S2 episode 9
Mama namjua ni mtu wa maneno mengi nikawa nimempotezea tu mpaka kesho yake nikampigia tukaongea nakamuambia jipangane tu mje mumuone mjukuu sasa akasema hakuna shaka
Baada ya Rachel kujifungua imepita kama wiki 2 ivi kuna siku mama mkwe ananipigia anauliza baba upo wapi namuambia npo najiandaa kutoka kazini hapa akaniambia njoo mara moja kuna shida nyumbani, basi nikatoka haraka nikaenda kufika pale nakuta kama kuna hali ambayo siielewi kama kuna watu watu wengi, nafika nikamvuta mama mkwe pembeni namuuliza nini tena hapa ndo ananiambia kua Rachel anadaiwa na wanakikundi wenzake sijui wameenda dukani kwake wamesafisha kila kitu hapa wapo kwangu wanataka kuchukua tv yangu kwa nguvu, nikachoka kwanza nikauliza kikundi gani hiki, na dukani wamechukuaje vitu mbona pamefungwa yeye mwenyewe ni kama haelewi
Basi nikamuita sijui ndo mkubwa wa kikundi naona wanakuja kama wote nikawapiga biti pale nataka kuongea na mmoja tu, akaja namuuliza mnadai bei gani anadai bado kama laki 6, kutokana na ile hali ya aibu pale nikaingia kwenye gari nikatoa laki 3 nikampa na namba zangu nikamuambia hio nyingine ntakupa kesho, ni kama alitaka kugoma ila kuna jicho fulani nilimkata akapokea hio pesa
Mama mkwe nae akaanza kuniomba msamaha pale ananiambia mwenzako sijui ana shida gani mbona mambo ya aibu haya mwanangu, sikumjibu kitu mi nikaondoka zangu, nikawa nawaza hapa sichezewi michezo ya kiswahili kweli? Hivi kweli ndo nimekuja tengeneza familia na watu kama hawa kweli? Hio siku yalinishinda kuna rafiki yangu mmoja nilimpigia nikamuelezea situation zote aisee mpaka akashangaa, mwishowe akanionea huruma akaniambia tu we angalia jinsi utavyokuja kumpata mwanao basi
Huku maisha yakasonga mi nikawa naenda tu wasalimia pale kwa kina Rachel nawapelekea mahitaji na nini, sasa ikapita zaidi ya mwezi mama na sister wakawa wanakuja mwanza, hapa katikati mahusiano na Rachel ndo yapo ivo ivo sema moyoni nilikua nishamtoa namuwaza mwanangu tu, nikampa taarifa mama mkwe kua amuandae binti aje huku kwangu ila akifika mama amkute nipo nae huku
Sasa sijui ni kiburi au ujinga wa huyu binti, akagoma kutoka kwao akasema watakuja kumsalimia huko huko, hapa nadhani alikua ananikomoa maana baada ya kumlipia lile deni na kuona ameua biashara niliacha kumpa financial favour yoyote, nikawa mme kwa kipemba kila kitu nanunua au namtuma boda, maisha ya kuniomba mara laki laki 2 nikapiga full stop, kwanza nikawa nawaza huyu sina hata malengo nae, hio siku nilichukia nikaenda kwao kufika baada ya maongezi ndo nikawaambia mama na dada wanakuja inabidi mje kwangu sasa, rachel anadai mi siendi kama kunisalimia watakuja huku huku, nikawa nimechukia nikawaambia basi nipeni mtoto wamkute kwangu kama we hutaki kuja baki
Rachel nae sijui ni wehu au nini akaropoka " mtoto mwenyewe hata mahari hujamlipia unaongelea mtoto gani? "
Sijakaa sawa mama yake akanyanyuka akaanza kumpiga huku analia "mwanangu mbona unanitia aibu kiasi hiki una shida gani mbona huniheshimu au mimi sio mama yako, unajua nimehangaika na wewe vipi?"
Nikaona huu ujinga sasa mimi huyo nikaondoka zangu, nikaanza utaratibu mpya, situmi matumizi wala simu zao nikawa sipokei, haikupita siku mama na sister wakaja tukafanya mpango tukaenda wasalimia, sasa sijui kina mama wanakua na nini naona mama akawa busy tu anamkagua mtoto muda tunaondoka akaniambia huyu ni wa kwetu kuna kishimo nimekiona sikioni wanangu wote niliwazaa mkiwa nacho, nikapata faraja kidogo ila hapo bado machale yanacheza tu
Basi kina mama wakawa wanaenda kusalimia huko wanashinda jioni wanarudi kwangu, sister sasa ndo akaanza kunchamba ananiambia mdogo wangu kweli ulimuacha Mary ndo umeanguka huku..... Nakuonea huruma...... Walikaa kama siku 4 wakaaga wakaondoka wakiwa njiani naona sms ya mama "mwanangu asante kwa mjukuu, anza sasa kutafuta mke hapo hamna mke"