Ushawahi kuhisi upo single ndani ya ndoa?

Ukisema wanawake tunakera vipi mleta mada angesema wanaume wanakera?!

Sema mkeo anakera, usiunganishe wengine kwa madhaifu ya mkeo! Kila mtu ana mapungufu yake na tunatofautiana!
 
Wewe unapenda usipopendwa, alafu mwanaume alishakuonyesha tabia za ajabu toka mwanzo (mlivyonuniana hadi kwenye kufunga ndoa mkasemeshana muda wa kuvishana pete) tatizo wanawake tunapenda kujidanganya kwamba atabadilika akinioa, kumbe tunabeba mabomu ambayo ndio km ilo lako!

Fanya maamuzi ambayo moyo wako utakuwa na amani na kuanza mwanzo si ujinga kuliko kukaa na mtu km upo jehanamu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mchukue Masai dada mkae mahali patulivu muongelee changamoto zenu kwa kina mnaweza kupata ufumbuzi.....ila inauma mnara unasoma 6G alafu simu inazingua kuwaka[emoji16][emoji16] pole sana mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukisema wanawake tunakera vipi mleta mada angesema wanaume wanakera?!

Sema mkeo anakera, usiunganishe wengine kwa madhaifu ya mkeo! Kila mtu ana mapungufu yake na tunatofautiana!
Mh!....
 
Umetuchamba mkuu [emoji3][emoji3][emoji3] vice versa is true
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sister nakosa hata cha kushauri, ngoja nile pozi kwanza
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Samahani Kama nitakukwaza mkuu, laiti ya kwamba wewe ndio ungekuwa dada au ndugu wa karibu hiyo ndoa ingekuwa imeshavunjika. Ndugu wengi (hasa wanawake) wanahukumu kwa kusikiliza upande mmoja.

Nakushauri Kama una ndugu ana matatizo au itatokea ana matatizo ya ndoa tafdhali kwepa kumpa ushauri. You're too emotional!
 

Kuwa na amani hauwezi kunikwaza, Wala sipo emotional, nafikiria sawasawa tu, malalamiko ya masai dada hayajaanza kuletwa humu leo, unlike others mimi sio mnafiki na siwezi kuwa.

Btw hakuna aliyejibu maswali yangu hapo juu, mnataka huyu dada ayavumulie haya mpaka lini? Ofcourse mi huwa sishauri watu waachane huwa nawashauri watu watengane kwa muda, atakayeiona thamani ya mwenzie atatafuta suluhu mapema sana.
 
anitumia fursa ya wewe kuwajali watoto kukutesa wewe kivipi??

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Dear mi nimeshauri nilichoona ni sawa , Mwisho wa siku its HER VS HER, na wala sijamlenga masai dada tu, sikiliza cases nyingi za ndoa utagundua mambo ni hovyo hovyo sababu nafikiri watu hushindwa kuweka standars toka mwanzo na upendo ni mdogo baina yao au umeegamia sehemu moja.

Am afraid kuwa mnajitahidi kufit in na kuishi maisha ya wanaume ukija kushtuka una 55 hakuna ulichofurahia maishani zaidi ya kujitahidi kukubalika kwa mumeo na nduguze. Can’t life be win win out there, kwamba unamkopesha mtu furaha yako naye kesho anakukopesha ya kwake? I personally do believe maisha yoteee yanachangamoto na ya ndoa yakiwemo, je hii imekaaje mtu aliyeratajiwa kuwa a shoulder to lean on ndiye anageuka mtesaji? Nani atampa unafuu huyu dada!? Jamii inataka aanze kuchepuka ili ipate pa kubebea bango?

And hakuna popote nimeandika uzungu dear, toka lini self love ikawa uzungu? kuna mtu huko juu kanishauri nisipende kusikiliza upande mmoja, hebu katika hali ya kawaida tujiulizeni huyu dada alimkosea nini mumewe tangu mwanzo kudeserve haya? Kuna makosa makubwa kama usaliti, ushirikina, kutukana au kudharau wazazi ambayo adhabu zake zinafahamika na si hizi anazopitia!? Na je ameambiwa ataadhibiwa hadi lini ili ajue kabisa anavumilia hadi lini hahaha!
 
Ndoa ikishaingiliwa na ndugu na mwanaume asipate akili ya namna ya kusimama na nafasi yake ni kazi sana! Kitu ambacho ungepuuza ni hao ndugu na kuwa strong na vimaneno vyao maana uko kwako, pili kubaliana na hali ya upweke na wewe mpuuze kwa muda ingawa inauma ila inaweza saidia kiasi kuwa bize na mambo yako km ni job nenda kawaida isikuathiri ukashindwa kazi, pambana lipa deni na usiulizie tena habari za nyumba, usiulize habari za baby mama wake, vumilia japo inauma ila simama kivyako ata km mnalala kitanda kimoja fanya km hujishuhulishi naye ila ukimhudumia kwa nafasi ya mume......baada ya hapo waza maendeleo ya mwanao kivyako kama uko job au ni biashara unafanya wekeza kwa ajili yako na mwanao huyo mwanaume kama hana akili ya kuisimamia familia yake ukimwendekeza utaishi kwa dhiki sana ni lazima ajue maisha yanaenda hata bila yeye kuwepo
 
Masai its obviously bado unampenda sana mumeo na unatamani mambo yakae sawa. From the look of things; mumeo hivyo anavyokufanyia ndivyo alivyo na hana mpango wa kubadilika (labda akishakuwa mzee ndo atambue thamani yako as majority ya wanaume wa kiafrika walivyo). Kama unataka amani; amua kubadilika wewe mweyewe. Hupati furaha kwa mumeo so jifunze kujipa furaha wewe mwenyewe. Ukiishi kutegemea kuwa mume atabadilika utazidi kujiumiza mwenyewe; he ain't gonna change soon

Kama baby momma ndugu ndo walimuondoa; dont be surprised ndugu wakikuletea hekaheka. Kwa sababu bado unataka kuendelea na mumeo

1. Ujinga/ visa vya mtu yoyote visikupe stress. Wakija wakigoma kupika sijui kufua, waaache. Hao ni wapita njia tu; waache wafanye wafanyavyo as long as hawakutoi roho, basi wewe wapotezee. Kwa sababu hata ukilia au ukinung'unika, mume wako still atasimama na ndugu zake; sasa kwa nini ujiumize. Let Karma sort that shit itself

2. Huna control juu ya mtoto wa mumeo. Whatever opinion you have on her, keep that to yoursef. Mumeo labda anakuwa over-protective kwa binti yake ili kucompensate muda ambao anakuwa hayupo. Hata akihama chumba na mwanae wewe relax, uzuri mtoto si anakuja na kuondoka tu. Chochote utakachokisema ndo utageuziwa kibao kuwa humpendi mtoto, so inamfanya mumeo aendelee kumchagua mtoto wake over you.

Usicriticize malezi anayolelewa; utaonekana tu kama unajifanya ndo kungwi wa malezi. Since mtoto ana wazazi wake; waache wao ndo waamue wanamlea kwa style gani
Seems like you spoil that girl so much hadi kufikia kumlipia ada. Kama unafanya kutoka moyoni basi Mungu akubariki. Ila kama unafanya just to prove that you are a good step mom; just quit it. Itakuumiza sana pale utakapoona hauwi appreciated and siku utakapoacha kumfanyia baadhi ya vitu; utaonekana mnafiki tu. And mwingine anaweza define kama unataka kuichukua nafasi ya mama mtu kwa mtoto wake; utazua ugomvi bure. So know and stay in your limits when it comes to that lil gal.

3. Get a life. Maisha yako yasi-revolve around mumeo, mtoto wake na ndugu zake. Its high time you start investing in yourself and your kid. Yape na ongeza thamani kwenye maisha yako. Hayo mawazo ya sijui nta-deal vipi na mume na ndugu zake; yaelekeze kwenye kujijenga wewe zaidi. Tafuta vitu vya kufanya vya kukuweka busy kiasi kwamba unakuwa too busy to notice "matatizo" ya hapo home. Dont neglect your wifely duties though.

4. Jiweke karibu na Mungu zaidi. Sisi huku tutakushauri kibinadamu zaidi kila mtu na mtazamo wake. Lakini Mungu atakupa majibu/mawazo ambao hayatokuwa na majuto. Kuwa karibu na Mungu hakutopunguza baadhi ya changamoto zako; in fact zinaweza kuongezeka; lakini Mungu atakupa nguvu na akili itakayokuwezesha kukabili changamoto zako kwa busara; bila kupanic wala kudhoofishwa. Zaidi ya yote utapata amani ya kweli; come what may; you will keep on smiling.

Kikubwa jisamehe na wasamehe mumeo na ndugu zake. Umewajaza sana moyoni mwako; nothing good will come out of you. Waachilie, toa uchungu huo; usitamani mabaya yawapate kwa sababu tu wamekukosea, usiwahukumu. Ukunjue moyo, ukafurahi katika Bwana maana moyo uliochangamka ni dawa nzuri. Usiiinamishe nafsi yako; usikubali huzuni ikuzamishe. Concentrate na mambo positive yanayokupa furaha

Huo uchungu na msongo wa mawazo; una direct impact kwa mtoto wako. Ukiwa na huzuni utampa nini mwanao? If you cant think of yourself; think of your son. You are all he needs and has. Usije ukajistress ukafa bure afu mwanao ukamuacha anateseka; baba mwenyewe ndo huyo. Be strong for him pleasee
 

Yani ndoa nyingi zimekuwa all about men's happiness; mke wewe ni kuvumilia tu hadi parapanda. Na bado utaenda motoni kwa uchungu na malalamiko yako juu ya ndoa khaa
 
Mimi uyu binti kiziwi ndo angenipa ushauri maana ako sawa na fikra zangu,
 
Heaven Sent katika mada kama hizi huwa nakusubiri kusoma your two cents always. Umeongea vizuri sana. Hasa kitendo cha kuyaachilia hayo mambo.

Lakini dear umesahau point ya msingi sana, mumewe alimnyima haki yake ya ndoa, juu ya hili afanyaje? Okay nafahamu wanawake tunaweza survive muda mrefu sana bila kupata hiyo kitu, lakini je huoni kuwa ni haki ambayo atakuwa akiikosa kwa muda mrefu, since she is married kuchepuka ni kosa na ni dhambi pia afanyaje sasa?
 
Basi mwenzio nilijifanyia assumptions zangu tu lol. Nikasema kwa situation aliyonayo hadi ananza na kuumwa now kisa stress sidhani kama hata kama ana hamu ya tendo. Though it will reach a time atarelax kidogo so hamu zitarudi tu afu ndo hivyo mume analala naye daily; mwili u dhaifu nao. Sasa sijui aendelee kujiombesha dudu la yuyu au asubiri hadi siku akipewa offer mweeh. But ikifika stage tendo la ndoa limekuwa kitendawili na yeye analihitaji haswa; ataamua afanyaje of coz itabidi afanye maamuzi magumu tu. Siwezi kumshauri achepuke though kwa sababu atakuwa ameongeza petrol kwenye moto and cheating sio hata temporary solution; ni kujichimbia kaburi. Ni dhambi itakayomzalia mauti

Btw nikawa najiuliza kitu moyoni mwangu hapa; mtu mwenye situation kama hii; je asiongeze mtoto kwa sababu mume haeleweki na hata yeye uchumi wake haupo stable for now? Au akishakuwa stable aongeze watoto atakaoona yeye binafsi ataweza kuwatunza? Maana wanawake wa kiafrica tuna ile notion kwamba; kwanza ni mume wa ndoa lakini pia hatupendi kuchanganya mababa kwa watoto wetu (naamini bado ana ndoto ya kuongeza watoto wengine). Your general opinion please
 

Kichwa kinauma mamdogo, nikitulia tutaendelea na udadavuzi, btw amesema ameugua gafla masai dada, watu hawaoni kama huyu dada anahitaji msaada!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…