white wizard
JF-Expert Member
- May 18, 2011
- 8,566
- 13,770
sawa!kule biashara sio mbaya ila changamoto ni nyingi sana, hasa kwa mgeni, kuanzia usafiri toka kigoma, njoo pmMkuu mimi naye naitaji kujaribu kuipeleka uko congo ila kwa jf ni platform nzuri imenikutajisha na ww apo naomba msaada wako niweze kufika
Mkuu naweza pata hiyo connection? Kutoka Dar mpaka huko ni shingapi? Na je usafiri wa kuleta Dar unapatikana kwa urahisi?Halafu mchele mzuri kabisa huku Turiani, Morogoro (kwenye mashine) ni elfu moja mkuu so next time usihangaike mpaka Mbeya ambako ni mbali
Nimechukua ushauri wako japo kuna changamoto nyingi mpaka kupata meza, mtaji n.k nimeulizia na wenye meza wanataka kuanzia miezi 4+Mtaji wa laki saba pekee hautoshi kabisa kufanya biashara ya mchele, ni ndogo sana.
Ushauri wangu tu, pambana kwanza upate meza hapo Sokoni, uza chochote cha rejareja chenye mtaji mdogo (hata kama ni nyanya), kisha anza kuuza mchele kwa reja reja (hata kama utakopeshwa kwa mali kauli na wauzaji wakubwa) huku ukiongeza 'thamani' (wauzaji wazuri wa mchele watakuwa wamenielewa).
Lengo la kufanya hayo ni nini?
1. Kukuza mtaji wako.
2. Kujenga mtandao mpana wa kibiashara (wauzaji wakufahamu na wateja wakufahamu)
3. Kujenga uzoefu wa kibiashara.
Mkuu ningejua hizo harakati za mtandao nisingekua napambana huku I wish na Mimi nijue hizo issue za mtandaoBro hizi manual kazi ni ngumu , cheza na mtandao upate hela boss ..!! Hzi ni ngumu mno , unatakiwa upoteze hela nyingi Sana ili ukae kwenye mstari , au upate mtu wa kukushika mkono , Dar es salaam vijana wengi wanapoteza mda Sana ,ni mji unaohtaji akili nyingi Sana kama huna proffessional ya maana lazima mji ukufurahshe
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Nipo [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ntaondokaje na mimi ndio nimechora ramani ya Dar. View attachment 2000905
Mkuu kwa mzigo ulionao...kilo moja unaiuza kwa kiasi gani?Mkuu ningejua hizo harakati za mtandao nisingekua napambana huku I wish na Mimi nijue hizo issue za mtandao
Nenda kwa mamantilie jaribu kuongea nao pengine wanaweza kununua kutoka kwako. Au jaribu kusikilizia wapi kuna shuhuli ya ubwabwa unaweza kuwapelekea wakaununua.
Lunatic [emoji2957][emoji2957][emoji2957]
Hujui kazi ya mfanyabiashara ni kupata faida.Unataka upate faida wakati ndiyo umeanza??
Biashara haziko hivyo
Naomba chimbo unakotoa mchele. Kuna mdau ananisumbua nimtumie mcheleNdio hivyo kikubwa ni mtaji sasa kwa sisi wenye laki 7 ni ngumu kwetu
Sidhani kama bado kuna karanga za kutosha maana huu msimu hazikukubaliMkuu Kuna biashara ya karanga wengi hawajaijua ni mzr maduka ya jumla kwa Sasa ni 2900 mpaka 3000.maduka ya reja reja ni 3500.Nenda Dodoma karanga za kubangua na mkono ni 2200/za mashine ni 2000 mpaka 1900 Lete mjini then deal na maduka ya reja reja au nenda moja kwa moja kwa wamama wauza karanga fanya nao biashara .utarudi kunitafuta
Faida ataipata tu akiendelea kukaza na kujifunza changamoto za biashara hiyo.Hujui kazi ya mfanyabiashara ni kupata faida.
Dah we jamaa wewe [emoji23]Mkuu usikate tamaa...umenikumbusha 2013 nilipofanya biashara ya kununua mahindi maporini na kwenda kuuza sokoni ...nliambulia tsh 1000 faida baada ya kutoa gharama zote..kwa hasira nkaenda kununua sayona ya jero nipoze machungu
Katika Maisha, suala la kukata tamaa ni dhambi kubwa Sana! Hata hivyo imelinganishwa na Mtu alisafiri hadi katikati ya msitu halafu akajichimbia shimo la kutosha na kujizika mzima mzima, haiko hivyo. Hakuna biashara/kazi nyepesi Duniani lazima upambane hadi tone la mwisho la damu. Utawaza kwenda kijijini kulima ukidhani kuwa kilimo ni jambo jepesi, LA hasha!! Unaweza ukalima vizuri tu halafu usipate chochote Je, utaenda wapi baada ya hapo? Nakushauri, Kwa kuwa ulishaanza hiyo biashara usiiache, hizo ni changamoto za AWALI tu, huko mbeleni utapata akili tu.Kijana wenu baada ya kumaliza chuo nikaona nijimix kwenye harakati za maisha nipo Dar es Salaaam japo Nina mda mfupi sana hapa.
Nimezunguka masoko yote hapa dsm kuanzia mabibo mpaka mbagala nilikuja na idea nyingine kwa sababu mtaji sikua nao mkubwa nikashindwa kwa sababu ilihitajika sehemu ya kukodi meza kununua mizani so nikashindwa nikaona nijiingize kwenye issue zingine.
Mkuu kama hutojali naomba mawasiliano yako au nikucheck DM mzigo wangu huu wa Mchele ukiisha nikafate mtama. Leo nimeshinda hapo Mwananyamala kuanzia asubuhi mpaka jioni gunia zangu 5 zilishushwa hapo wakawa wananiambia kwa mtaji wangu hii biashara itanishinda na nitaona ugumu wake, wakanishauri nijaribu kwenye mtama au kunde, choroko pia alinambia Maharage japo mtaji wake ni Mkubwa.
Niliulizia meza hapo Sokoni gharama yake ni kubwa Mara mbili ya mtaji wangu Kesho Mimi nitakua hapo nione sample mzuri inayohitajika Sokoni ili weekend hii nikatafute mtama kiongozi.
Sahizi umeamka unaenda kuwanga eeh,
Tupo katika zile nchi Maskini sana, wafanyabiashara ni wengi kuliko wanunuzi