Ushindi mtamu ni ushindani katika uwanja sawa, sio ule wa mezani. Magufuli, kasi yako ni ushindi wa kishindo. Ruhusu ushindani wa haki, sawa na wazi

Ushindi mtamu ni ushindani katika uwanja sawa, sio ule wa mezani. Magufuli, kasi yako ni ushindi wa kishindo. Ruhusu ushindani wa haki, sawa na wazi

Jiwe kachizi, laiti angejua asingesumbuka na upinzani kwa kutumia nguvu bali akatumia akili angekua sa hivi ana support ya kila mtu. Ujuaji wake umemfanya sa hivi kabaki anapendwa na wanaomuogopa au vilaza tu. Mtu yeyote mwenye akili timamu anamuona ovyo, ndiyo atashinda kwa nguvu au hata bila nguvu nyingi atashinda kwa kua vilaza ndiyo the majority Tanzania ila hatuendi popote, anazidi kujinufaisha mwenyewe tu nchi ipo palepale au inazidi kugawanyika. Ovyo sana yule jamaa level za yule tako wa venezuela, anahisi anafanya sawa kumbe anavuruga
 
Mohamed Said,

Asante sana Mzee Mohamed Said, uchambuzi wa kisayansi kabisa huu, na jibu li wazi, "intervening cause".
Huyo aliyeweka hiyo "intervening cause" anaogopa nini kama anajiamini chama chake kimefanya kazi nzuri katika hii miaka 4? Kampeni yote aliyofanya kwenye mikutano ya hadhara ambayo washindani wake amewakataza, makala za redio na TV zinazomwimbia sifa kedekede, nini kinamtisha mbele ya watu ambao alishawaziba pumzi?
 
Mohamed Said,

Sikubaliani sana na hii hoja.

Huu ni mwendo wa kuviziana; mtu mwenye nguvu, nia mbaya na dhamira kubwa akiamua kukutega kwa namna yoyote atakupata tu. Kwenye uchaguzi mdogo wa Korogwe msimamizi si alitoroka ofisi ili asipokee fomu za wagombea lakini ya ccm akaipokelea chooni? Wasimamizi wa uchaguzi huu waliitwa Ikulu for the first time in history na karibu na uchaguzi! Bila shaka kikubwa walichoitiwa ni uchaguzi.

Prof. Lumumba amedai kuwa hawajaitwa kwa ajili ya maendeleo vinginevyo hicho kikao kingefanyika mara baada ya uchaguzi 2015! Bila shaka yoyote pia moja ya mambo yaliyofanyika kwenye mkutano huo ni kuwafundisha namna ya kutumia sheria kukibeba chama chenye serikali. Kwa mkakati huo mgombea akijaza ACT Wazalendo ni kosa; chama hicho hakipo. Katibu wa Itikadi wa ccm alikuwepo kwenye mkutano huo na kwa jinsi Mbunge zilizotumika zilivyokuwa "shallow and trivial" sitashangaa kama zimebuniwa Lumumba.

Na baada ya kukubaliana hivyo bila shaka uliwekwa utaratibu wa kufanya wagombea wa ccm kupunguza hayo makosa madogo madogo yatakayotumika kuwaengua washindani wao. Na kwa vyovyote vile, hata wangefanya hayo makosa ccm hawawezi kuenguliwa!.
 
Pongezi kwako P kwa andiko zuri.
Na maswali 2 kwako.
(1) ni kweli kua huna kadi ya chama?
(2) umeyaandika haya kutoka moyoni mwako?
Mkuu Mbeba Maono,
Kwanza asante kwa pongezi zako.
1. Sio tuu ni kweli sina kadi ya chama chochote cha siasa, bali sijawahi kujiunga na chama chochote, sio mfuasi wa chama chochote na sio mshabiki wa chama chochote.

Kwa sasa niko over 50, baada ya kuhudumu kwenye habari kwa miaka 30, sasa ni wakati wa kustaafu hivyo nami najipanga kurudisha kidogo kwenye jamii kwa kuwatumikia wananchi, nana Bora kabisa ya kuwatumikia wananchi ni kujitolea kuwa mtumishi wao.

Kwa vile kwa Tanzania ili kuwatumikia wananchi ni lazima ujiunge na chama cha siasa, hivyo nami nikistaafu uandishi wa habari, nitalazimika kujiunga na chama cha siasa kuwatumikia wananchi, kama wakati huo ukifika Tanzania tutakuwa tumeruhusu mgombea binafsi, then mimi nitasimama kama mgombea binafsi kuwatumikia wananchi.

2. Hili la kuandika kutoka moyoni naomba nisilijibu bali nikufundishe kitu na wewe ili next time kuna maswali ukijiuliza unajijibu mwenyewe sio mpaka kuuliza.

Namna ya kujua kama mwandishi ameandika kutoka moyoni au amejiandikia tuu kwasababu anaweza kuandika, ni kupitia kwako wewe msomaji moyo wako umekuambia nini baada ya kusoma bandiko hili.

Kuusikilizia moyo kwenye maandishi ya mtu kunaitwa "reading in between the lines " huu ni uwezo wa kusoma andiko na kujua mwandishi alidhamiria nini, ukimaliza kusoma na kutafakari ni wewe mwenyewe ndio utagundua kama mwandishi alidhamiria or was just paying lip services.
P
 
Hizi ni dalili za ubinafsi wa kipuuzi!!! Hujui kuwa gharama kubwa inayotokana na matumizi makubwa ya nishati ya mafuta kwenye foleni pale makutano Ubungo itapungua sana!? Upungufu huo utasidia ela zilizokuwa zinatumika kununulia mafuta za zitatumika kununulia vitu vingine vya muhimu kwa watanzania wote hata na huyo mkulima wa chikichi Kigoma!?

Acha ubinafsi wa kipuuzi!!!

Hoja ya mafuta nayo ni dhaifu....

Jenga hoja ya kushawishi na kueleweka, sio habari za mafuta.
 
Pascal Mayalla,
.Mkuu unapotoka hapa. Vyama vya upinzani kama havikufanya training kwa wagombea wao hilo sio tatizo la Chama Cha mapinduzi. Hatuwezi kuwa na viongozi ambao hawawezi hata kujaza form za kugombea nafasi za uongozi. Ndio sababu kubwa Mwalimu Enzi zake alipeleka watu Gumbaro ili waendane na wakati. Uchaguzi utafanyika na JPM hawezi kuingilia. Vyama vya upinzani wajipange upya hapa kazi tu.
 
Kuishi kwingi kuona mengi tunaposema uongozi haujalibishwi tunamanisha kutokumjalibisha mtu katika uongozi Mkubwa Kama RAIS Tanzania ni kubwa kuriko RAIS rakini kwasababu tunachagua kwakufanya majalibio acha tusoteshwe kwenye inchi yetu wenyewe tumepokwa hata ile kusema hili Hapana inamana hata Huko ccm hawayaoni Haya wanamuona magufuli Kama kashuka toka mbinguni Kumbe tupo nae miaka yote hata nyumba zetu aliuzia hawala na ndugu zake. Dah Ngoja niishie Hapa japo inatia uchungu Sana
 
Pascal Mayalla,
Aache ukandamizaji. Asiongoze nchi hii kwa mihemko yake ambayo kwa sasa inazidi kushangiliwa na vibaraka wachumia tumbo waliomzunguka, wakiwamo hata wasomi ambao wanajipendekeza kwa kujinasibu kuwa waliokotwa 'jalalani'.
Anakotupeleka bado kidogo kutaifanya nchi yetu ifikie hali ile waliowahi kuwa nayo SA, Zimbabwe, Mozambique, Angola, Guinea Bisau, Cape Verde etc.ambayo Tanzania (iliyoongozwa na Nyerere) ilisaidia kuwakomboa. Mgonjwa wa malaria sugu anahitaji tiba ya haraka na SIO kumuomba aonje kwanza Dawa. AMEN
 
Nimekuuliza hayo maswali makusudi tu ili kupima uelewa wako kwenye suala mzima la sheria za uchaguzi. ila kwa nilichojibiwa moja kwa moja Inaonyesha ndugu yangu Umekunywa maji ya bendera ya kijani na njano.
Nimekuwa mchambuzi wa kanuni na taratibu za uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2014 na 2019 kwenye Redio FM za huku kwetu. Kwahiyo sio mgeni kama unavyonifikiria.
 
nikuteue nikupe nyumba na gari halafu umtangaze mpinzani - Pascal haya maneno uliyasoma na kuyachambua kwa ufahamu wa kiasi gani, imagine upo kwenye hii ajira na umeipokea - What will u do?
 
Wanabodi,

Tangu kuanza kwa pilika pilika za uchaguzi wa Serikali za Mitaa, sijawahi kuzungumza lolote kutokana na kuwa bize na shughuli za kitaifa, kwanza ni Wiki ya Msaada wa Kisheria iliyofanyika kitaifa mjini Bariadi Mkoani Simiyu na kufuatiwa na Wiki ya Azaki iliyomalizika jana Jijini Dodoma, hivyo leo ndio nimepata fursa kuendelea na zile makala zangu za " Kwa Maslahi ya Taifa".

Mada kuu kuhusu makala ya leo ni hizi figisu figisu za uchaguzi serikali za mitaa zilizopelekea Chama kikuu cha upinzani kwa huku bara, Chadema, kujitoa kikifuatiwa na Chama cha ACT.
This is not good at all kwa mustakabali mwema wa nchi yetu.

Sitaki kuingia ndani kwenye technicalities zilizopelekea wagombea wa upinzani kuenguliwa, bali natoa wito kwa rais Magufuli aingilie kati hali hii au yeye mwenyewe kama rais wa JMT, au kupitia kwa Waziri Jaffo wa Tamisemi, ayafute makosa yote ya wagombea wote wa vyama vyote walioenguliwa kwa sababu zozote, ziwe ni za kweli za halali au ni figisu, watoe amnesty kila aliyegombea apitishwe tuu hivyo hivyo despite all the odds ili Tanzania tuingie kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu Mwakani kwa Ushindani wa haki, uwazi na Usawa kwa vyama vyote kutendewa haki sawa, hivyo waliosusa wote warudi.

Ushindi mnono na mtamu ni ule ushindi unaotokana na ushindani wa haki unaopatikana uwanjani kwenye uwanja ulio sawa, level ground na sio uwanja tange, wala sio ushindi wa mezani!.

Kwa observation yangu, kwa kasi ya rais Dr. John Pombe Joseph Magufuli, JPM, kwa haya tuu aliyowafanyia Watanzania kwa miaka hii minne tuu tangu alipoingia madarakani, na mambo anayoendelea kuyafanya kila uchao, ni mambo mkubwa kuliko rais mwingine yoyote ayeyewahi kufanya, ukimuondoa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliyetupatia uhuru na kutujengea Umoja, Upendo na Mshikamano wa Watanzania kuwa kitu kimoja, Taifa moja lenye umoja, lisilo na ubaguzi wa udini, ukabila, rangi, jinsia na hali.

Kutokana na kasi ya rais Magufuli kutuletea maendeleo ya vitu vya kuonekanika, Midege, Reli ya SGR, Mabarabara nchi nzima, madaraja ya Juu kwa Juu, Mradi wa umeme wa Stigler , Tanzania ya Viwanda, Elimu Bure, Vituo vya Afya kila kuna, etc, etc, just to mention but few, vinaipa CCM fursa ya ushindi wa kishindo cha wazi kabisa katika uchaguzi wowote nchini Tanzania kati ya sasa hadi 2025, hivyo mamlaka zinazosimamia uchaguzi huu, waruhusuni wagombea wote waliopitishwa na vyama vyao wapite tuu bila kujalisha kama wanekidhi sifa na vigezo, ili tuu kuruhusu ushindani wa haki, ushindani wa uwazi na mshindi apatikane kihalali katika uchaguzi huru na wa haki.

Nakumbuka nilipokuwa Baba Kijana, nilikuwa nikicheza na watoto wangu michezo mbalimbali kama kukimbia, mnashindana kukimbia, ili kumjengea mtoto ari ya kushinda, wewe unakimbia kidogo kidogo ili usimshinde mtoto ukamvunja moyo, unamuacha mtoto akupite na akushinde na akiisha shinda, anafurahi kweli kweli kuwa amemshinda baba!. Hivyo tukubali tukatae, kwa hali ya sasa ya siasa zetu na hii kasi ya JPM, ili Tanzania tuendelee kuwa ni nchi ya vyama vingi, kuna maeneo CCM inabidi tuu ijifanye baba anacheza na watoto kwa kuwaachia tuu washinde, vinginevyo ni tunarudi kwenye nchi ya chama kimoja!.

Hivyo natoa wito kwa serikali ya CCM, chini ya Jemedari wake, JPM, kiukweli labisa, hata kabila ya uchaguzi, CCM tayari imeishashinda kwa ushindi wa kishindo sio tuu huu
Uchanguzi wa Serikali za Mitaa, bali hadi Uchanguzi Mkuu ujao wa mwakani 2020 kutokana na sababu za ki political social dynamics ya Magufulification, lakini ili CCM iweze kuufurahia huo ushindi kwa fursa ya kweli na hivyo kusheherekea ushindi huo, kazima CCM ishinde kwenye ushindani wa kweli na sio kuchukua mpira kwapani, au kufanya figisu ushindani wasuse, wewe upewe ushindi wa mezani.

Nakuomba Rais Magufuli na Waziri Jafo, jifanyeni kama mnacheza na watoto, wafungulieni njia watoto wote washiriki kwenye uchaguzi huu kwa uhuru na kwa haki sawa kwa vyama vyote despite mapungufu walionayo ili hata uchaguzi Mkuu wa mwaka kesho, wakati Watanzania watakapo irejesha Tanzania kwenye mfumo wa Chama kimoja CCM, iwe ni Watanzania wenyewe ndio wameamua kupitia uchaguzi huru na wa haki ulioendeshwa na Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi ulioendeshwa kwenye uwanja sawa na tambarare, na sio CCM ishinde katika ule ushindani wa kugombea kisu cha makali kuwili, huku mshindani mmoja ameshika kwenye mpini. Hivyo CCM ishinde kihalali kwa Miami wa kazi nzuri ya rais JPM na sio kwa sababu ndio iliyokamata mpini.

Tena kwa maoni yangu uchaguzi huu wa serikali za mitaa unaosimamiwa na TAMISEMI ndio uwe wa mwisho, tubadili sheria zetu za uchaguzi, uchaguzi zote zisimamiwe na sheria moja, chini ya Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi, zuio la mikutano ya siasa liondolewe, wagombea huru waruhusiwe ili hata watu kama akina sisi tusio wanachama wa chama chochote, tuweze kushiriki kugombea, hivyo uchaguzi wa 2025 tuchague viongozi wa serikali za mtaa, madiwani, wabunge na rais kwa siku moja. Hoja kuwa zitakuwa kura nyingi haina mashiko. Kwenye uchaguzi Mkuu wa Zanzibar kila mpiga kura anapiga kura 5 kuchagua
  1. Diwani,
  2. Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi
  3. Mbunge wa Bunge la JMT
  4. Rais wa Zanzibar
  5. Rais wa JMT
Hivyo Tanzania tukiamua kufanya uchaguzi huru na wa haki, unaofusta mfumo wa uchaguzi wa kidemokrasia ya ukweli, tunaweza. Mimi naamini kabisa kwa mambo makubwa na mazuri ya Rais Magufuli anayoyafanya, We have nothing to loose rais Magufuli akiruhusu demokrasia ikashamiri, akatoa haki sawa kwa vyama vyote kufanya siasa ikiwemo kuondoa zuio la mikutano ya siasa, bado rais Magufuli anaweza kuyaleta maendeleo yote aliyokusudia at the same time huku akiruhusu demokrasia nayo ishamiri, ila ukweli utaendelea kubaki ni ukweli daima kwa katiba hii na kasi hili ya rais Magufuli, CCM bado itaendelea kutawala Tanzania milele.

Naomba nimalizie kwa ile kauli ya thread hii
"Ushindi Mtamu ni Ushindi Unaopatikana kwa Ushindani Wa Haki Kwenye Uchaguzi Huru na Wa Haki, Unaendeshwa na Tume Huru na Shirikishi, na Unaofanyika Kwenye Uwanja Sawa wa Ushindani wa Kisiasa, Sio Ushindi wa Mezani!. Mheshimiwa Rais, Dr. John Pombe Magufuli, aka.JPM, Kasi Yako ya Maendeleo ya Tanzania Unaoifanya, Utailetea CCM Ushindi Kishindo Katika Uchaguzi Wowote, Tunakuomba Please Please Please, Ruhusu Tuu Ushindani wa Haki, Wazi na Usawa Kwa Vyama Vyote,
Utabarikiwa Zaidi na Zaidi, na Tanzania Tutabarikiwa.

Nawatakia Jumapili Njema
Na mimi nawahi kanisani
Misa ya Kwanza pale kanisa langu la St.Peters

Paskali
Umenikumbusha bao la mkono
 
Wanabodi,

Tangu kuanza kwa pilika pilika za uchaguzi wa Serikali za Mitaa, sijawahi kuzungumza lolote kutokana na kuwa bize na shughuli za kitaifa, kwanza ni Wiki ya Msaada wa Kisheria iliyofanyika kitaifa mjini Bariadi Mkoani Simiyu na kufuatiwa na Wiki ya Azaki iliyomalizika jana Jijini Dodoma, hivyo leo ndio nimepata fursa kuendelea na zile makala zangu za " Kwa Maslahi ya Taifa".

Mada kuu kuhusu makala ya leo ni hizi figisu figisu za uchaguzi serikali za mitaa zilizopelekea Chama kikuu cha upinzani kwa huku bara, Chadema, kujitoa kikifuatiwa na Chama cha ACT.
This is not good at all kwa mustakabali mwema wa nchi yetu.

Sitaki kuingia ndani kwenye technicalities zilizopelekea wagombea wa upinzani kuenguliwa, bali natoa wito kwa rais Magufuli aingilie kati hali hii au yeye mwenyewe kama rais wa JMT, au kupitia kwa Waziri Jaffo wa Tamisemi, ayafute makosa yote ya wagombea wote wa vyama vyote walioenguliwa kwa sababu zozote, ziwe ni za kweli za halali au ni figisu, watoe amnesty kila aliyegombea apitishwe tuu hivyo hivyo despite all the odds ili Tanzania tuingie kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu Mwakani kwa Ushindani wa haki, uwazi na Usawa kwa vyama vyote kutendewa haki sawa, hivyo waliosusa wote warudi.

Ushindi mnono na mtamu ni ule ushindi unaotokana na ushindani wa haki unaopatikana uwanjani kwenye uwanja ulio sawa, level ground na sio uwanja tange, wala sio ushindi wa mezani!.

Kwa observation yangu, kwa kasi ya rais Dr. John Pombe Joseph Magufuli, JPM, kwa haya tuu aliyowafanyia Watanzania kwa miaka hii minne tuu tangu alipoingia madarakani, na mambo anayoendelea kuyafanya kila uchao, ni mambo mkubwa kuliko rais mwingine yoyote ayeyewahi kufanya, ukimuondoa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliyetupatia uhuru na kutujengea Umoja, Upendo na Mshikamano wa Watanzania kuwa kitu kimoja, Taifa moja lenye umoja, lisilo na ubaguzi wa udini, ukabila, rangi, jinsia na hali.

Kutokana na kasi ya rais Magufuli kutuletea maendeleo ya vitu vya kuonekanika, Midege, Reli ya SGR, Mabarabara nchi nzima, madaraja ya Juu kwa Juu, Mradi wa umeme wa Stigler , Tanzania ya Viwanda, Elimu Bure, Vituo vya Afya kila kuna, etc, etc, just to mention but few, vinaipa CCM fursa ya ushindi wa kishindo cha wazi kabisa katika uchaguzi wowote nchini Tanzania kati ya sasa hadi 2025, hivyo mamlaka zinazosimamia uchaguzi huu, waruhusuni wagombea wote waliopitishwa na vyama vyao wapite tuu bila kujalisha kama wanekidhi sifa na vigezo, ili tuu kuruhusu ushindani wa haki, ushindani wa uwazi na mshindi apatikane kihalali katika uchaguzi huru na wa haki.

Nakumbuka nilipokuwa Baba Kijana, nilikuwa nikicheza na watoto wangu michezo mbalimbali kama kukimbia, mnashindana kukimbia, ili kumjengea mtoto ari ya kushinda, wewe unakimbia kidogo kidogo ili usimshinde mtoto ukamvunja moyo, unamuacha mtoto akupite na akushinde na akiisha shinda, anafurahi kweli kweli kuwa amemshinda baba!. Hivyo tukubali tukatae, kwa hali ya sasa ya siasa zetu na hii kasi ya JPM, ili Tanzania tuendelee kuwa ni nchi ya vyama vingi, kuna maeneo CCM inabidi tuu ijifanye baba anacheza na watoto kwa kuwaachia tuu washinde, vinginevyo ni tunarudi kwenye nchi ya chama kimoja!.

Hivyo natoa wito kwa serikali ya CCM, chini ya Jemedari wake, JPM, kiukweli labisa, hata kabila ya uchaguzi, CCM tayari imeishashinda kwa ushindi wa kishindo sio tuu huu
Uchanguzi wa Serikali za Mitaa, bali hadi Uchanguzi Mkuu ujao wa mwakani 2020 kutokana na sababu za ki political social dynamics ya Magufulification, lakini ili CCM iweze kuufurahia huo ushindi kwa fursa ya kweli na hivyo kusheherekea ushindi huo, kazima CCM ishinde kwenye ushindani wa kweli na sio kuchukua mpira kwapani, au kufanya figisu ushindani wasuse, wewe upewe ushindi wa mezani.

Nakuomba Rais Magufuli na Waziri Jafo, jifanyeni kama mnacheza na watoto, wafungulieni njia watoto wote washiriki kwenye uchaguzi huu kwa uhuru na kwa haki sawa kwa vyama vyote despite mapungufu walionayo ili hata uchaguzi Mkuu wa mwaka kesho, wakati Watanzania watakapo irejesha Tanzania kwenye mfumo wa Chama kimoja CCM, iwe ni Watanzania wenyewe ndio wameamua kupitia uchaguzi huru na wa haki ulioendeshwa na Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi ulioendeshwa kwenye uwanja sawa na tambarare, na sio CCM ishinde katika ule ushindani wa kugombea kisu cha makali kuwili, huku mshindani mmoja ameshika kwenye mpini. Hivyo CCM ishinde kihalali kwa Miami wa kazi nzuri ya rais JPM na sio kwa sababu ndio iliyokamata mpini.

Tena kwa maoni yangu uchaguzi huu wa serikali za mitaa unaosimamiwa na TAMISEMI ndio uwe wa mwisho, tubadili sheria zetu za uchaguzi, uchaguzi zote zisimamiwe na sheria moja, chini ya Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi, zuio la mikutano ya siasa liondolewe, wagombea huru waruhusiwe ili hata watu kama akina sisi tusio wanachama wa chama chochote, tuweze kushiriki kugombea, hivyo uchaguzi wa 2025 tuchague viongozi wa serikali za mtaa, madiwani, wabunge na rais kwa siku moja. Hoja kuwa zitakuwa kura nyingi haina mashiko. Kwenye uchaguzi Mkuu wa Zanzibar kila mpiga kura anapiga kura 5 kuchagua
  1. Diwani,
  2. Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi
  3. Mbunge wa Bunge la JMT
  4. Rais wa Zanzibar
  5. Rais wa JMT
Hivyo Tanzania tukiamua kufanya uchaguzi huru na wa haki, unaofusta mfumo wa uchaguzi wa kidemokrasia ya ukweli, tunaweza. Mimi naamini kabisa kwa mambo makubwa na mazuri ya Rais Magufuli anayoyafanya, We have nothing to loose rais Magufuli akiruhusu demokrasia ikashamiri, akatoa haki sawa kwa vyama vyote kufanya siasa ikiwemo kuondoa zuio la mikutano ya siasa, bado rais Magufuli anaweza kuyaleta maendeleo yote aliyokusudia at the same time huku akiruhusu demokrasia nayo ishamiri, ila ukweli utaendelea kubaki ni ukweli daima kwa katiba hii na kasi hili ya rais Magufuli, CCM bado itaendelea kutawala Tanzania milele.

Naomba nimalizie kwa ile kauli ya thread hii
"Ushindi Mtamu ni Ushindi Unaopatikana kwa Ushindani Wa Haki Kwenye Uchaguzi Huru na Wa Haki, Unaendeshwa na Tume Huru na Shirikishi, na Unaofanyika Kwenye Uwanja Sawa wa Ushindani wa Kisiasa, Sio Ushindi wa Mezani!. Mheshimiwa Rais, Dr. John Pombe Magufuli, aka.JPM, Kasi Yako ya Maendeleo ya Tanzania Unaoifanya, Utailetea CCM Ushindi Kishindo Katika Uchaguzi Wowote, Tunakuomba Please Please Please, Ruhusu Tuu Ushindani wa Haki, Wazi na Usawa Kwa Vyama Vyote,
Utabarikiwa Zaidi na Zaidi, na Tanzania Tutabarikiwa.

Nawatakia Jumapili Njema
Na mimi nawahi kanisani
Misa ya Kwanza pale kanisa langu la St.Peters

Paskali
Who knows km yy no1 ndo alitoa maekekezo hayo na yanamfurahisha? Kumbuka alishawahi kusema hataki upinzani ktk wake. Nakumbuka vizuri kaka pascal uliwahi muuliza katumia sheria gani kufuta mikutano ya siasa na alikujibu blaa blaa kwamba mayala kwao ni njaa, ss huyo hawezi kuingilia haya maana yanamfurahisha na inawezekana yana baraka zake.
 
Pascal Mayalla,

Muhimu sana kuacha uchaguzi uwe huru. Upinzani ukishinda sehemu flani inamaanisha wananchi wanawaamini. Labda wamefanya vitu vya maana.


Serikali ijikite kuleta maendeleo, maji, umeme, barabara, elimu, Afya, baadaye makazi bora, kuwawezesha wafanyabiashara wadogo, wakulima wawe wakubwa, ili watoe ajira kwa vijana.

Time is most important asset for human being, (binadamu). How your use time, money,where, when, in what projects is very important, Crucial.

Serikali itumie muda wake kwa mambo yatayowasadia Watanzania wengi.

Wapinzani wakipata viti asilimia tano, kumi, sio kesi.

Muhimu ku- avoiid distractions, kutoyumbishwa, kuwekewa vikwazo.
Serikali should, must, is necessary, inabidi to focus on important issues.
.
 
Back
Top Bottom