#COVID19 Ushuhuda wa Mchungaji Godwin Chilewa kuhusu COVID-19: Je, tunamficha nani, kwanini na kwa Faida gani?

#COVID19 Ushuhuda wa Mchungaji Godwin Chilewa kuhusu COVID-19: Je, tunamficha nani, kwanini na kwa Faida gani?

huyu ni muongo na mnafiki, sibezi uwepo wa huu ugonjwa ila mwandishi wa hii story ni muongo na ana lengo lake spesheli
Hata kama ni muongo ushauri wake una hasara gani kwetu au wewe ndie mnafiki? Kwa nini hutaki serikali na wananchi wachukue tahadhali ili kuokoa maisha?
 
Bahati yako umeongea haya ukiwa ughaibuni. Hapa ndani hapakaliki sasa hivi mkuu, natumai wewe mwenyewe ulijionea/unajionea. Covid19 imegeuzwa ni script ambayo msimamizi mkuu ni jiwe. Ukijaribu kusema ukweli utaundiwa zengwe kwa namna yoyote ile, ili uje ukanushe. Na kwakuwa huyu jamaa ameshajua sisi WaTz tumemshindwa anatupeleka anavyotaka. Iwapo jumuiya za kimataifa hawatachukua hatua dhidi ya Kayafa, basi tutaona mengi sana.
 
bwahaahahah... hiyo sio tafiti. siitaji kuuziwa.
weka publication ya research zilizofanyika na results zake.
Watakuambia hatuthamini vya kwetu, tunathamini vya beberu!

Watu hawajui kwamba hata Panadol tunayoiona dawa ya kawaida mno, ilifanyiwa utafiti, ikaandikiwa publications.

Hizi cortisol, nimrcaf, athletes wagonjwa wangapi, controls, wengine walipewa zenye pilipili mbuzi, mtama, kichaa, tunakosea kwa sababu na mambo tunafanya kienyeji! Tuweeke records, mabandiko, tuende na usasa!

Everyday is Saturday............................... 😎
 
huyu ni muongo na mnafiki, sibezi uwepo wa huu ugonjwa ila mwandishi wa hii story ni muongo na ana lengo lake spesheli
Lengo gani mkuu? He tueleze wewe ulieliona, na kuna kitu gani alichoandika hapo ni uongo?
 
mkuu utaambiwa umetumwa na mabeberu
IMG_20210212_102235.jpg
 
Sasa wanavyo tuhamasisha tujifukize lengo lao nini haswa? Kama hata hiyo ina madhara mbona watanzania tutaisha kwa mtindo huo
Ukienda hospital ndio unaona hali halisi. Wanaosaidiwa oxygen ni watu wengi mpk nafasi zimejaa. Acha mkuu. Izi story zisikie tu.
 
Hata huko hospital mkuu watu hawapigwi nyungu bali wanawekewa oxygen.Nyungu ziko promoted Sana na wanasiasa uchwara wanaokwepa majukumu yao
Habari ya nyungu ni upumbavu mkubwa! Kama unaumwa corona, ukitaka hali iwe mbaya zaidi, au uwahi kuondoka, piga nyungu.

Mbunge yule aliyefia Dodoma mwakajana, alijisikia vibaya, akadanganywa na wenzake, jioni akapiga nyungu - hakuna anayejua alifariki saa ngapi, asubuhi walishuhudia maiti.
 
Back
Top Bottom