Ushuhuda: Wanaochomwa moto kwa kuiba siyo kweli wote ni wezi

Ushuhuda: Wanaochomwa moto kwa kuiba siyo kweli wote ni wezi

Pamoja na yote, wakuu nashauri vitu viwili, cha kwanza tuangalie namna tunajiweka weka. Yani mavazi yetu, mtindo wa nywele mpaka maongezi. Na pili tujiamini vya kutosha, hata linapotokea tatizo na raia wanaangalia reaction yako baada ya kuitwa mwizi.

Sisemi ambao wanajiweka kiheshima na kujiamini hawapigwi kwa kelele za mwizi, bali asilimia kubwa ya wanaouwawa ukiwaona hata wewe unapata wasiwasi, unakuta mtu amenyoa kihuni, amevaa manguo yamechanika kwamba ndio fasheni na kibaya zaidi hajiamini, akiitiwa mwizi anakimbia akidhani atawazidi spidi raia 500 wenye ushirikiano.

Hata mtoa mada naamini kwa sehemu kubwa hivi viwili ndivyo vimemuokoa, angekuwa amevaa hovyo hovyo na hajiamini hata muda wa kumsikiliza watu wasingempa, wangeshamaliza kazi.
True ni nadra sana watu waanze kukurukia na kukupiga kama mazingira hayaruhusu kufanya hivyo. Na ni muhimu pia kuwa makini na mazingira ya kwenda kuna sehemu unaenda hata usalama wako mwenyewe unaona upo matatani sasa ukiitiwa mwizi na hakuna mtu anayekujua huko si ni rahisi kupatwa na shida.
 
Sasa hapo kuna mazingira ambayo yatashawishi raia kutokukusikiliza. Mfano umekimbia kipande umeenda kukamatiwa huko mbeleni. Au mtu kaanza kukuitia mwizi wewe unakimbia sababu unataka kuokoa maisha yako. Raia wakikukamata hawatakuwa na muda wa kukuhoji wataenda straight kukupa kichapo.

The best option ni kusimama na kuomba kusikilizana na uombe muende mlipotoka na kuhakikisha kuwa hapo hakuna wizi wala uhalifu bali kuna mtu ameamua kukukomesha. Kwenye mazingira ya haki ukweli huwa unaonekana wazi. Na mtu aliyepanga kukufanyia ubaya huwa anafeli akiambiwa afunguke wewe utasema ukweli wako yeye itabidi story yake atunge ili kutengeneza ukweli batili ambao utaumbuliwa na maswali ya msingi.
Speaking from experience, chance ya kusikilizwa ni 10% out of 100%.

Yaani ushakua tagged ni mwizi then usikilizwe? wakati jamaa wanazozana huyu mwizi au sio mwizi anatokea jamaa ambaye hata hajui mjadala umefikia wapi anakupiga na shoka la kichwa, unapotua chini unasindikizwa na tofali, Mara mtu kakutia mpini wa jembe kichwani! hapo kutakua na kikao tena?
 
Jana limenitokea tukio la kusingiziwa utapeli, ilikuwa hivi:

Nilikuwa bar fulani mchana wa saa 10 karibu na ofisi kwetu napumzika, sasa nikaishiwa hela nikamwambia muhudumu naenda kuchukua 10000 nimeiacha ofisini me nikaondoka. Nikafika ofisini baada ya kama dakika 6 nipo kwa nje anakuja dogo muuza mayai ananiulizia wewe ndo ndege nikamjibu ndio, akauliza nimetapeliwa na mtu anafanana na wewe karibu na bar uliyokuwa unakunywa ameniambia nimpe 7000 anaingia ghetto kwake akirudi na 10000 atakula mayai ya 3000 na alikuwa amevaa shati la ki draft kama wewe.akaenda bar akaambiwa ndege ametoka sasa hivi akaelekezwa ofisini kwetu aje aone kama ni mimi.

Nilistajaabu sana nikahamaki una uhakika ni mimi nimekuibia? Dogo hana uhakika point yake ni kwamba mwizi wake ni mrefu na mweupe kama mimi na anaongea kichaga kama mimi. Kama masihara wakajaa bodaboda na watu wa mtaani kwetu na wakanigeuka mimi wakidai nimpe 7000 yake dogo ili nimalize huo mzozo na ukicheki mfukoni nina 10000 iliyobaki.

Nilibisha sana kwa kuwa mimi, sihusiki. Watu wakajaa ikawa aibu maana ni mazingira karibu na ofisi mambo yakawa mengi tukarudi mpaka bar kuuliza mpaka njia niliyopita watu kibao kama 15 hivi wananifuata baada ya mzozo mkubwa ushahidi ukaonekana kuwa sihusiki.

Nimewaza kumbe wako watu wanachomwa moto kwa kusingiziwa, usijichukulie sheria mkononi kama huna uhakika hujaibiwa acha wampige wao, we usimguse mtuhumiwa achana nae.
Ungemuachia tu hiyo Msimbazi aka Ngada FC dogo ajinome.
 
Jana limenitokea tukio la kusingiziwa utapeli, ilikuwa hivi:

Nilikuwa bar fulani mchana wa saa 10 karibu na ofisi kwetu napumzika, sasa nikaishiwa hela nikamwambia muhudumu naenda kuchukua 10000 nimeiacha ofisini me nikaondoka. Nikafika ofisini baada ya kama dakika 6 nipo kwa nje anakuja dogo muuza mayai ananiulizia wewe ndo ndege nikamjibu ndio, akauliza nimetapeliwa na mtu anafanana na wewe karibu na bar uliyokuwa unakunywa ameniambia nimpe 7000 anaingia ghetto kwake akirudi na 10000 atakula mayai ya 3000 na alikuwa amevaa shati la ki draft kama wewe.akaenda bar akaambiwa ndege ametoka sasa hivi akaelekezwa ofisini kwetu aje aone kama ni mimi.

Nilistajaabu sana nikahamaki una uhakika ni mimi nimekuibia? Dogo hana uhakika point yake ni kwamba mwizi wake ni mrefu na mweupe kama mimi na anaongea kichaga kama mimi. Kama masihara wakajaa bodaboda na watu wa mtaani kwetu na wakanigeuka mimi wakidai nimpe 7000 yake dogo ili nimalize huo mzozo na ukicheki mfukoni nina 10000 iliyobaki.

Nilibisha sana kwa kuwa mimi, sihusiki. Watu wakajaa ikawa aibu maana ni mazingira karibu na ofisi mambo yakawa mengi tukarudi mpaka bar kuuliza mpaka njia niliyopita watu kibao kama 15 hivi wananifuata baada ya mzozo mkubwa ushahidi ukaonekana kuwa sihusiki.

Nimewaza kumbe wako watu wanachomwa moto kwa kusingiziwa, usijichukulie sheria mkononi kama huna uhakika hujaibiwa acha wampige wao, we usimguse mtuhumiwa achana nae.
Dah yaani leo ningefika kwako ningekuta turubai? Wallah ningewahi mochwari ya Mwananyamala kukuhifadhi vema! Pole sana
 
Jana limenitokea tukio la kusingiziwa utapeli, ilikuwa hivi:

Nilikuwa bar fulani mchana wa saa 10 karibu na ofisi kwetu napumzika, sasa nikaishiwa hela nikamwambia muhudumu naenda kuchukua 10000 nimeiacha ofisini me nikaondoka. Nikafika ofisini baada ya kama dakika 6 nipo kwa nje anakuja dogo muuza mayai ananiulizia wewe ndo ndege nikamjibu ndio, akauliza nimetapeliwa na mtu anafanana na wewe karibu na bar uliyokuwa unakunywa ameniambia nimpe 7000 anaingia ghetto kwake akirudi na 10000 atakula mayai ya 3000 na alikuwa amevaa shati la ki draft kama wewe.akaenda bar akaambiwa ndege ametoka sasa hivi akaelekezwa ofisini kwetu aje aone kama ni mimi.

Nilistajaabu sana nikahamaki una uhakika ni mimi nimekuibia? Dogo hana uhakika point yake ni kwamba mwizi wake ni mrefu na mweupe kama mimi na anaongea kichaga kama mimi. Kama masihara wakajaa bodaboda na watu wa mtaani kwetu na wakanigeuka mimi wakidai nimpe 7000 yake dogo ili nimalize huo mzozo na ukicheki mfukoni nina 10000 iliyobaki.

Nilibisha sana kwa kuwa mimi, sihusiki. Watu wakajaa ikawa aibu maana ni mazingira karibu na ofisi mambo yakawa mengi tukarudi mpaka bar kuuliza mpaka njia niliyopita watu kibao kama 15 hivi wananifuata baada ya mzozo mkubwa ushahidi ukaonekana kuwa sihusiki.

Nimewaza kumbe wako watu wanachomwa moto kwa kusingiziwa, usijichukulie sheria mkononi kama huna uhakika hujaibiwa acha wampige wao, we usimguse mtuhumiwa achana nae.
Hiyo cha mtoto unampa demu lift añafika anapokwenda unasimama ashuke anakwambia mlipe pesa zake kwa uchi aliyokuuzia usiku kucha, hapo ndio utajuwa maharage ni mboga au kitoweo, halafu RAIA wamejaa pembeni wanawazoom tu.
 
Kawaida mkuu sema uzuri nilikuwa nishavesha kidogo thus nilijiamini kujitetea kwa maneno mengi ila nilichojifunza washikaji sio watu yaani hata niliowaambia wanisubiri bar nirudi niwachukulie smart wananiwekea mazingira magumu ya kuingia hatiani badala wao ambao wanajua tabia yangu wanitetee.
Tena Sasa nimegundua hivi vishikaji vya kuvinunilia smart, wengi ni vinafki na waongo waongo sana na ndiyo hai kutwa vinashinda bar huku mfukoni havina kitu!
 
Hiyo cha mtoto unampa demu lift añafika anapokwenda unasimama ashuke anakwambia mlipe pesa zake kwa uchi aliyokuuzia usiku kucha, hapo ndio utajuwa maharage ni mboga au kitoweo, halafu RAIA wamejaa pembeni wanawazoom tu.
Alafu wanapenda uwashushe karibu na boda boda naunapomshusha lazima Kuna boda anamjua utajuta!
Yaaan kwa dar kumuamini mtu usiyefahamiana naye ni risk sana.
 
Muda mwingine hao madogo wao ndio wezi.. Na wanajua kabisa kuepusha zogo na kwa usalama wako utatoa hela yaishe.

15 years old si ndio panya road hao.

Pole sana chief.
 
Nini kifanyike kupata suluhu ya hili tatizo?
Wahusika wanaojichukuliwa sheria mkononi wakamatwe na wafungwe maisha na Habari ziwafikie wote wenye tabia hiyo

Unakuta muuwaji yeye mwenyewe mwizi
Asilimia kubwa ya watu huko ni waizi halafu wanajifanya wema
Mwema unaua
 
Jana limenitokea tukio la kusingiziwa utapeli, ilikuwa hivi:

Nilikuwa bar fulani mchana wa saa 10 karibu na ofisi kwetu napumzika, sasa nikaishiwa hela nikamwambia muhudumu naenda kuchukua 10000 nimeiacha ofisini me nikaondoka. Nikafika ofisini baada ya kama dakika 6 nipo kwa nje anakuja dogo muuza mayai ananiulizia wewe ndo ndege nikamjibu ndio, akauliza nimetapeliwa na mtu anafanana na wewe karibu na bar uliyokuwa unakunywa ameniambia nimpe 7000 anaingia ghetto kwake akirudi na 10000 atakula mayai ya 3000 na alikuwa amevaa shati la ki draft kama wewe.akaenda bar akaambiwa ndege ametoka sasa hivi akaelekezwa ofisini kwetu aje aone kama ni mimi.

Nilistajaabu sana nikahamaki una uhakika ni mimi nimekuibia? Dogo hana uhakika point yake ni kwamba mwizi wake ni mrefu na mweupe kama mimi na anaongea kichaga kama mimi. Kama masihara wakajaa bodaboda na watu wa mtaani kwetu na wakanigeuka mimi wakidai nimpe 7000 yake dogo ili nimalize huo mzozo na ukicheki mfukoni nina 10000 iliyobaki.

Nilibisha sana kwa kuwa mimi, sihusiki. Watu wakajaa ikawa aibu maana ni mazingira karibu na ofisi mambo yakawa mengi tukarudi mpaka bar kuuliza mpaka njia niliyopita watu kibao kama 15 hivi wananifuata baada ya mzozo mkubwa ushahidi ukaonekana kuwa sihusiki.

Nimewaza kumbe wako watu wanachomwa moto kwa kusingiziwa, usijichukulie sheria mkononi kama huna uhakika hujaibiwa acha wampige wao, we usimguse mtuhumiwa achana nae.
Punguza ulevi mkuu...toka umepata hiyo ajira umekuwa chapombe sana...naona unasahau ulipotoka
 
Wanaochoma moto watuhumiwa wanapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria kwa kujichukulia maamuzi kuchoma watuhumiwa bila kuwafikisha mahakamani. Hao nao ni wahalifu washughulikiwe kisheria
Tatizo serikali yenyewe ndio hio wanaona kuwa jambazi lingine limeuwawa kumbe wengi wanasingiziwa
Unakuta mtu kaiba karanga au kuku wanamchoma moto
 
Dawa akikuitia mwizi kaa hapo hapo. Usiondoke. Halafu wakifika pale wale watu anza kutoa vielelezo kuwa unajuana na huyu mtu na ulifikajefikaje hapo mlipo.

Mwisho wa siku msikilizwe nyote ukweli utajulikana. Hakikisha unamalizana nae kwa gharama kubwa upande wake ili iwe fundisho kwake na kwa wenzake wenye tabia kama yake.
Kaka unawajua wanawake? Huo muda wa kuongea kwa amani hautakuwepo. Yaani kila utakapotaka kuongea ukweli, na yeye ili kufunika madhambi yake anakuwa anapiga keleke kama kachanganyikiwa "mwiziii"

Wengi wanakufa kwa staili hiyo kwa sababu nafasi ya kujitetea inaingiliwa na mwanamke.
 
Pole sana Mkuu, bora wewe kisa chako ni cha mazingira ya maisha ya kawaida! Nimeshuhudia kwa macho yangu mawili hivi watu wawili wakifa kwa kupigwa na kuchomwa moto kwa kuitiwa wezi na wapenzi wao baada ya kuzinguana..
Unachokisema ni kweli kabisaa, kijichi huku wiki iliopita saa moja saa mbili jamaa mmoja braza men baunsa baunsa kaitiwa mwizi, watu fasta makofi yakaanza Bahati akatokea mtu kuanza kuhoji kaiba nn?? kimyaa ndo jamaa anajitetea ana mgogoro na demu wake Ss huyoo mdada kampigia kelele ya mwizi, ajabu Ss Kumbe yule mdada yupo hapo hapo kwenye kundi la kumshambulia jamaa, mdada kuulizwa anauma uma midomo tuu, jamaa kwa hasira akiwa analia alimtwanga huyoo demu wake kisha akapandishwa bodaboda aondoke eneo lilee
Umati ukabaki na yule maluuuni bi dada
 
Kigogo Cha wote natembea nakutana na mtiti wa watu wanatokea kama kichochoroni ikabidi nihamaki!


Ghafla namuona jamaa kakabwa shingo nyuma Kuna mtiti wa watu wakimsindikiza huku akila mimbata na mitama Hadi kwenye nyumba Fulani hivi.


Kumbe yule jamaa ni muuza sandals Sasa yule machinga katika harakati zake Kuna dada kwenye Moja ya nyumba alimuita akihitaji kuona au kununua sandals yule dada baada ya kuangalia sandals na kushindwana yule machinga ikabidi aondoke Sasa yule dada kwa mawenge ikabidi ajisachi simu yake haioni hapohapo akaanza kumpigia kelele za mwizi yule machinga ndipo watu walipoanza kumkimbiza na kumkamata bahati nzuri Kuna wenye busara walisema twendeni nae kwa aliyeibiwa tupate uhakika lkn huku akisindikizwa na mambata


Kufika kwenye Ile nyumba simu inapigwa inakutwa ipo ukumbini daah na ilikuwa chipuchupu achomwe moto Dogo wa watu machinga ..aliishia kulia na kulalamika tu
 
Asee hii ya kutaka kumpiga mtu kisa eti mwizi au vipi Kuna siku nimeshuhudia ubabe wa kutisha sana.
Bwana wee Kuna bodaboda mmoja pale mabibo sokoni alimgonga dogo mmja kwa pikipiki mitaa ya kupita pale NIT . Baada ya kukimbia Kuna watu walimuona wakamsevu kichwani.. ah mbona tunamjua Yule! Anapaki mabibo sokoni. Basi wakatoka humo watu mamia wanamsaka jamaa. Ghafla wanamuona . Wana mawe, wengine visu na mitarimbo wakataka kumdandia wapige waue. Ghafla akatokea jamaa mmoja mbavu hivi akawambiaje ujue .. dogo njoo Hapa ole wake arushe mtu hata jiwe hapa. Huyo dogo aliyegongwa tutashughulikia tatizo lake.
Ghafla watu wakasambaratika. Nilishangaa ujue..
Mwisho.
 
Back
Top Bottom