Ushawahi kuhisi upo single ndani ya ndoa?

Ushawahi kuhisi upo single ndani ya ndoa?

Yani, ukigoma masimango ukaondoka unaambiwa umevunja ndoa yako kipumbavu. Wanataka uvumilie kudharauliwa hapo ndo utaitwa mwanamke


Sent using Jamii Forums mobile app
Mke bora ni yule anayevumilia upuuzi wa mume, kiufupi mzigo wa ndoa wote unamwangukia mwanamke hata kama tatizo ni la mume.
Na ndio maana mwanamke anafundwa kabla ya ndoa lakini mwanaume hakuna anachofundishwa..matabia yake yote mabaya anampelekea mkewe aliyefundwa na kuhimizwa uvumilivu. Ukiwa boya sana lazima uteseke .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama hela inakatwa itachukua mda gani hari hilo deni limalizike?uwe mpole huku deni linaisha na kichwani una plan b,ila kama deni la mda mrefu hapo pagumu
Kazi nafanya ila nakwata almost pesa yote.

Na aliniambia iwe hivyo yeye atakua ananisapoti kw kiasi flan cha pesa ambacho nitakiweka ili nifanye biashara za hapa na pale. Hata hapo ambapo pameharibika kutokana na ujenzi wa barabara nilifaiti mwenye mpaka kupaweka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuwa kwenye mahusiano na mtu mwenye watoto kabla yako ni ngumu sana. Birthday yangu ni New Year, huo mwaka nilichukua holiday kazini nilijua New Year na birthday itakuwa romantic time. Khee nimeambiwa wanakwenda sea side

Hii ya kuwa na mtoto kabla yako inanitesa mimi sana...kuna wakati najuta ila dada yangu anaitia moyo ,napata ujasiri maisha yanasonga
 
Aisee.....kuwa uyaone...kuna wanawake wanapitia machungu sana...tunakosea wapi wakati wa uchaguzi jamani.....ila up n down....NDOA ni ya watu wawili pekee...akiongezeka wa tatu....ni iblisi sheitwan......
Dada pole sana, ila bado unayo nafasi, ongea na nafsi yako unachotaka kufanya....amua kufanya tekeleza.....huwezi kuwa na matokeo bila kufanya mtihani.....pigania FURAHA yako milele. umeolewa na mme asiye wako dada...wewe bado kijana pambana na nafsi yako...anza hatua moja mbili tatu...sogea....Mungu hakutuumba tuteseke...why....pole DADA yangu.....
 
Nilitaka kuchangia kama wewe maana mie ni muhanga wa issue kama hiyo nimemuachia nyumba mwanamke maana kwa sasa mwanamke akienda mahakamani mwanaume huna chako nikaona isiwe tabu kwa sasa naanza upya

Sent using Jamii Forums mobile app
Victim tuko wengi sana...kiukkweli.........niliacha kila kitu....nguo na kafriji na kiti alinikuta navyo......nimeanza upya kabisa
 
Mumewe anakukata wenge,wewe utakuwa una mawenge flani hivi hasa kwenye kauli .

Nahisi una kauli za ajabu na hapo mumewe ana kinyongo na wewe ndo analipa kisasi kwa namna yake.


Hapa na comment kwa hisia tu mdomo kuna sehemu utakuwa unakuponza
 
Heri ya mwaka wandugu.

Ukweli nimeona nije na hii ID kabisa tu maana uchungu nilionao moyoni nahisi kufikia point ya kuhitaji msaada.
Nilikuja na ID hii mamii90 kuomba ushauri tu. Naomba uangalie ule uzi wa familia ya mume ndo utapata muendelezo wa hii.

Watu wengi walionishauri walisema ongea na mume wako moja kwa moja aisee ile siku najuta kwanini niliongea naye kwa uchungu sana, maana aliniambia mama yangu anakuja December kukutoa. Kwa hasira nikamjibu sitoki akasema "Hii nyumba haikuhusu, inamhusu mwanangu" ambaye sio mtoto wangu ni mtoto wake aliyemzaa kabla hatujafunga ndoa.

Ki ukweli roho iliniuma maana hii nyumba pia mimi nilikopa na ni pesa nyingi bado napambana riba. Baada ya ile siku niliona isiwe shida; zile ni hasira nikajirudi maisha yakaenda. Ila katika ushauri pia kuna member aliniambia jitahidi kumuweka karibu na mwanaye huyo (E).

Kweli nikamwambia likizo hii kamlete walau akae wiki kadhaa akamshawishi mama ake kweli mama yake akakubali mtoto akaja. Ki ukweli mtoto ni mtulivu sana, yaani ni rahisi mno kuishi naye. Yaani ni mpole mpaka raha, nilimpendaga tangu hapo lakini ni wa kike.

Sasa wakati amekuja kuna kitanda nilishamuandaliaga siku nyingi ila alitokea mgeni tukakifungua tukakiamishia chumba cha wanaume. Alivyokuja mchana nikamwambia mume wangu nisaidie tuhamishe hiki kitanda chumba cha dada
akajibu haina haja nitalala naye mimi. Kumbuka chumbani kwetu kuna vitanda viwili, kimoja cha mtoto wangu wa 2yrs bado ananyonya so huwaga nanyonyesha namlaza nahamia kitanda kingine, hiki chetu sasa.

Sasa wakati kaniambia vile nikamwambia huyu binti mkubwa hivyo tutalala naye vipi? Anaendea 7yrs. Ki ukweli haikuwa kwa ubaya kabisa ila hata katika hali ya kawaida ni ngumu; alibadilika sura pale ikabidi niwe mpole.

Kweli usiku ukaingia binti akaanza kulala na baba ake kwenye kile kitanda. Usiku wake mpaka niliota mandoto ya ajabu maana nilikuwa nawatizama tu, sikulala ki ukweli.

Ni kama wiki hivi tupo naye. So mimi nina maugwadu kama yote maana wiki ile nilikua period na hii tangu majuzi ndiyo dogo tunapoa naye rum. Mi nikawa namuonesha ishara tuingie hata chooni, anani-ignore.

So jana anacheki mpira watoto wanachenza nje nikamfata nikamwambia twende chumbani nikamwambie kitu, aliniangalia kabisa akagoma. Nikasema ngoja mpira uishe aisee hakuja, niliumia jana sana. Sema nikapotezea kiutu uzima. Ki ukweli dogo huyu wa kike namkubali sana aisee so nikasema ngoja nimute nijikaze mpaka nione mambo yatakavyojipambanua.

Leo asubuhi madogo kama kawa wakaamka wakasepa tukawa tumebaki wawili tu chumbani, akanifata kwenye kitanda changu; ki ukweli sikua hata na hamu kabisa maana nilishaishiwa na nguvu tangu majuzi huko. Nikamwambia tu ukweli tangu juzi nakubembeleza unanitolea nje (kiutani ila siriaz)

Nikamwambia tumuandalie kitanda cha dogo cha pamanent kwa dada maana huwa anakuja weekend sometimes ila huwa halali, ili hili lisitokee. Nikawa naendelea kumwambia, nikamwambia nilim-miss hatari.

Nikiri Mungu ananiona japo nina ID fake niliongea hilo bila chuki yoyote ila bila kutarajia akaniambia "HATAKUJA TENA ILI ASIKUSUMBUE"

Aisee maini yalikatika, daah moyo uliniuma nikakosa hata cha kuongea. Nikamwambia jamani ita hata mtu mzima kweli ni haki wewe kulala na binti mkubwa hivi kitanda kimoja, hakunijibu akaendelea kunipapasa.

Aiseee sikuloa hata chembe, nilikuwa mkavu wakati nina ugwadu kama wa 2wks na hii ni hilo neno liliniumiza sana. Ukicheki huyu binti nampenda namnunuliaga mazaga hadi mama ake ananikubali.

Angaika pale akafanya yake, akaondoka.

Kiukweli nikamtext kwamba najihisi mpweke kwenye hii ndoa.

Pale tuli-exchange texts kadhaa ila nikamwambia najuta kwa nini nilikopa nikaweka katika hii nyumba na siyo kwa sababu ulisema hii nyumba hainihusu, bali ni kwakua sina hata shilingi na unaninyanyasa kihisia namna hii. Akaniambia "Ndiyo nishakwambia haikuhusu, inamuhusu mwanangu mkubwa"

Nikamjibu sasa mimi na mwanangu twende wapi? Akasema omba Mungu nipate hela nitamjengea yeye ila jua hiyo nyumba haiwahusu.

Wakuu, kuna mengi hapo nayaskip, ila hii nyumba nimekopa kiasi cha pesa nikampa bado napambana na riba
Lakini kingine huyu ni mume wa ndoa kabisa.

Nakatwa kiasi kikubwa cha pesa kulipa ule mkopo na nilikuwa na biashara mwezi wa 11 walikuwa wanatengeneza ile barabara pale imeathiri hadi huo mradi. So namtegemea kwa kila kitu kwa sasa. Sitaki kufaiti kwa chochote nahitaji kuanza upya wakuu

Am soo scared nahisi naweza kuumia nikiendelea au kumuumiza mwanangu maana sijawaigi kuona ule upendo wa dhati kwa huyo dogo kutoka kwake japo wanafanana utafikiri wa mama mmoja. Sina namna yoyote ya kuanza upya ila natamani nianze upya niachane na hii nightmare.

Sina mia na sina chochote kile na ndo amepata point ya kunipiga vizuri. Kwa kifupi mwanangu nimepambana naye tangu hajazaliwa; nikielezea hili itachukua mada nzima.

Nimelia mpaka nahisi kuumwa.

Nisaidieni wakuu. Nikiri pamoja na changamoto zote sijawahi msaliti mune wangu hata tone.
Pole sana..Dada kwa unayopitiaa..jitaidi uwonanee na ustawi wa jamii, au mashirikaa ya kutetea haki za wanawake, watakusaidia. Pole sana..najua jinsi unavyoumia.
 
Kuna kitu ngoja nikufundishe, kamwe usizamishe moyo wako.kwa mwanadamu hata umpendeje, manake wanadamu huwa wanabadilika wakati wowote. Penda mtu atkeast 50 percent hata awe mumeo.manake wanadam wana asili ya kuwa washenzi tu kuna siku atakuzingua, 50.percent unajibakishia mwenyewe siku akizingua unakua stable.

Lakini hata usiogope, kwa kuwa sa hv huna kitu we kuwa mpolee huku ukingoja uchumi wako ukae sawa, tena mpende huyo mumeo keshakuambia ukweli kuliko angekwambia ushajizeekea huna namna. Cha msingi kwa sasa msikilize akitoa hoja yoyote kuhusu mwanae au hapo ndani ili upunguze kumkwaza, huku we unamark time mambo yako yatengemae,..mbona utakuja kwenda nae sawa tu. Kuwa mpole sana na usioneshe kama unajali maneno yake we kuwa bwege huku ukitulia we ukae sawa manake hapo kama huna kipato usijemzingua akakufukuza ikawa majanga.@masai dada

Sent using Jamii Forums mobile app
Well said...@masai dada soma hapa
 
Pole sana mpenzi. Kama mtu hajapitia unachopitia anaweza fikiri ni story tu kama za Iddi Makengo ila kiukweli haya mambo yapo na yanaumiza.

Kuna muda najikuta najipongeza kwasabu sikufikiri kama maumivu yangu yangeisha na ningekua hivi nilivyo leo.
Kama bado unaipenda ndoa yako fight na pambana hadi isimame na irudi sawa.

Mara nyingine kum-ignore na kupambana kivyako inaweza saidia kumrudisha katika mstari.
Usiishi kwa maumivu kwasabu ukiumia na kukosa furaha itamuathiri mwanao.

Ukishindwa kumbadilisha basi kubali kua imeshindikana na focus on your life n child.

Praying for You.


Sent using Jamii Forums mobile app
I second you.
 
Tafuta mwanasheria akusaidia kuhusu haki zako .. na mlikua na makubaliano gani mpaka ukajiingiza kwenye mambo ya kukopa visivyokuhusu?!
 
  • Thanks
Reactions: amu
Back
Top Bottom