Ushimen: Ebu ngoja leo niwape mawazo machache ya kujikwamua

#3, hiyo inaweza zidi zaidi ya hapo,,

Hapa mwanza kuna sehem huwa naenda mida ya jion kupata sahan moja ya matunda mix,, ni buku tu sahan moja,,

Aiseh anapiga pesa yule,,

[emoji19]
Mkuu, hii nime mention kabisa tayari sehemu na maeneo kadhaa kwenye comments zilizo tangulia.
Naokuomba tu upitie huu uzi taratibu na mengi utayapata hapahapa ndani
 
Aisee
 
Nataka kufungua makeup studio huko Dom wapi patanifaa mkuu?
Mkuu, niliulizwa swali kama hili, ingawa halifanani na hili kwa eneo kubwa.
Ebu pata nafasi upitie post namba 57/58
 
[emoji120][emoji120]
Mkuu, kijiografia Dodoma imegawanyika kwa makundi kadhaa.
Na makundi haya yamejitenga kati ya watumishi, wanafunzi/chuo pamoja na akina sisi wenye maisha ya kuungaunga.
Kwa mtazamo wangu, wapo wateja wanao penda kupelekewa bidhaa karibu sana na sehem wanazo fanyia kazi ili wakipita waone vitu vizuri. Na hili kundi ni aina ya watu wavivu ambao baada ya kutoka job wao wanakuwa wamechoka na wavivu kutembea, ingawa wanakuwa wanatamani waone vitu vizuri.
Kundi la pili ni wanafunzi wa vyuoni kama CBE, UDOM, MIPANGO, ST JOHN, DECCA na kadhalika. Kundi hili linapenda vitu vizuri na vyenye unafuu, ingawa pengine hili ni kundi ambalo linatamani kilasiku mtu awe na kitu kizuri na apendeze kwa gharama yeyote.
Kundi la tatu ni kundi ambalo mimi nimo. Kundi hili ni kwanza wabahili kwelikweli, na ili tununuwe kitu basi lazima tunazungukaga sana ili kulingamisha bei pamoja na kupata unafuu....
Sasa mkuu, haya makundi yote unaweza ukafanikiwa kutoka ikiwa tu wewe utaamua ni aina gani ya biashara yenye unafikiria kuifanya.

Karibu sana Dodoma
 
Bro inabidi nikufind
Mkuu, ebu kwanza fanya zowezi moja ambalo pengine linaweza likakufaa kwa siku ya ijumaa.
Jipe muda na uende pale Stella Bar Nkuhungu, kisha kaa mwanzo kabisa kwenye kilinge cha pale mwanzoni kabisa kama unaingia Stella.
Ukishapata eneo la kukaa, hakikisha utakapo kaa unakuwa unamuona/unamtazama vizuri sana yule kijana pale anaeuza Popcorn/Bisi pembeni ya kibanda cha M-pesa.
Fanya zowezi la kumuhesabia mifuko ya kaki ambayo anafungashia bidhaa zake, na angalia ni wateja wangapi wanachukua mzigo pale kwa masaa hata matatu.
Baada ya hapo, siku inayo fuata nenda pale Malaika Annex Bar, kisha fanya tathmini kwa ile biashara uliyo iona Jana pale Stella, na kisha linganisha na wingi/idadi ya watu/wateja utakao waona pale Annex, alafu jitathmini na wewe kwamba nini ama kipi kinakufaa kufanya.
Na hizi biashara hazihitaji nguvu wala muda wako mwingi sanakuu, zaidi ukipata kijana mnazungumza na kisha mnakubaliana akulipe posho ngapi/day ama weekly.

Ahsante sana kwa hoja
 
Katika pitapita, pamoja na kuhangaika kwangu hasa kwenye kipindi tatanishi cha awamu hii ni:-

1. Sitaki kuwaza kufanya biashara kubwa inayo zidi 1M kwasababu mimi bado ninamaisha ya kawaida.
2. Sitaki kuwaza biashara kubwa kwasababu ninahisi huu sio wakati muafaka kwa kuwekeza fedha nyingi.
3. Nimeamua kufanya kitu ambacho kwanza kitanifanya nimlipe 20 elfu ili nipate kitambulisho chake na nisibughudhiwe nao.
4. Sitaki kuruhusu masikio yangu yakubaliane na mitazamo ya watu ambao watanivunja moyo ama hata kumicheka.
5. Nikifanya utafiti wowote na nikajiridhisha kufanya ujasiriamali, sinto ruhusu kusikiliza ushauri wa walio shindwa.

............. Nitaendelea badae, maana naona saizi whatever-vant imeanza kukamata hatamu....[emoji28][emoji28]
 

No 4&5 huyo ni mimi kabisa
 
No 4&5 huyo ni mimi kabisa
Watu wengi sana tumekuwa tukijikuta tunashindwa kufanya maaamuzi muhimu Katika Maisha tu Kwa kuogopa "WATU WATANIONAJE "
hii Watanionaje Syndrome ni ugonjwa mmbaya sana sababu ni Kitu ambacho ni beyond your control..... Huwezi control vile watu wanafikiria juu yako hata ukifanya jambo in good faith yaani kwa nia njema kabisa jua tu kuna watu wata kutafsiri vingine.... Utasikia.. ..hana lolote.... Anajifanya anajua..... Ana agenda ya siri..... .sio hivi hivi kuna mkono wa mtu..... Ni baadhi tu ya maneno watu watakusema.... Cha msingi weee tenda wema nenda zako usijali watu Watanionaje. Jali katika hili Mungu ananionaje .
Mtu yeyote akitaka kubaini ana akili/maarifa ya kusonga mbele , basi mtu huyo hapaswi kutazama huu ugonjwa wa watu watanionaje.
 
Shukrani Sana kiongozi.. Wala hujachelewa kabisa. Hahaaaaa hiyo whatever K-vant hiyooo ooogh...
 
Hahaaha...
! Malinyi
Malinyi wanalima sana mpunga ila jiandae kupambana na wasukuma wenye ng'ombe maeneo ya Iragua, Itete na Mtimbira wanaopenda kulisha mifugo yao kwenye mashamba ya watu.
Aisee!!
Mwezi uliopita nilikuwa pale Iragua nikakutana na hiyo stori ya Wasukuma nilichoka.
Ila kuna sehemu niliwakuta Warundi wanalima sana nyanya. Mkuu manengelo nadhani utafanikiwa maana wale wafugaji wanapenda waisikie lugha ya kwao tu
 
Shukrani Sana kiongozi.. Wala hujachelewa kabisa. Hahaaaaa hiyo whatever K-vant hiyooo ooogh...
.............[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
Mkuu, karibu sana Dodoma
 
.............[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
Mkuu, karibu sana Dodoma
Asantee Sana.. Nitakutafuta pia unipe kiwanja sehemu rafiki kwa ajili ya makazi.. Najua wewe ni jungu kuu...
 
Aisee!!
Mwezi uliopita nilikuwa pale Iragua nikakutana na hiyo stori ya Wasukuma nilichoka.
Ila kuna sehemu niliwakuta Warundi wanalima sana nyanya. Mkuu manengelo nadhani utafanikiwa maana wale wafugaji wanapenda waisikie lugha ya kwao tu
Wale wafugaji wanakata sana miti na kuharibu misitu hasa maeneo ya Sofi Mission ukiwa unaelekea Malinyi hadi kando kando ya mto Fulua. Mamlaka husika inabidi ziwachukulie hatua wale jamaa.
 
Wale wafugaji wanakata sana miti na kuharibu misitu hasa maeneo ya Sofi Mission ukiwa unaelekea Malinyi hadi kando kando ya mto Fulua. Mamlaka husika inabidi ziwachukulie hatua wale jamaa.
Ni kweli mkuu, niliambiwa wenyewe wanavamia eneo na kuanza kulifyeka bila kujulisha mamlaka. Kuna uoto wa asili wameuharibu sana. Kuna miti imeadimika sana kama vile mipingo, mivule, n.k. sehemu nyingi za nchi yetu lakini kule nimeikuta imejiotea hovyo hovyo tu...
Ila kusema ukweli kule kuna vyanzo vingi sana vya pesa...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…