Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
P kwani la broken clock linani? Au msemo haujaeleweka niifafanue!🙂Mkuu Nguruvi, asante kunirudishia watu kwenye mstari, ila hilo la the broken clock is right twice a day.
P
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
P kwani la broken clock linani? Au msemo haujaeleweka niifafanue!🙂Mkuu Nguruvi, asante kunirudishia watu kwenye mstari, ila hilo la the broken clock is right twice a day.
P
Mkuu Jingalao, huu usemi japo mchungu lakini ndio ukweli wenyewe, kama ilivyo kwa penzi ni kama kiti cha basi, unaposhuka, anakaa mwenzio, na ganda la mua la jana, chungu aona kivuno, ukisusa, wao wala!. Kabla hata ya uchaguzi, CCM itakuwa imeshinda ushindi wa mezani kwa more than 75%, uchaguzi ni kukamilisha tuu ile 25%.Jaffo alie kwa lipi??wewe susa sie twala
Mkuu ulilosema ni kweli TUPU..Sio tu apimwe afya ya akili bali kuwe na kiwango maalumu cha IQ inayofaa at that time for presidential post.
Kwa sasa sina hakika kama wataendelea na msimamo wa kujitoa; ila hawa wajitoe wasijitoe ule mkakati wa kuhakikisha chama tawala kinachukua ushindi, kwenye hayo maeneo ambayo wapinzani wamesimama bado upo pale pale. Niliposema too late nilikuwa naliona hilo. Wapinzani walitakiwa kuwa na msimamo mapema na sio kubadilisha gia angani. Wakitaka uzoefu wawaulize wapinzani kule Zanzibar watajua what CCM is.Mkuu Zawadin, kama sababu za kujitoa ni kitendo cha wagombea wao kukatwa, sasa wagombea wote wamerudishwa, kwanini waendelee kujitoa?.
P
Mkuu Bishweko, kwanza asante kwa swali zuri tena ni swali la msingi sana na jibu la swali hili ndilo linaifanya CCM ishinde chaguzi zote na CCM itatawala milele Tanzania, unless katiba ya sasa ibadilishwe.Nirudi kwa Paskali..inawezekana vipi leo unatuambia kua Serikali ya CCM huku Katiba ikitamka kua ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?
UMEKUWA MTABIRI WA KINDAKI NDAKI!Huyu bwana ni mzuri wa kutengeneza tatizo na kulitatua ili apate umaarufu zaidi. Sitashangaa nikisika Dr Abasi akisema “Mheshimiwa rais Dk John Pombe Magufuli amewasamehe wote waliojaza fomu kimakosa”.
Hili haliwezi kutokea kwa CCM.'Kutokana na kasi ya rais Magufuli kutuletea maendeleo ya vitu vya kuonekanika, Midege, Reli ya SGR, Mabarabara nchi nzima, madaraja ya Juu kwa Juu, Mradi wa umeme wa Stigler , Tanzania ya Viwanda, Elimu Bure, Vituo vya Afya kila kuna, etc, etc, just to mention but few, vinaipa CCM fursa ya ushindi wa kishindo cha wazi kabisa katika uchaguzi wowote nchini Tanzania kati ya sasa hadi 2025, hivyo mamlaka zinazosimamia uchaguzi huu, waruhusuni wagombea wote waliopitishwa na vyama vyao wapite tuu bila kujalisha kama wanekidhi sifa na vigezo, ili tuu kuruhusu ushindani wa haki, ushindani wa uwazi na mshindi apatikane kihalali katika uchaguzi huru na wa haki'.
Nimekuelewa vizuri mkuu Pascal Mayalla
Ulijisumbua kufikiri kabla ya kuandika hiki ulichoandika?Watu Hawachagui Rais kwenye uchaguzi huu. Unapotaja reli sijui ndege elimu bure na mwingine kama huo ni mwenyekiti gani wa mtaa ataweza kununua kwa ajili ya mtaa wake?
Kuna wasomi wengine hovyo sana aisee.
Mkuu Flulanga, kila mtu mwenye kujua kusoma na kuandika anaweza kusoma chochote na kuandika chochote, ila binadamu tumetofautiana uwezo wa kuandika na kuelewa, wengine wanaweza kuandika chochote muda wowote hata akiwa kwenye dala dala, sisi wengine ili kuandika baadhi ya vitu unahitaji kutulia kutafakari ndipo uandike, wiki jana nzima nilikuwa Dodoma na Azaki.Acha uongo kusema ulikuwa bize. wakati kila mara ulikuwepo humu kufufua nyuzi zako mfu!!
Mkuu Bila Bila, mimi ni mkweli daima na nilichokisema humu ni ukweli mtupu.Bora umemwambia wazi. Pascal ni mhuni wa kisiasa, ni mwandishi mtafuta fursa wa kiwango cha juu. Anaandika kwa kulembalemba ili aonekane mwema kwa kaka yake. Ni eneo gani nchini ambako CCM yake haijatoa maelekezo kwa watendaji kukata majina ya Wapinzani? Leo anajifanya mwema anauma na kupuliza? Aache unafiki, kama ni mkweli auseme ukweli wote na siyo mafumbo na kujitafutia sifa binafsi.
lisemwalo lipo kama halipo laja... hutakiwi kua na pupa.. subili kwanza.Wanasamehewa vipi ilhali wamejitoa? Kama mlizira kwa kumdeshi jiwe imekula kwenu. Subirini 2024
wanakuaje na vigezo? ikiwa kwanza wamekosea kuja fomu.. pili hawana chama? je? wagombea binfsi wameanza kuruhusiwa tz? ama kweli siku ya kutembea uchi ndio hiyo hiyo utakutana na mkweo .fedhea kubwa hiiKama wana vigezo vyote majina yao yatabandikwa. Ni utaratibu na kanuni za uchaguzi. Wao hawafuati porojo za vyama kujitoa ingawaje wenye majina yatakayobandikwa wana hiari ya kufanya kampeni au la. Kimbembe kitakuwa endapo watashinda, Chadema itawatambua? Itawafukuza? Tunasubiria!
Wanabodi,
Tangu kuanza kwa pilika pilika za uchaguzi wa Serikali za Mitaa, sijawahi kuzungumza lolote kutokana na kuwa bize na shughuli za kitaifa, kwanza ni Wiki ya Msaada wa Kisheria iliyofanyika kitaifa mjini Bariadi Mkoani Simiyu na kufuatiwa na Wiki ya Azaki iliyomalizika jana Jijini Dodoma, hivyo leo ndio nimepata fursa kuendelea na zile makala zangu za " Kwa Maslahi ya Taifa".
Mada kuu kuhusu makala ya leo ni hizi figisu figisu za uchaguzi serikali za mitaa zilizopelekea Chama kikuu cha upinzani kwa huku bara, Chadema, kujitoa kikifuatiwa na Chama cha ACT.
This is not good at all kwa mustakabali mwema wa nchi yetu.
Sitaki kuingia ndani kwenye technicalities zilizopelekea wagombea wa upinzani kuenguliwa, bali natoa wito kwa rais Magufuli aingilie kati hali hii au yeye mwenyewe kama rais wa JMT, au kupitia kwa Waziri Jaffo wa Tamisemi, ayafute makosa yote ya wagombea wote wa vyama vyote walioenguliwa kwa sababu zozote, ziwe ni za kweli za halali au ni figisu, watoe amnesty kila aliyegombea apitishwe tuu hivyo hivyo despite all the odds ili Tanzania tuingie kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu Mwakani kwa Ushindani wa haki, uwazi na Usawa kwa vyama vyote kutendewa haki sawa, hivyo waliosusa wote warudi.
Ushindi mnono na mtamu ni ule ushindi unaotokana na ushindani wa haki unaopatikana uwanjani kwenye uwanja ulio sawa, level ground na sio uwanja tange, wala sio ushindi wa mezani!.
Kwa observation yangu, kwa kasi ya rais Dr. John Pombe Joseph Magufuli, JPM, kwa haya tuu aliyowafanyia Watanzania kwa miaka hii minne tuu tangu alipoingia madarakani, na mambo anayoendelea kuyafanya kila uchao, ni mambo mkubwa kuliko rais mwingine yoyote ayeyewahi kufanya, ukimuondoa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliyetupatia uhuru na kutujengea Umoja, Upendo na Mshikamano wa Watanzania kuwa kitu kimoja, Taifa moja lenye umoja, lisilo na ubaguzi wa udini, ukabila, rangi, jinsia na hali.
Kutokana na kasi ya rais Magufuli kutuletea maendeleo ya vitu vya kuonekanika, Midege, Reli ya SGR, Mabarabara nchi nzima, madaraja ya Juu kwa Juu, Mradi wa umeme wa Stigler , Tanzania ya Viwanda, Elimu Bure, Vituo vya Afya kila kuna, etc, etc, just to mention but few, vinaipa CCM fursa ya ushindi wa kishindo cha wazi kabisa katika uchaguzi wowote nchini Tanzania kati ya sasa hadi 2025, hivyo mamlaka zinazosimamia uchaguzi huu, waruhusuni wagombea wote waliopitishwa na vyama vyao wapite tuu bila kujalisha kama wanekidhi sifa na vigezo, ili tuu kuruhusu ushindani wa haki, ushindani wa uwazi na mshindi apatikane kihalali katika uchaguzi huru na wa haki.
Nakumbuka nilipokuwa Baba Kijana, nilikuwa nikicheza na watoto wangu michezo mbalimbali kama kukimbia, mnashindana kukimbia, ili kumjengea mtoto ari ya kushinda, wewe unakimbia kidogo kidogo ili usimshinde mtoto ukamvunja moyo, unamuacha mtoto akupite na akushinde na akiisha shinda, anafurahi kweli kweli kuwa amemshinda baba!. Hivyo tukubali tukatae, kwa hali ya sasa ya siasa zetu na hii kasi ya JPM, ili Tanzania tuendelee kuwa ni nchi ya vyama vingi, kuna maeneo CCM inabidi tuu ijifanye baba anacheza na watoto kwa kuwaachia tuu washinde, vinginevyo ni tunarudi kwenye nchi ya chama kimoja!.
Hivyo natoa wito kwa serikali ya CCM, chini ya Jemedari wake, JPM, kiukweli labisa, hata kabila ya uchaguzi, CCM tayari imeishashinda kwa ushindi wa kishindo sio tuu huu
Uchanguzi wa Serikali za Mitaa, bali hadi Uchanguzi Mkuu ujao wa mwakani 2020 kutokana na sababu za ki political social dynamics ya Magufulification, lakini ili CCM iweze kuufurahia huo ushindi kwa fursa ya kweli na hivyo kusheherekea ushindi huo, kazima CCM ishinde kwenye ushindani wa kweli na sio kuchukua mpira kwapani, au kufanya figisu ushindani wasuse, wewe upewe ushindi wa mezani.
Nakuomba Rais Magufuli na Waziri Jafo, jifanyeni kama mnacheza na watoto, wafungulieni njia watoto wote washiriki kwenye uchaguzi huu kwa uhuru na kwa haki sawa kwa vyama vyote despite mapungufu walionayo ili hata uchaguzi Mkuu wa mwaka kesho, wakati Watanzania watakapo irejesha Tanzania kwenye mfumo wa Chama kimoja CCM, iwe ni Watanzania wenyewe ndio wameamua kupitia uchaguzi huru na wa haki ulioendeshwa na Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi ulioendeshwa kwenye uwanja sawa na tambarare, na sio CCM ishinde katika ule ushindani wa kugombea kisu cha makali kuwili, huku mshindani mmoja ameshika kwenye mpini. Hivyo CCM ishinde kihalali kwa Miami wa kazi nzuri ya rais JPM na sio kwa sababu ndio iliyokamata mpini.
Tena kwa maoni yangu uchaguzi huu wa serikali za mitaa unaosimamiwa na TAMISEMI ndio uwe wa mwisho, tubadili sheria zetu za uchaguzi, uchaguzi zote zisimamiwe na sheria moja, chini ya Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi, zuio la mikutano ya siasa liondolewe, wagombea huru waruhusiwe ili hata watu kama akina sisi tusio wanachama wa chama chochote, tuweze kushiriki kugombea, hivyo uchaguzi wa 2025 tuchague viongozi wa serikali za mtaa, madiwani, wabunge na rais kwa siku moja. Hoja kuwa zitakuwa kura nyingi haina mashiko. Kwenye uchaguzi Mkuu wa Zanzibar kila mpiga kura anapiga kura 5 kuchagua
Hivyo Tanzania tukiamua kufanya uchaguzi huru na wa haki, unaofusta mfumo wa uchaguzi wa kidemokrasia ya ukweli, tunaweza. Mimi naamini kabisa kwa mambo makubwa na mazuri ya Rais Magufuli anayoyafanya, We have nothing to loose rais Magufuli akiruhusu demokrasia ikashamiri, akatoa haki sawa kwa vyama vyote kufanya siasa ikiwemo kuondoa zuio la mikutano ya siasa, bado rais Magufuli anaweza kuyaleta maendeleo yote aliyokusudia at the same time huku akiruhusu demokrasia nayo ishamiri, ila ukweli utaendelea kubaki ni ukweli daima kwa katiba hii na kasi hili ya rais Magufuli, CCM bado itaendelea kutawala Tanzania milele.
- Diwani,
- Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi
- Mbunge wa Bunge la JMT
- Rais wa Zanzibar
- Rais wa JMT
Naomba nimalizie kwa ile kauli ya thread hii
"Ushindi Mtamu ni Ushindi Unaopatikana kwa Ushindani Wa Haki Kwenye Uchaguzi Huru na Wa Haki, Unaendeshwa na Tume Huru na Shirikishi, na Unaofanyika Kwenye Uwanja Sawa wa Ushindani wa Kisiasa, Sio Ushindi wa Mezani!. Mheshimiwa Rais, Dr. John Pombe Magufuli, aka.JPM, Kasi Yako ya Maendeleo ya Tanzania Unaoifanya, Utailetea CCM Ushindi Kishindo Katika Uchaguzi Wowote, Tunakuomba Please Please Please, Ruhusu Tuu Ushindani wa Haki, Wazi na Usawa Kwa Vyama Vyote,
Utabarikiwa Zaidi na Zaidi, na Tanzania Tutabarikiwa.
Nawatakia Jumapili Njema
Na mimi nawahi kanisani
Misa ya Kwanza pale kanisa langu la St.Peters
Paskali
Wenye pupa ni wale waliokimbilia kusema wamejitoa bila kupima consequences za baadae.lisemwalo lipo kama halipo laja... hutakiwi kua na pupa.. subili kwanza.