Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

Mimi kuna jamaa tumesoma wote form 1&2 tulikuwa washkaji maana ndo tulikuwa tunaongoza class
Nikafukuzwa so 3&4 tulikuwa tunakutana likizo tu
Baada tukapotezana Ila me nilikuwa napata data zake alimaliza degree ya mambo ya afya akaingiza jeshi then akapelekwa mondul kusomea sijui vyeo then akapangwa mikoan huko
2020 sm inaita ni jamaa " Flan vip? Za siku niomeambiwa uliacha kazi ya ualim now unapiga umachinga dar? Tuonane basi ndg" ni kweli niliachaga ualim nikajichanganya kariakoo kabla sijatoboa kibiashara ambayo hakuwa anajua kuwa nilitoboa tena kwa kiwango kikubwa
Basi tukakutana Mliman me ndo nilitangulia pale Grano
Jamaa akaja "agiza chochote ntalipa kaka " mbwembwe nyingi
Me na mwili mdogo halaf kwenye uvaaji me ni 0% so ngumu sana mtu kujua huyu yuko vzr au la!
Tukiwa pale dem wangu akaniambia nimfate kazin kumrudisha home alkkuwa mjamzito nikamwambia mshkaji akajibu " haina shida na usafir kaka twende tutamchukua tu nishanunua gari siku hizi mambo yangu fresh "
Nikakubali tukatoka nikamwambia tupite nichukue langu tuongozane ndo anaanza kushangaa " kwan una gari? Machinga ana gari mura au nimedanganywa!?"
Tumefika mzee anaona BIMA imepaki nafungua namwambia twende na hii tukirud tutapitia yako
Jamaa alikosa aman sikujua why ila alikosa aman kabisa
Tumemaliza kule namrudisha Mliman kumbe ana Swift old mole dah jamaa tangu pale alikata mawasiliano mpk leo tunaview tu status
😅😅😅Hii chai wakati et kaka Extrovert
 
It was a suprise kwangu.

Jirani yangu aliekuwa anajifanya ni boss wa Ikulu mtaani muda wote kanuna na miwani yake mieusi alikuja kunihudumia Chai Ofisini kwa Mama Salma Kikwete wakati wa WAMA, kumbe Alikuwa Office attendant pale tena wale wa oya oya na mie na wenzangu tulienda kupeleka project paper ya ki NGO chetu ambacho ni Hayati kwa sasa kuanzia 2015.
😂😂😂😂🙌🙌
 
Story
Kuna dada mmoja tajiri sana alikuwa anamiliki ndinga lake kali aina ya mercedez benz latest model.
Bac siku moja akawa amesafiri nnje ya mji(country side) isivyo bahati gari lake likaharibika na alipokuwepo hamna garage au usaidiz wowote! Maeneo hayo palikuwa na mzee ambaye umri umeenda (mstaafu ambaye ameamua kutulia zake nnje ya mji),Bac mzee baada ya kuona gari la bibie limeharibika at the middle of nowhere,

Mzee:Akamuuliza naweza kukusaidia?
Bibie:Akawa anampuuzia huku akionekana kumtafuta mtu kwenye simu.
Mzee:Acha niangalie tatizo ni lipi mzee akasisitiza
Bibie:Hutaweza kufanya chochote haya sio yale magari ya enzi zenu.
Mzee:Hakujibu akasogea karibia na gari akafungua boneti hazikupita dakika 3 akawa amemaliza akamwabia bibie awashe saa ngapi gari halijaitika!
Bibie:Kwa mshangao akamwambia mzee nikupe kitu gani kwa msaada huu sema chochote!
Mzee:Sihitaji chochote
Bac kwasababu mzee alionekana kutotaka chochote bac....
Bibie:Akamwambia Ahsante akajitambulisha kuwa anaitwa Nataliah
Mzee: Akajibu karibu naitwa mercedez benz.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣Chai
 
Kuna siku niliazima gari nikaenda pale best bite kuchukua zaga.

Sasa nilivyoingia ndani nikakutana na pisi tatu za kwenda zinatoka ndani, nikazipa hi zikachuna full kunipandisha na kunishusha, nikaona POA tu nikafuata kilichonipeleka.

Sasa ile natoka nje nikazikuta ziko bize zinajisnap kwenye gari niliyokua nayo, hiii bagoshaaa, mbona walikoma kunijua.

Nilianzisha zogo la maana makusudi kabisa, nikaita mpaka uongozi wa pale nikawaambia wawaambie wateja wao wafute picha zote walizopiga gari yangu otherwise niite Askari pale Obey waniambie wana lengo gani na picha za mkwaju wangu?
😂😂😂😂 hii kali!!
Km nakuona ulivyokiwasha afu ukute ni kafupi
 
Naenda zangu dar mida saa 3 ivi kutoka dodoma, nimekurupushwa tu kwa ofis nikaona sio mbaya nikapita zangu pale stend ya cbe kwa mama bwashee hua ana supu nzuri gari niliacha inaoshwa kona pale, basi wakat naingia pale nikakuta wadada wanne pisi haswa na mshkaji moja nao wanaingia na mabegi yao nikawasalimia kwa mbwembwe sana mi ni mtu utani sana, duh nilipandishwa na kushushwa aisee, binti mmoja tu ndo alipokea salam wengine hata habar na mimi hawana.

sijakoma nikaendelea kuwachangamkia jamani mnaenda dar nina usafiri? wakaniangalia tena juu mpaka chini nimevaa simpo sana kipensi na sendoz, yule yule dada aliyenipokelea salam ndo akajibu ndio boss, nikamwambia mbele yao we unaonekana mstaarabu sana hutolipa nauli, ajabu hata mwanaume mwenzangu eti kama hanioni....
basi tumekula pale nikainuka nikamuaga yule mrembo nakuja nafata gari sogea pale pemben ya barabara akacheka akasema sawa bos, nikafata chuma nafika pale nawaona wanajivuta lakin wadada wa3, mdada mmoja na mshkaji wamekaa zao hawana hata habari...
Punguza shobo
 
Mtu akikuchukulia poa mdharau na muone yeye ndio mjinga mtu mwerevu siku zote amchukulii poa tu ila mtu mjinga ndiio anachukulia mtu kinamna gani ....Its just a matter how you handle stupid people and ignore the situation
 
Kitasa kilijilock akiwa yupo nje ndani kawasha Jiko la Gesi
Ni Manzi fulani anajiona sana
Alafu MTU pekee wa kumsaidia ni Mimi
Siku za nyuma alikua hanisalimii akiniona ananiona namna gan fulani
Kaanza kuomba Msaada
Mwisho akaambiwa aje kwangu
Akanigongea mlango kwa aibu
Still bado akawa ananidharau kwamba nitaweza kweli kutoa lock?
Siku HIO hata ningeomba Mbunye nahisi ningepewa
SIO kwa kuomba kule
Nikagoma akaniganda km ruba
Kidume nikaenda kushugulika mlango ukafunguka
Nusura aniambie njoo ndani uniwashe kimoja alivyofurahi
Kuanzia hapo ananiheshimu
Dharau zimeisha

Usimdharau usiemjua haujui lini atakusaidia na Wapi atakusaidia
 
Kuna siku niliazima gari nikaenda pale best bite kuchukua zaga.

Sasa nilivyoingia ndani nikakutana na pisi tatu za kwenda zinatoka ndani, nikazipa hi zikachuna full kunipandisha na kunishusha, nikaona POA tu nikafuata kilichonipeleka.

Sasa ile natoka nje nikazikuta ziko bize zinajisnap kwenye gari niliyokua nayo, hiii bagoshaaa, mbona walikoma kunijua.

Nilianzisha zogo la maana makusudi kabisa, nikaita mpaka uongozi wa pale nikawaambia wawaambie wateja wao wafute picha zote walizopiga gari yangu otherwise niite Askari pale Obey waniambie wana lengo gani na picha za mkwaju wangu?
Hapo walikoma kulinga Mijuto kwasana 🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom