Ushawahi kuhisi upo single ndani ya ndoa?

Nimegundua wengi wamezoea kunyanyasa au kunyanyaswa kiasi kwamba kwao hiyo ni kawaida tu na inatakiwa iwe hivyo. Ndio maana watu wanakuja na kauli za "ndoa ngumu, vumilia tu"

[emoji124][emoji124][emoji124][emoji124][emoji124][emoji124][emoji124]
Na asiyetaka kunyanyaswa ndo anaitwaga "mwanamke mpumbavu". Nafikiri watu wengi hawajui kutofautisha kati ya uvumilivu na kuishi na manyanyaso
 
All your narration hujaeleza the 'root cause' yeye kubadilika to such extent.

Unasema kuwa hujawahi kutoka nje ya ndoa yenu (sexually) even once.

Lakini common sense yangu inaangazia zaidi kwenye situation hii: "... mtoto uliyemzalia wewe hamthamini unlike to the other kid..." WHY?

Pole sana dada kwa masaibu hayo ya ndoa. Wanaume tuna mambo mengi.

Mie binafsi huwa naamini kitu kimoja kwamba I CAN'T stick staying in a horrible miserable relationship eti kisa 'ndoa'... never!

Sometimes Mwenyezi Mungu hutuepusha na majanga mazito zaidi kwa style mbali mbali. So, jitahidi kadri ya uwezo wako kupalilia ndoa yako. But when things seems not working out persistently, you just let it go and you move on!

In life, shits happen. Listen to your heart ma'am.

-Kaveli-
 
Aisee pole sana kwa yanayokusibu. Binafsi nimejifunza jambo moja kubwa, katika haya maisha ili uweze kukabiliana na changamoto,unahitaji kujijengea 'a supreme sense of self-confidence and self-trust'. self-confidence ni kutokuwa na hofu kabisa na self-trust: ni kujua nini unatakiwa ufanye kwa wakati ambao jambo husika linatakiwa lifanyike, na kisha unalifanya bila kusitasita. Kusitasita kunazaa hofu na self-doubt. Kiwango cha selfdoubt ulichonacho kinalingana sawa na kiwango cha hofu, wasiwasi na mkanganyiko unaoupata.

Kwa hiyo, mimi nashauri ukae chini upembue mambo kwa uhalisia wake, moja baada ya jingine, kisha uamue nini cha kufanya next kulingana na majibu utakayojipa na hatimaye utekeleze utachoamua. Kwa mfano; wewe unadhani chanzo ni nini? Je, unaweza kufanya lolote kushughulikia hicho chanzo ili mambo yakae sawa? Kama huwezi, nini mbadala wake? Zipi faida na hasara za kubaki katika hayo mahusiano? Na nini faida na hasara za kujiondoa? Kipi kinakupa hofu zaidi na kwanini? Je, unaweza kukabiliana na kinachokupa hofu? Kipi kibaya zaidi (The worst thing possible) kinachoweza kutokea kama ukibaki kwenye mahusiano hayo au ukiondoka? Je, upo tayari kukabiliana nacho? endelea kujiuliza maswali kama hayo na ujipe majibu halisi (real answers)... kisha chukua hatua bila kusita.

Kwasababu kuna mawili yanaweza kutokea, aidha uwe proactive uchukue hatua mapema au uwe reactive usubiri mpaka utakapolazimika kuchukua hatua (when you will be forced to act bcoz you'll 've no choice). Na historia inaonesha watu wengi huwa wanalazimika kuchukua hatua wakati wameshachelewa, wakati wameshapoteza kila kitu, wakati hawana tena cha kupoteza... na ambacho huwalizimisha kuchukua hatua ni MAUMIVU MAKALI.

You either decide or the nature decides for you.

Nawasilisha.
 
ammoshi,

Ushauri bomba sana.

Atalia mpaka lini?? Hapo tu anaonekana wamemfrastrate Kwa vitu vidogo vidogo hadi anajikuta amebeba dunia nzima. Uzi wa kwanza nilichukulia kawaida Ila uzi wa Leo baada ya mumeo kuonekana Ana njaa na nyumba na kumpendelea huyo mwanae wa kwanza nimeona huyo mume ana tatizo
 
Pole sana masai dada you can just decide to wage a war pata haki zako songa mbele mda mwingine sisi wanaume tunazingua sana

Haya maisha ukijifanya innocent sana utaishi kama upo jehanamu na ukifa unaenda kuishi tena jehanamu...uamuzi ni wako, ushauri wangu anzisha vita, omba divorce kila mtu afe na chake akitaka watoto pia muachie

Unapata ushauri kutoka kwa mtu ambae ana deal na divorce process mda huu...run sister run
 
Kama apigani na haonyeshi dalili za ukatili, maneno hayavunji mfupa, uvumilie tu ni kipindi cha mpito akili ikimurudia atatulia. Wakati mwingine ukute ni michepuko yake inamtia jeuri. Hivyo anajaribu kukutikisa kuona ukoje kimsimamo.

Mwanamme makini hatishii mke kwa nyumba eti ni ya mtoto sijui mkubwa au mdogo. Sasa kama hiyo ni ya mtoto, muulize ya kwake yeye iko wapi, aoni aibu kuishi kwenye nyumba ya mtoto?

Lakini kama ni mgomvi na anaonyesha dalili za ukatili bora uondoke yasije kuwa yale ya kigamboni ya kuchomwa moto kwa gunia mbili za mkaa!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…