#COVID19 Ushuhuda wa Mchungaji Godwin Chilewa kuhusu COVID-19: Je, tunamficha nani, kwanini na kwa Faida gani?

#COVID19 Ushuhuda wa Mchungaji Godwin Chilewa kuhusu COVID-19: Je, tunamficha nani, kwanini na kwa Faida gani?

Unajenga immunity kwa gharama ya watu wasio na hatia? Je kujenga immunity ndo kunatufanya tuseme uongo kuhusu Corona? Kujenga immunity ndo kunatufanya tusitunze data sahihi ili kutuwezesha kufanya tadhimini kesho kujua Kama njia tuliyochukua was good or no ukilinganisha na njia walizo chagua wengine?
Tunaihujumu dunia kwa haya. Kama kweli nyungu inaponya basi tuweke bayana tafiti ya kisayansi jinsi ilivyo na tuisadie dunia kupona. Kwa nini hii ni pekee kwa Tanzania. Mbona tunajimwambafy hivi.

Huu mtindo wa Kinjekitile unaaminika vipi. Au tuseme Tanzania ni mteule wa Mungu kama ilivyosemwa kwa Israeli.
Ikiwa watu watateswa na ugonjwa huu kwa sababu ya misimamo yetu basi na tuwe tayari kuwajibika. Na kama kwa msimamo huu tunaleta uponyaji basi sifa zije kwetu.
 
Tunaihujumu dunia kwa haya. Kama kweli nyungu inaponya basi tuweke bayana tafiti ya kisayansi jinsi ilivyo na tuisadie dunia kupona. Kwa nini hii ni pekee kwa Tanzania. Mbona tunajimwambafy hivi.

Huu mtindo wa Kinjekitile unaaminika vipi. Au tuseme Tanzania ni mteule wa Mungu kama ilivyosemwa kwa Israeli.
Ikiwa watu watateswa na ugonjwa huu kwa sababu ya misimamo yetu basi na tuwe tayari kuwajibika. Na kama kwa msimamo huu tunaleta uponyaji basi sifa zije kwetu.
Utashangaa zaidi ukienda hospital hata zile za chato, huambiwi kupiga nyungo bali unawekewa oxygen.Tanzania tuna bahati mbaya kuwa na viongozi wa aina hii tuliyonayo.
 
Watanzania wenzangu lini mtajifunza kuangalia mambo kwa undani wake....huyo mchungaji huko alipo USA Uongozi wa jiji la New York kwa makusudi walificha kuripoti 50% ya vifo vya wagonjwa kutoka katika nyumba za kutunza wazee kwa kisingizio kuwa wangesema vifo vyote ingwashtua sana watu na pia ingewaghalimu kwenye kampeni za uchaguzi!
Tatizo la binadamu anapofanya upumbavu anadhani watu wote wanafanya upumbavu kama wake!
 
Huyu anataka kuwachanganya watanzania!
Anawachanganya au anawaambia ukweli ili mjinasue huko kwenye nyungu zenu na mpaze sauti za kutaka serikali iwajibike juu ya vipimo na matibabu sahihi?
Siyo kila kitu unakiingia kichwakichwa na kiitikadi! Mleta hoja ni mhanga na anashare uzoefu wake jinsi alivyopambana pamoja na ushauri wa madaktari ili wahusika waamke na kutimiza wajibu wao na sio kututangazia habari ya mitishamba isiyofanyiwa tafiti za kisayansi kuuzwa kwenye hospitali za umma!
 
Kabla hata sijaendelea mbele wewe ugonjwa umeupatia marekani na siyo Tanzania

Tarehe sita na tarehe 14 ukapata majibu covid hana incubation period fupi hivyo waweza mulaumu lambda vipimo although navyo vimetoka huko huko unakoishi na still vina error kama kawa
Hujaelewa. Soma tena.

Aliingia Tanzania lini?
 
Kuna watu walikuwa hawaamini kuwa tuna katiba mbovu hasa kwenye madaraka ya urais, ila kwa sasa kila mtu amejionea madhara ya madaraka makubwa ya cheo cha urais. Maamuzi yote ya serikali kupambana na hili gonjwa yanatolewa kwa hulka binafsi za rais, na sio maamuzi yoyote ya kitaalamu. Iwapo yangekuwa ni maamuzi ya kitaalamu na sio hisia za rais, msimamo usingekuwa huu. Eneo pekee alilopata rais kwenye ugonjwa huu ni kutokuweka watu lockdown, mengine yote ni approach za kishirikina.
 
Nimeisoma makala yake yote na kushika nukta kadhaa kuhusiana nayo.
Kwanza kuhisi kuumwa ukiwa kwenye ndege haimaanishi hiyo corona imepatikana Tanzania.Ni dhahiri hakuna ndege ya moja kwa moja kutoka Tanzania mpaka Marekani.Na si kweli kuwa kila anayezungumzia corona kwa mtazamo tofauti basi anamuunga mkono raisi wa chama chake.

Hii michango inaweza kuwa na maana kuliko fikra na hofu iliyompata yeye.
Matumizi ya huduma za mwanzo alizofanya yeye kama hazikumsaidia isiwe sababu ya kudharau tiba hizo na kuhimiza tiba za kisasa na za hali ya juu zinazopatikana Marekani na ambazo Tanzania tuko mbali kuzifikia

Kupona kwake ajue ni rehma za Mwenyezi Mungu pekee na kwamba siku yake ya kufa bado .Huu ulikuwa ni mtihani tu wa kumzindua yeye na kuujua ufalme mkubwa kuliko anaojuwa yeye.

Vidudu vya corona si kwamba havina dawa zilizo dhidi yake katika hatua zote na uwezekano ni mkubwa kuwa tiba asili zinawasambaratisha hasa katika muda huo wa awali na ni kinga bora kwa wale waisomudu gharama kubwa za tiba na katika nchi ambayo haijafikia maendeleo makubwa ya huduma za afya mfano unapata majibu ya vipimo 15 katika saa 1
Kwanini huyu mchungaji hawezi kuamini kuwa alirudi Marekani na tatizo jengine la kiafya na baadae akapata corona huko ambako imepamba moto muda mrefu.

Kama kweli kuvaa barakoa na kukaa ndani na kujitenga na watu kwa mita 2 kunazuia maambukizi basi ugonjwa huu usingewapata watu wa nchi za ulaya na wala viongozi wakubwa na wabunge ambao kwa ubora wa maisha wanayoishi yanayowafanya wawe pekee pekee mbali na majirani.
 
Msimamo serikai ya Tanziania kuwa tangawizi, pilipili kichaa, kitunguu swaumu kuwa ni dawa ya korona haina tofauti na msimamo wa Kitaifa wa Madagascar kuwa dawa yao ya mtishamba inatibu korona. Sote tuliona kilichofuata madagascar
 
Tuone kama nyungu zitawaokoa hao Mawaziri wawili wanaopumulia mashine hapo Jakaya Kikwete Muhimbili.
 
huyu ni muongo na mnafiki, sibezi uwepo wa huu ugonjwa ila mwandishi wa hii story ni muongo na ana lengo lake spesheli
Hata amesema uwongo lakini unakaribia kabisa kuwa na ukweli. Mie nimempoteza mke wangu. Na yote aliyoyasema hapa yalipitia humohumo. In fact nilianza mimi kupata maambukizi yenye dalili zinazoshabihiana na andiko lake. Hivyo kama wewe hayajakufika ni rahisi tu kubisha.

La msingi serikali iweke miundo mbinu ya kushughulikia tatizo hili. Liko serious na watu wanateketea ndugu
 
Nashauri tu; wataalamu wetu wa AFYA msomeni huyu jamaa na fanyieni kazi hizo njia alizozisema cause najua nyie tafiti hua hamfanyi either kwa uvivu wenu au kwa kukosa pesa za ku finance tafiti zenu au sababu zote mbili kwa pamoja; nafikir kuna bonge la desa kwa uzi wa huyu mchungaji; siasa imetawala mahakamani, bungeni, maofisini, kwenye afya, elimu nk; nimeanza kutilia mashaka hata matokeo ya mitihani ya watoto wetu, hasa mitihani ya form 2 na form 4, huenda haina uhalisia hasa kwa shule za serikali
 
Nimesoma simulizi kwa makini - na sitabisha kama ni kweli au uongo. Kwa kutafakari tu,nasikitika sana maana hospitali zetu TZ bado sana (hata hao Aga Khan) kupambana na pandemics kama hizi - hata emergency plans za kuokoa maisha hamna. Hivyo silaha yetu ni kuchukua tahadhari ili tujiokoe wenyewe - huu ndio ukweli mchungu.
 
Matatizo ya kisiasa hata ukipima corona Tanzania unapewa majibu ya uongo!
 
Matatizo ya kisiasa hata ukipima corona Tanzania unapewa majibu ya uongo!
Yawezekana hii mitambo ya corona ndiyo inayosema uwongo.Siamini kuwa kuna siasa hapo.Kuna ndege imeondoka Tanzania wiki 2 zilizopita kwenda nchi ya ughaibuni.Kufika ndege nzima waliokosa corona ni 3 tu. Jee na hao siasa zao ni kuwa watu wote wawe na corona.
Kama tukiondoa hofu na tukamtegemea Mungu na halafu kutumia tiba na vyakula vya kiasili naamini corona haitatumaliza kama wanavyotabiri wengine.
 
Watanzania wana ujinga mmoja. Hawawezi kuchukua tahadhari hadi waambiwe na sauti ya mtu mmoja tu. Wimbi la kwanza ulifanikiwa sana kudhibiti kwa sababu ile sauti ya mtu mmoja pamoja na ile taharuki kila mtu alichukua tahadhari na maambukizi yakapungua sana. Bila mamlaka kuu kuwaambia kama walivyozoea watanzania basi tusubiri maafa siku chache zijazo.
 
Back
Top Bottom