Ushawahi kujichanganya kimapenzi mpaka ukawa unawaza hapo nyuma ulikosea wapi?

Ushawahi kujichanganya kimapenzi mpaka ukawa unawaza hapo nyuma ulikosea wapi?

Najitahidi Sana nitafute pesa Ili mwenzangu akitumia za kwake hata kama ni Kwa ujinga zisiniume


Kuna madogo wawili nilisoma nao, connection wakapata kazi wizara ya fedha, Hawa Kila siku hua wananiambia wanachowaza wao sio kupata tena pesa ni jinsi ya kuzitumia


Waliwahi Kuja huku likizo, mtu anakodi V8 Kila siku laki 3 Kwa siku 21, hio hata mimi iliniuma nauliza kwanini usinunue tu Sasa la kwako, anakuambia tutanunua tu sa hivi Bado Bado kazini watatushtukia


Sasa mimi laki 6 tu watu roho zinawatoka
Na mimi nimeshangaa sana yani laki 6?? Nikajua milioni 6 maana nilikua sijajua chanzo cha kelele ni nini?

Halafu kwa waelewa ni kwamba hii kesi sio ndogo kimila na kiutamaduni..sasa ili mambo yako yakae poa na uendelee na kazi kwa amani lazima utoe hela..mbona hela zenyewe ndogo sana.

Hebu watupishe watutolee makasiriko...watu wana hela bana tunafautiana matumizi na moyo wa kutoa tuu..
 
Kuna ule uzi wa kulinda vitu upitie, kuna point niliipata kule, kwamba kitu kigumu siyo kupata ila kulinda... Yaaani kupata laki siyo tatizo kuilinda ubaki nayo ndo kazi ...
Usiachie kirahisi kitu ambacho umekipata eti kisa kuna kamtu kanaleta zogo, panda naye juu mpaka haki yako ibaki...

Au tu uwe karibu yangu niwe nakufundisha mara kwa mara 😂😂
Mkuu tuwekee huo uzi tuishi nao bhana huenda tukaokota cha kujifunza huko
 
Nimeishia hapo kwa samira hotelini sijawahi kufanya
FB_IMG_17357426957159619.jpg
 
S3 epi 19


Tukatoka pale nikapata muda kidogo wa kukaa na mwanangu pale, badae tukaaga tukawa tumeondoka, hapo ba mdogo ananiuliza wale wazee mmeishia wapi, hapo mi hata sikutaka kumjibu, akawa ananiambia wale ungeniachia mimi ndo kiboko Yao, nikawa namshangaa tu Sasa maana ye aliwakimbia akaniachia mimi msala.....



Muda unaenda likizo ikafa, nikaanza kwenda kazini kama kawaida, haikupita muda Sana nikaja kupata mkopo kazini, nikamalizia kibanda changu kule Kuna mtu akawa anakaa sikuhamia Bado, sister akanishauri nifungue mini supermarket, nikawa nawaza makorokoro yote Yale siku ya kupiga hesabu si ntakua mwehu mimi nikaachana na Hilo wazo, nikatafuta mahali nikafungua duka la kuuza electronics na accessories zake maana hivi vitu tangia chuo nilishafanya Sana hizi biashara, nikajichanganya mbele nikaweka kibanda Cha miamala ya Simu.... Hii ilikufa mapema tu kuna kipindi huyu dada niliyemueka walikuja wakamtapeli zaidi ya million 2, nikawaza na hizi commission hazifiki hata milioni hapa ntakua nafanyia kazi wajanja nikaachana na hio biashara, G hapo Bado yupo Kwa shangazi yake Wala sikutaka kupeleka mambo Kwa papara, ba mdogo Bado nipo nae town tu.....



Ikaenda mpaka siku Sasa tukahama pale tukahamia nilipojenga Sasa, nikanunua vitu vya ndani ambavyo havipo mpaka kiasi pakaonekana ni nyumba Sasa, kuratibu mawasiliano pale nakumbuka siku wanamleta G Sasa pale alikuja na shangazi yake, yule mama mwenye nyumba kule kwao, mtoto wangu na dada wake wa kazi, mama mkwe alikataa kuja, yule mama mwingine akawa tu ananiambia usijali mwanangu Bado huyu mama hajakaa sawa ila mtakaa sawa tu Wala usiwe na mawazo



Hio siku kwakweli ni kama nikaanza Sasa kupata amani, hatimae naanza kuishi na mwanangu, G nae huyu hapa, nikiangalia hata kama Bado Kuna vinyongo ila Kwa mama yake na wale wazee wake Kwa upande wangu naona nimeshamalizana nao, basi tukala pale ikawa kama kasherehe flani pale



Yule mama na shangazi yake G badae wakampa pale ushauri, wakawa wanamwambia usijione mdogo ndo Sasa ushakua na mji Sasa hivi...badae nikatoka nikawaacha wanashauriana pale sijui waliishia wapi badae wageni wakaaga wakaondoka




Tumebaki Sasa wenyewe, ba mdogo hapo hio siku ana Raha yeye anapiga zake mitungi tu mimi npo kimya ila moyoni Nina amani Kwa kiasi chake, ba mdogo nae sijui ndo kulewa akaanza kujisifu pale mbele ya G, " mimi sijawahi kushindwa jambo, umeona Sasa hili jambo jinsi lilivyokuja kuisha kitaalam" hapo namcheki tu G anacheka zake tu.....



Basi tumekaa pale mpaka muda wa kulala, ba mdogo tumemuacha, dada alikua kashalala, sisi hao na mtoto mpaka chumbani, G anafika kanilalia anacheka tu namuuliza vipi na wewe, akaanza yani tulianza kama matani tu Leo siamini tumefikia hapa..... Nikawa namwambia ndo utulie Sasa ukiniletea ujinga narudi kwenu natafuta mdogo wako hata Kwa ndugu zako naoa huko siwezi kutoa mahari mara mbilimbili kwanza kwenu wamenisumbua Sana, akawa anacheka tu



Kuna kulala Sasa hio siku? Sex kiasi maana tulikua na muda Sana na muda mwingi ni kama tulikesha tu tunaongea mipango ya hapa na pale na Sana Sana kukumbushiana mabalaa yetu, haipiti muda atanitania " kaka unakumbuka ulinibaka?".....



Fast forward.....

Ba mdogo akaja kuondoka, Huku G nae tumbo linazidi kukua tu, maisha yashakua ya amani Sana, tofauti na Rachel G alikua na heshima flani Sana kwangu, zile heshima za kuniheshimu kama kaka kuanzia kipindi kile hazikuwahi kumtoka, mambo yanaenda vizuri tu Sana japokua mama mkwe hakuwahi kuja pale ila tulikua tunaenda kumsalimia na kwenye Simu pia sio kama zamani ila mawasiliano yapo...


Muda ukaenda Sasa G anakaribia kujifungua, mama yangu mzazi mada za G ni kama alikua anazikwepa Sana ikafika muda nikawa nimemsoma na mimi nikaacha kumwambia mambo yake, Sasa Kila kitu hapo tunaona kinaenda sawa, balaa likaja kutokea, Rachel kule sijui alitibua nini, akarudi rasmi mwanza, yule rafiki yake mwenye mgahawa hapo nae kashavutwa sogea tukae na mshkaji mmoja, ikabidi afikie Kwa mama yake, kumbuka hapa mama yake Bado wamepanga pale hajahamia kwake.....




Sasa huyu Binti(Rachel) kumbe kichwa chake kina wadudu, nilikua simjui vizuri
Aisee
 
Kuna ule uzi wa kulinda vitu upitie, kuna point niliipata kule, kwamba kitu kigumu siyo kupata ila kulinda... Yaaani kupata laki siyo tatizo kuilinda ubaki nayo ndo kazi ...
Usiachie kirahisi kitu ambacho umekipata eti kisa kuna kamtu kanaleta zogo, panda naye juu mpaka haki yako ibaki...

Au tu uwe karibu yangu niwe nakufundisha mara kwa mara 😂😂
Hebu nitag kwenye huo Uzi
 
Episode 10

Nipo bar nawaza tu, kwanza ishakua aibu kwa mashemeji, pili bado kuna samira kuna msala kama huu unanisubiri tena,nikasema kazi ninayo, kesho yake nikampigia simu samira hapokei, badae akapokea rafiki yake anasema samira anaumwa sana, mpo wapi anasema hostel... Nikaenda.... Kule kwa mary naogopa hata kupiga simu mashemeji sijui wananichukulia aje,


Kumbe hizi siku nimepotea samira alishafunga sana safari kwenda kwenye lile ghetto lingine, kanitafuta bila mafanikio, mpaka siku majirani wakamwambia hua sikai hapo na wao hata hawajui naishi wapi maana kila nikija hapo nipo na samira sasa, tukiondoka sionekani tena mpaka tuje wote, majirani nyoko😔, samira nae akapanick akawa haelewi anajua naishi hapo siku zote


Nimefika pale nilikaa zaidi ya lisaa hata kunsemesha neno moja aligoma mpaka baadae nikaamua niondoke zangu tu, huku kwa Mary dada angu mkubwa akafunga safari kuja tukae kikao, siku ya kikao tunafanyia nilipokua naishi na Mary wanaongea Mary analia tu, sijui nilishikwa na nini nikasema acha tu mi nimuachie kila kitu Mary mi ntaenda kuanza upya maana naona hawezi kunsamehe huyu akiendelea kuniona atakuja kujiua



Kikao hakijaisha nikaingia ndani, nikasomba vyeti vyangu, begi la kazini, vitu vyangu vidogo vidogo na baadhi ya nguo sikutaka kikao tena nikaondoka zangu.... Kiutani utani tu hivo nikaondoka, nikaenda kule kwenye nyumba ya magendo nikamuita samira akaja, nikasema kuja kuua watoto wa watu kisa nini, amefika nikamueleza kila kitu a to z wala sikumficha kitu, akaanza kulia ananiuliza ulikua na mpango wa kumuacha mkeo au, nikamwambia hapana, aise alilia sana akawa ananiambia usione mpaka umri huu nilikua nimejitunza mimi mpaka ukubwa huu tukirudi nyumbani hua tunakaguliwa na mama mambo ya aibu kabisa, nilipanga nikirudi nikatae tu maana ndo nishafanya sasa, akaniambia najua familia hata ningetengwa ila kwasababu yako niliamua liwalo na liwe, nilikua hata nipo radhi nibadili dini unioe, aisee aliongea sana baadae akaondoka analia tu akaniambia kwaheri Mungu atakulipa
Hii chai ya moto sana
 
Back
Top Bottom