Ushuhuda: Biashara ya mchele ni ngumu mno!

Ushuhuda: Biashara ya mchele ni ngumu mno!

Mkuu mimi naye naitaji kujaribu kuipeleka uko congo ila kwa jf ni platform nzuri imenikutajisha na ww apo naomba msaada wako niweze kufika
sawa!kule biashara sio mbaya ila changamoto ni nyingi sana, hasa kwa mgeni, kuanzia usafiri toka kigoma, njoo pm
 
Halafu mchele mzuri kabisa huku Turiani, Morogoro (kwenye mashine) ni elfu moja mkuu so next time usihangaike mpaka Mbeya ambako ni mbali
Mkuu naweza pata hiyo connection? Kutoka Dar mpaka huko ni shingapi? Na je usafiri wa kuleta Dar unapatikana kwa urahisi?
 
Mtaji wa laki saba pekee hautoshi kabisa kufanya biashara ya mchele, ni ndogo sana.

Ushauri wangu tu, pambana kwanza upate meza hapo Sokoni, uza chochote cha rejareja chenye mtaji mdogo (hata kama ni nyanya), kisha anza kuuza mchele kwa reja reja (hata kama utakopeshwa kwa mali kauli na wauzaji wakubwa) huku ukiongeza 'thamani' (wauzaji wazuri wa mchele watakuwa wamenielewa).

Lengo la kufanya hayo ni nini?
1. Kukuza mtaji wako.
2. Kujenga mtandao mpana wa kibiashara (wauzaji wakufahamu na wateja wakufahamu)
3. Kujenga uzoefu wa kibiashara.
Nimechukua ushauri wako japo kuna changamoto nyingi mpaka kupata meza, mtaji n.k nimeulizia na wenye meza wanataka kuanzia miezi 4+
 
Bro hizi manual kazi ni ngumu , cheza na mtandao upate hela boss ..!! Hzi ni ngumu mno , unatakiwa upoteze hela nyingi Sana ili ukae kwenye mstari , au upate mtu wa kukushika mkono , Dar es salaam vijana wengi wanapoteza mda Sana ,ni mji unaohtaji akili nyingi Sana kama huna proffessional ya maana lazima mji ukufurahshe
Mkuu ningejua hizo harakati za mtandao nisingekua napambana huku I wish na Mimi nijue hizo issue za mtandao
 
Wakuu wapi nitapata mkopo wa laki 5 au 3 nitaweka vyeti bond
 
Nenda kwa mamantilie jaribu kuongea nao pengine wanaweza kununua kutoka kwako. Au jaribu kusikilizia wapi kuna shuhuli ya ubwabwa unaweza kuwapelekea wakaununua.



Lunatic [emoji2957][emoji2957][emoji2957]

Yes hasa kariakoo wale wanapika kg nyingi per day na wapo wengi sana

Akitengeneza connection kule atafanya biashara
 
Mkuu Kuna biashara ya karanga wengi hawajaijua ni mzr maduka ya jumla kwa Sasa ni 2900 mpaka 3000.maduka ya reja reja ni 3500.Nenda Dodoma karanga za kubangua na mkono ni 2200/za mashine ni 2000 mpaka 1900 Lete mjini then deal na maduka ya reja reja au nenda moja kwa moja kwa wamama wauza karanga fanya nao biashara .utarudi kunitafuta
Sidhani kama bado kuna karanga za kutosha maana huu msimu hazikukubali
 
Mkuu usikate tamaa...umenikumbusha 2013 nilipofanya biashara ya kununua mahindi maporini na kwenda kuuza sokoni ...nliambulia tsh 1000 faida baada ya kutoa gharama zote..kwa hasira nkaenda kununua sayona ya jero nipoze machungu
Dah we jamaa wewe [emoji23]
 
Aisee..

Miaka ya mwisho ya tisini, nilijiingiza kwenye biashara ya mchele, unakusanya maeneo ya Kagongwa, wilaya ya Kahama, halafu unapeleka kuuza Rwanda, miaka hiyo Faranga 1 ni sawa na shillingi 2 za TZ,

Nlianza na tu Tani tuwili tu, sababu Rwanda wananunua vigunia vya sandarusi vya kilo 50, kwao ndio standard ya manunuzi
Hapo na tugunia 40, usafiri ni unamlipa dereva wa semi trela anavipanga nje juu ya kontena.

Nimefika Kigali maeneo ya Majerwa ambapo ndio magari yote yanasimama, naisubiria Semi ifike, nimekaa gesti siku mbili, na ugeni ule natumia tuu, burusheti na Primus kwa sana, kumbe nakula hela ya ziada na sijui lini nitauza mchele, baada ya mchele kufika, nikachukua sample kama kilo 5 nazungusha kwenye maduka, duuh noma kweli naonekana mgeni kabisa mpaka wajeshi wakanibabatiza mjini miaka hiyo, maana kumbe wananiangalia naingia duka hili natoka mara duka hili nikakalishwa chini, nikahojiwa na nikatoa passpoti na kujieleza huku na kibegi changu cha sample ndio wakaniamini na kuniachia.

Nikampata Mzee wa kinyarwanda anataka vigunia 25, nikamletea lakini bei hata sio hivyo nzuri, hapo nimeshachoka nikakubali, sasa mbinde kuifata hela kila siku, zaidi ya wiki nafuatilia hela, gharama ndio zinazidi, na nikamalizia vigunia vingine kwa Mama mwingine wa Kiganda, kwa hasara tu, nikasema sirudii tena ndio ikawa mwisho kufanya biashara hizi hazieleweki.......

Sijui kwa sasa biashara ikoje kupeleka mchele Rwanda...
 
Kijana wenu baada ya kumaliza chuo nikaona nijimix kwenye harakati za maisha nipo Dar es Salaaam japo Nina mda mfupi sana hapa.

Nimezunguka masoko yote hapa dsm kuanzia mabibo mpaka mbagala nilikuja na idea nyingine kwa sababu mtaji sikua nao mkubwa nikashindwa kwa sababu ilihitajika sehemu ya kukodi meza kununua mizani so nikashindwa nikaona nijiingize kwenye issue zingine.
Katika Maisha, suala la kukata tamaa ni dhambi kubwa Sana! Hata hivyo imelinganishwa na Mtu alisafiri hadi katikati ya msitu halafu akajichimbia shimo la kutosha na kujizika mzima mzima, haiko hivyo. Hakuna biashara/kazi nyepesi Duniani lazima upambane hadi tone la mwisho la damu. Utawaza kwenda kijijini kulima ukidhani kuwa kilimo ni jambo jepesi, LA hasha!! Unaweza ukalima vizuri tu halafu usipate chochote Je, utaenda wapi baada ya hapo? Nakushauri, Kwa kuwa ulishaanza hiyo biashara usiiache, hizo ni changamoto za AWALI tu, huko mbeleni utapata akili tu.
 
😂Si mchezo...hii biashara sijawahi kuifanya exactly ila nimetoka kuifuatilia juzi juzi tu, huko huko Mbeya.ndani ndani huko kunaitwa Kamsamba, ni biashara yenye mbinde kdg na ukifanya masihara unachezea za uso...namshukuru mkuu Insigne kwa kunipa connection na kwenda kunitoa tongo tongo pande hizo...nimejifunza vitu vingi nikiwa na ndugu yangu...

Tunajipanga tena mambo yakiwa mazuri tunategemea kurudi msimu wa mavuno ya mpunga ukianza...bro huo mtaji wako kwa hii biashara hutoboi, mimi nilipiga hesabu nikiwa na mtaji wa milioni 10 nikajikuta napata faida ya laki mbili (200,000/) hapo hujatoa gharama za usafiri na chakula, na malazi...Noma Sanaa ila inawezekana
 
Mkuu kama hutojali naomba mawasiliano yako au nikucheck DM mzigo wangu huu wa Mchele ukiisha nikafate mtama. Leo nimeshinda hapo Mwananyamala kuanzia asubuhi mpaka jioni gunia zangu 5 zilishushwa hapo wakawa wananiambia kwa mtaji wangu hii biashara itanishinda na nitaona ugumu wake, wakanishauri nijaribu kwenye mtama au kunde, choroko pia alinambia Maharage japo mtaji wake ni Mkubwa.

Niliulizia meza hapo Sokoni gharama yake ni kubwa Mara mbili ya mtaji wangu Kesho Mimi nitakua hapo nione sample mzuri inayohitajika Sokoni ili weekend hii nikatafute mtama kiongozi.

Keep going usikate tamaa hakuna kitu kirahisi[emoji1376][emoji1376][emoji1376]tunakomaa mpaka kinaeleweka
Yani kuna mda huoni kitu mbele giza tu keep going
Kitu umekosa ni mentor kwenye biashara yako otherwise hio biashara sio ngumu ni biashara kama nyingine
 
Back
Top Bottom