Umeambiwa mashine ilikuwa mpyaSidhani kwamba katika kazi zao kama hizi wanatumia uchawi, mara nyingi wanatumia elimu na vifaa bora ili kufanikisha malengo yao, naamini uchawi au ushirikina wanao ila sidhani kama wanatumia ktk mambo kama ya sayansi, Mm naishi nao huku
Cha kushangaza akija mzungu, mchina au muarabu kuchimba kunakua hakuna vikwazo kama hivyo na wanafanikiwa kuchimba na kupata wanachokihitaji
Pia ninashangaa Serikali haiamini uchawi ila anapokamatwa mchawi kaanguka uchi wanatia pingu na kumpeleka kituo cha polisi je kule anaenda kama mtuhumiwa wa nini au anaenda kuhukumiwa kwa kutokuvaa nguo yaani anatembea uchi
Naamini ni wachawi sana ndio pia wanaomiliki freemanson, but sisi uchawi wetu mara nyingi tunatumia kudhuruTunayo sheria ya uchawi, witchcraft Act ya siku nyingi sana hii sheria tangu mkoloni miaka ya 1930s kama sijakosea. Uchawi Tz ni kosa kisheria Mkuu na kesi zipo.
Ndugu wazungu ni washirikina walioshindikanika hasa hawa wanaokuja kutalii huwa wana mambo mengi sana huwezi ukaamini kabisa.
Mchawi analoga machine au mashine ''inaharibiwa'' na mizimu? Karne hii bado unaamini? Pole sana.Mambo vipi wakuu,
Kwanza nitajikita kwenye mada kutokana na personal experience ya hapa home Tz. Binafsi nimekulia mazingira ya dini sana , kwa hiyo mambo ya uchawi au ku-practice masuala ya kiganga /jadi sikuwahi.
Lakini kwa uzoefu na namna nilivyoona katika kutembea mikoa ya hapa Tanzania, hasa huko vijijini watu wamelazimika kutofanya Maendeleo, kuyahama makazi yao kwa kuogopa kulogwa. Unakuta eti Kijijini mtu alikuwa hawezi kujenga nyumba nzuri na kuezeka bati, ukifanya hiyo kitu unaanza kuandamwa na mambo mengine kama hayo.
Personal Experience.
Nilipoamua ku-resign kazi na kuanza mishe zangu binafsi, niliingia kwenye kazi za mining na huku ndio nilikutana na hayo mambo.
Tulienda kuanzisha mining site Handeni- Tanga. Aisee, nilikuwa nausikia tu ushirikina sasa kule ndio nilienda kuona. Yaani mtu analoga machine (Excavator) inakuwa haifanyi chochote, tunaita mafundi wa kila aina wanachokonoa wee ila waapi, na machine bado mpya.
Baadae one of the labors niliokuwa nao pale site akaniita na wenzake pembeni, wakaniambia ndugu yetu, hapa kutakuwa na kitu kimefanyika, wakanitaka twende na mganga ili tuka unlock. Mimi nikawa siamini kama mashine inaweza logwa na sikuwa na imani na zile mambo kbs.
Basi nikawauliza kama wanaweza kwenda wenyewe wafanye kwa niaba wakasema poa niwape elfu 20 wanunue kuku, basi mshikaji akanambia tuwape. Mini nikawapa wakaondoka bwana, hapo tumehangaika na fundi wiring na hydrologic system wote wanasema hawaona tatizo, ila machine haina kabisa nguvu ya kuchimba.
Wale wadau walirudi time za jioni around 5pm, na maji yenye dawa kwenye chupa pamoja na vimiti viwili. Wakasema Operator wa machine aweke mfukoni kimti kimoja na kingine aweke chini ya seat yake, na yale maji ya dawa imwagiwe machine na kuzunguka eneo la mgodi. Operator akasema fresh ,yeye alikuwa anaamini sana, wale jamaa wakamwaga maji kwny machine nakuzunguka pale site, na mwingine akaenda akaleta ka kuku kadogo akachimba shimbo pembezon mwa site akakafukia kale kakuku kakiwa kazima.
Baada ya hapo wakamwambia Operator awashe machine . Mi naangalia tuu km movie, aisee huezi amin machine ikawa na power kuzidi hata uwezo wake siku zote. Nikashangaa sana , jamaa wale wenyeji wanacheka wananiambia "karibu Tanga mgosi".
Hii ni kwa ufupi tuu, nina mengi sana nime experience sehemu mbali mbali hasa katika kazi ya mining, maana mnaenda kuanzisha kazi sehem porini kumbe palikua ni mahali pa matambiko, basi vituko ni vingi nikijaaliwa muda nitakua naandika matukio mengine . Watu wana uwezo wakupoteza madini aridhini, yaani unachimba wee nakuunguza hela ila huoni kitu, wakati mwanzo mambo yalikua fresh kbs. Lakini mwisho wa siku nina Imani na Mungu , hatutakiwi kuweka Imani kwa waganga kwasababu nao ni binadam, uchawi upo na Mungu yupo.
Serikali haiamini katika uchawi, ni sawa kbs lakini ukweli ni kwamba uchawi umelostisha sana watu, pengine watu wangekuwa na maendeleo sehemu mbali mbali isingekuwa haya mambo. Siku hizi kidogo yanapungua ,nadhani muingiliano wa wageni na wenyeji sehemu mbalimbali unafanya watu ku-focus kwenye maendeleo. I'm not sure kama tumeshawah kuwa na sheria inayokemea haya mambo kwa kuwa ni invisible world.
Naomba niishie hapo kwa leo, najua wengi wetu tuna experience tofauti tofauti, kuwa huru ku share nasi tujifunze kitu.
Usijidanganye kuwa wanakuja kifaraCha kushangaza akija mzungu, mchina au muarabu kuchimba kunakua hakuna vikwazo kama hivyo na wanafanikiwa kuchimba na kupata wanachokihitaji
Pia ninashangaa Serikali haiamini uchawi ila anapokamatwa mchawi kaanguka uchi wanatia pingu na kumpeleka kituo cha polisi je kule anaenda kama mtuhumiwa wa nini au anaenda kuhukumiwa kwa kutokuvaa nguo yaani anatembea uchi
FYI, Waarabu wapo Oman wanaangalia, wanatazamia karai la maji wanaona MADINI YA KILA AINA huku Tanzania....Kwani waarabu ,Wachina na wazungu hawana hizo mbanga MIGODINI?!!
Ungeishi nao ungekuwa na la kuhadithia hapa....π€£π€£
Mkuu, hapo kwenye VIFAA bora; hivi Excavator ya mshkaji yenyewe haiingii kwenye vifaa bora?Sidhani kwamba katika kazi zao kama hizi wanatumia uchawi, mara nyingi wanatumia elimu na vifaa bora ili kufanikisha malengo yao, naamini uchawi au ushirikina wanao ila sidhani kama wanatumia ktk mambo kama ya sayansi, Mm naishi nao huku
Kuna mshua mmoja alipata teuzi, kwa bahati mbaya alivyofika kwenye ofisi ya alietenguliwa hakujisumbua kutoka furniture alizozikuta.Kwa wale ambao ndio kwaza mnaingia makazini, nyie mjifanye waluga luga tu mbadili viti vilivyotumika na wastaafu, huwa vimebeba mambo mazito
Yaan mkuu, hao wazungu na wachina wanafanya sn ushirikina kwenye sites kuliko unavyofikiri. Kuna mchina nilimshuhudia anachinja Mbuzi mwenyewe na dam ya mbuzi anaimwaga eneo la kazi huku anaongea kikwao. We waulize washkaji walofanya kaz na Chinese kwenye kandarasi mbalimbali watakwambia.
ππππKwa wale ambao ndio kwaza mnaingia makazini, nyie mjifanye waluga luga tu mbadili viti vilivyotumika na wastaafu, huwa vimebeba mambo mazito
Kule anaenda kupewa nguo kisha anaachiwa Ili raia wasimdhuruCha kushangaza akija mzungu, mchina au muarabu kuchimba kunakua hakuna vikwazo kama hivyo na wanafanikiwa kuchimba na kupata wanachokihitaji.
Pia ninashangaa Serikali haiamini uchawi ila anapokamatwa mchawi kaanguka uchi wanatia pingu na kumpeleka kituo cha polisi je kule anaenda kama mtuhumiwa wa nini au anaenda kuhukumiwa kwa kutokuvaa nguo yaani anatembea uchi.
Ukijua tofauti ya polisi na kibaka utaelewa tofauti ya mganga na mchawiHivi kuna tofauti gani kati ya mganga na mchawi
Lunatic [emoji2957][emoji2957][emoji2957]
Mikoa ya tanga, Lindi, pwani hii imefungwa kichawi ni ngumu Sana kuwa na maendeleo hadi zindiko liondolewe upo uchawi wa kuuroga mkoa mzima usiwe na maendeleo.Afrika ya weusi yote ni kama imerogwa thus hakuna maendeleoHiyo ndy Tanga bwana ...
Mwaka juzi Ndugu yangu form six alipangiwa JKT mkoa wa Tanga .Siku moja wanakimbia mchakamchaka,kundi Lao kwenye uelekeo wanakokwenda wakawaona watu wawili wanakuja.Watu wale walionekana km wanaenda shambani hivi,Ile wanataka wakaribiane wapishane Yule mtu mmoja akadondosha Mia 5 .Kwa sababu hakujua km ameangusha ela akaendelea kutembea Tu km hakuna kilichotokea,kumbe lile kundi la mchakamchaka wale wote waliopo mbele waliiona Ile Mia 5.Walipopishana na wale watu wawili mbio zikaanza kukimbilia Ile ela, Kwa bahati akafanikiwa kuiokota ndugu yangu.
Mchakamchaka ukaendelea kurudi kambini.Njiani Hali ya dogo ikachenji ghafla,kichwa kilimuuma Hadi akaanguka chini.kwa sababu ilichukuliwa ni Hali ya kawaida Kwa watu ku-faint wakati wa mazoezi makali basi wakambeba wakajua ni Hali ya kawaida ambayo huwakuta wengi wakiwa mazoezini.Hali ikazidi kuwa mbaya zaidi.wakati ananisimulia akanambia wakati amelala chini akafikiria kwamba mbn hii Hali imemkuta ghafla sn na wala hakuwa amechoka na mazoezi makali km walivyomtafsiri watu?Ghafla mwili ukazidi kuisha nguvu. Akakumbuka dakika km kumi hivi nyuma alikimbizana na wenzie na kufanikiwa kuiokota Ile Mia 5,alichokifanya ni kuingiza mkono mfukoni na kuitoa Ile hela akaitupa.Dakika km mbili jasho Kali lilimtoka kisha akapata nguvu akainuka Hadi watu wote waliopo pale wakamshangaa maana Walikuwa wanafanya utaratibu wamkimbize hospitali
Alipowasimulia kwamba baada ya kuitupa Ile Mia 5 aliyoiokota ndy akajiskia vizuri,wataalamu wa mambo wakamwambia nyie wa kuja mujiangalie sn hapa Tanga.Ndugu yetu Una bahati sn maana wale jamaa wawili mliopishana Walikuwa ni wachawi na muda si mrefu ulikuwa ufe kisha uwe msukule