIBOY.hiyo namba iliyochukuliwa hiyo.
 
Binafsi huwa sipendi MTU anayependekeza salamu. Ujue salamu ni aina ya malipo ama kumnunua MTU moyo wake ili akusaidie kitu Fulani. Ina mana bila ya salamu husaidiwi.
MIE hata ukinipita bila ya salamu afu unarudi umepotea njia nakuelekeza kiroho safi na hata ukinisalimia kama kuninunua ili ndipo nikuelekeze MIE naipotezea salamu yako na kama Nina muda nakupeleka mpaka unakoenda.

Warusi ukiwauliza kitu afu wakakusaidia na ukiwashukuru wanaikataa shukrani yako kwa kuuliza ya nini iyo shukrani. Ina mana wako willing kukusaidia bila hata kuwalipa.

Sasa bongo ndipo utashangaa MTU anakomalia salamu utadhani itamuwekea chakula mezani.

Binafsi sipendi kusalimiwa naonaga kama ni utumwa Fulani yaani ni lazima usalimie kila asubuhi. MIE wangu aishanielewa hakuna salamu hata kama nikitoka kwa wiki nzima. Nikirudi unapita muda kidogo tunaanza story za huku home na huko nilikokuwa.

Wazazi wangu hawakuwa watu wa kudemand salamu kila siku asubuhi. Ilikuwa ni kuamshwa kuwahi shambani basis.
Mpaka umri huu huwa nikienda home salamu ni zile siku za ugeni wiki ikishapita hakuna salamu.

Pia siamini kuwa salamu ndio heshima.

Nina imani masikini anapenda sana salamu mana kwa njia hiyo anajisikia faraja sana anadhani naye anajariwa. Masikini ndiye anayetembelea ndugu zake waliofanikiwa na kuwaongelea na kuringishia watu. Kuwa usinidharau yule karibu mkuu ni mdogo wangu nimemsomesha MIE. Ni kama Mwita weitara akasomeshwa na kaka yake aliyekuwa nauza mayai hapo kipunguni saivi sijui wanakaa kivule.
Ni mfano tu nimetolea hapa kwa karibu mkuu.

Salamu ni muhimu ila isiwe lazima jamani .yaani kuna watu wanaifanya kuwa basic needs kwao.
Binafsi nikiwaga home kwetu huwa siishi kwa furaha mana kila unayepishana naye yabidi u pay attention kwake na umpatie salamu tena usimame mpige story kidogo.sasa ole wako uje upite usalimie ukipunga mkono nakuambia ,Fulani anaringa kisa akasoma ,ama ana Hela.

Ila nikiwa town salamu sio lazima naishi kwa Uhuru hakuna MTU anayejiliza kuwa umetupita bila ya salamu rafiki.

Binafsi kunyenyekea ama kunyenyekewa sipendi.

Haya shikamooni wana jf wote waliozaliwa 65 kurudi nyuma. Wa 66 mpaka 1990 mambo vipi. Waliozaliwa 90 mpaka 2020 mnipe heshima Yangu

Unadhani kwa salamu Umepata nini katika maisha yako hata nisingekusamia si ungebaki na shida zako zilezile ama kuna kitu kimeongezeka.


Binafsi I hate salamu ingawa ni opener ya maongezi. Kuna watu naowakubali sana binafsi unamuuliza MTU kitu anakujibu mwishoni unashukuru na kumpatia salamu yake unasepa. Watu wa ivyo huwa naowanga ni matajiri rohoni kwao ni matajiri rohoni mwao!!!!!
10 kilotons of TNT pitia hapa..
 
Kuna jamaa mmoja alishawahi kunikejeli na kunidhihaki..
Akitaka kunipiga,,hata watu wakimsihi asinipige,,
Anatamba tupewe dk 10 aning,oe meno..yote ya mbele.

Basi alijaza watu sana pale mtaani.

Si unajuwa tena unapohamia mitaa mipya? Watu hawakujui vzr.

Basi niliokolewa na Mzee mmoja Mwenye busara,,ili jamaa asinipige.

Lakini jamaa alikuwa serious kutaka kupigana na mm,,kisa cha kijinga kabisa..
Basi ikawa jamaa kila akiniona,,ananikoromea,,Mimi nampuuza tu.

Siku moja huyo jamaa alikuja kwenye gym yetu ya mazoezi bila kujuwa.

akataka aanze kujiunga,,ili afundishwe ngumi..

Alipokuja akapewa utaratibu ,halafu akaambiwa na vijana subiri mwandende afike..
Yeye ndy mpango mzima humu.

Jamaa alishtuka sana aliponiona kumbe mwandende mwenyewe ngumi cherehani ni Mimi..

Jamaa uso wake ulikuwa mdogo kama kijiko cha chai..

Nilichokifanya jamaa niliomba aanze na mimi ulingoni,,
Ili kupima uwezo wake,,

Kilichofata ni mayowe na kilio kwa jamaa..

Usimdharau usiyemjuwa.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ukampa za chembe?
 
Napenda kusema ila kutokana na mambo usiri wangu ngoja niendelee kusoma comment zenu
 
Sio kuwasimanga ndio uhalisia huo... Nakumbuka nilienda duka moja la dawa kubwa tu kuulizia dawa flani hivi.. nikafika nikamsalimia anaitikia kama hataki. Nikamuulizia jina la dawa akanitajia na bei ilochagamka kwa kweli, Kwa jinsi nilivokuwa nimevaa ni kawaida tu basi alidhani sitoweza kununua akashangaa tu nafungua mkoba nampa hela yake na ghafla akaanza kunichangamkia na mie nikampuuza tu

Sent from my Redmi 8 using JamiiForums mobile app
mkoba tena
 
Mimi kila nikienda kutembea sehemu moja hivi walikuwa wanajua mimi ni dw
Dereva tu , kutokana na uvaaji wangu simple na kujichanganya.

Kuna mitaa naenda ,natembelea hawajawahi kujua km mimi ni mtu wa aina gani ,naonekan mlugaluga tu ,maana kuna mda wa kazi nakuwa smart na weekend kuzugazuga tu....


Huwa naruhusu wanchukulie poa tu .....i dont need attention or mtu kuniheshimu kwaajili ya kitu au kwa sabanu ni fulani ....


Heshimu kila mtu , mtu yoyote anaeza kuwa msaaada kwako wakati wowote

I JUST MET MY TWIN IN THIS COMMENT . Cheers to that [emoji3577] you are truly living a true life . Mimi pia ndio huishi hivyo
 
dah na mim umenifanya nilete kisa changu ambacho hakina hata miezi miwili.
kuna mdada jina yupo katika ofisi fulani ni majirani zetu(home).Ni wale watu wanaoringa kupita kiasi ukimsalimia kama hakuoni vile( hii ishatokea kama mara 3) last time niko zangu na town anafanya kazi pale benjamin mkapa,nmemkuta yupo na wenzake wakati huo nilikuwa niko na kaka yangu mkubwa.

Nikamchangamkia ila mwenzangu kanilia buyu namtambulisha kwa bro kuwa huyu ndo jirani dah mixer mfyonyo juu hakuna siku roho ilikuwa inaniuma kama siku siyo.

sasa week kama 3 nyuma natokea moro nmeingia kama saa 6 hivi nikasema ngoja sku ya leo nikasalie pale upanga maamur ni mskiti ambao waislamu wengi sana wanapenda kuosha maiti pale na kwenda kuzikia makaburi ya kisutu.

Nilivyofika pale pakawa kama na stori za chini kwa chini kuwa muosha maiti amekimbia baada ya kuosha maiti zaidi ya tano kitu ambacho syo cha kawaida, basi kwenye maongezi maongezi ikajulikana kuwa kuna maiti kama 2 zimeshndwa kuoshwa ndugu hawajui na muoshaji kakimbia(hofu ya corona)

Basi tukajitokeza mimi na mwenzangu tukaingia chumba cha maiti tulikuwa kama wa 4,tukaiosha ile ya kwanza,then tukafata ile ya pili zote tukaandaa safi kabisa ila ile ya pili niligundua alikuwa na baba wa yule dada maringo.

wakati tunatoka kuosha ndugu wakatuvuta pembeni wakatupa kama laki 3,wenzangu walichukua ila mimi sikuchukua hata cent sasa kumbe aliyekuwa anatoa hela ni mdogo wa yule(dada maringo) ambae anaishi nairobi kaja kumzika mzee wake but hanijui.

basi tukachukua maiti tukaenda zetu kuzika makaburi ya kisutu, wakati narudi zangu maeneo ya home ndo nakuta msiba sasa huku zogo pembeni likiwa ni muosha maiti kukimbi, basi jamaa akaniona mdogo mtu tukasalimiana pale ile furaha aliyokuwa nayo akanishika mkono mpaka uwani ambako kulikuwa na dada zake na mjane akanitambulisha na jinsi nilivyowasaidia dada mtu(cha maringo) aliangua kilio kupita maeleozo akaniomba namba nkampa.

baada ya kama dakika 30 baada ya kurudi home nikatumiwa mesage kama gazeti ya kuniomba radhi/msamaha mie nka act humble tu japo kila siku anataka tuonane but kila akinipigia namwambia niko moro japo anafosi anitumie hata nauli nikaonane nae au aje yeye but namchomolea.

katika maisha usimdharau mtu kwani huwezi jua nani atakaekufaa kwani unaweza kuwa trilionea but msaada wako ukatoka kwa mwenye kupata sh 500 kwa siku
 
Back
Top Bottom