Ushuhuda: Biashara ya mchele ni ngumu mno!

Ushuhuda: Biashara ya mchele ni ngumu mno!

Mkuu Kuna biashara ya karanga wengi hawajaijua ni mzr maduka ya jumla kwa Sasa ni 2900 mpaka 3000.maduka ya reja reja ni 3500.Nenda Dodoma karanga za kubangua na mkono ni 2200/za mashine ni 2000 mpaka 1900 Lete mjini then deal na maduka ya reja reja au nenda moja kwa moja kwa wamama wauza karanga fanya nao biashara .utarudi kunitafuta
Katanga Sokoni zipo za aina nyingi sana mkuu, sijajua ni karanga gani unazungumzia
 
mimi nipo mwananyamala kwenye biashara za nafaka ila sio mchele ni mahindi mtama kunde na vitu kama hivyo.... kuhusu mchele wewe umejichanganya kwenda mbeya kununua mchele uje umuuzie mtu ili na yeye auze dukani kwake... kwasabab mimi nipo hapa sokoni najua jinsi biashara hiyo inavyoenda... fanya hivii tafuta ubao sokoni mwananyamala halafu uuze mchele wako wewe mwenyewe ukimaliza unaenda tena mbeya pale unamuacha kijana... sio kama unavyofanya wewe ila mtaji wako mdogo huwezi biashara hii ya mchele ungetakiwa uwe angalau milioni 20 ... fanya hivi nenda dodoma kanunue mtama kwa laki 7 yako utapata gunia 10 za mtama niletee mimi nitanunua

Ni mtama upi unatoka???
 
Pole sana mkuu!!hiyo biashara ina hitaji uzoefu mkubwa sana!!mala ya kwanza napeleka DRC, nilikuwa na kama tani 30!!kidogo niukimbie mzigo, kwani fitina niliyokutana nayo kutoka kwa wabongo wenzangu, uchanganye na lugha ya lingala na French, zinazozungumzwa huko, ilikuwa balaa, huku faranga, kule dola!!!utambue dola halali/fake!!ila nilipambana hadi nikatoboa!!siku ya kwanza niliuza kama faranga milioni 2, kuzibeba kwenye begi la mgongoni hadi bega linauma, kuzihesabu mate yalikauka, nikatafuta bakuli la maji ili kuhesabu.

Mkuu mimi naye naitaji kujaribu kuipeleka uko congo ila kwa jf ni platform nzuri imenikutajisha na ww apo naomba msaada wako niweze kufika
 
Mtaji wa laki saba pekee hautoshi kabisa kufanya biashara ya mchele, ni ndogo sana.

Ushauri wangu tu, pambana kwanza upate meza hapo Sokoni, uza chochote cha rejareja chenye mtaji mdogo (hata kama ni nyanya), kisha anza kuuza mchele kwa reja reja (hata kama utakopeshwa kwa mali kauli na wauzaji wakubwa) huku ukiongeza 'thamani' (wauzaji wazuri wa mchele watakuwa wamenielewa).

Lengo la kufanya hayo ni nini?
1. Kukuza mtaji wako.
2. Kujenga mtandao mpana wa kibiashara (wauzaji wakufahamu na wateja wakufahamu)
3. Kujenga uzoefu wa kibiashara.
 
Kijana wenu baada ya kumaliza chuo nikaona nijimix kwenye harakati za maisha nipo Dar es Salaaam japo Nina mda mfupi sana hapa.

Nimezunguka masoko yote hapa dsm kuanzia mabibo mpaka mbagala nilikuja na idea nyingine kwa sababu mtaji sikua nao mkubwa nikashindwa kwa sababu ilihitajika sehemu ya kukodi meza kununua mizani so nikashindwa nikaona nijiingize kwenye issue zingine.

Nilifan
Bro hizi manual kazi ni ngumu , cheza na mtandao upate hela boss ..!! Hzi ni ngumu mno , unatakiwa upoteze hela nyingi Sana ili ukae kwenye mstari , au upate mtu wa kukushika mkono , Dar es salaam vijana wengi wanapoteza mda Sana ,ni mji unaohtaji akili nyingi Sana kama huna proffessional ya maana lazima mji ukufurahshe
 
Biashara za bongo zinakuwa ngumu kwa sababu ya watu wakati(Madalali),hawa jamaa wamekuwa kikwazo kila sekta nashauri kuwe na govern body kwa hawa watu maisha yetu yataweza kuwa rahisi zaidi.
Dalali by universal Code anatakiwa kupata si zaid ya 20% ya mauzo kama kamisheni. Hawa wabongo ni resale agents maana wanauza na kutaka kufunga au kuclose deal na zaidi ya 80% profit hapo bado hajataka na cha juu.

Madalali ndio moja ya sababu kubwa sana ya hii inflation tunayopitia bongo.
 
Ukinunua mchele usiende kuuza sokoni, wale madalali nao wanataka wapige cha juu, shusha mzigo wako kisha ingia kitaa jwa wenye maduka ambao ndio wauzaji wa mwisho
Hawa mafala nao siku hizi wameanza tabia za kibinafsi wananunua kwa watu wanaowajua.
 
Imekuchukua muda gani tangu kuanza biashara hadi kukata tamaa!?

Unadhani kuna biashara ambayo ni rahisi kwamba utaanza leo kesho uone faida?

Kwenye kuanza biashara inatakiwa uvumilivu, kuna changamoto huwa hazikwepeki hasa kwa biashara mpya.

Kutokujua sehemu ya kuchukua mzigo, unapataje wateja na unafanyaje ili mteja atayenunua leo na kesho aje, huchangia ugumu wa biashara mwanzo.

NAKUSHAURI chagua biashara Moja na upambane nayo iwe jua iwe mvua.

Hata hao unawaona Wana mitaji mikubwa na wanapata faida walishapita hiyo stage ambayo wewe upo wakavumilia ndio unaona wapo hapo walipo.

MWISHO asije kukudanganya mtu kuwa kuna biashara rahisi, biashara ni rahisi ikiwa kwa mwenzio, kinachoonesha urahisi wa biashara ni uvumilivu, uzoefu na ubunifu mpya kila kukicha.

La SIVYO utakuwa mtu wa kuanza biashara mpya na kuacha
Wacha weeeeee.

Mekumith[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mimi nipo mwananyamala kwenye biashara za nafaka ila sio mchele ni mahindi mtama kunde na vitu kama hivyo.... kuhusu mchele wewe umejichanganya kwenda mbeya kununua mchele uje umuuzie mtu ili na yeye auze dukani kwake... kwasabab mimi nipo hapa sokoni najua jinsi biashara hiyo inavyoenda...

Fanya hivii tafuta ubao sokoni mwananyamala halafu uuze mchele wako wewe mwenyewe ukimaliza unaenda tena mbeya pale unamuacha kijana... sio kama unavyofanya wewe ila mtaji wako mdogo huwezi biashara hii ya mchele ungetakiwa uwe angalau milioni 20 ... fanya hivi nenda dodoma kanunue mtama kwa laki 7 yako utapata gunia 10 za mtama niletee mimi nitanunua
Haya ushapewa mchongo huo hapo changamkia fursa.
 
Mkuu kama hutojali naomba mawasiliano yako au nikucheck DM mzigo wangu huu wa Mchele ukiisha nikafate mtama. Leo nimeshinda hapo Mwananyamala kuanzia asubuhi mpaka jioni gunia zangu 5 zilishushwa hapo wakawa wananiambia kwa mtaji wangu hii biashara itanishinda na nitaona ugumu wake, wakanishauri nijaribu kwenye mtama au kunde, choroko pia alinambia Maharage japo mtaji wake ni Mkubwa.

Niliulizia meza hapo Sokoni gharama yake ni kubwa Mara mbili ya mtaji wangu Kesho Mimi nitakua hapo nione sample mzuri inayohitajika Sokoni ili weekend hii nikatafute mtama kiongozi.
Halafu mchele mzuri kabisa huku Turiani, Morogoro (kwenye mashine) ni elfu moja mkuu so next time usihangaike mpaka Mbeya ambako ni mbali
 
Nakupa maneno ya akiba ukiona mfanyabiashara anakwambia Bora biashara ya mtama wakati yeye anauza mchele huyo mwanga usoni na moyoni mchawi. Yaani jiulize wewe kwake kama nani hata akupe mchongo huo na yeye asifanye?



Lunatic [emoji2957][emoji2957][emoji2957]
Nadhani wamemshauri vizuri kulingana na mtaji wake wa laki saba kwamba anaweza kupata gunia 10 za mtama na pia ikatosha kwa usafiri mpaka sokoni. Mchele hizo hizo gunia 10 lazima awe na zaidi ya milioni moja.
 
Nilichojifunza pia biashara yoyote ile ni mtaji ukiwa na elimu husika ya biashara mtaji NI muhimu saana ni ngumu sana kuanza na laki 7 then uje ufikishe million 100 ni ngumu sana wakuu
Hilo nalo ndio tatizo lako la pili pia. Usijenge fikra za mtaji mkubwa wakati ndiyo unaanza. Mtaji wako wa kwanza ni wazo, umefanikiwa, wa pili ni uthubutu umefanikiwa wa tatu ni rasilimali watu umeamua kujikatisha tamaa. Hapo ndipo unapotakiwa kutengeneza network na ujasiri, hapo ndipo ubunifu wa kutafuta wateja wa kudumu, usitegemee kupata faida mara hiyo hiyo ya kwanza wakati bado hujajuana na wateja. Kuna muda inabidi uendelee ili mtaji ukue na ukishazoeana na wateja utakuwa unachukua mzigo kwa mali kauli tu baada ya kujengeka kwa imani, pili tumia resources ulizonazo kutengeneza soko, mfano unaingia kwenye magroup ya whatsapp ya mapambo, wapishi yaani yale yanayohusika na maharusi unajitangaza biashara ya mchele, ingia magroup ya kilimo na mifugo, whatsapp, fb, hata account yako instagram unajitangaza, ukishaanza kukomaa kibiashara unamtafuta graphic designer anakutengenezea posters.

Hata hili lalamiko lako uliloandika jf unaweza kwenda kwenye matangazo ya biashara ndogondogo jf ukilifanya kuwa fursa ya unauza biashara ya mchele na kufanya delivery kwa gharama za mteja.








Kijana wenu baada ya kumaliza chuo nikaona nijimix kwenye harakati za maisha nipo Dar es Salaaam japo Nina mda mfupi sana hapa.
Hilo nalo ndio tatizo lako la pili pia. Usijenge fikra za mtaji mkubwa wakati ndiyo unaanza. Mtaji wako wa kwanza ni wazo, umefanikiwa, wa pili ni uthubutu umefanikiwa wa tatu ni rasilimali watu umeamua kujikatisha tamaa. Hapo ndipo unapotakiwa kutengeneza network na ujasiri, hapo ndipo ubunifu wa kutafuta wateja wa kudumu, usitegemee kupata faida mara hiyo hiyo ya kwanza wakati bado hujajuana na wateja. Kuna muda inabidi uendelee ili mtaji ukue na ukishazoeana na wateja utakuwa unachukua mzigo kwa mali kauli tu baada ya kujengeka kwa imani, pili tumia resources ulizonazo kutengeneza soko, mfano unaingia kwenye magroup ya whatsapp ya mapambo, wapishi yaani yale yanayohusika na maharusi unajitangaza biashara ya mchele, ingia magroup ya kilimo na mifugo, whatsapp, fb, hata account yako instagram unajitangaza, ukishaanza kukomaa kibiashara unamtafuta graphic designer anakutengenezea posters.

Hata hili lalamiko lako uliloandika jf unaweza kwenda kwenye matangazo ya biashara ndogondogo jf ukilifanya kuwa fursa ya unauza biashara ya mchele na kufanya delivery kwa gharama za mteja.
Nimezunguka masoko yote hapa dsm kuanzia mabibo mpaka mbagala nilikuja na idea nyingine kwa sababu mtaji sikua nao mkubwa nikashindwa kwa sababu ilihitajika sehemu ya kukodi meza kununua mizani so nikashindwa nikaona nijiingize kwenye issue zingine.

Nilifanikiwa kupita tandale Sokoni kuna soko kubwa linajengwa. kwa nje kuna wafanyabiashara weengi sana nikaanza kufanya research kuhusu biashara ya Mchele kwamba nautoa Mbeya then nawapa madalali wananiuzia, kwa vile niliona sihitaji kutafuta en

Awali ya yote nilienda pale mwananyamala Sokoni nikakutana na wafanyabiashara wakubwa wa Mchele pale wakaanza kuniambia mwenyewe pale kila kilo waliochukulia mbeya wanapata faida tsh 30_50 yaani anauchukua mbeya kwa 1100 kila kilo kufika Sokoni anauza 1250/1300 akiondoa gharama zake zoote faida hiyo (sema hao wana mitaji mikubwa saana).

Turudi tandale sokoni.

Mimi kwa sababu sikua na mtaji Mkubwa nilikua na around laki 7 nikajitosa kwenda kununua Mchele mzuri sio super saana ila ni mzuri.
Nilichukua mbeya kwa 1300 nikachukua kama kilo 500 total inakua ni 650,000 ukiondoa na gharama zoote na usafiri unajikuta umetumia laki saba na ishirini (720k).

Kufika Sokoni nilitaka niuze kwa 1750@ kilo ili nirudishe gharama zangu lakini naona watu wengi wanahitaji kwa 1600-1650 na mwingine anakwambia umuuzie kwa 1300/1400.

Changamoto nyingine unaweza shusha mzigo Mkubwa kama gunia 30 ukawa unauza 1300 kwa kilo, kesho yake anakuja mwingine anashusha Mchele kama wako anauza 1000/1100 kwa kilo inakua changamoto.

View attachment 1996258

Nilichogundua kwenye hii biashara wafanyabiashara wengi ambao wanauza wenyewe wengi wanachanganya mzigo anachukua Mchele super then anachanganya na Mchele mbaya kwa macho mteja hawezi kugundua kwa haraka.
 
Mosi hongera sana kwa kujaribu [emoji109][emoji122][emoji122][emoji122]

Pili, hakuna jambo lolote especially biashara isiyokuwa na changamoto. Hivyo chukulia changamoto kuwa ni sehem ya biashara.

Tatu, umeingia kwenye nafasi isiyoendana na mtaji wako.

Ushauri
Kwa mtaji ulionao, rudi katika step za mwanzo za biashara hio (kulima) ikiwa moyo wako bado unawaza mchele, japo wengi wanakushauri ukaze lkn ukweli mchungu, UTAPOTEZA hata huo mtaji ulionao ikiwa utaendelea kukomaa hapo.


Yaani wasikutie kabisa moyo ukaendelea kubaki hapo,
 
Mkuu usikate tamaa...umenikumbusha 2013 nilipofanya biashara ya kununua mahindi maporini na kwenda kuuza sokoni ...nliambulia tsh 1000 faida baada ya kutoa gharama zote..kwa hasira nkaenda kununua sayona ya jero nipoze machungu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
[emoji28][emoji28][emoji28]

We jamaa upo?
Nipo [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ntaondokaje na mimi ndio nimechora ramani ya Dar.
IMG_20210819_144657.jpg
 
Back
Top Bottom