Ushuhuda: Wanaochomwa moto kwa kuiba siyo kweli wote ni wezi

Ushuhuda: Wanaochomwa moto kwa kuiba siyo kweli wote ni wezi

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
21,643
Reaction score
51,642
Jana limenitokea tukio la kusingiziwa utapeli, ilikuwa hivi:

Nilikuwa bar fulani mchana wa saa 10 karibu na ofisi kwetu napumzika, sasa nikaishiwa hela nikamwambia muhudumu naenda kuchukua 10000 nimeiacha ofisini me nikaondoka. Nikafika ofisini baada ya kama dakika 6 nipo kwa nje anakuja dogo muuza mayai ananiulizia wewe ndo ndege nikamjibu ndio, akauliza nimetapeliwa na mtu anafanana na wewe karibu na bar uliyokuwa unakunywa ameniambia nimpe 7000 anaingia ghetto kwake akirudi na 10000 atakula mayai ya 3000 na alikuwa amevaa shati la ki draft kama wewe.akaenda bar akaambiwa ndege ametoka sasa hivi akaelekezwa ofisini kwetu aje aone kama ni mimi.

Nilistajaabu sana nikahamaki una uhakika ni mimi nimekuibia? Dogo hana uhakika point yake ni kwamba mwizi wake ni mrefu na mweupe kama mimi na anaongea kichaga kama mimi. Kama masihara wakajaa bodaboda na watu wa mtaani kwetu na wakanigeuka mimi wakidai nimpe 7000 yake dogo ili nimalize huo mzozo na ukicheki mfukoni nina 10000 iliyobaki.

Nilibisha sana kwa kuwa mimi, sihusiki. Watu wakajaa ikawa aibu maana ni mazingira karibu na ofisi mambo yakawa mengi tukarudi mpaka bar kuuliza mpaka njia niliyopita watu kibao kama 15 hivi wananifuata baada ya mzozo mkubwa ushahidi ukaonekana kuwa sihusiki.

Nimewaza kumbe wako watu wanachomwa moto kwa kusingiziwa, usijichukulie sheria mkononi kama huna uhakika hujaibiwa acha wampige wao, we usimguse mtuhumiwa achana nae.
 
Pole sana Mkuu, bora wewe kisa chako ni cha mazingira ya maisha ya kawaida! Nimeshuhudia kwa macho yangu mawili hivi watu wawili wakifa kwa kupigwa na kuchomwa moto kwa kuitiwa wezi na wapenzi wao baada ya kuzinguana..
 
Pana tukio la wizi lilitokea mahali alfajiri wakawakurupusha wezi akatokea mtumishi anafanya mazoezi jogging alfajiri njia hio hio waliyokurupusha wezi jamaa ajui hili wala lile wakamuungia yeye wakamuua,
Masikini mtumishi, inasikitisha sana.
 
Pole sana ndege john
Kawaida mkuu sema uzuri nilikuwa nishavesha kidogo thus nilijiamini kujitetea kwa maneno mengi ila nilichojifunza washikaji sio watu yaani hata niliowaambia wanisubiri bar nirudi niwachukulie smart wananiwekea mazingira magumu ya kuingia hatiani badala wao ambao wanajua tabia yangu wanitetee.
 
Juz jamaa kapandwa na maleria kichwan katoroka hosptal hadi kuingia ndan mwa mtu maeneo ya kiwalani na kukaa seblen haelew chochote.

Mara wenyeji wa pale wakaanza kumpiga na kumkatakata na mapanga..jamaa ni kama Mungu file lake hakuligusa.

Kakimbia na kutumbukia kweny mfereji uliokuwa karbia na kituo cha bodabdo..waliokuwa wanamkimbiza wakadhan kapanda boda nao wakaunga wasidhan yupo palepale kweny mfereji ....ndo ilikuwa pona pona yake...
 
Pole Ndege
Ni kweli watoto wanatapeliwa sana kwa style hio ila duh hapana kwakweli mimi ambaye sijui hata tabia za dude nashikiwa bango mkukumkuku, maana me anytime napokaa niko busy na wakuu wa JF ni kuperuzi tu iwe nina hela sina hela.
 
Jana limenitokea tukio la kusingiziwa utapeli, ilikuwa hivi;

Nilikuwa bar fulani karibu na ofisi kwetu napumzika, sasa nikaishiwa hela nikamwambia muhudumu naenda kuchukua 10000 nimeiacha ofisini me nikaondoka...
Pole sana ndugu
 
Wanaochoma moto watuhumiwa wanapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria kwa kujichukulia maamuzi kuchoma watuhumiwa bila kuwafikisha mahakamani. Hao nao ni wahalifu washughulikiwe kisheria
 
Jana limenitokea tukio la kusingiziwa utapeli, ilikuwa hivi;

Nilikuwa bar fulani karibu na ofisi kwetu napumzika, sasa nikaishiwa hela nikamwambia muhudumu naenda kuchukua 10000 nimeiacha ofisini me nikaondoka...

Yapo mamburula yenye kushabikia kuuwawa hovyo kwa watuhumiwa hayatakaa KATU yaelimike, niko pale.
 
Pole sana mkuu,

Mwaka 2016 kuna dogo alimnunulia Godoro mpenzi wake, sasa siku moja dogo kampigia simu huyo babe wake huyo akawa hapatikani, licha ya kupiga Mara kadhaa hali ikawa ile ile, dogo akaona isiwe kesi, akatimba kwa mpenzi bila taarifa, ndipo alipomkuta bonge la bwana miraba minne, ambapo hangeweza hata kuanzisha ugomvi.

Njemba ikaondoka ikamwacha yeye dogo na demu wake,kama kupatana wapatane au waachane njemba haikutaka kujua,

Dogo akaona kuliko kuendelea na demu Malaya na mchafu, bora achukue godoro lake,
Akaingia inside akachomoa mattress yake tano kwa sita inches nane, akatoka nalo nje, ndipo ukawa mwisho wa maisha yake baada ya kupigiwa kelele moja tu.,

Mwiziiiiiiiiiio ananibia godoroooo,

Raia walikotoka na hasira zao, na ukizingatia dogo kakutwa na ushahidi, Godoro Dodoma ipo mgongoni?

Hili tukio lilinitesa kwa muda mrefu sana kulingana na nilivyomjua yule dogo, tuliheshimiana, aliniita Faza , alinikubali na nilimkubali kinomanoma, yaani Kuna wale madogo hata ukimtuma kitu hakatai kutokana na mnavyoheshimiana, nililia sana, ama kweli Dunia haina huruma.
 
Huyo fara ungemkata Banzi Kwanza .

Kila kitu huanzaga Kama uzushi vile ila ndio kinatokea.
 
Pole sana Mkuu, bora wewe kisa chako ni cha mazingira ya maisha ya kawaida! Nimeshuhudia kwa macho yangu mawili hivi watu wawili wakifa kwa kupigwa na kuchomwa moto kwa kuitiwa wezi na wapenzi wao baada ya kuzinguana..
Duuuh,kuna watu makatili sana
 
Pole sana mkuu,

Mwaka 2016 kuna dogo alimnunulia Godoro mpenzi wake, sasa siku moja dogo kampigia simu huyo babe wake huyo akawa hapatikani, licha ya kupiga Mara kadhaa hali ikawa ile ile, dogo akaona isiwe kesi, akatimba kwa mpenzi bila taarifa, ndipo alipomkuta bonge la bwana miraba minne, ambapo hangeweza hata kuanzisha ugomvi.

Njemba ikaondoka ikamwacha yeye dogo na demu wake,kama kupatana wapatane au waachane njemba haikutaka kujua,

Dogo akaona kuliko kuendelea na demu Malaya na mchafu, bora achukue godoro lake,
Akaingia inside akachomoa mattress yake tano kwa sita inches nane, akatoka nalo nje, ndipo ukawa mwisho wa maisha yake baada ya kupigiwa kelele moja tu.,

Mwiziiiiiiiiiio ananibia godoroooo,

Raia walikotoka na hasira zao, na ukizingatia dogo kakutwa na ushahidi, Godoro Dodoma ipo mgongoni?

Hili tukio lilinitesa kwa muda mrefu sana kulingana na nilivyomjua yule dogo, tuliheshimiana, aliniita Faza , alinikubali na nilimkubali kinomanoma, yaani Kuna wale madogo hata ukimtuma kitu hakatai kutokana na mnavyoheshimiana, nililia sana, ama kweli Dunia haina huruma.
Huyo binti alichukuliwa hatua yoyote?
 
Back
Top Bottom