Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
😄You have some issues,😀
Nimeamua kukupuuza mkuu,nimeshajua shida Yako ni kubwa kuliko nilivyokuwa nafikiria,kukusaidia ni nje ya uwezo wangu endelea kutukana tu ndo akili Yako ilipoishia,matusi Yako na yakurudie wewenaona bado unaendelea kudhihirisha kwa public kuwa we ni bwege, ila shida ni kwamba ulikuzwa kwa ugali dagaa (vyakula vya mifugo) ndo maana uelewa wako ni mdogo kuliko wa ng'ombe.
Mkuu acha uzapunga,wanawake ni magaidi,Kama hana hisia nawe hata uumwe ufe hapo ataondoka akuache aende kwa mwenye hisia zake,so hapo anakupanga tu maana ashakuona we zamwamwa kama yeye tu.kabisa mkuu mm kuna mmoja japo nilikuwa nimepitapita kwingine ila it was the first real love, ana maisha yake na mm yangu ila kila tukipata muda wa kuongea huwa tunaulizana "hv kwa nn hatukuoanaga" juz kat uzalendo umemshinda kaniambia lazima atatafuta siku tukumbushie japo anampenda sana mumewe, ila kitu napenda anamjali na kumuheshimu sana mumewe, mwamba anang'aa tu, kuna siku nikamtani muache mumeo uje kwangu, akajbu natamani hvo ila nikimuacha huyu hatomaliza mwaka atakufa.
Duh hatarS3 epi 10
Mama namjua akianza kuongea hamalizi Leo sikumjibu chochote nikampotezea, kesho yake Sasa nawasiliana na ba mdogo yaani tunapanga mbinu utasema tuko vitani, kwanza akaniambia amefanya mawasiliano Kuna mtu kampata mwanza Mzee mmoja wa kwenda nae, akaniambia yule Mzee wa kwanza tulieenda nae wakati wa kujitambulisha Kwa Rachel hafai, anadai yule ni mlaini Sana hii vita hatoiweza inahitaji makamanda kweli, hapo mimi simbishii kitu chochote nipo kimya maana nilishamuachia msala apambane nao....
Ba mdogo akaja Sasa na idea Moja, operation ya kuua ndege wawili Kwa jiwe Moja....
Akaniambia hapa inabidi tulipue mabomu kotekote ibaki tu kazi ya kukabiliana na madhara yatakayojitokeza, jumapili akienda Kwa mama mkwe na mimi huku nikae na mama nimuambie tu Kila kitu, maana hata nisiposema akasema mama mkwe ni lazima tu atampigia mama, hapo Sasa naona nimeruka nimejichanganya tu, mama yangu namjua ataongea mpaka nyumba ipate ufa, ila nikiwaza msala wa mama mkwe kule naona Bora nipambane tu huku kule ni kwa moto zaidi, hapo Rachel yeye Bado Sasa, nawaza huyu nae hawezi kuacha ipite hivi hivi lazima tu ataleta vita ya aina yake,
Hua sifanyi kitu bila ya kua na plan b, nawaza haya mambo yanaweza yakaenda tofauti kabisa na tunavyotarajia hivo plan b yangu ni kua nikiona mambo yameharibika Sana nifanye mpango mtoto nimlete huku Kwa mama maana nilihofia Rachel anaweza pata sababu ya kumchukua mtoto....... Nikishamleta huku mimi Sasa nibaki nipambane na lolote litalokuja
Usiku wa deni haukawi kufika, jumapili hio hapo, nipo busy na askari wangu( ba mdogo) tunapanga mipango wa mwisho, nikampa idea usiende mikono mitupu nunua zawadi za mama mkwe na mtoto kwanza mpate hata pa kuanzia mkienda, Sasa ba mdogo hii ishu yeye anachukulia simple tu yaani anasema " hii ya Leo Haina Cha zawadi Wala nini, Leo tunaenda uwanja wa vita zawadi za nini tena"
Mimi huku swala la kumuambia mama likanishinda, Kuna rafiki yake mmoja mama mtu mzima Sana tulikua tunatenganishwa na ukuta tu huyu mama alikua mcheshi na simple Sana, nikawa nimeshamuambia majanga yote nikamwambia jumapili we njoo umueleze tu huyu Mzee mwenzako akasema hakuna shaka.........
Hio siku yule mama kafika Sasa home, tumekaa Kaa pale ikabidi mi nizuge nikatoka zangu nimuache Sasa afikishe msala huku, nimetoka nimekaa bar Moja nampigia ba mdogo kujua kafikia wapi, anapokea anauliza vipi wewe uko wapi? Namuambia npo bar hapa natuliza kichwa kidogo, jamaa nae anacheka anasema na si tumepitia hapa tunapiga Moja Moja kwanza hii vita sio ya kwenda ivi ivi
G hapo tunawasiliana kawaida ila sijamwambia chochote asije akavujisha taarifa akaharibu, ikafika muda ba mdogo ananiambia wapo njiani wanakaribia kufika....
Mimi ni nani??
Nikachukua Simu yangu, mama mkwe nikamtupia kwenye blacklist, Rachel nae nikamuunga huko huko.... Hapa nasema mpaka nipate kwanza feedback kutoka Kwa ba mdogo ndo ntajua Cha kuongea nao....
Basi wao wakafika kule hapo tukaacha kuwasiliana, hapo Nina mawazo najiuliza mbona nimejiingiza kwenye matatizo kiasi hiki, upande wa mama Wala siwazi Sana najua tu atasema mpaka nikome, huku Sasa Kwa mama mkwe.... Nikakaa pale yaani navyosubiri Simu ya ba mdogo ni sawa na mtu ammepeleka mwenzie labor anasubiri ajifungue
Nikiwa nashusha bia taratibu pale, mama yangu akaanza kupiga nikawa kimya tu Wala simpokelei, akapiga kama mara tatu mie kimya tu.... Nakaa kama dakika 10 naona sms kutoka kwake
" Hivi wewe hizo akili zako umezitoa wapi , mbona baba Yako hakua na akili kama hizo"
Nikawaza hapa bomu la kwanza lishalipuka...
Sijapata hata muda wa kuwaza ba mdogo nae anatuma sms
" Mzee hii Ngoma nzito, tushachemka huku"
Ni kweli. Ndio maana wanatoa mimbaKaka Patrick kazana na kanisani Sasa na maombi. ...ila wamama Mungu awabariki sana....hata ukosee kiasi Gani lazima wawajali watoto wao....
Tupo basi dondoo zake na yeye yupo wapi na vipi keshaolewa au vipi? Mary je anaendeleaje na vipi ulishaacha kuwasiliana nae? Ila story nzuri ina mafunzo mengi sana kwa kweliMaisha haya 😀, 10 minutes ago nimetoka kuongea na Samira hapa
Umemaliza?Mkuu acha uzapunga,wanawake ni magaidi,Kama hana hisia nawe hata uumwe ufe hapo ataondoka akuache aende kwa mwenye hisia zake,so hapo anakupanga tu maana ashakuona we zamwamwa kama yeye tu.
na yako yakurudie ww pia,Nimeamua kukupuuza mkuu,nimeshajua shida Yako ni kubwa kuliko nilivyokuwa nafikiria,kukusaidia ni nje ya uwezo wangu endelea kutukana tu ndo akili Yako ilipoishia,matusi Yako na yakurudie wewe
Kama hutojali mkuu tuambie hizo pills zinaitwaje. Kuna tuvitu nimekuwa addicted to isijekuwa ndio hutoNpo mkuu
lazima Patrick tu, au hata sisi wengine??Nikitaka kuwa mchepuko wako mwenye adabu nafasi ipo?
Season 5 soon ina anza.Maisha haya 😀, 10 minutes ago nimetoka kuongea na Samira hapa
Kwa faida ya wengi naomba nisijibu hiliKama hutojali mkuu tuambie hizo pills zinaitwaje. Kuna tuvitu nimekuwa addicted to isijekuwa ndio huto
Bado Sana bahari sa hivi imetulia kabisaSeason 5 soon ina anza.
Siyo valium kweli hizo?Kama hutojali mkuu tuambie hizo pills zinaitwaje. Kuna tuvitu nimekuwa addicted to isijekuwa ndio huto
Not even close, Sasa valium ndo za kuagiza dar kweli?Siyo valium kweli hizo?
Umepona naona unataka kuvulumua mengine.Maisha haya 😀, 10 minutes ago nimetoka kuongea na Samira hapa