Heaven Sent
JF-Expert Member
- Sep 27, 2013
- 32,682
- 98,253
Ma mkubwa hali ni tete. Watu wakiamua kutoka ndoani tunawatukana na kuwaita majina mabaya na kuwaona ni wajinga na waliokosa uvumilivu. Sasa kwa hali kama hii jamani hadi mtu anaumwa mmmmmmmmmhKichwa kinauma mamdogo, nikitulia tutaendelea na udadavuzi, btw amesema ameugua gafla masai dada, watu hawaoni kama huyu dada anahitaji msaada!
Hahhaaa pole sana..sio wote wako kama huyo wakoPoole sana, ila nahisi kuna kitu ulishamkosea. Naye angepata fursa ya kuandika hapa makosa yako lazima tungejua nani mbaya.
Ila nachojua mwanaume mpaka kadiriki kufunga ndoa na wewe na akakuweka ndani, ujue alikupenda kwa dhati, ila kuna mahali pengine ulimkosea, kama sio wewe basi itakuwa mama mkwe wako anahusika, na kama si hivo basi kuna nguvu za giza.
Ila mi nilimpenda saana mke wangu nikamfungulia kila aina ya biashara zinafirisika tu, nikampa mtaji unakwisha tu, na mbaya zaidi hajawahi kuonyesha upendo wa dhati kwangu (hajawahi kuwa romantic), na mpaka sasa nampenda. Nimezaa naye watoto watatu wote wanasoma private schools.
Ki ukweli ananitesa saana, namvumilia tu kwa kuwa wanangu sipendi waje walelewe na mama wa kambo kwani wanaweza athirika kisaikolojia.
Nimetokea kuwachukia sana wanawake, siwezi kuwatetea hata kidogo, mke wangu anatumia fursa ya mimi kuwajali wanangu kunitesa na kuishi anavyotaka. Hivi naandika ujumbe huu nikiwa nimejilaza kitandani asbh hii nina mawazo sana huku nimenyimwa unyumba, nikaona bora niingie Jf kuperuzi nakutana tena na hii mada.
Siku nikimaliza majukum kwa wanangu na ishu zingine ndgndg hapa hom hakika naye atajuta. Atakuja kuandika hapa Jf kutaka huruma ya wanazego. Wanawake mnakera sana bhaana, siku janaume likifanya maamuzi magumu mnakimbilia jamii forum kutafuta huruma.
Pambaneni na madhambi yenu, ila samahani kama wee hauko hivo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa hiyo hapa unaweza kupata justifications za kuvunja ndoa? Kwenda kinyume na maaandiko matakatifu.Ma mkubwa hali ni tete. Watu wakiamua kutoka ndoani tunawatukana na kuwaita majina mabaya na kuwaona ni wajinga na waliokosa uvumilivu. Sasa kwa hali kama hii jamani hadi mtu anaumwa mmmmmmmmmh
Niliongelea generally; nitakujibu specifially.Kwa hiyo hapa unaweza kupata justifications za kuvunja ndoa? Kwenda kinyume na maaandiko matakatifu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Pole mkuuMh!....
Heaven Sent katika mada kama hizi huwa nakusubiri kusoma your two cents always. Umeongea vizuri sana. Hasa kitendo cha kuyaachilia hayo mambo.
Lakini dear umesahau point ya msingi sana, mumewe alimnyima haki yake ya ndoa, juu ya hili afanyaje? Okay nafahamu wanawake tunaweza survive muda mrefu sana bila kupata hiyo kitu, lakini je huoni kuwa ni haki ambayo atakuwa akiikosa kwa muda mrefu, since she is married kuchepuka ni kosa na ni dhambi pia afanyaje sasa?
na sasa hivi na tendo la ndoa linasuasua.
Wiki 2 bila tendo la ndoa ni nyingi za kulalamika JF?
Labda sio nyingi, ni chache swali ni je chache kwako ni chache kwangu? Ilibidi ziwe ngapi ili aruhusiwe kulalamika JF?
Wamama hawakosei kwenye ndoa huwa wanakosewa siku zote.Samahani Kama nitakukwaza mkuu, laiti ya kwamba wewe ndio ungekuwa dada au ndugu wa karibu hiyo ndoa ingekuwa imeshavunjika. Ndugu wengi (hasa wanawake) wanahukumu kwa kusikiliza upande mmoja.
Nakushauri Kama una ndugu ana matatizo au itatokea ana matatizo ya ndoa tafdhali kwepa kumpa ushauri. You're too emotional!
Ninachoona mwanamke anapambana na nguvu za giza.Ilianzia hapa.
[emoji116][emoji116][emoji116]
Habari,
Hili jambo limenitesa miaka nenda miaka rudi, natamani lifike mwisho.
Wakati naingia kwenye mahusiano na huyu ambae ni mume wangu sasa, alikuja binti mmoja ambaye alikuwa ndo kamaliza form 4 (mdogo wake) akaanza kusoma cozi kwenye chuo flani.
Nikapata ujauzito so ikabidi nilete binti wa kazi. Na mimi katika maisha yetu nimelelewa na mabinti wa kazi, sipendi wateseke kabisa maana niliona walivyomsaidia mama enzi tunakua, so shida ikaanza anamuachia yule binti kila kitu afanye, hadi ampikie amuamshe chumbani, yale mambo yalikua yananikera nikaanza kumsema kwa nguvu sana, hakubadilika. Ikabidi nimwambie kaka yake. Kaka yake akasema kama unamuona msichana wako anapata shida basi nitamuekea msichana wake yeye
Ile hali ikaendelea sana kwa muda na yule binti alikua mdogo kwa hiyo ikabidi niwe napika mwenyewe, siku zikaenda akaja tena mdogo wake wa kiume, wote kazi ikawa ile ile, huyu wa kiume hadi anamwambia dada amfulie nguo. Nilikua naongea napiga mzigo nadeki mpaka mimba ina miezi nane ndo mama angu akaja.
Kiukweli niliteseka mimba ya huyu mtoto, ugomvi ndani ya nyumba hautuliii kabisaa; wakaungana wote na mama zake kwamba niachike. Na kweli mume wangu akasema natamani kukuacha ni vile tu tumefunga ndoa.
Hapo nimeskip kipindi cha ndoa maana tulifunga ndoa tayari huyu binti tunaishi nae kuna mengi yalitokea lakini nitaeleza tu tukio moja.
Usiku wa kesho yake ndio ndoa akaniambia kwa hiyo kwenye hiyo saluni uliyofanya booking na mimi nitasuka? Nikamwambia ni maids tu wewe hautaenda pale, aliangua kilio imagne na kuna wageni, mume wangu haya maswala ya maids hajui anasema kwanini unaenda kuremba watu baki unamuacha huyu? Akaninuia tumeenda kusameshana wakati wakuvalishana pete ya ndoa.
Unaweza ukahisi movie ila sio movie ni maisha watu tunapitia.
Wakati wa sherehe huyu binti na wenzake kwenye ile meza ya wazazi wangu hawakupeleka vinywaji kabisa maana wao ndo walikua kwenye hiyo kamati ya vinywaji na mama zake wadogo.
Sasa huyu binti alikuja baadae kwenda hostel mimi mimba ikiwa kubwa kama miezi 8 ambapo na mama ndo akaja. Sasa wakati wa X-mass maana ilikuwa hata bado sijajifungua kaka yake akampigia simu aje kula sikukuu nyumbani, hakuja kabisa akaenda kwa dada mmoja ambae alikuja baadae kuwa mtu wa karibu na mimi. Huyo dada akamwambia mbona hujaenda kwa kaka kula sikukuu? Akasema, KAJAZA NDUGU ZAKE SIWEZI KWENDA PALE.
Kiukweli alikua kaja mama yangu na mjukuu wake na mdogo wangu, alikuja kusalimia, nikihesabu muda kwa ujumla waliokaa pale ni kama wiki tatu, dogo akaondoka na mimi nikawa nimejifungua nikakaa wiki2 nikaondoka na mama kurudi nyumbani.
Sasa imagne watu hawajakaa hata mwezi yeye kaona kero ila wenyewe miaka nenda rudi wapo.
Alikuja kumaliza chuo ila hakupata kazi, akaenda kwao akarudi tena akasoma tena akamaliza hakupata kazi. Na hii ya mara ya pili, wembe ukawa ule ule, hafanyi chochote analala tu dada amfanyie kila kitu.
Sasa hii mara ya tatu anasoma tena ila anawahi kuondoka asubuhi jion kuna siku anachelewa kuna siku anawahi kurudi, ila ndo hivyo hasaidii chochote, yaani dada ndo afanye kila kitu.
Namuuliza anasema naoshaga sahani yangu pekee. Namuuliza na hivyo vingine anasema nawahi kuamka kwa hiyo siwezi.
Leo mpaka naandika niko bize napika yeye amekaa anachat, nikamwambia mimi siwez kukupikia wewe unachat hapo jipe shuhuli wala hajanisikia kitu. Kaenda kununua chips.
Mbaya zaidi nyuma ya pazia kuna rafiki yake mume wangu wametafutana wanapanga yao huko (na huyo kaka alihusika sana kwa yule baby mama wa mr kumuondoa)
Na kingine kikubwa ni kwamba mama yake anaona kawaida tu hata ukimwambia.
Ashawahi iba nguo zangu akaenda kugawa, aliyempa akapiga picha akaweka Insta nikaiona ile nguo nikambana akasema alimpa, nikamwambia akaifate akampigia mama ake na mama ake akasema muulize (yaani aniulize mimi) hiyo nguo ni bei gani atume ela.
Nimeruka mambo mengi ila kuna dada wa saluni pia alishawahi kuniita akaniambia kuwa makini na huyu binti anaweza akakuua.
Sasa ndugu zangu nifanyaje hapa, wako wawili yeye na huyo shemeji wote wanataka tuwahudumie kama ambavyo namuhudumia kaka yao yaani mimi na dada ndo tuwafanyie kila kitu.
Na kingine kikubwa ana mawasiliano ya karibu mno na yule dada aliyezaa na mume wangu pamoja na yule aliyehusika kupika figisu.
Nifanyaje kuimaliza hii nightmare wandugu maana kila nikimuona anapita nakumbuka machungu hasa enzi za mimba maana ilikua niachwe kwa sababu yake.
Roho inaniuma, nina uchungu sana
=======
Sent using Jamii Forums mobile app
Tafuta maana ya neno hili: "nymphomania".
masai dada anaitaji msaada kisaokolojia maana adi kufikia kuumwa anaumia sanaKichwa kinauma mamdogo, nikitulia tutaendelea na udadavuzi, btw amesema ameugua gafla masai dada, watu hawaoni kama huyu dada anahitaji msaada!
Heri ya mwaka wandugu.
Ukweli nimeona nije na hii ID kabisa tu maana uchungu nilionao moyoni nahisi kufikia point ya kuhitaji msaada.
Nilikuja na ID hii mamii90 kuomba ushauri tu. Naomba uangalie ule uzi wa familia ya mume ndo utapata muendelezo wa hii.
Watu wengi walionishauri walisema ongea na mume wako moja kwa moja aisee ile siku najuta kwanini niliongea naye kwa uchungu sana, maana aliniambia mama yangu anakuja December kukutoa. Kwa hasira nikamjibu sitoki akasema "Hii nyumba haikuhusu, inamhusu mwanangu" ambaye sio mtoto wangu ni mtoto wake aliyemzaa kabla hatujafunga ndoa.
Ki ukweli roho iliniuma maana hii nyumba pia mimi nilikopa na ni pesa nyingi bado napambana riba. Baada ya ile siku niliona isiwe shida; zile ni hasira nikajirudi maisha yakaenda. Ila katika ushauri pia kuna member aliniambia jitahidi kumuweka karibu na mwanaye huyo (E).
Kweli nikamwambia likizo hii kamlete walau akae wiki kadhaa akamshawishi mama ake kweli mama yake akakubali mtoto akaja. Ki ukweli mtoto ni mtulivu sana, yaani ni rahisi mno kuishi naye. Yaani ni mpole mpaka raha, nilimpendaga tangu hapo lakini ni wa kike.
Sasa wakati amekuja kuna kitanda nilishamuandaliaga siku nyingi ila alitokea mgeni tukakifungua tukakiamishia chumba cha wanaume. Alivyokuja mchana nikamwambia mume wangu nisaidie tuhamishe hiki kitanda chumba cha dada
akajibu haina haja nitalala naye mimi. Kumbuka chumbani kwetu kuna vitanda viwili, kimoja cha mtoto wangu wa 2yrs bado ananyonya so huwaga nanyonyesha namlaza nahamia kitanda kingine, hiki chetu sasa.
Sasa wakati kaniambia vile nikamwambia huyu binti mkubwa hivyo tutalala naye vipi? Anaendea 7yrs. Ki ukweli haikuwa kwa ubaya kabisa ila hata katika hali ya kawaida ni ngumu; alibadilika sura pale ikabidi niwe mpole.
Kweli usiku ukaingia binti akaanza kulala na baba ake kwenye kile kitanda. Usiku wake mpaka niliota mandoto ya ajabu maana nilikuwa nawatizama tu, sikulala ki ukweli.
Ni kama wiki hivi tupo naye. So mimi nina maugwadu kama yote maana wiki ile nilikua period na hii tangu majuzi ndiyo dogo tunapoa naye rum. Mi nikawa namuonesha ishara tuingie hata chooni, anani-ignore.
So jana anacheki mpira watoto wanachenza nje nikamfata nikamwambia twende chumbani nikamwambie kitu, aliniangalia kabisa akagoma. Nikasema ngoja mpira uishe aisee hakuja, niliumia jana sana. Sema nikapotezea kiutu uzima. Ki ukweli dogo huyu wa kike namkubali sana aisee so nikasema ngoja nimute nijikaze mpaka nione mambo yatakavyojipambanua.
Leo asubuhi madogo kama kawa wakaamka wakasepa tukawa tumebaki wawili tu chumbani, akanifata kwenye kitanda changu; ki ukweli sikua hata na hamu kabisa maana nilishaishiwa na nguvu tangu majuzi huko. Nikamwambia tu ukweli tangu juzi nakubembeleza unanitolea nje (kiutani ila siriaz)
Nikamwambia tumuandalie kitanda cha dogo cha pamanent kwa dada maana huwa anakuja weekend sometimes ila huwa halali, ili hili lisitokee. Nikawa naendelea kumwambia, nikamwambia nilim-miss hatari.
Nikiri Mungu ananiona japo nina ID fake niliongea hilo bila chuki yoyote ila bila kutarajia akaniambia "HATAKUJA TENA ILI ASIKUSUMBUE"
Aisee maini yalikatika, daah moyo uliniuma nikakosa hata cha kuongea. Nikamwambia jamani ita hata mtu mzima kweli ni haki wewe kulala na binti mkubwa hivi kitanda kimoja, hakunijibu akaendelea kunipapasa.
Aiseee sikuloa hata chembe, nilikuwa mkavu wakati nina ugwadu kama wa 2wks na hii ni hilo neno liliniumiza sana. Ukicheki huyu binti nampenda namnunuliaga mazaga hadi mama ake ananikubali.
Angaika pale akafanya yake, akaondoka.
Kiukweli nikamtext kwamba najihisi mpweke kwenye hii ndoa.
Pale tuli-exchange texts kadhaa ila nikamwambia najuta kwa nini nilikopa nikaweka katika hii nyumba na siyo kwa sababu ulisema hii nyumba hainihusu, bali ni kwakua sina hata shilingi na unaninyanyasa kihisia namna hii. Akaniambia "Ndiyo nishakwambia haikuhusu, inamuhusu mwanangu mkubwa"
Nikamjibu sasa mimi na mwanangu twende wapi? Akasema omba Mungu nipate hela nitamjengea yeye ila jua hiyo nyumba haiwahusu.
Wakuu, kuna mengi hapo nayaskip, ila hii nyumba nimekopa kiasi cha pesa nikampa bado napambana na riba
Lakini kingine huyu ni mume wa ndoa kabisa.
Nakatwa kiasi kikubwa cha pesa kulipa ule mkopo na nilikuwa na biashara mwezi wa 11 walikuwa wanatengeneza ile barabara pale imeathiri hadi huo mradi. So namtegemea kwa kila kitu kwa sasa. Sitaki kufaiti kwa chochote nahitaji kuanza upya wakuu
Am soo scared nahisi naweza kuumia nikiendelea au kumuumiza mwanangu maana sijawaigi kuona ule upendo wa dhati kwa huyo dogo kutoka kwake japo wanafanana utafikiri wa mama mmoja. Sina namna yoyote ya kuanza upya ila natamani nianze upya niachane na hii nightmare.
Sina mia na sina chochote kile na ndo amepata point ya kunipiga vizuri. Kwa kifupi mwanangu nimepambana naye tangu hajazaliwa; nikielezea hili itachukua mada nzima.
Nimelia mpaka nahisi kuumwa.
Nisaidieni wakuu. Nikiri pamoja na changamoto zote sijawahi msaliti mune wangu hata tone.
JF sio sehemu salama ya kuchukua ushauri unaoenda kuamua maisha tako. Huku ni sehemu salama ya kutua mizigo uliyoshindwa kuitua uraiani tu ila sio utatuzi wa matatizo kama haya.
-Humu utashauriwa na watu walio-single vijana wa kiume na wake ambao bado wanakula kwao.
-Huku utashauriwa na wanawake wasio ndani ya ndoa walioumizwa na wanaume kibao kilichobaki mioyoni mwao ni mwanaume nini bwana. Waogope saana hawa.
-Huku utashauriwa na wanaume walioshindwana na wake zao kwasababu zao wazijuayo wenyewe.
-Huku utashauriwa na single parents hasa wanawake.. hawa kamwe hawawezi kukupa ushauri wa kukujenga..hawaamini katika ndoa wengi wao.
Tafuta watu walioishi kwenye ndoa miaka na miaka na wanaojiheshimu kwenye jamii yako wapo wengi tu. Waeleze A- Z ya mkasa wako au kama wamekuwa wakiyashuhudia utapata mawili matatu ya kuchukua. Wao wanamjua mmeo ni mtu wa namna gani na wanakujua wewe ni mwanamke wa namna gani.
Ila hapa unatuomba ushauri kuntu kama huu tusiokujua tutasema nini? Hatumjui mmeo tutasema nini? Hili suala yapaswa uwajue wote kwa undani ndipo utie neno. Ndiyo maana nikauliza kwanini unahisi mmeo alianza kubadilika???