Mpuuze jitahidi sana hili itakusaidia kupunguza presha msongo wa mawazo na sonona
Punguza kudeka labda ni vile bado uko mchanga kwenye ishu za ndoa
Hongera bado unakaupendo kwa mumeo wengine tumepoa kuzidi na barafu sababu ya maudhi
Pambana upate tuhela twako mamii hapa tupatilie sana mkazo wanawake wote
Hukukosea kukopa na kujenga nae ila kakuonyesha alivyo mbinafsi, umejifunza kitu fanya kama uliwekeza kwenye biashara ukala hasara yani usiumie kabisaaa
Uzuri umemjua bado hujamzalia watoto wengi,, hivyo usizae nae mtoto mwingine jipe muda hata wa miaka 3
Shemeji ni furushi anajisemeaga shosti yangu mmoja humu unambembeleza na kumpa k anajitia nunda,, ana mchepuko piga ua anao
Mpaka najisikia kuumia maana upo katika hali ya kutoka kwenye uwife material na utaingia kwenye ununda tuliopo wengine kina sie hahahahahah
Hakuna mwanamke mbaya kama aliyejeruhiwa kihisia sababu sie tukipoa tunapoa kweli hata ulete busta dunia nzima hisia zikifa zimekufa kuzifufua ni mtihani mzito,, na mbaya ni mumeo tu ndo mwenye uwezo wa kuzuia hali hiyo lakini kwa vile ni lifurushi nakuhakikishia muda si mrefu hisia ulizonazo kwake zitapoa na zikipoa hutaumizwa na kauli yake yoyote hapa ndipo utaweza kupuuza,,
Ndoa ni ngumu si nyepesi kuna siku wanandoa mnakuwa km kaka na dada, kuna siku mnakua km majirani kuna siku maadui kabisa na kuna siku mnakuwa marafiki
Mwisho kabisa nawatakia heri ya mwaka mpya wote mnipendao notification zenu nimeziona mapendo yenu nimeyaona sitaweza kutaja wote, sakayo jael heavensent depal nimewamiss sana sana