Ushuhuda kutoka kwa wanandoa waliowahi kuachana, hasa mliokuwa na watoto mkaamua kuacha kila kitu na kuanza upya

Kuna jamaa yangu anatumia gari ya mke wake kama guest inaniuma sana
Kwakweli kuelezea kila kilichotekea nitareaveal identity za watu...ila kikubwa ni usaliti uliovuka mipaka..na yaliyotokana na usaliti ndio mazito zaidi...naombeni msaaada juu ua uzoefu wenu...mimi na mume wangu hatuwezi kurudi kama mwanzo...
 
Kwa umri nilionao.... Nimekuja kugundua.... Ukijaribu kummiliki Mwamamume.... Utaumia sana kihisia, kimwili, kisaikolojia, kimatendo, kifikra.... Utaumia Kila Kona. Utakuwa mtu wa mawazo na kununa muda wote. Nimeacha kabisa hii TABIA.
Uko sahihi kabisa
 
Mimi nimerelax mda wote shida Ni nyie watu msiopenda different opinions za wengine.
Thanks for ur wishes.
Unaonekana Kama uko dunia yako tofauti! Shtuka something is wrong
 
Hauhitaji msaada wa kweli wewe,hapo ni sawasawa unaenda kuonana na daktari anakuuliza historia ya tatizo unamficha,unadhani hapo unasaidiwaje
 
Mkuu suala la talaka ni la kisheria, huwezi kukwepa mchakato wake na kwa kweli ni jambo linalochukua muda na linaumiza hisia na hata uchumi, mleta mada anahitaji kupata ushauri wa kumuandaa kisaikolojia kama kweli amedhamiria kudai talaka
Mimi nilikuwa muhanga wa talaka nilipotengana na mzazi mwenzangu. Alikuwa na rafiki yake ambae ni hakimu wa kiteto. Akamuuliza namna tunaweza talikiana akasema mimi ninatakiwa kwenda mahakamani kifungua kesi ya madai ya talaka. Nilipoenda nikapewa maelekezo ya kufuata kufungua file na kulipia. Alafu nikapewa barua ya wito ya mwanaume nimpelekee alafu tukapewa tarehe ya kuja.

Siku ya kusikilizwa tulisikilizwa wote na hukumu ikatoka siku hiyo hiyo na mwenzangu alilipia hati ya talaka akapewa nakala yake.

Kinachofanya suala la talaka kuchukua muda mrefu ni mali. Hili la tulichuma wote tugawane ndio linafanya mchakato unakuwa mgumu na mrefu
 
Hakuna unachokikwepa, tukikupa ushauri wa kuondoka na kuanza upya,mwosho wa siku ukiondoka si watataka kujua kwa Nini mmetengana?. Si ni bora ukawaeleza Sasa?.
 
Pole na hongera kwa maisha mapya...je mlikua mmejenga au kua na assets pamoja?
 
Ushauri kwenye mambo ndoa ni mgumu sana,hasa katika kipengere cha usalti.
Sanasana nakushauri tu jipe moyo kwanza ikiwezekana ukae mbali na mume wako akili yako itakupa solution either uendelee naye au aendelee na maisha yake.
Bila hata ya kukaa kutafakari..hawezi kubadilika kamwe...i know him more than ten yrs
 
Ya Kwanza ndo Yenyewe hakuna zaidi ya hiyo inayoweza kumuumiza mwanamke maisha yake yote,ndo maana akasema “matokeo” ndio yanayomuumiza
kama ni hilo la kwanza linasameheka.
Anatakiwa afikirie ugumu wa maisha atakayopitia yeye pamoja na watoto wake.
Kisha alinganishe akimsamehe na kuendelea na mume wake anapata hasara gani kama mume anaitunza familia,anajua wajibu wake.
Wenzake huwa wanasusa na kuomba talaka endapo huyo mume hatunzi familia yaani endapo pesa zote na mahitaji yote anapelekewa mchepuko
 
Kwakweli kuelezea kila kilichotekea nitareaveal identity za watu...ila kikubwa ni usaliti uliovuka mipaka..na yaliyotokana na usaliti ndio mazito zaidi...naombeni msaaada juu ua uzoefu wenu...mimi na mume wangu hatuwezi kurudi kama mwanzo...
Kubalianeni tu kutunza watoto na kwa kweli moyo wa mwanamke hauna reverse milele. We Anza zako upya na watoto wako kuwa busy na Kaz zako na nakuapia utapata mtu atakupendaaa na wanao wotee, usiogope chochote
 
Kubalianeni tu kutunza watoto na kwa kweli moyo wa mwanamke hauna reverse milele. We Anza zako upya na watoto wako kuwa busy na Kaz zako na nakuapia utapata mtu atakupendaaa na wanao wotee, usiogope chochote
Nashukuru sana. Mume wangu alikua kila kitu changu...sahivi ninavyomuona...kamwe na katu siwezi kurudisha lile pendo...nimejeruhika na kuathirika kimwili, kiroho na kiakili..
 
Exactly, hata akipona ukimwi bado magonjwa ya moyo na mambo mengine mengii, imagine huyo mume hayupo dunian tu Anza zako freshhh
 
Kubalianeni tu kutunza watoto na kwa kweli moyo wa mwanamke hauna reverse milele. We Anza zako upya na watoto wako kuwa busy na Kaz zako na nakuapia utapata mtu atakupendaaa na wanao wotee, usiogope chochote
Kwakweli naogopa haswa kuanza upya..idadi ya watoto nilionao na sina ajira...nakata tamaa kabisa
 
Hivi wewe umeolewa kweli?mbona huwa unarahisisha tu mambo in a negative way
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…