Ushawahi kujichanganya kimapenzi mpaka ukawa unawaza hapo nyuma ulikosea wapi?

Yaani "MKUU" ndio tumeishia hapa kweeli,,, umesababsha nichelewe bas la kwenda Mwz zen unaishia hapa,!!?

Mwisho wa Mary tumeuona ila wa Samira naona km Kuna kitu umeficha tusikijue kuhusu yy maana Kwa Akili za kawaida baada ya kukutana na yote hayo Opportunity cost baada ya kuforgone Mary na Recho tulijua ungekua na akili ya kumrudia Samira ili kuondokana na uswahili usio na na chembe ya ustaarab
Nilichikiona kingne wee ulikua mchanga sana wa mapenzi, nginjangija umekuja kutana nazo kwenye kuoa badala ya uteenager,,
Pia amini usiamini after a long run kwenye Maisha ya ndoa either na Samira/Mary uliowatoba wangekuja kuchepuka tu kutaman kulonja zingine maana ndio kitu hawakua wamefanya ktk ujana wao, yaani ingefka time wangetaka kufanya "ujana"
 
Duuh jf umejiunga ukiwa mdogo sana
Yes since 2011 nipo humu. Naifahamu tangia nikiwa Primary school kipindi ambacho ukitaka kujua mambo ya ufisadi na mambo mengi yanayofanyika kwenye taasisi mbalimbali za serikali inakubidi uchungulie humu.
 
Bro, You're a great Thinker. Ndo maana me sipendi kujilaumu kwa yaliyokwisha tokea, huwezi kuikimbia hatima. Huenda angebaki na huyo marry/samira still kuna wakati ambao angejutia kuwaamini. Angeanzisha tena uzi wa kwanini asingechepuka mapema. Marry na samira hawajapitia hekaheka za ujana wangekuja kumsumbua sana

"Normal is boring"
 
Nafikiri ilibidi iwe hivyo ilivyo ๐Ÿ˜‚ HAKUNA kosa lolote zaidi ya matokeo ya machaguo๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„

Maisha yana ladha zote (chungu,tamu,furaha,majonzi) yote hayo nimatokeo ya chaguzi HAKUNA chaguzi yenye furaha pekeee...ila akili inaturejesha kwenye hadidu za ulinganifu nakuona kuna kosa๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚enewei

Ukimchagua mwanamke kadiri ya maandiko ametokana na ubavu bas jua umechagua kilicho dhaifu kadhalika ukimchagua mwanaume tambua Hana mbavu moja๐Ÿคฃ๐Ÿ˜‚ NI dhaifu pia....๐Ÿ˜„๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
 
S2 episode 10


Mama namjua nikampotezea tu japo nafsi yangu ilikua inaniambia kile kile ambacho kilikua kipo moyoni mwangu, lakini kitendo cha kuendelea kufanyiwa kiburi na Rachel ch kugoma kuja nyumbani hata wageni walipokuwepo nikasema hakitapita hivi hivi, nikasema ni muda muafaka sasa wa kuacha kujifanya kijana mwema sana, mimi huyo sasa nikakata mawasiliano na Rachel pamoja na mama yake, yaani hivo tu, simu sipokei, sms sijibu, hakuna cha matumizi wala nini, kitu pekee nachokumbuka kutuma tena namtuma mtu ilikua pampers za mtoto, sabuni za kufulia, mafuta ya mgando ya mtoto na wipes!! Nikitoka kazini nachelewa kurudi nyumbani basi tu nikaanza ratiba mpya nazojua mimi



Wakalalamika sana kwa sms lakini wapi mi npo kimya tu, wanakuambia dawa ya jeuri ni kiburi, imepita kama mwezi siku natoka zangu kazini nafika nyumbani namkuta Rachel yupo na mtoto, mama mkwe na mdogo wake(Grace) wananisubiri, nikajifanya kama sijashtuka wala nini nikafungua nikawakaribisha ndani, basi na wao wakazuga kama hakuna tofauti yoyote tukawa tunapiga story kawaida badae nikamwagiza boda akaleta mahitaji pale wakawa wanapika mi nikatoka nikawaacha pale, nimerudi badae mama mkwe kashaondoka yupo Rachel na mdogo wake



Rachel ndo akawa karudi sasa kwa style hio maisha yakaendelea badae tukawa sawa tu ila ndo hivyo ukishakosa imani na mtu mnaishi kwa machale tu sana, kufupisha sana mambo japo katikati hapo ugomvi haukosekani, mtoto ndo ana kama miezi 9 ivi, ikatokea nafasi kazini za kwenda training nje, mwanzo sikutaka kwenda ila kuna bosi wangu akanishauri niende nikirudi anaweza nibadilisha kitengo chenye maslahi zaidi, nika apply zile nafasi nikakaa kimya kusikilizia majibu maana waliokua wanataka walizidi nafasi zilizotolewa



Baada ya kama mwezi majibu yakatoka nimepata nafasi ila kuondoka ilikua kama baada ya miezi miwili, na kule ni kwenda kukaa wiki 8, nilivyoona posho ambayo tutakua tunalipwa kule nikaona si haba nikapata msukumo nitafute eneo ninunue nijenge hata msingi kabla sijaondoka, nilikua na akiba yangu fulani kweli nikafanya mpango nikapata kiwanja kikubwa tu pembezoni kidogo ya jiji nikaanza kujenga msingi kimya kimya hapo sijamwambia mtu wala hata sikuona sababu....



Hapo swala la safari wanalijua sema muda bado ulikua haujafika, sasa kuna notebook moja nilikua naandika mahesabu ya site ili co monitor cost Rachel akaja kuiona akawa ananiuliza hayo mahesabu ya nini, nikamwambia kuna mahali nimenunua najenga msingi huko, akakaa kimya ni kama mtu ambae hakufurahishwa maana hata hakuniuliza ni wapi, mchana npo kazini napata ujumbe toka kwake nae kaandika business proposal yake sijui biashara gani anataka milion 3 kabla sijaondoka ya biashara yake, nikamjibu tu plain sina pesa kwa sasa huoni kama najenga



Aisee ni kama nilipalilia moto, huyu binti kumbe alikua na mdomo sana nilikua simjui vizuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ